HTML - somo la 1: Maana ya HTML na kazi zake
Somo hili linakufundisha maana ya HTML, kwa nini inatumika, na jinsi ya kuandaa simu au kompyuta yako kwa ajili ya kuanza kutengeneza tovuti. Pia tutatengeneza ukurasa wetu wa kwanza wa HTML hatua kwa hatua.
Utangulizi
HTML ni lugha ya msingi inayotumika kutengenezea kurasa za tovuti na blogu. Bila HTML hakuna website inayoonekana duniani. Unaweza kutengeneza tovuti kwa kutumia HTML pekee, kisha ukaboresha baadaye kwa kutumia CSS na JavaScript.
Katika somo hili, tunaanza kwa kukuweka tayari ili uweze kuandika code zako bila shida—iwe unatumia simu au kompyuta.
Sasa tuingie kwenye somo letu…
1. HTML ni nini?
HTML ni ufupisho wa:
-
Hypertext
-
Markup
-
Language
Ni lugha ya kimataifa inayotumiwa kutengeneza kurasa za tovuti (website pages). HTML haihitaji umiliki wa vifaa ghali; unaweza kuanza hata kwa kutumia simu yako ya mkononi.
Ikiwa una ndoto za kuanzisha blog, tovuti ya biashara au portfolio, basi uko mahali sahihi. Mafunzo haya yatakufundisha kuanzia hatua ya mwanzo kabisa hadi kutengeneza tovuti inayoweza kwenda live.
2. Vigezo vya kuanza kujifunza
Ili uweze kufanikiwa kwenye kozi hii, unahitaji:
-
Simu ya smartphone au kompyuta
-
Uwezo wa kusoma na kuandika
-
Utayari wa kujifunza
-
Umakini na ujanja
-
Kufanya mazoezi kila baada ya somo
Kozi ya msingi (Basics) itachukua wiki moja, kisha tutaendelea na hatua ya pili.
3. Namna ya kuandaa kifaa chako (Simu)
Kwa watumiaji wa simu, utatumia app inayoitwa Acode (badala ya TrebEdit kwa sababu Acode ni nyepesi na ya kisasa).
Hatua za kuandaa Acode
-
Pakua app ya Acode kwenye Play Store:
https://play.google.com/store/apps/details?id=com.foxdebug.acodefree -
Fungua Acode
-
Bofya icon ya “folder” kisha tengeneza folder jipya
-
Lipe jina mfano: html-project
-
Ndani ya hilo folder, tengeneza folder lingine liitwe images
-
Rudi kwenye folder la html-project
-
Bonyeza alama ya “+” kutengeneza faili jipya
-
Lipe jina: index.html
-
Lifungue faili hilo
-
Andika au kopia code zifuatazo:
<!DOCTYPE html>
<...help_outlineZoezi la Maswali
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 Simulizi za Hadithi Audio 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
HTML - somo la 3: Tags za HTML zinazotumiwa katika uandishi
Katika somo hili nitakuletea orodhabya tag 25 za html ambazo hugumiwa katikabuandishi.
Soma Zaidi...Sababu Zinazofanya Betri Iishe Haraka
Betri ni sehemu muhimu sana ya simu, kompyuta mpakato, saa janja na vifaa vingine vya kielektroniki. Hata hivyo, watu wengi hukutana na tatizo la betri kuisha haraka bila kujua chanzo chake. Wakati mwingine tatizo halitokani na ubora wa simu au betri, bali hutokana na namna kifaa kinavyotumika kila siku. Katika makala hii utajifunza sababu kuu zinazofanya betri iishe haraka, jinsi ya kutambua tatizo, pamoja na njia rahisi za kuongeza muda wa matumizi ya betri. Maelezo haya yameandikwa kwa lugha rahisi ili kila mtu ayaelewe, hata kama hana ujuzi wa teknolojia.
Soma Zaidi...HTML - somo la 8: Mgawanyiko wa Tag za HTML na kazi zake
Katika somo hili tunakwenda kugawanya tag za HTML, pia nitakwenda kukuletea tag 70 za HTML
Soma Zaidi...Jinsi ya Kutatua Tatizo la Mtandao wa Simu
Posti hii inatoa mwongozo rahisi na wa hatua kwa hatua kuhusu jinsi ya kurekebisha matatizo ya mtandao kwenye simu yako ya mkononi. Umejifunza njia za haraka kama kuwasha ‘Upepo’ (Flight Mode), kuwasha upya simu, na kuangalia kadi ya SIM ili kurudisha mawasiliano haraka bila kuhitaji fundi.
Soma Zaidi...Jinsi ya Kutambua Kama Memory Card Imeharibika
Memory card (kadi ya kumbukumbu) ni kifaa kidogo kinachotunza vitu vyetu vya thamani kama picha, video, nyimbo na nyaraka muhimu katika simu au kamera. Hata hivyo, vifaa hivi mara nyingi huharibika bila kutoa taarifa. Makala hii imelenga kukusaidia wewe mtumiaji wa kawaida utambue kirahisi dalili za memory card iliyokufa au inayoelekea kuharibika. Utajifunza ishara za wazi kama faili kupotea, simu kuwa nzito, au ujumbe wa makosa (errors). Pia, tumekuwekea hatua rahisi za kufanya ili kulinda data zako zisipotee kabisa na jinsi ya kuepuka kununua kadi feki. Kila kitu kimeelekezwa kwa lugha rahisi ya Kiswahili isiyo na maneno magumu ya kiteknolojia.
Soma Zaidi...HTML - somo la 9: Jinsi ya kutumia tag za HTML katika uandishi wa maudhui
Katika somo hili utakwenda kuona jinsi ya kuzitumia tag balimbali za html
Soma Zaidi...