image

HTML- somo la 2: Kazi za HTML, code na tag kwenye website.

Katika somo somo hili utajifunza maana ya code, tag na mpangilio wa faili la HTML

Karibi tena kwenye mafunzo ya HTML na hili ni somo la pili. Kama hujalipata somo la kwanza tumia linki itakayopatikana mwisho wa posti hii ili uweze kulipata somo la kwanza.

Somo la kwanza utalipata kwa link hii https://web.facebook.com/groups/androbongo/permalink/568341711186808/


 

HTML ni nini?

HTML ni kifupisho cha maneno Hypertext Markup language. Hii ni moja ya lugha za kikompyuta yaani computer language. Ni moja katka lugha za kikompyuta zilizo rahisi sana na ni rahisi kuelewa. Pia matumizi yake ni mara nyingi tumekuwa tukikutana nayo kwenye mitandao.

 

Je  HTML ina kazi gani?

Kazi kuu ya HTML ni kutengeneza kurasa za website (tovuti) na blog. Kwa mfano ukurasa wa facebook wenyewe una mchanganyiko wa code za HT,L na lugha nyingine za kikompyuta. Siku hizi HTML inaweza kutumika hata katika kutengenezea App za simu na software za kompyuta (desktop App).

 

Je code ni nini?

Code ni maandishi yanayobeba maelekezo ambayo hupewa kompyuta maelekezo hayo ili iweze kufanya shughuli fulani. Lugha zote za kikompyuta hutumia code. Hivyo HTML kwa kuwa ni mojaya lugha za kikompyuta nayo hutumia code, kama ulivyoona kwenye somo lililotangulia.

 

Je HTML ni programming language.

Hapana HTML ni Markup Language, haiingii kwenye programming language kwa sababu sio logic.

 

HTML inafanyaje kazi kwenye blog ama website?

  1. Inaboresha muonekano wa ukurasa wa blog ama tovuti kwa mfano kutia rangi, kuweka picha na kupangilia maandishi, paragraph na vichwa vya habari
  2. HTML inaweka mpangilio wa ukurasa vyema kwa ajili ya kutumika na lugha nyingine kama php na javascript
  3. Hutumika kutengenezea font end yaani ukurasa ambao mtembeleaji wa blog ama website (tovuti) atakutana nao
  4. Hutumika kutengeneza fomu ya kukusanya taarifa na kujisajili

 

Je naweza kutengeneza blog ama website mwenyewe kwa kutumia HTML pekee?

Ndio unaweza kutengeneza website (tovuti) kwa html tu na ikawa live na watu wakaitembele. Ila kwa blog, sirahisi utahitajika uchanganye na lugha nyingine za kompyuta kama php ilikupata dynamic page yaani kurasa ambazo zinauwezo wa kufanyiwa update kama kupost, kukoment na kulike n.k

 

Ni nni ukomo wa mafunzo haya?

Ukomo wa mafunzo haya ni kukuwezesha kujifunza HTML, kwa simu yako, uweze kutengeneza website ama kurasa za mtandao kwa simu yako na kuziweka live yaani kuhost. Mafunzo haya yote ni bure na yatakuwa katika hatua kwa hatuwa. Hatuwa ya kwanza ndio hii imeanza na itachukuwa wiki moja. Kisha itafata ya pilie

 

Endelea na somo……..

 

TUANZE SOMO LETU HAPA:

Kwa kuwa umeshajifnza mambo adhaa. Pia umeweza kuandaa simu yako ili kuweza kuendana na somo. Sasa somo letu litaanzia pale ulipo ishia kwenye somo lililopita. Kwanza funguwa App yako TrebEdit, ingia menu kisha workplace kisha bofya jina la project uliotengenez jana. Kisha bofya, utakutana na faili lako la index.html. Bofya hilo faili hapo code za HTML zitafunguka. Kama tumekwenda pamoja, code ambazo ulipest katika somo lililotangulia ni hizi hapa chini:-




 

<!DOCTYPE html>

<html lang="en">

<head>

<meta charset="utf-8">

<title>Home Page</title>

</head>

<body>

<h1>Mafunzo ya HTML</h1>

<h2><u>Jifunze bure</u></h2>

<p>Haya ni mafunzo ya HTML kwa kutumia simu</p>

<br><br><br><h2>

<i>From <br>Bongoclass</i>

</body>

</html>



 

Kama unatumia PC kopi hizo code kisha pest kwenye notepad kisha sevu index.html

 

MPANGILIO WA FAILI LA HTML

1.Sehemu kuu mbili za ukurasa wa HTML

Faili la HTML lina sehemu kuu mbili ambazo ni <head> na <body>. Katika sehemu hii ya <head> ndipo ambapo panakaa taarifa muhimu kuhusu faili lako, ikiwepo kichwa cha habari ama maudhui au title hii huwakilishwa na <title>, pia katika sehemu hii ya <head> kukaa taarifa zingine kama icon, link, icon, muadndishi, muhutasari kuhusu maudhui  na nyinginezo.

 

Taarifa hizi mara nyingi hazionekani kwa watumiaji wa mtandao huo, kwani hazibebi maudhui ila zinabeba mpangilio. Katika taarifa hizi chache kuonekana na watumiaji wa mtanda kwa mfano icon na title.

 

Sehemu ya pili ni <body>. sehemu hii ndio hubeba malengo ya ukurasa huo. Sehemu hii dio ambayo mtumiaji wa mtandao atakutana nayo na kuvinjari. Kama unataka kuandika ukurasa wa website unaohusu faida za hewa, basi maudhui yako utayaweka kwenye sehemu hii.

 

  1. Mpangilio wa code katika ukurasa wa HTML

Ukiangalia kwa ukaribu code hizo hapo juu utajifunza kuwa:-

<">...



Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 454


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

HTML - somo la 3: Tags za HTML zinazotumiwa katika uandishi
Katika somo hili nitakuletea orodhabya tag 25 za html ambazo hugumiwa katikabuandishi. Soma Zaidi...

HTML-somo la 5: Jinsi ya kupangilia munekano wa maudhui kwenye website
Katika somo hili utajifunza Kuweka picha Kuweka rangi Kuweka linki Kupangilia position na alignment ya maandishi Kuongeza ukubwa wa herufi Kukoment Soma Zaidi...

haloo word
all haloo Soma Zaidi...

HATML - somo la 4: Jinsi ya kutumia tag za html
Katka somo hi utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia tag za html ili kupangilia muonekano wa maudhui Soma Zaidi...

HTML - somo la 15: Jinsi ya kutengeneza website kwa kutumia HTML
Katika somo hili tutakwenda kutengeneza website yetu kutoka mwanzo hadi mwisho Soma Zaidi...

HTML - somo la 16: Jinsi ya ku host website bure
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ku host website yako bila malipo Soma Zaidi...

HTML- somo la 2: Kazi za HTML, code na tag kwenye website.
Katika somo somo hili utajifunza maana ya code, tag na mpangilio wa faili la HTML Soma Zaidi...

HTML - somo la 11: Jinsi ya kuweka style mbalimbali kwenye html
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuweka style mbalimbali kwenye ukurasa wa html Soma Zaidi...

HTML - somo la 9: Jinsi ya kutumia tag za HTML katika uandishi wa maudhui
Katika somo hili utakwenda kuona jinsi ya kuzitumia tag balimbali za html Soma Zaidi...

HTML - somo la 6: Jinsi ya kuweka menyu kwenye faili la HTML
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuweka menyu kwenye faili la html na kuweka rangi ya background. Pia utajifunza kufanya ukurasa uwe responsive yaani uendani na ukubwa wa kifaa. Soma Zaidi...

HTML - somo la 10: Maana ya HTML attribute na jinsi zinavyofanya kazi
Katika somo hili utakwenda kijifunza kuhusu HTML attributes na jinsi ambavyo zinafanya kazi Soma Zaidi...

HTML - somo la 14: Hatua za kutengeneza website
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza website hatuwa kwa hatuwa Soma Zaidi...