image

HTML - somo la 11: Jinsi ya kuweka style mbalimbali kwenye html

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuweka style mbalimbali kwenye ukurasa wa html

ATTRIBUTE AU TAG YA STYLE
Katika somo lililotangulia tuliweza kuona namna ambavyo attribute zinavyofanya kazi. Pia tuliona aina mbalimbali za attributes na mifano yake. Katika somo hili tutakwenda kuangalia attribute ya style tu. Hii ni moja kati ya mwanzo mzuri wa kujifunza CSS.

 

Style inaweza kuwekwa ndani ya element na nje ya element. Stayle ikiwa nje ya element inaweza kutumika kwa element zaidi ya moja. Na ikiwa ndani ya element hutumika kwa element husika tu. Wakati mwingine kama kumetokea ufungaji mbaya wa style inaweza kuathiri element nyingi tofauti na makusudiwa.

 


STYLE INAYOWEKWA NJE YA ELEMENT:
Style ikiwa nje ya element huwekwa kwa kutumia tag ya CSS ambayo ni <style> kisha tribute zote zinakuwa ndani ya tag hii. Kuna faida kubwa ya kutumia style hii ya nje ya element kuliko ya ndani ya element.

Kwa mfano style ya nje ya element hufanya code ziwe nzuri, hupunguza mrundikano wa code ndani ya element pia huweza kuweka stayle kwenye element zaidi ya moja. Hapo chini nitakuletea mifano ya style za nje:-

 

1.JINSI YA KUWEKA RANGI
Tume jifunza katika masomo yaliotangulia kuwa unapotaka kuweka rangi utatumia attribute ya color.  Kwa mfano: <p style=”color:yellow”>hellow</p> katika mfano huu neno hellow litakuwa na rangi nyekundu. Sasa ninataka kuweka kila element na rangi yake. Chukulia mfano una element tag hizi <b>, <p>, <h1> kila moja uwe na rangi yake. Kwa mfano kama huu wa style ya ndani utafanya hivi:-
 <b style=”color:yellow”>hellow</b>
 <p style=”color:red”>hellow</p>
 <h1 style=”color:blue”>hellow</h1>

 

Sasa kwa kutumia style ya nche utafanya hivi:-
1.Kwanza utaweka tag ya style
2.Utaandika tag mfano p
3.Utaweka bano hili {}
4.Attribute zote ziwe ndani ya hayo mabano
5.Kama utakuwa na attribute zaidi ya moja tengenisha kwa alama hii ;
6.Usisahau kufunga tag ya style.
7.Kisha andika element zako.

MFANO:
<html>
<style>
 b {color: yellow}
 p {color:   red}
 h1 {color: blue}
</style>
<b>hellow i'm yellow</b><br>
<p>hellow i'm red</p>
<h1>hellow I'm blue</h1>
</html>

Katika mfano huo utaona maandishi yaliyo kwenye tag ya b ni ya njano, na ya kwenye <p> ni ya wekundu na ya kwenye <h1> ni ya buluu.


2.KUWEKA BACKGROUND COLOR
Kama tulivyoona kwenye mfano wa hapo juu jinsi ya kuweka rangi kwa kutumia style iliyo nje ya element. Na hapa tutaona jinsi ya kutumia style ya nje ya element kueweka background color. 

 

Katika hali ya kawaida background color kwenye element huwekwa kwa kutumia style= kisha utaweka value ya atribute style. Kwa mfano
<p style=”background-color:green”>Hellow I’m green</p> Katika mfano huu maneno haya yatakuwa na rangi ya kijani. Sasa ikiwaninataka kutumia background color moja kwenye element zaidi ya moja, mfano kwenye tag ya <p>, <b> na <I>. Hapa nitatumia kwanza tag ambayo inaweza kubeba tag zote hizo kw amfano unaweza kutumia tag ya <body> lakini hii itaweka backrond kwenye ukurasamzina. Ama unaweza kutumia tag kama <div> hii inaweza kubeba tag nyingi ndani yake. Katika mfano wa hapo chini nitatumia zote mbili <body> na <div>

<html>
<style>
 body {background-color: pink;}
</style>
<body>
 <p>hellow i'm paragraph</p>
 <b>hrllow I'm bolded text</b>
 <i>hellow I'm italic</i>
</body>
</html>

Kwa kutumia <div> mfano:-
<html>
<style>
 div {background-color: purple;}
</style>
<div>
 <p>hellow i'm paragraph</p>
 <b>hrllow I'm bolded text</b><">...



Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 254


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

HTML - somo la 6: Jinsi ya kuweka menyu kwenye faili la HTML
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuweka menyu kwenye faili la html na kuweka rangi ya background. Pia utajifunza kufanya ukurasa uwe responsive yaani uendani na ukubwa wa kifaa. Soma Zaidi...

HTML - somo la 7: Vitu vya kuzingatia unapoandika HTML
Katika somo hili utajifunza sehemu muhimu katika faili la HTML kama vile tag, attribute na element Soma Zaidi...

HTML - somo la 8: Mgawanyiko wa Tag za HTML na kazi zake
Katika somo hili tunakwenda kugawanya tag za HTML, pia nitakwenda kukuletea tag 70 za HTML Soma Zaidi...

HTML - somo la 3: Tags za HTML zinazotumiwa katika uandishi
Katika somo hili nitakuletea orodhabya tag 25 za html ambazo hugumiwa katikabuandishi. Soma Zaidi...

HTML - somo la 13: Jinsi ya kugawa ukurasa wa HTML
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kugawanya ukurasa wa HTML katika column Soma Zaidi...

HTML - somo la 10: Maana ya HTML attribute na jinsi zinavyofanya kazi
Katika somo hili utakwenda kijifunza kuhusu HTML attributes na jinsi ambavyo zinafanya kazi Soma Zaidi...

HTML - somo la 15: Jinsi ya kutengeneza website kwa kutumia HTML
Katika somo hili tutakwenda kutengeneza website yetu kutoka mwanzo hadi mwisho Soma Zaidi...

HTML - somo la 1: Maana ya HTML na kazi zake
Katika somo hili utajifunza maana ya HTML na jinsi inavyofanya kazi Soma Zaidi...

HATML - somo la 4: Jinsi ya kutumia tag za html
Katka somo hi utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia tag za html ili kupangilia muonekano wa maudhui Soma Zaidi...

HTML- somo la 2: Kazi za HTML, code na tag kwenye website.
Katika somo somo hili utajifunza maana ya code, tag na mpangilio wa faili la HTML Soma Zaidi...

HTML - somo la 9: Jinsi ya kutumia tag za HTML katika uandishi wa maudhui
Katika somo hili utakwenda kuona jinsi ya kuzitumia tag balimbali za html Soma Zaidi...

haloo word
all haloo Soma Zaidi...