picha

HTML - somo la 11: Jinsi ya kuweka style mbalimbali kwenye html

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuweka style mbalimbali kwenye ukurasa wa html

ATTRIBUTE AU TAG YA STYLE
Katika somo lililotangulia tuliweza kuona namna ambavyo attribute zinavyofanya kazi. Pia tuliona aina mbalimbali za attributes na mifano yake. Katika somo hili tutakwenda kuangalia attribute ya style tu. Hii ni moja kati ya mwanzo mzuri wa kujifunza CSS.

 

Style inaweza kuwekwa ndani ya element na nje ya element. Stayle ikiwa nje ya element inaweza kutumika kwa element zaidi ya moja. Na ikiwa ndani ya element hutumika kwa element husika tu. Wakati mwingine kama kumetokea ufungaji mbaya wa style inaweza kuathiri element nyingi tofauti na makusudiwa.

 


STYLE INAYOWEKWA NJE YA ELEMENT:
Style ikiwa nje ya element huwekwa kwa kutumia tag ya CSS ambayo ni <style> kisha tribute zote zinakuwa ndani ya tag hii. Kuna faida kubwa ya kutumia style hii ya nje ya element kuliko ya ndani ya element.

Kwa mfano style ya nje ya element hufanya code ziwe nzuri, hupunguza mrundikano wa code ndani ya element pia huweza kuweka stayle kwenye element zaidi ya moja. Hapo chini nitakuletea mifano ya style za nje:-

 

1.JINSI YA KUWEKA RANGI
Tume jifunza katika masomo yaliotangulia kuwa unapotaka kuweka rangi utatumia attribute ya color.  Kwa mfano: <p style=”color:yellow”>hellow</p> katika mfano huu neno hellow litakuwa na rangi nyekundu. Sasa ninataka kuweka kila element na rangi yake. Chukulia mfano una element tag hizi <b>, <p>, <h1> kila moja uwe na rangi yake. Kwa mfano kama huu wa style ya ndani utafanya hivi:-
 <b style=”color:yellow”>hellow</b>
 <p style=”color:red”>hellow</p>
 <h1 style=”color:blue”>hellow</h1>

 

Sasa kwa kutumia style ya nche utafanya hivi:-
1.Kwanza utaweka tag ya style
2.Utaandika tag mfano p
3.Utaweka bano hili {}
4.Attribute zote ziwe ndani ya hayo mabano
5.Kama utakuwa na attribute zaidi ya moja tengenisha kwa alama hii ;
6.Usisahau kufunga tag ya style.
7.Kisha andika element zako.

MFANO:
<html>
<style>
 b {color: yellow}
 p {color:   red}
 h1 {color: blue}
</style>
<b>hellow i'm yellow</b><br>
<p>hellow i'm red</p>
<h1>hellow I'm blue</h1>
</html>

Katika mfano huo utaona maandishi yaliyo kwenye tag ya b ni ya njano, na ya kwenye <p> ni ya wekundu na ya kwenye <h1> ni ya buluu.


2.KUWEKA BACKGROUND COLOR
Kama tulivyoona kwenye mfano wa hapo juu jinsi ya kuweka rangi kwa kutumia style iliyo nje ya element. Na hapa tutaona jinsi ya kutumia style ya nje ya element kueweka background color. 

 

Katika hali ya kawaida background color kwenye element huwekwa kwa kutumia style= kisha utaweka value ya atribute style. Kwa mfano
<p style=”background-color:green”>Hellow I’m green</p> Katika mfano huu maneno haya yatakuwa na rangi ya kijani. Sasa ikiwaninataka kutumia background color moja kwenye element zaidi ya moja, mfano kwenye tag ya <p>, <b> na <I>. Hapa nitatumia kwanza tag ambayo inaweza kubeba tag zote hizo kw amfano unaweza kutumia tag ya <body> lakini hii itaweka backrond kwenye ukurasamzina. Ama unaweza kutumia tag kama <div> hii inaweza kubeba tag nyingi ndani yake. Katika mfano wa hapo chini nitatumia zote mbili <body> na <div>

<html>
<style>
 body {background-color: pink;}
</style>
<body>
 <p>hellow i'm paragraph</p>
 <b>hrllow I'm bolded text</b>
 <i>hellow I'm italic</i>
</body>
</html>

Kwa kutumia <div> mfano:-
<html>
<style>
 div {background-color: purple;}
</style>
<div>
 <p>hellow i'm paragraph</p>
 <b>hrllow I'm bolded text</b>
 <i>hellow I'm italic</i>
</div>
</html>

3.KUWEKA MIPANGIL...

Ingia sasa ili uweze kusoma makala hii yote.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: HTML Main: Masomo File: Download PDF Views 1262

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 web hosting    

Post zinazofanana:

Jinsi ya Kutatua Tatizo la Simu Kutopiga Simu

Kama simu yako haipigi au haipokei simu, usipaniki. Mara nyingi tatizo hili linasababishwa na mambo madogo unayoweza kuyarekebisha mwenyewe nyumbani. Angalia salio na bando lako, washa na uzime mfumo wa ndege (Airplane Mode), au zima simu na kuiwasha tena. Kama hayo hayajasaidia, hakikisha laini yako (SIM card) imekaa vizuri au wasiliana na kampuni yako ya simu. Kwenye makala hii, tutaenda hatua kwa hatua kwa lugha rahisi kabisa ili urudishe simu yako kwenye hali ya kawaida haraka

Soma Zaidi...
HTML - somo la 14: Hatua za kutengeneza website

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza website hatuwa kwa hatuwa

Soma Zaidi...
Jinsi ya Kutatua Tatizo la Speaker

Spika ni kifaa kinachobadilisha mawimbi ya umeme kuwa sauti tunayosikia. Ndani ya spika kuna sumaku na utando laini unaotikisika ili kutoa sauti. Spika inapogoma kufanya kazi, vyanzo vikuu huwa ni vitatu: matatizo ya kiufundi (waya/uchafu), matatizo ya mipangilio (settings), au hitilafu za mfumo wa kompyuta/simu.Uzuri ni kwamba, matatizo mengi yanayotokea kila siku unaweza kuyatatua mwenyewe kwa kufuata hatua rahisi tulizokuandalia hapa chini

Soma Zaidi...
Jinsi ya Kutatua Tatizo la Kamera Kutofanya Kazi

Kamera ya simu au kompyuta yako imegoma kufanya kazi? Usipaniki. Tatizo hili hutokea mara kwa mara na mara nyingi halihitaji ufundi mkubwa. Makala hii inakupa suluhisho la haraka na rahisi kuanzia kusafisha lenzi, kuwasha upya vifaa, hadi kuangalia mipangilio ya ndani (permissions). Utafanya kamera yako ianze kazi tena ndani ya dakika chache bila kutumia gharama yoyote.

Soma Zaidi...
HTML - somo la 10: Maana ya HTML attribute na jinsi zinavyofanya kazi

Katika somo hili utakwenda kijifunza kuhusu HTML attributes na jinsi ambavyo zinafanya kazi

Soma Zaidi...
HTML-somo la 5: Jinsi ya kupangilia munekano wa maudhui kwenye website

Katika somo hili utajifunza Kuweka picha Kuweka rangi Kuweka linki Kupangilia position na alignment ya maandishi Kuongeza ukubwa wa herufi Kukoment

Soma Zaidi...