HTML-somo la 5: Jinsi ya kupangilia munekano wa maudhui kwenye website
Katika somo hili utajifunza Kuweka picha Kuweka rangi Kuweka linki Kupangilia position na alignment ya maandishi Kuongeza ukubwa wa herufi Kukoment
Karibu kwa mara nyingine tena katika mafunzo yetu ya HTML na namna ya kutengeneza website (tovuti) na blog. Katika somo lililopita tuliona tag 25 muhimu zinazotumika katika kuandika document na ikawa na muonekano mzuri katika blog ama tovuti yako. Hatika somo hili tutakwenda kuona namna ya kuweka staili kwenye document yako.
Somo hili litakwenda kuangalia yafuatayo:-
- Kuweka picha
- Kuweka rangi
- Kuweka linki
- Kupangilia position na alignment ya maandishi
- Kuongeza ukubwa wa herufi
- Kukoment
Hakikisha umeshapitia masomo yetu manne yaliyotangulia kabla ya kuanza somo hili, hii itakupa uwanja mpana sana wa kuelewa zaidi. Kumbuka masomo haya yanaendeshwa kwa kutumia App inayotambulika kama TrebEdit, link yake utaipata kwenye somo la kwanza ama ingia playstore. Kupata masomo manne yaliyotangulia bofya link za hapo chini.
CODE ZITAKAZOTUMIKA KWENYE SOMO:
Kopi code hizi kisha pestu kwenye faili utakalolipatina staili.html. Maelezo zaidi utayapata hapo chini baada ya hizi code:-
<!DOCTYPE html>
<html lang="en">
<head>
<meta charset="UTF-8">
<meta name="viewport" content="width=device-width, initial-scale=1, shrink-to-fit=no">
<title>kuweka staili</title>
</head>
<body>
<h1>kuweka picha</h1>
<img src="image/P2.JPEG" WIDTH="100%">
<BR></BR>
<H2>KUWEKA RANGI</H2>
<p style="color:red"> mimi mwekundu</p>
<p style="color:green"> mimi mkijani</p>
<H1>KUWEKA LINK</H1>
<a href="tag.html">tag 25, bofya hapa</a><BR></BR>
<a href="index.html">go to home page</a>
<br><br>
<H1>
Kuongeza ukubwa wa maneno</H1>
<b style="font-size:100">mimi niko kawaida 100%</b>
<br>
<b style="font-size:200%">Ukubwa wa 200%</b>
<br>
<b style="font-size:300%">Ukubwa wa 300%</b>
<br>
<b style="font-size:50%">ukubwa wa 50%</b>
<BR><BR></BR></BR>
<p style="text-align:center;">Nipo kati</p>
<br>
<p style="text-align:left;">Nipo kushoto</p>
<br>
<p style="text-align:right;">Nipo kulia</p>
<br>
<p style="text-align:justify;">Nipo Nimejaa</p>
<br><br>
<h1>KUKOMENT</H1>
<!--- WEKA KOMENT HAPA -->
</body>
</html>
MAANDALIZI HA SOMO:
Kama tayari App ya Treb Edit unayo:
- Ingia kwenye App ya Trebedit, nenda menu kisha kwenye project yako bofya kwenye jina hilo, ingia kwenye folda la image, create file, kisha import file, chaguwa picha moja uiclick. Rudi nyuma utaiona picha yako ipo kwenye folda la image. Kama unatumia kompyuta tumia notepad ama text editor yoyote unayotumia kuandika code.
- Kwenye folda kuu la project yako create file kkisha lipe jina la “staili.html”. hivyo kwenye folda lako kuu kutakuwa na mafaili matatu moja ni lile na index.html, jingine ni la tag.html na la mwisho litakuwa hili la staili.html. Huwenda ukawa umeweka mafaili mengine ya html. Hakuna shida.
- Baada ya hapo utakopi code nitakazozileta hapo chini kwenye faili hili la staili.html kisha sevu.
- Utapreview kwa kubofya kitufe cha kuplay.
- Endelea na somo sasa kuona namna ambavyo code zinavyofanya kazi
UFAFANUZI WA CODE ZILIZOTUMIKA:
- Kuweka Picha
Kuweka picha kwenye faili la html tunatumiatag hii <img kisha unaweka source yaani chanzo ambacho hiyopicha itakuwepo. Utafanya hivi kwa kutumia src=” ” ndani ya hizo fungasemi na funguwa semiutaweka jina la faili au picha na jina la folda lilipo kwa mfano picha niliotumiamimi itaitwa P2 na ipokatika fomati ya jpeg, hivyo inasomoka kama P2.jpeg. Ukiweka na jina la folda ilipo utapata image/P2.pjeg. Hivyo tag nzima itasomeka hivi
<img src=”image/P2.jpeg”>
Hiyo tupu inatosha kuweka icha yako na ikaonekana. Utaona kuna code nimeziongeza kwa ajili ya kupunguza upana wa picha na...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 Kitabu cha Afya 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Jinsi ya Kusafisha Simu Isifanye Kazi Polepole
Je, simu yako imekuwa ikifungua programu kwa kuchelewa, kuganda mara kwa mara au kufanya kazi polepole kuliko ilivyokuwa mwanzo? Tatizo hili ni la kawaida kwa watumiaji wengi wa simu za Android na hata iPhone. Mara nyingi watu hudhani kuwa simu imeharibika au imezeeka, wakati ukweli ni kwamba kuna uchafu wa kidijitali unaokusanyika ndani ya simu na kuifanya ishindwe kufanya kazi kwa kasi. Katika makala hii utajifunza jinsi ya kusafisha simu ili irudi kufanya kazi vizuri. Utaelewa sababu zinazofanya simu iwe polepole, namna ya kufuta faili zisizo muhimu, kusafisha kumbukumbu ya programu, kuondoa programu zisizotumika, kusasisha mfumo wa simu pamoja na mbinu nyingine zinazoweza kuongeza kasi ya simu bila kutumia fedha.
Soma Zaidi...Jinsi ya Kutafuta Simu Iliyopotea
Kupoteza simu ni jambo linaloweza kumpata mtu yeyote wakati wowote. Simu ya kisasa si kifaa cha kupigia simu tu, bali pia huhifadhi picha, namba za watu unaowasiliana nao, ujumbe, taarifa za benki, akaunti za mitandao ya kijamii na taarifa nyingine muhimu. Ndiyo maana kupoteza simu kunaweza kusababisha usumbufu mkubwa na hata hatari ya taarifa binafsi kuibiwa. Habari njema ni kwamba kuna njia mbalimbali zinazoweza kukusaidia kuitafuta simu iliyopotea. Unaweza kutumia huduma zilizopo ndani ya simu kama vile programu za kuitafuta simu, kutumia namba ya simu, kuwasiliana na kampuni ya mtandao, au kutumia taarifa za mwisho zilipoonekana. Makala hii inaeleza hatua kwa hatua jinsi ya kutafuta simu iliyopotea kwa njia rahisi ambayo kila mtu anaweza kuelewa.
Soma Zaidi...Jinsi ya Kujua Kama Wi-Fi Ni Salama
Wi-Fi imekuwa sehemu muhimu ya maisha yetu ya kila siku. Tunaitumia kuingia kwenye mitandao ya kijamii, kutuma ujumbe, kufanya biashara mtandaoni, kusoma, kutazama video na hata kufanya malipo. Lakini pamoja na faida zake nyingi, Wi-Fi inaweza kuwa hatari ikiwa haijalindwa vizuri. Mtandao wa Wi-Fi usio salama unaweza kuruhusu watu wasiohusika kuona taarifa zako binafsi, kuiba nywila zako au kutumia intaneti yako bila ruhusa. Kujua kama Wi-Fi ni salama ni jambo muhimu kwa kila mtu anayemiliki simu, kompyuta au kifaa kingine kinachounganishwa na intaneti. Makala hii inaeleza kwa lugha rahisi jinsi ya kutambua Wi-Fi salama, dalili za Wi-Fi hatari, hatua za kulinda mtandao wako na mambo muhimu ya kuzingatia ili kutumia intaneti kwa usalama
Soma Zaidi...Je, Kuchaji Simu Usiku Kucha Ni Salama?
Je, ni salama kuacha simu kwenye chaji usiku kucha unapolala? Watu wengi wanaamini kuwa tabia hii inalipua simu au kuharibu betri kabisa. Katika makala hii, utajifunza ukweli wa kisayansi kuhusu simu za kisasa, jinsi mifumo ya usalama inavyofanya kazi, na mbinu rahisi za kurefusha maisha ya betri yako bila hofu. Soma ujue jinsi ya kulinda simu yako leo!
Soma Zaidi...Jinsi ya Kutambua Kama Memory Card Imeharibika
Memory card (kadi ya kumbukumbu) ni kifaa kidogo kinachotunza vitu vyetu vya thamani kama picha, video, nyimbo na nyaraka muhimu katika simu au kamera. Hata hivyo, vifaa hivi mara nyingi huharibika bila kutoa taarifa. Makala hii imelenga kukusaidia wewe mtumiaji wa kawaida utambue kirahisi dalili za memory card iliyokufa au inayoelekea kuharibika. Utajifunza ishara za wazi kama faili kupotea, simu kuwa nzito, au ujumbe wa makosa (errors). Pia, tumekuwekea hatua rahisi za kufanya ili kulinda data zako zisipotee kabisa na jinsi ya kuepuka kununua kadi feki. Kila kitu kimeelekezwa kwa lugha rahisi ya Kiswahili isiyo na maneno magumu ya kiteknolojia.
Soma Zaidi...HTML- somo la 2: Kazi za HTML, code na tag kwenye website.
Katika somo somo hili utajifunza maana ya code, tag na mpangilio wa faili la HTML
Soma Zaidi...