HATML - somo la 4: Jinsi ya kutumia tag za html
Katka somo hi utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia tag za html ili kupangilia muonekano wa maudhui
Karibu tena lwenye mafunzo haya ya HTML lugha ya kompyuta inayotumika katika kutengenezea website, blog na web application. Html hutumika na mchanganyiko wa lugha nyingine za kompyuta kutengeneza software na system. Hata hivyo unaweza kutumia html peke yake kutengeneza website (tovuti) na ikawa live watu wakaweza kuitembelea.
Je na kama na wewe ni mmoja kati ya wenye ndoto za kuweza kufanya haya, karibu tena kwenye somo hili. Katika somo la kwanza hadi la tatu tuliona namna ambavyo HTML inavyofanya kazi, pia tuliona mpangilio wa faili lake na tukaona tag na element. Katika somo la tatu tulijifunza code 25 muhimu zinazotumuka katika uandidhi. Unaweza kupata somo la kwanza la pili na tatu kwenye linki hizo hapo chini:-
Katika somo hili la nne tutaona jinsi ambavyo tag 25 tulizozitaja kwenye somo la tatu zinavyoweza ktumika na kuandikia makala katika ukurasa wa mtandao. Kama utakuwa unatumia kompyuta funguwa note pad kisha fatilia somo hili, tumia notepad kuandikia code kama somo litakavyoonyesha. Kwa wale wanaotumia simu kama mimi, utaratibu umetangulia katika somo la kwanza, unatakiwa utumie App inayojulikana kama TrebEdit ipo playstore, linki utaipata kwenye somo la kwanza.
FILE EXTENTION KATIKA FAILI LA HTML
Tunapozungumzia file extension huwenda likaonekana kama neno gumu, ila kwa ufupi nitolee mifano. Unapotaka kusevu faili katika microsoft office unaweza kusave as document (.doc), extensive document (.docx) portable document file (.pdf). pia katika media kuna (.mp3, .mp4) kwenye web site kuna (.com, .net, .io, .co, .ac). hivyo extension ndio ambayo huiambia kompyuta aina ya faili. Sasa unapoandika faili lako la code za HTML, wakati wa ku save lazima uweke (.html) mfano katika somo la kwanza tulitumia faili tuliloliita “index.html” usisahau kuweka doti.
Sasa funguwa App yako ya Treb editi kisha menu, kisha workplace, kisha click project yako kama tulivyofanya kwenye somo la kwanza na pili. Kisha new file, weka jina mfano “tag.html” kisha save. Click hilo faili, kisha bofya HTML snippet chini, hapo ukurasa mpya wa code utatokea. Kwa watumiaji wa kompyuta kweka code hizi kwenye notepad yako:
Kama unatumia kompyuta basi tengeneza faili jipya kwa kutumia text editor yako unayotumia.
<!DOCTYPE html>
<html lang="en">
<head>
<meta charset="utf-8">
<title>Tag Muhimu</title>
</head>
<body>
</body>
</html>
Kisa saveas all files kija weka tag.html
Sasa hadi kufikia hapa tupo tayari kuanza somo. Somo
Katika tag zote 25 tulizoziona katika somo la tatu, baadhi yake tutakuja kuziona tena kwenye masomo yajayo kutokana yanahitaji ufafanuzi zaidi. Kwa mgano tag hii <img na <a> hizi tutakuja kuziona zaidi katika somo lijalo. Sasa kama ulishafunguwa TrebEdit yako ama notepad, sasa kopi code hizo hapo chini kisha paste kwenye faili lako ulilolisave kwa jina la tag.html. Kisha previes, kwa kubofya kitufe cha kuplay au click file kwenye komputer litafunguka kama website.
Code zenyewe ni hizi:-
<!DOCTYPE html>
<html lang="en">
<he...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
Jinsi ya Kufanya Backup ya Simu
Simu ya mkononi imekuwa sehemu muhimu sana ya maisha yetu ya kila siku. Tunatumia simu kuhifadhi namba za watu tunaowajua, picha za familia, video muhimu, ujumbe, nyaraka, programu na taarifa nyingine nyingi. Lakini tatizo linaweza kutokea wakati wowote. Simu inaweza kupotea, kuharibika, kuibiwa au kufutika taarifa zake kwa bahati mbaya. Hapo ndipo umuhimu wa kufanya backup ya simu unapokuwa mkubwa. Backup ya simu ni njia ya kutengeneza nakala ya taarifa zako muhimu na kuzihifadhi sehemu salama ili uweze kuzirudisha pale unapohitaji. Kwa kufanya backup mara kwa mara, unapunguza hatari ya kupoteza vitu muhimu vilivyokuwa kwenye simu yako. Katika makala hii tutajifunza maana ya backup ya simu, umuhimu wake, njia mbalimbali za kufanya backup kwenye simu za Android na iPhone, vitu vinavyoweza kuhifadhiwa, makosa ya kuepuka na hatua rahisi ambazo kila mtu anaweza kufuata hata kama hana ujuzi mkubwa wa teknolojia.
Soma Zaidi...Jinsi ya Kutatua Simu Isiyochaji
Simu yako ikikataa kuingiza umeme (kuchaji), usipaniki. Tatizo hili mara nyingi husababishwa na vitu vidogo kama uchafu kwenye tundu la chaji, kebo mbovu, au mfumo wa simu kukwama. Makala hii inakupa hatua rahisi na za haraka unazoweza kufanya nyumbani ili kutatua tatizo hili bila kulipia fundi. Utafiti unaonyesha kuwa asilimia kubwa ya simu zinazodhaniwa zimekufa, hufufuliwa kwa kusafisha tundu la chaji au kubadili kifaa cha kuchajia.
Soma Zaidi...Jinsi ya Kutatua Tatizo la Mikrofoni
Je, unajaribu kupiga simu, kurekodi sauti, au kuingia kwenye mkutano wa mtandaoni lakini mikrofoni yako haifanyi kazi? Huu ni mwongozo rahisi na wa hatua kwa hatua unaoelezea jinsi ya kutatua matatizo yote ya mikrofoni kwenye simu au kompyuta yako. Tumeandika mwongozo huu kwa lugha rahisi ya Kiswahili ili kila mtu, hata asiye na ujuzi wa teknolojia, aweze kuelewa na kurekebisha kifaa chake mara moja bila kuhitaji fundi.
Soma Zaidi...Jinsi ya Kusakinisha (Install) App kwa Usalama
Siku hizi simu za mkononi zimekuwa sehemu muhimu ya maisha ya kila siku. Tunazitumia kuwasiliana, kufanya biashara, kusoma, kulipa bili, kutazama video, kusikiliza muziki na hata kuhifadhi taarifa muhimu. Ili simu iweze kufanya kazi hizi, tunahitaji kusakinisha (install) programu mbalimbali zinazojulikana kama app. Lakini si kila app ni salama. Baadhi ya app zinaweza kuiba taarifa zako binafsi, kuharibu simu, kuonyesha matangazo mengi yasiyofaa au hata kusababisha akaunti zako kuporwa. Ndiyo maana ni muhimu kujifunza jinsi ya kusakinisha app kwa usalama. Katika makala hii utajifunza hatua zote muhimu za kusakinisha app kwa usalama, namna ya kutambua app halisi, mambo ya kuzingatia kabla na baada ya kusakinisha app, pamoja na makosa ambayo watu wengi hufanya bila kujua.
Soma Zaidi...Dalili Zinazoonyesha Simu Ina Virusi
Virusi vya simu ni mojawapo ya matatizo yanayoweza kuathiri utendaji wa simu yako bila wewe kutambua mapema. Watu wengi hudhani kuwa ni kompyuta pekee zinazoshambuliwa na virusi, lakini ukweli ni kwamba simu za Android na hata baadhi ya simu nyingine zinaweza pia kuathirika na programu hatari zinazojulikana kama virusi au malware. Makala hii inaeleza kwa kina dalili zinazoonyesha simu ina virusi, sababu zinazofanya simu ipate virusi, namna ya kujilinda, pamoja na hatua unazoweza kuchukua ili kuondoa tatizo hilo. Ikiwa simu yako imeanza kufanya mambo yasiyo ya kawaida, makala hii itakusaidia kutambua tatizo kabla halijawa kubwa
Soma Zaidi...HTML- somo la 2: Kazi za HTML, code na tag kwenye website.
Katika somo somo hili utajifunza maana ya code, tag na mpangilio wa faili la HTML
Soma Zaidi...