picha

HTML - somo la 1: Maana ya HTML na kazi zake

Somo hili linakufundisha maana ya HTML, kwa nini inatumika, na jinsi ya kuandaa simu au kompyuta yako kwa ajili ya kuanza kutengeneza tovuti. Pia tutatengeneza ukurasa wetu wa kwanza wa HTML hatua kwa hatua.

Utangulizi

HTML ni lugha ya msingi inayotumika kutengenezea kurasa za tovuti na blogu. Bila HTML hakuna website inayoonekana duniani. Unaweza kutengeneza tovuti kwa kutumia HTML pekee, kisha ukaboresha baadaye kwa kutumia CSS na JavaScript.

Katika somo hili, tunaanza kwa kukuweka tayari ili uweze kuandika code zako bila shida—iwe unatumia simu au kompyuta.


Sasa tuingie kwenye somo letu…


1. HTML ni nini?

HTML ni ufupisho wa:

Ni lugha ya kimataifa inayotumiwa kutengeneza kurasa za tovuti (website pages). HTML haihitaji umiliki wa vifaa ghali; unaweza kuanza hata kwa kutumia simu yako ya mkononi.

Ikiwa una ndoto za kuanzisha blog, tovuti ya biashara au portfolio, basi uko mahali sahihi. Mafunzo haya yatakufundisha kuanzia hatua ya mwanzo kabisa hadi kutengeneza tovuti inayoweza kwenda live.


2. Vigezo vya kuanza kujifunza

Ili uweze kufanikiwa kwenye kozi hii, unahitaji:

Kozi ya msingi (Basics) itachukua wiki moja, kisha tutaendelea na hatua ya pili.


3. Namna ya kuandaa kifaa chako (Simu)

Kwa watumiaji wa simu, utatumia app inayoitwa Acode (badala ya TrebEdit kwa sababu Acode ni nyepesi na ya kisasa).

Hatua za kuandaa Acode

  1. Pakua app ya Acode kwenye Play Store:
    https://play.google.com/store/apps/details?id=com.foxdebug.acodefree

  2. Fungua Acode

  3. Bofya icon ya “folder” kisha tengeneza folder jipya

  4. Lipe jina mfano: html-project

  5. Ndani ya hilo folder, tengeneza folder lingine liitwe images

  6. Rudi kwenye folder la html-project

  7. Bonyeza alama ya “+” kutengeneza faili jipya

  8. Lipe jina: index.html

  9. Lifungue faili hilo

  10. Andika au kopia code zifuatazo:

<!DOCTYPE html>
<...
Ingia sasa ili uweze kusoma makala hii yote.

Zoezi la Maswali

help_outlineZoezi la Maswali

info Jaza maswali yote au baadhi kisha bofya kitufe cha kutuma majibu hapo chini.
1 HTML ni kifupisho cha maneno __________
2 Kurasa za wavuti tunaweza kuziona kwenye ____
3 HTML hasa inatumika katika kutengenezea ______

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: HTML Main: Masomo File: Download PDF Views 2344

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 web hosting     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉6 Madrasa kiganjani    

Post zinazofanana:

Jinsi ya Kutafuta Simu Iliyopotea

Kupoteza simu ni jambo linaloweza kumpata mtu yeyote wakati wowote. Simu ya kisasa si kifaa cha kupigia simu tu, bali pia huhifadhi picha, namba za watu unaowasiliana nao, ujumbe, taarifa za benki, akaunti za mitandao ya kijamii na taarifa nyingine muhimu. Ndiyo maana kupoteza simu kunaweza kusababisha usumbufu mkubwa na hata hatari ya taarifa binafsi kuibiwa. Habari njema ni kwamba kuna njia mbalimbali zinazoweza kukusaidia kuitafuta simu iliyopotea. Unaweza kutumia huduma zilizopo ndani ya simu kama vile programu za kuitafuta simu, kutumia namba ya simu, kuwasiliana na kampuni ya mtandao, au kutumia taarifa za mwisho zilipoonekana. Makala hii inaeleza hatua kwa hatua jinsi ya kutafuta simu iliyopotea kwa njia rahisi ambayo kila mtu anaweza kuelewa.

Soma Zaidi...
Jinsi ya Kutatua Tatizo la Mikrofoni

Je, unajaribu kupiga simu, kurekodi sauti, au kuingia kwenye mkutano wa mtandaoni lakini mikrofoni yako haifanyi kazi? Huu ni mwongozo rahisi na wa hatua kwa hatua unaoelezea jinsi ya kutatua matatizo yote ya mikrofoni kwenye simu au kompyuta yako. Tumeandika mwongozo huu kwa lugha rahisi ya Kiswahili ili kila mtu, hata asiye na ujuzi wa teknolojia, aweze kuelewa na kurekebisha kifaa chake mara moja bila kuhitaji fundi.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kutengeneza cheti kwa kutumia HTML

Katika post hii utakwenda kujifunz ajinsi ya kutengeneza cheti kwa kutumia html na css.

Soma Zaidi...
Jinsi ya Kusafisha Simu Isifanye Kazi Polepole

Je, simu yako imekuwa ikifungua programu kwa kuchelewa, kuganda mara kwa mara au kufanya kazi polepole kuliko ilivyokuwa mwanzo? Tatizo hili ni la kawaida kwa watumiaji wengi wa simu za Android na hata iPhone. Mara nyingi watu hudhani kuwa simu imeharibika au imezeeka, wakati ukweli ni kwamba kuna uchafu wa kidijitali unaokusanyika ndani ya simu na kuifanya ishindwe kufanya kazi kwa kasi. Katika makala hii utajifunza jinsi ya kusafisha simu ili irudi kufanya kazi vizuri. Utaelewa sababu zinazofanya simu iwe polepole, namna ya kufuta faili zisizo muhimu, kusafisha kumbukumbu ya programu, kuondoa programu zisizotumika, kusasisha mfumo wa simu pamoja na mbinu nyingine zinazoweza kuongeza kasi ya simu bila kutumia fedha.

Soma Zaidi...
Jinsi ya Kujua Kama Wi-Fi Ni Salama

Wi-Fi imekuwa sehemu muhimu ya maisha yetu ya kila siku. Tunaitumia kuingia kwenye mitandao ya kijamii, kutuma ujumbe, kufanya biashara mtandaoni, kusoma, kutazama video na hata kufanya malipo. Lakini pamoja na faida zake nyingi, Wi-Fi inaweza kuwa hatari ikiwa haijalindwa vizuri. Mtandao wa Wi-Fi usio salama unaweza kuruhusu watu wasiohusika kuona taarifa zako binafsi, kuiba nywila zako au kutumia intaneti yako bila ruhusa. Kujua kama Wi-Fi ni salama ni jambo muhimu kwa kila mtu anayemiliki simu, kompyuta au kifaa kingine kinachounganishwa na intaneti. Makala hii inaeleza kwa lugha rahisi jinsi ya kutambua Wi-Fi salama, dalili za Wi-Fi hatari, hatua za kulinda mtandao wako na mambo muhimu ya kuzingatia ili kutumia intaneti kwa usalama

Soma Zaidi...
Jinsi ya Kuhifadhi Picha Kwenye Cloud

Picha ni kumbukumbu muhimu zinazohifadhi matukio ya maisha yetu kama vile harusi, sherehe, safari, watoto, familia na kazi mbalimbali. Tatizo kubwa ambalo watu wengi hukutana nalo ni kupoteza picha kutokana na simu kuharibika, kuibiwa, kupotea au kufutwa kimakosa. Njia salama ya kulinda picha zako ni kuzihifadhi kwenye Cloud. Katika makala hii utajifunza cloud ni nini, jinsi inavyofanya kazi, faida za kuhifadhi picha kwenye cloud, hatua za kuhifadhi picha zako kwa usalama pamoja na mambo muhimu ya kuzingatia ili kuhakikisha kumbukumbu zako zinabaki salama kwa muda mrefu.

Soma Zaidi...