HTML - somo la 1: Maana ya HTML na kazi zake

Katika somo hili utajifunza maana ya HTML na jinsi inavyofanya kazi

HTML ni ufupisho wa maneno yanayosomeka kama:-

Hypertext

Markup

Language

 

Ni lugha ya komputa inayotumika katika kutengenezea kurasa za tovuti (website) ama blog.Inaungana na lugha nyingine katika kuboresha kurrasa za tovuti ama blog na kuzifanya ziweze kufanya kazi iliyokusudiwa vyema. Unaweza kutumia HTML tu ukatengeneza website yako bila ya lugha nyingine. Hata hivyo muonekano wake hautakuwa vyema sana kama hutatumia nyinggine.

 

Je na wewe una ndoto za kuwa na blog ama website uliyoitengeneza wewe mwenyewe. Mafunzo haya ni kwa ajili yako. Katika mafunzo haya utajifunza namna ya kutengeneza website yako kupitia kiganja chako yaani simu yako ya mkononi. Kama utakuwa na kompyuta hatutakuacha pia.

 

Somo hili la kwanza utajifunza namna ya kuandaa simu yako kwa ajili ya kutengeneza website, ama kwa ajili ya kutumia HTML. Kama tutaenda vyema na mafunzo haya hadi mwisho nakuhakikishia kama Mwenyezi Mungu akitujaalia nguvu, uwezo na uhai, utaweza kutengeneza website yako na kuiweka live.

 

Muda wa masomo haya kwa hatuwa za Awali (Basics) itakuwa na wiki moja. Kisha baada ya hapo hatuwa ya pili ya mafunzo itaendelea. Tafadhali kuwa tayari kujifunza, kuwa muulizaji na mchangiaji:

 

VIGEZO VYA KUJIFUNZA:

  1. Kuwa na simu ya smartphone
  2. Uwe unajuwa kusoma na kuandika
  3. Kuwa tayari kujifunza
  4. Kuwa mjanja
  5. Uwe mwenye kufanyi akazi (fanya mazoezi)

 

NAMNA YA KUANDAA KIFAA CHAKO

KWA WANAOTUMIA SIMU:

  1. Download App inayoitwa TrebEdit. Tumia link hii https://play.google.com/store/apps/details?id=com.teejay.trebedit
  2. Funguwa App yako kisha bofya  Menu
  3. Bofya palipoandikwa Workplace 
  4. Bofya kitufe chenye alama ya kujumlisha chini
  5. Kisha bofya palipandikwa New Project
  6. Andika jina la Project (mimi natumia HTML) kisha bofya save.
  7. Ingia kwenye project uliotengeneza kwa kubofya jina lake, ukurasa mpya utafunguka
  8. Bofya tena kitufe cha alama ya kujumlisha
  9. Bofya palipoandikwa new folder (hapa tunatengeneza folda la kuweka picha tutakazokuja kuzitumia kwenye tovutu tutakayotengeneza)
  10. Andika jina la folda tumia image kisha bofya save.
  11. Baada ya hapo rudi nyuma hatuwa moja kwenye project yako.
  12. Bofya tena jina la project yako
  13. Bofya kitufe cha alama ya kujumlisha
  14. Bofya palipandika New file (hapa ndipo tutakapoanzia kuweka code za kutengeneza tovuti ">...

    Download App Yetu

    Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

    Download Now Bongoclass

    ZOEZI

    Jaza maswali yote ama baadhi kisha bofya kitufe za kutuma majibu hapo chini.



    1 : HTML ni kifupisho cha maneno __________



    2 : HTML hasa inatumika katika kutengenezea ______



    3 : Kurasa za wavuti tunaweza kuziona kwenye ____

    Endelea


    Je umeipenda post hii ?

    Ndio            Hapana            Save post
    Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: HTML Main: ICT File: Download PDF Views 1076

    Share On:

    Facebook WhatsApp
    Sponsored links
    👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 kitabu cha Simulizi   

    Post zinazofanana:

    HTML-somo la 5: Jinsi ya kupangilia munekano wa maudhui kwenye website

    Katika somo hili utajifunza Kuweka picha Kuweka rangi Kuweka linki Kupangilia position na alignment ya maandishi Kuongeza ukubwa wa herufi Kukoment

    Soma Zaidi...
    HTML - somo la 11: Jinsi ya kuweka style mbalimbali kwenye html

    Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuweka style mbalimbali kwenye ukurasa wa html

    Soma Zaidi...
    HTML somo la 17: Jinsi ya kuunganisha HTML na CSS au JavaScript

    Katika somo hili utakwend akujifunz ahatuwa kwa hatuwa jinsi ya Kuunganisha HTML na CSS au JavaScript

    Soma Zaidi...
    HTML - somo la 14: Hatua za kutengeneza website

    Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza website hatuwa kwa hatuwa

    Soma Zaidi...
    Jinsi ya kutengeneza cheti kwa kutumia HTML

    Katika post hii utakwenda kujifunz ajinsi ya kutengeneza cheti kwa kutumia html na css.

    Soma Zaidi...
    HTML - somo la 7: Vitu vya kuzingatia unapoandika HTML

    Katika somo hili utajifunza sehemu muhimu katika faili la HTML kama vile tag, attribute na element

    Soma Zaidi...
    HTML- somo la 2: Kazi za HTML, code na tag kwenye website.

    Katika somo somo hili utajifunza maana ya code, tag na mpangilio wa faili la HTML

    Soma Zaidi...
    HTML - somo la 10: Maana ya HTML attribute na jinsi zinavyofanya kazi

    Katika somo hili utakwenda kijifunza kuhusu HTML attributes na jinsi ambavyo zinafanya kazi

    Soma Zaidi...
    HTML - somo la 16: Jinsi ya ku host website bure

    Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ku host website yako bila malipo

    Soma Zaidi...