HTML - somo la 1: Maana ya HTML na kazi zake
Somo hili linakufundisha maana ya HTML, kwa nini inatumika, na jinsi ya kuandaa simu au kompyuta yako kwa ajili ya kuanza kutengeneza tovuti. Pia tutatengeneza ukurasa wetu wa kwanza wa HTML hatua kwa hatua.
Utangulizi
HTML ni lugha ya msingi inayotumika kutengenezea kurasa za tovuti na blogu. Bila HTML hakuna website inayoonekana duniani. Unaweza kutengeneza tovuti kwa kutumia HTML pekee, kisha ukaboresha baadaye kwa kutumia CSS na JavaScript.
Katika somo hili, tunaanza kwa kukuweka tayari ili uweze kuandika code zako bila shida—iwe unatumia simu au kompyuta.
Sasa tuingie kwenye somo letu…
1. HTML ni nini?
HTML ni ufupisho wa:
-
Hypertext
-
Markup
-
Language
Ni lugha ya kimataifa inayotumiwa kutengeneza kurasa za tovuti (website pages). HTML haihitaji umiliki wa vifaa ghali; unaweza kuanza hata kwa kutumia simu yako ya mkononi.
Ikiwa una ndoto za kuanzisha blog, tovuti ya biashara au portfolio, basi uko mahali sahihi. Mafunzo haya yatakufundisha kuanzia hatua ya mwanzo kabisa hadi kutengeneza tovuti inayoweza kwenda live.
2. Vigezo vya kuanza kujifunza
Ili uweze kufanikiwa kwenye kozi hii, unahitaji:
-
Simu ya smartphone au kompyuta
-
Uwezo wa kusoma na kuandika
-
Utayari wa kujifunza
-
Umakini na ujanja
-
Kufanya mazoezi kila baada ya somo
Kozi ya msingi (Basics) itachukua wiki moja, kisha tutaendelea na hatua ya pili.
3. Namna ya kuandaa kifaa chako (Simu)
Kwa watumiaji wa simu, utatumia app inayoitwa Acode (badala ya TrebEdit kwa sababu Acode ni nyepesi na ya kisasa).
Hatua za kuandaa Acode
-
Pakua app ya Acode kwenye Play Store:
https://play.google.com/store/apps/details?id=com.foxdebug.acodefree -
Fungua Acode
-
Bofya icon ya “folder” kisha tengeneza folder jipya
-
Lipe jina mfano: html-project
-
Ndani ya hilo folder, tengeneza folder lingine liitwe images
-
Rudi kwenye folder la html-project
-
Bonyeza alama ya “+” kutengeneza faili jipya
-
Lipe jina: index.html
-
Lifungue faili hilo
-
Andika au kopia code zifuatazo:
<!DOCTYPE html>
<...help_outlineZoezi la Maswali
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Jinsi ya Kutatua Simu Isiyochaji
Simu yako ikikataa kuingiza umeme (kuchaji), usipaniki. Tatizo hili mara nyingi husababishwa na vitu vidogo kama uchafu kwenye tundu la chaji, kebo mbovu, au mfumo wa simu kukwama. Makala hii inakupa hatua rahisi na za haraka unazoweza kufanya nyumbani ili kutatua tatizo hili bila kulipia fundi. Utafiti unaonyesha kuwa asilimia kubwa ya simu zinazodhaniwa zimekufa, hufufuliwa kwa kusafisha tundu la chaji au kubadili kifaa cha kuchajia.
Soma Zaidi...HTML - somo la 11: Jinsi ya kuweka style mbalimbali kwenye html
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuweka style mbalimbali kwenye ukurasa wa html
Soma Zaidi...HTML - somo la 3: Tags za HTML zinazotumiwa katika uandishi
Katika somo hili nitakuletea orodhabya tag 25 za html ambazo hugumiwa katikabuandishi.
Soma Zaidi...Jinsi ya Kutambua Kama Memory Card Imeharibika
Memory card (kadi ya kumbukumbu) ni kifaa kidogo kinachotunza vitu vyetu vya thamani kama picha, video, nyimbo na nyaraka muhimu katika simu au kamera. Hata hivyo, vifaa hivi mara nyingi huharibika bila kutoa taarifa. Makala hii imelenga kukusaidia wewe mtumiaji wa kawaida utambue kirahisi dalili za memory card iliyokufa au inayoelekea kuharibika. Utajifunza ishara za wazi kama faili kupotea, simu kuwa nzito, au ujumbe wa makosa (errors). Pia, tumekuwekea hatua rahisi za kufanya ili kulinda data zako zisipotee kabisa na jinsi ya kuepuka kununua kadi feki. Kila kitu kimeelekezwa kwa lugha rahisi ya Kiswahili isiyo na maneno magumu ya kiteknolojia.
Soma Zaidi...Jinsi ya Kufuta Data za Simu Ukiwa Mbali
Kupoteza simu au kuibiwa kwa simu ni jambo linaloweza kumpata mtu yeyote. Simu zetu siku hizi hazitumiki tu kupiga simu na kutuma ujumbe, bali pia huhifadhi taarifa nyingi muhimu kama picha, video, namba za simu, akaunti za mitandao ya kijamii, taarifa za benki, barua pepe na nyaraka binafsi. Ikiwa simu itaangukia mikononi mwa mtu asiye mwaminifu, taarifa hizo zinaweza kutumiwa vibaya. Njia moja ya kujilinda ni kujifunza jinsi ya kufuta data za simu ukiwa mbali. Hii ina maana kwamba unaweza kuondoa taarifa zote zilizomo kwenye simu yako hata kama simu hiyo haipo karibu nawe. Njia hii husaidia kulinda faragha yako na kuzuia watu wengine kuona au kutumia taarifa zako binafsi. Katika makala hii tutajifunza maana ya kufuta data za simu ukiwa mbali, sababu za kufanya hivyo, hatua za kufuata, mambo muhimu ya kuzingatia kabla ya kufuta taarifa, pamoja na ukweli muhimu kuhusu usalama wa simu
Soma Zaidi...HTML - somo la 8: Mgawanyiko wa Tag za HTML na kazi zake
Katika somo hili tunakwenda kugawanya tag za HTML, pia nitakwenda kukuletea tag 70 za HTML
Soma Zaidi...