HTML - somo la 11: Jinsi ya kuweka style mbalimbali kwenye html

HTML - somo la 11: Jinsi ya kuweka style mbalimbali kwenye html

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuweka style mbalimbali kwenye ukurasa wa html

ATTRIBUTE AU TAG YA STYLE
Katika somo lililotangulia tuliweza kuona namna ambavyo attribute zinavyofanya kazi. Pia tuliona aina mbalimbali za attributes na mifano yake. Katika somo hili tutakwenda kuangalia attribute ya style tu. Hii ni moja kati ya mwanzo mzuri wa kujifunza CSS.

 

Style inaweza kuwekwa ndani ya element na nje ya element. Stayle ikiwa nje ya element inaweza kutumika kwa element zaidi ya moja. Na ikiwa ndani ya element hutumika kwa element husika tu. Wakati mwingine kama kumetokea ufungaji mbaya wa style inaweza kuathiri element nyingi tofauti na makusudiwa.

 


STYLE INAYOWEKWA NJE YA ELEMENT:
Style ikiwa nje ya element huwekwa kwa kutumia tag ya CSS ambayo ni <style> kisha tribute zote zinakuwa ndani ya tag hii. Kuna faida kubwa ya kutumia style hii ya nje ya element kuliko ya ndani ya element.

Kwa mfano style ya nje ya element hufanya code ziwe nzuri, hupunguza mrundikano wa code ndani ya element pia huweza kuweka stayle kwenye element zaidi ya moja. Hapo chini nitakuletea mifano ya style za nje:-

 

1.JINSI YA KUWEKA RANGI
Tume jifunza katika masomo yaliotangulia kuwa unapotaka kuweka rangi utatumia attribute ya color.  Kwa mfano: <p style=”color:yellow”>hellow</p> katika mfano huu neno hellow litakuwa na rangi nyekundu. Sasa ninataka kuweka kila element na rangi yake. Chukulia mfano una element tag hizi <b>, <p>, <h1> kila moja uwe na rangi yake. Kwa mfano kama huu wa style ya ndani utafanya hivi:-
 <b style=”color:yellow”>hellow</b>
 <p style=”color:red”>hellow</p>
 <h1 style=”color:blue”>hellow</h1>

 

Sasa kwa kutumia style ya nche utafanya hivi:-
1.Kwanza utaweka tag ya style
2.Utaandika tag mfano p
3.Utaweka bano hili {}
4.Attribute zote ziwe ndani ya hayo mabano
5.Kama utakuwa na attribute zaidi ya moja tengenisha kwa alama hii ;
6.Usisahau kufunga tag ya style.
7.Kisha andika element zako.

MFANO:
<html>
<style>
 b {color: yellow}
 p {color:   red}
 h1 {color: blue}
</style>
<b>hellow i'm yellow</b><br>
<p>hellow i'm red</p>
<h1>hellow I'm blue</h1>
</html>

Katika mfano huo utaona maandishi yaliyo kwenye tag ya b ni ya njano, na ya kwenye <p> ni ya wekundu na ya kwenye <h1> ni ya buluu.


2.KUWEKA BACKGROUND COLOR
Kama tulivyoona kwenye mfano wa hapo juu jinsi ya kuweka rangi kwa kutumia style iliyo nje ya element. Na hapa tutaona jinsi ya kutumia style ya nje ya element kueweka background color. 

 

Katika hali ya kawaida background color kwenye element huwekwa kwa kutumia style= kisha utaweka value ya atribute style. Kwa mfano
<p style=”background-color:green”>Hellow I’m green</p> Katika mfano huu maneno haya yatakuwa na rangi ya kijani. Sasa ikiwaninataka kutumia background color moja kwenye element zaidi ya moja, mfano kwenye tag ya <p>, <b> na <I>. Hapa nitatumia kwanza tag ambayo inaweza kubeba tag zote hizo kw amfano unaweza kutumia tag ya <body> lakini hii itaweka backrond kwenye ukurasamzina. Ama unaweza kutumia tag kama <div> hii inaweza kubeba tag nyingi ndani yake. Katika mfano wa hapo chini nitatumia zote mbili <body> na <div>

<html>
<style>
 body {background-color: pink;}
</style>
<body>
 <p>hellow i'm paragraph</p>
 <b>hrllow I'm bolded text</b>
 <i>hellow I'm italic</i>
</body>
</html>

Kwa kutumia <div> mfano:-
<html>
<style>
 div {background-color: purple;}
</style>
<div>
 <p>hellow i'm paragraph</p>
 <b>hrllow I'm bolded text</b>
 <i>hellow I'm italic</i>
</div>
</html>

3.KUWEKA MIPANGIL...

Ingia sasa ili uweze kusoma makala hii yote.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu Rajabu
Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: HTML Main: Masomo File: Download PDF Views: 1274

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 ai web app     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

Faida za Screen Protector

Screen Protector ni kifaa chembamba kinachowekwa juu ya skrini ya simu ili kuilinda dhidi ya mikwaruzo, mipasuko na uharibifu mwingine unaoweza kutokea wakati wa matumizi ya kila siku. Watu wengi hununua simu za gharama kubwa lakini husahau kulinda sehemu muhimu zaidi ya simu hiyo, ambayo ni skrini. Makala hii inaelezea kwa kina faida za Screen Protector, aina zake, jinsi ya kuchagua inayofaa, na sababu zinazofanya iwe uwekezaji muhimu kwa kila mwenye simu.

Soma Zaidi...
Jinsi ya Kutafuta Simu Iliyopotea

Kupoteza simu ni jambo linaloweza kumpata mtu yeyote wakati wowote. Simu ya kisasa si kifaa cha kupigia simu tu, bali pia huhifadhi picha, namba za watu unaowasiliana nao, ujumbe, taarifa za benki, akaunti za mitandao ya kijamii na taarifa nyingine muhimu. Ndiyo maana kupoteza simu kunaweza kusababisha usumbufu mkubwa na hata hatari ya taarifa binafsi kuibiwa. Habari njema ni kwamba kuna njia mbalimbali zinazoweza kukusaidia kuitafuta simu iliyopotea. Unaweza kutumia huduma zilizopo ndani ya simu kama vile programu za kuitafuta simu, kutumia namba ya simu, kuwasiliana na kampuni ya mtandao, au kutumia taarifa za mwisho zilipoonekana. Makala hii inaeleza hatua kwa hatua jinsi ya kutafuta simu iliyopotea kwa njia rahisi ambayo kila mtu anaweza kuelewa.

Soma Zaidi...
Jinsi ya Kutatua Tatizo la Simu Kutopiga Simu

Kama simu yako haipigi au haipokei simu, usipaniki. Mara nyingi tatizo hili linasababishwa na mambo madogo unayoweza kuyarekebisha mwenyewe nyumbani. Angalia salio na bando lako, washa na uzime mfumo wa ndege (Airplane Mode), au zima simu na kuiwasha tena. Kama hayo hayajasaidia, hakikisha laini yako (SIM card) imekaa vizuri au wasiliana na kampuni yako ya simu. Kwenye makala hii, tutaenda hatua kwa hatua kwa lugha rahisi kabisa ili urudishe simu yako kwenye hali ya kawaida haraka

Soma Zaidi...
Sababu Zinazofanya Betri Iishe Haraka

Betri ni sehemu muhimu sana ya simu, kompyuta mpakato, saa janja na vifaa vingine vya kielektroniki. Hata hivyo, watu wengi hukutana na tatizo la betri kuisha haraka bila kujua chanzo chake. Wakati mwingine tatizo halitokani na ubora wa simu au betri, bali hutokana na namna kifaa kinavyotumika kila siku. Katika makala hii utajifunza sababu kuu zinazofanya betri iishe haraka, jinsi ya kutambua tatizo, pamoja na njia rahisi za kuongeza muda wa matumizi ya betri. Maelezo haya yameandikwa kwa lugha rahisi ili kila mtu ayaelewe, hata kama hana ujuzi wa teknolojia.

Soma Zaidi...
Jinsi ya Kuhamisha Data Kati ya Simu Mbili

Kubadilisha simu mpya ni jambo la kufurahisha, lakini watu wengi hupata changamoto wanapofikiria jinsi ya kuhamisha taarifa zao kutoka simu ya zamani kwenda simu mpya. Data muhimu kama picha, video, namba za simu, ujumbe, nyaraka, programu na mipangilio inaweza kuonekana kuwa ngumu kuhamisha, hasa kwa mtu ambaye hajawahi kufanya zoezi hilo. Habari njema ni kwamba leo kuna njia rahisi na salama za kuhamisha data kati ya simu mbili bila kupoteza taarifa muhimu. Unaweza kutumia intaneti, huduma za kuhifadhi taarifa mtandaoni, kebo maalumu, Bluetooth au programu zinazosaidia kufanya uhamishaji huo kwa haraka. Makala hii inaelezea hatua kwa hatua jinsi ya kuhamisha data kati ya simu mbili kwa njia rahisi ambayo kila mtu anaweza kuelewa, hata kama hana elimu kubwa ya teknolojia.

Soma Zaidi...
HTML - somo la 9: Jinsi ya kutumia tag za HTML katika uandishi wa maudhui

Katika somo hili utakwenda kuona jinsi ya kuzitumia tag balimbali za html

Soma Zaidi...