picha

HTML - somo la 1: Maana ya HTML na kazi zake

Somo hili linakufundisha maana ya HTML, kwa nini inatumika, na jinsi ya kuandaa simu au kompyuta yako kwa ajili ya kuanza kutengeneza tovuti. Pia tutatengeneza ukurasa wetu wa kwanza wa HTML hatua kwa hatua.

Utangulizi

HTML ni lugha ya msingi inayotumika kutengenezea kurasa za tovuti na blogu. Bila HTML hakuna website inayoonekana duniani. Unaweza kutengeneza tovuti kwa kutumia HTML pekee, kisha ukaboresha baadaye kwa kutumia CSS na JavaScript.

Katika somo hili, tunaanza kwa kukuweka tayari ili uweze kuandika code zako bila shida—iwe unatumia simu au kompyuta.


Sasa tuingie kwenye somo letu…


1. HTML ni nini?

HTML ni ufupisho wa:

Ni lugha ya kimataifa inayotumiwa kutengeneza kurasa za tovuti (website pages). HTML haihitaji umiliki wa vifaa ghali; unaweza kuanza hata kwa kutumia simu yako ya mkononi.

Ikiwa una ndoto za kuanzisha blog, tovuti ya biashara au portfolio, basi uko mahali sahihi. Mafunzo haya yatakufundisha kuanzia hatua ya mwanzo kabisa hadi kutengeneza tovuti inayoweza kwenda live.


2. Vigezo vya kuanza kujifunza

Ili uweze kufanikiwa kwenye kozi hii, unahitaji:

Kozi ya msingi (Basics) itachukua wiki moja, kisha tutaendelea na hatua ya pili.


3. Namna ya kuandaa kifaa chako (Simu)

Kwa watumiaji wa simu, utatumia app inayoitwa Acode (badala ya TrebEdit kwa sababu Acode ni nyepesi na ya kisasa).

Hatua za kuandaa Acode

  1. Pakua app ya Acode kwenye Play Store:
    https://play.google.com/store/apps/details?id=com.foxdebug.acodefree

  2. Fungua Acode

  3. Bofya icon ya “folder” kisha tengeneza folder jipya

  4. Lipe jina mfano: html-project

  5. Ndani ya hilo folder, tengeneza folder lingine liitwe images

  6. Rudi kwenye folder la html-project

  7. Bonyeza alama ya “+” kutengeneza faili jipya

  8. Lipe jina: index.html

  9. Lifungue faili hilo

  10. Andika au kopia code zifuatazo:

<!DOCTYPE html>
<...
Ingia sasa ili uweze kusoma makala hii yote.

Zoezi la Maswali

help_outlineZoezi la Maswali

info Jaza maswali yote au baadhi kisha bofya kitufe cha kutuma majibu hapo chini.
1 HTML hasa inatumika katika kutengenezea ______
2 Kurasa za wavuti tunaweza kuziona kwenye ____
3 HTML ni kifupisho cha maneno __________

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: HTML Main: Masomo File: Download PDF Views 2273

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 ai web app     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 Bongolite - Game zone - Play free game     👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zinazofanana:

Jinsi ya Kutambua Kama Memory Card Imeharibika

Memory card (kadi ya kumbukumbu) ni kifaa kidogo kinachotunza vitu vyetu vya thamani kama picha, video, nyimbo na nyaraka muhimu katika simu au kamera. Hata hivyo, vifaa hivi mara nyingi huharibika bila kutoa taarifa. Makala hii imelenga kukusaidia wewe mtumiaji wa kawaida utambue kirahisi dalili za memory card iliyokufa au inayoelekea kuharibika. Utajifunza ishara za wazi kama faili kupotea, simu kuwa nzito, au ujumbe wa makosa (errors). Pia, tumekuwekea hatua rahisi za kufanya ili kulinda data zako zisipotee kabisa na jinsi ya kuepuka kununua kadi feki. Kila kitu kimeelekezwa kwa lugha rahisi ya Kiswahili isiyo na maneno magumu ya kiteknolojia.

Soma Zaidi...
HTML - somo la 15: Jinsi ya kutengeneza website kwa kutumia HTML

Katika somo hili tutakwenda kutengeneza website yetu kutoka mwanzo hadi mwisho

Soma Zaidi...
Jinsi ya Kuunganisha Simu na Wi-Fi

Wi-Fi ni njia rahisi inayowezesha simu kuunganishwa na intaneti bila kutumia bando la kawaida la simu. Kwa kutumia Wi-Fi, mtu anaweza kutumia intaneti kwa gharama ndogo au wakati mwingine bila gharama yoyote, hasa anapokuwa sehemu yenye mtandao wa Wi-Fi kama nyumbani, kazini, shuleni, hotelini au sehemu nyingine za umma. Kuunganisha simu na Wi-Fi ni jambo rahisi ambalo mtu yeyote anaweza kufanya hata kama hajawahi kutumia teknolojia sana. Unachohitaji ni simu yenye uwezo wa kutumia Wi-Fi, jina la mtandao wa Wi-Fi, na nenosiri kama mtandao huo umefungwa. Makala hii inaelezea hatua kwa hatua jinsi ya kuunganisha simu na Wi-Fi, mambo ya kuzingatia wakati wa kutumia Wi-Fi, sababu zinazoweza kufanya simu ishindwe kuunganishwa, pamoja na faida za kutumia mtandao wa Wi-Fi.

Soma Zaidi...
Jinsi ya Kuhamisha Mawasiliano (Contacts)

Mawasiliano (Contacts) ni sehemu muhimu sana katika simu zetu kwa sababu huhifadhi majina na namba za simu za watu tunaowasiliana nao kama vile familia, marafiki, wateja na wafanyakazi wenzetu. Watu wengi hubadilisha simu mpya au hupoteza simu zao bila kujua namna ya kuhifadhi na kuhamisha mawasiliano yao. Hali hii inaweza kusababisha kupoteza namba muhimu na kuleta usumbufu mkubwa. Katika makala hii tutajifunza jinsi ya kuhamisha mawasiliano kutoka simu moja kwenda nyingine kwa njia rahisi. Tutaeleza njia mbalimbali zinazoweza kutumiwa kama vile kutumia akaunti ya Google, kuhifadhi kwenye SIM kadi, kutumia Bluetooth, programu maalum na njia nyingine salama. Maelezo haya yameandikwa kwa lugha rahisi ili hata mtu asiye na ujuzi mkubwa wa teknolojia aweze kuelewa na kufuata hatua bila shida.

Soma Zaidi...
Jinsi ya Kujua Kama Wi-Fi Ni Salama

Wi-Fi imekuwa sehemu muhimu ya maisha yetu ya kila siku. Tunaitumia kuingia kwenye mitandao ya kijamii, kutuma ujumbe, kufanya biashara mtandaoni, kusoma, kutazama video na hata kufanya malipo. Lakini pamoja na faida zake nyingi, Wi-Fi inaweza kuwa hatari ikiwa haijalindwa vizuri. Mtandao wa Wi-Fi usio salama unaweza kuruhusu watu wasiohusika kuona taarifa zako binafsi, kuiba nywila zako au kutumia intaneti yako bila ruhusa. Kujua kama Wi-Fi ni salama ni jambo muhimu kwa kila mtu anayemiliki simu, kompyuta au kifaa kingine kinachounganishwa na intaneti. Makala hii inaeleza kwa lugha rahisi jinsi ya kutambua Wi-Fi salama, dalili za Wi-Fi hatari, hatua za kulinda mtandao wako na mambo muhimu ya kuzingatia ili kutumia intaneti kwa usalama

Soma Zaidi...
HTML - somo la 8: Mgawanyiko wa Tag za HTML na kazi zake

Katika somo hili tunakwenda kugawanya tag za HTML, pia nitakwenda kukuletea tag 70 za HTML

Soma Zaidi...