HTML - somo la 1: Maana ya HTML na kazi zake
Somo hili linakufundisha maana ya HTML, kwa nini inatumika, na jinsi ya kuandaa simu au kompyuta yako kwa ajili ya kuanza kutengeneza tovuti. Pia tutatengeneza ukurasa wetu wa kwanza wa HTML hatua kwa hatua.
Utangulizi
HTML ni lugha ya msingi inayotumika kutengenezea kurasa za tovuti na blogu. Bila HTML hakuna website inayoonekana duniani. Unaweza kutengeneza tovuti kwa kutumia HTML pekee, kisha ukaboresha baadaye kwa kutumia CSS na JavaScript.
Katika somo hili, tunaanza kwa kukuweka tayari ili uweze kuandika code zako bila shida—iwe unatumia simu au kompyuta.
Sasa tuingie kwenye somo letu…
1. HTML ni nini?
HTML ni ufupisho wa:
-
Hypertext
-
Markup
-
Language
Ni lugha ya kimataifa inayotumiwa kutengeneza kurasa za tovuti (website pages). HTML haihitaji umiliki wa vifaa ghali; unaweza kuanza hata kwa kutumia simu yako ya mkononi.
Ikiwa una ndoto za kuanzisha blog, tovuti ya biashara au portfolio, basi uko mahali sahihi. Mafunzo haya yatakufundisha kuanzia hatua ya mwanzo kabisa hadi kutengeneza tovuti inayoweza kwenda live.
2. Vigezo vya kuanza kujifunza
Ili uweze kufanikiwa kwenye kozi hii, unahitaji:
-
Simu ya smartphone au kompyuta
-
Uwezo wa kusoma na kuandika
-
Utayari wa kujifunza
-
Umakini na ujanja
-
Kufanya mazoezi kila baada ya somo
Kozi ya msingi (Basics) itachukua wiki moja, kisha tutaendelea na hatua ya pili.
3. Namna ya kuandaa kifaa chako (Simu)
Kwa watumiaji wa simu, utatumia app inayoitwa Acode (badala ya TrebEdit kwa sababu Acode ni nyepesi na ya kisasa).
Hatua za kuandaa Acode
-
Pakua app ya Acode kwenye Play Store:
https://play.google.com/store/apps/details?id=com.foxdebug.acodefree -
Fungua Acode
-
Bofya icon ya “folder” kisha tengeneza folder jipya
-
Lipe jina mfano: html-project
-
Ndani ya hilo folder, tengeneza folder lingine liitwe images
-
Rudi kwenye folder la html-project
-
Bonyeza alama ya “+” kutengeneza faili jipya
-
Lipe jina: index.html
-
Lifungue faili hilo
-
Andika au kopia code zifuatazo:
<!DOCTYPE html>
<...help_outlineZoezi la Maswali
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Simulizi za Hadithi Audio 👉2 Kitau cha Fiqh 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
HTML - somo la 9: Jinsi ya kutumia tag za HTML katika uandishi wa maudhui
Katika somo hili utakwenda kuona jinsi ya kuzitumia tag balimbali za html
Soma Zaidi...Faida za Screen Protector
Screen Protector ni kifaa chembamba kinachowekwa juu ya skrini ya simu ili kuilinda dhidi ya mikwaruzo, mipasuko na uharibifu mwingine unaoweza kutokea wakati wa matumizi ya kila siku. Watu wengi hununua simu za gharama kubwa lakini husahau kulinda sehemu muhimu zaidi ya simu hiyo, ambayo ni skrini. Makala hii inaelezea kwa kina faida za Screen Protector, aina zake, jinsi ya kuchagua inayofaa, na sababu zinazofanya iwe uwekezaji muhimu kwa kila mwenye simu.
Soma Zaidi...Jinsi ya Kusakinisha (Install) App kwa Usalama
Siku hizi simu za mkononi zimekuwa sehemu muhimu ya maisha ya kila siku. Tunazitumia kuwasiliana, kufanya biashara, kusoma, kulipa bili, kutazama video, kusikiliza muziki na hata kuhifadhi taarifa muhimu. Ili simu iweze kufanya kazi hizi, tunahitaji kusakinisha (install) programu mbalimbali zinazojulikana kama app. Lakini si kila app ni salama. Baadhi ya app zinaweza kuiba taarifa zako binafsi, kuharibu simu, kuonyesha matangazo mengi yasiyofaa au hata kusababisha akaunti zako kuporwa. Ndiyo maana ni muhimu kujifunza jinsi ya kusakinisha app kwa usalama. Katika makala hii utajifunza hatua zote muhimu za kusakinisha app kwa usalama, namna ya kutambua app halisi, mambo ya kuzingatia kabla na baada ya kusakinisha app, pamoja na makosa ambayo watu wengi hufanya bila kujua.
Soma Zaidi...HTML - somo la 14: Hatua za kutengeneza website
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza website hatuwa kwa hatuwa
Soma Zaidi...Jinsi ya Kufuta Data za Simu Ukiwa Mbali
Kupoteza simu au kuibiwa kwa simu ni jambo linaloweza kumpata mtu yeyote. Simu zetu siku hizi hazitumiki tu kupiga simu na kutuma ujumbe, bali pia huhifadhi taarifa nyingi muhimu kama picha, video, namba za simu, akaunti za mitandao ya kijamii, taarifa za benki, barua pepe na nyaraka binafsi. Ikiwa simu itaangukia mikononi mwa mtu asiye mwaminifu, taarifa hizo zinaweza kutumiwa vibaya. Njia moja ya kujilinda ni kujifunza jinsi ya kufuta data za simu ukiwa mbali. Hii ina maana kwamba unaweza kuondoa taarifa zote zilizomo kwenye simu yako hata kama simu hiyo haipo karibu nawe. Njia hii husaidia kulinda faragha yako na kuzuia watu wengine kuona au kutumia taarifa zako binafsi. Katika makala hii tutajifunza maana ya kufuta data za simu ukiwa mbali, sababu za kufanya hivyo, hatua za kufuata, mambo muhimu ya kuzingatia kabla ya kufuta taarifa, pamoja na ukweli muhimu kuhusu usalama wa simu
Soma Zaidi...HTML somo la 17: Jinsi ya kuunganisha HTML na CSS au JavaScript
Katika somo hili utakwend akujifunz ahatuwa kwa hatuwa jinsi ya Kuunganisha HTML na CSS au JavaScript
Soma Zaidi...