HTML - somo la 1: Maana ya HTML na kazi zake
Somo hili linakufundisha maana ya HTML, kwa nini inatumika, na jinsi ya kuandaa simu au kompyuta yako kwa ajili ya kuanza kutengeneza tovuti. Pia tutatengeneza ukurasa wetu wa kwanza wa HTML hatua kwa hatua.
Utangulizi
HTML ni lugha ya msingi inayotumika kutengenezea kurasa za tovuti na blogu. Bila HTML hakuna website inayoonekana duniani. Unaweza kutengeneza tovuti kwa kutumia HTML pekee, kisha ukaboresha baadaye kwa kutumia CSS na JavaScript.
Katika somo hili, tunaanza kwa kukuweka tayari ili uweze kuandika code zako bila shida—iwe unatumia simu au kompyuta.
Sasa tuingie kwenye somo letu…
1. HTML ni nini?
HTML ni ufupisho wa:
-
Hypertext
-
Markup
-
Language
Ni lugha ya kimataifa inayotumiwa kutengeneza kurasa za tovuti (website pages). HTML haihitaji umiliki wa vifaa ghali; unaweza kuanza hata kwa kutumia simu yako ya mkononi.
Ikiwa una ndoto za kuanzisha blog, tovuti ya biashara au portfolio, basi uko mahali sahihi. Mafunzo haya yatakufundisha kuanzia hatua ya mwanzo kabisa hadi kutengeneza tovuti inayoweza kwenda live.
2. Vigezo vya kuanza kujifunza
Ili uweze kufanikiwa kwenye kozi hii, unahitaji:
-
Simu ya smartphone au kompyuta
-
Uwezo wa kusoma na kuandika
-
Utayari wa kujifunza
-
Umakini na ujanja
-
Kufanya mazoezi kila baada ya somo
Kozi ya msingi (Basics) itachukua wiki moja, kisha tutaendelea na hatua ya pili.
3. Namna ya kuandaa kifaa chako (Simu)
Kwa watumiaji wa simu, utatumia app inayoitwa Acode (badala ya TrebEdit kwa sababu Acode ni nyepesi na ya kisasa).
Hatua za kuandaa Acode
-
Pakua app ya Acode kwenye Play Store:
https://play.google.com/store/apps/details?id=com.foxdebug.acodefree -
Fungua Acode
-
Bofya icon ya “folder” kisha tengeneza folder jipya
-
Lipe jina mfano: html-project
-
Ndani ya hilo folder, tengeneza folder lingine liitwe images
-
Rudi kwenye folder la html-project
-
Bonyeza alama ya “+” kutengeneza faili jipya
-
Lipe jina: index.html
-
Lifungue faili hilo
-
Andika au kopia code zifuatazo:
<!DOCTYPE html>
<...help_outlineZoezi la Maswali
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 Simulizi za Hadithi Audio 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Jinsi ya Kutatua Tatizo la Kamera Kutofanya Kazi
Kamera ya simu au kompyuta yako imegoma kufanya kazi? Usipaniki. Tatizo hili hutokea mara kwa mara na mara nyingi halihitaji ufundi mkubwa. Makala hii inakupa suluhisho la haraka na rahisi kuanzia kusafisha lenzi, kuwasha upya vifaa, hadi kuangalia mipangilio ya ndani (permissions). Utafanya kamera yako ianze kazi tena ndani ya dakika chache bila kutumia gharama yoyote.
Soma Zaidi...Sababu Zinazofanya Betri Iishe Haraka
Betri ni sehemu muhimu sana ya simu, kompyuta mpakato, saa janja na vifaa vingine vya kielektroniki. Hata hivyo, watu wengi hukutana na tatizo la betri kuisha haraka bila kujua chanzo chake. Wakati mwingine tatizo halitokani na ubora wa simu au betri, bali hutokana na namna kifaa kinavyotumika kila siku. Katika makala hii utajifunza sababu kuu zinazofanya betri iishe haraka, jinsi ya kutambua tatizo, pamoja na njia rahisi za kuongeza muda wa matumizi ya betri. Maelezo haya yameandikwa kwa lugha rahisi ili kila mtu ayaelewe, hata kama hana ujuzi wa teknolojia.
Soma Zaidi...HTML - somo la 15: Jinsi ya kutengeneza website kwa kutumia HTML
Katika somo hili tutakwenda kutengeneza website yetu kutoka mwanzo hadi mwisho
Soma Zaidi...HATML - somo la 4: Jinsi ya kutumia tag za html
Katka somo hi utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia tag za html ili kupangilia muonekano wa maudhui
Soma Zaidi...Jinsi ya Kuzima Matangazo Yanayojitokeza Kwenye Simu
Je, umechoka kuona matangazo yanayojitokeza ghafla (pop-ups) na kukuvuruga unapotumia simu yako ya mkononi? Makala hii inakupa mwongozo rahisi sana, wa hatua kwa hatua, kuhusu jinsi ya kuzima matangazo hayo yote yanayokera kwenye simu za Android na iPhone. Mwongozo huu umeandikwa kwa lugha rahisi sana ya Kiswahili ili kila mtu, hata wale ambao hawana kabisa elimu ya shule au ujuzi mkubwa wa mambo ya teknolojia, aweze kuelewa vizuri na kusafisha simu yake leo bila msaada wa fundi. Ukisoma somo hili, utajifunza mbinu za kufunga matangazo kwenye Google Chrome, kupitia mipangilio ya ndani ya simu (Settings), na jinsi ya kung'oa programu zote za siri zinazoleta usumbufu huu.
Soma Zaidi...