HTML - somo la 12: Sehemu kuu za faili la HTML
Katika somo hili utajifunza kuhusu sehemu kuu za faili la HTML
SEHEMU KUU ZA FAILI LA HTML
<head>, <header> na <footer>
Katika website sehemu hizi zina kazi ya kuweza kutambulisha zaidi website na mahusiano kati ya ukurasa na ukurasa. Sehemu hizi ni muhimu kwa SEO na wanaotaka kuichunguza blog ama website. Katika somo hili tutakwenda kuangalia sehemu hizi, na jinsi ya kuzitengeneza ama kuziwekea maudhui.
1.<head>
Shemehu hii inakaa taarifa muhimu kuhusu ukurasa. Taarifa hizi unawezakuziita metadata. Kwa mfano hapa unaweza kuweka taarifa hizi:-
A.Jina la faili kulingana na maudhui
B.Jina la mwandishi
C.Muhtasari kuhusu maudui
D.Character set
E.Viungo vingine muhimu kama link za style za nje
F.Taarifa kuhusu ukubwa wa kifaa kitakachofunguwa faili husika.
G.Icon n.k
Kwa mfano unaweza kuweka taarifa hizo
<head>
<meta charset="utf-8">
<meta name="viewport" content="width=device-width, initial-scale=1, shrink-to-fit=no">
<meta name="author" content="jina la mwandishi">
<meta name="description" content="weka muhtasari hapa">
<title>weka Title hapa</title>
</head>
2.<header> hii ni sehemu ya juu kabisa ama ya mwanzo. Sehemu hii ndio ambapo menu hukaa. Sehemu hii ndio inatakiwa ikae mwanza tu ndani ya tag ya <body> . tag ya <menu> inatakiwa ikae hapa ndani ya <header>. kwa ufupi <header> ni kama section ambazo hubeba tag nyingine ndani ake. Kama tulivyoona matumizi ya <div> katika masomo yaliyotangulia.
Kuweka menu tunatumia tag ya <menu> tag hii tutaiweka kwenye section ya <header> tunaweza kutumia style ili kubresha muonekano wa menu yetu. Tunaweza kutumia batanina link ili kuunganisha ukurasa mmoja na mwingine. Kwa mfano:-
<html>
<style>
menu {background-color: black;}
a {color: red;
text-decoration: none;
}
button {font-size: x-large;}
</style>
<heade>
<menu>
<button><a href="#">PHP</a></button>
<button><a href="#">HTML</a></button>
<button...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
Jinsi ya kutengeneza cheti kwa kutumia HTML
Katika post hii utakwenda kujifunz ajinsi ya kutengeneza cheti kwa kutumia html na css.
Soma Zaidi...HTML-somo la 5: Jinsi ya kupangilia munekano wa maudhui kwenye website
Katika somo hili utajifunza Kuweka picha Kuweka rangi Kuweka linki Kupangilia position na alignment ya maandishi Kuongeza ukubwa wa herufi Kukoment
Soma Zaidi...HATML - somo la 4: Jinsi ya kutumia tag za html
Katka somo hi utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia tag za html ili kupangilia muonekano wa maudhui
Soma Zaidi...HTML - somo la 15: Jinsi ya kutengeneza website kwa kutumia HTML
Katika somo hili tutakwenda kutengeneza website yetu kutoka mwanzo hadi mwisho
Soma Zaidi...HTML - somo la 3: Tags za HTML zinazotumiwa katika uandishi
Katika somo hili nitakuletea orodhabya tag 25 za html ambazo hugumiwa katikabuandishi.
Soma Zaidi...HTML - somo la 13: Jinsi ya kugawa ukurasa wa HTML
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kugawanya ukurasa wa HTML katika column
Soma Zaidi...