HTML - somo la 1: Maana ya HTML na kazi zake
Somo hili linakufundisha maana ya HTML, kwa nini inatumika, na jinsi ya kuandaa simu au kompyuta yako kwa ajili ya kuanza kutengeneza tovuti. Pia tutatengeneza ukurasa wetu wa kwanza wa HTML hatua kwa hatua.
Utangulizi
HTML ni lugha ya msingi inayotumika kutengenezea kurasa za tovuti na blogu. Bila HTML hakuna website inayoonekana duniani. Unaweza kutengeneza tovuti kwa kutumia HTML pekee, kisha ukaboresha baadaye kwa kutumia CSS na JavaScript.
Katika somo hili, tunaanza kwa kukuweka tayari ili uweze kuandika code zako bila shida—iwe unatumia simu au kompyuta.
Sasa tuingie kwenye somo letu…
1. HTML ni nini?
HTML ni ufupisho wa:
-
Hypertext
-
Markup
-
Language
Ni lugha ya kimataifa inayotumiwa kutengeneza kurasa za tovuti (website pages). HTML haihitaji umiliki wa vifaa ghali; unaweza kuanza hata kwa kutumia simu yako ya mkononi.
Ikiwa una ndoto za kuanzisha blog, tovuti ya biashara au portfolio, basi uko mahali sahihi. Mafunzo haya yatakufundisha kuanzia hatua ya mwanzo kabisa hadi kutengeneza tovuti inayoweza kwenda live.
2. Vigezo vya kuanza kujifunza
Ili uweze kufanikiwa kwenye kozi hii, unahitaji:
-
Simu ya smartphone au kompyuta
-
Uwezo wa kusoma na kuandika
-
Utayari wa kujifunza
-
Umakini na ujanja
-
Kufanya mazoezi kila baada ya somo
Kozi ya msingi (Basics) itachukua wiki moja, kisha tutaendelea na hatua ya pili.
3. Namna ya kuandaa kifaa chako (Simu)
Kwa watumiaji wa simu, utatumia app inayoitwa Acode (badala ya TrebEdit kwa sababu Acode ni nyepesi na ya kisasa).
Hatua za kuandaa Acode
-
Pakua app ya Acode kwenye Play Store:
https://play.google.com/store/apps/details?id=com.foxdebug.acodefree -
Fungua Acode
-
Bofya icon ya “folder” kisha tengeneza folder jipya
-
Lipe jina mfano: html-project
-
Ndani ya hilo folder, tengeneza folder lingine liitwe images
-
Rudi kwenye folder la html-project
-
Bonyeza alama ya “+” kutengeneza faili jipya
-
Lipe jina: index.html
-
Lifungue faili hilo
-
Andika au kopia code zifuatazo:
<!DOCTYPE html>
<...help_outlineZoezi la Maswali
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
HTML - somo la 10: Maana ya HTML attribute na jinsi zinavyofanya kazi
Katika somo hili utakwenda kijifunza kuhusu HTML attributes na jinsi ambavyo zinafanya kazi
Soma Zaidi...Jinsi ya Kuhifadhi Picha Kwenye Cloud
Picha ni kumbukumbu muhimu zinazohifadhi matukio ya maisha yetu kama vile harusi, sherehe, safari, watoto, familia na kazi mbalimbali. Tatizo kubwa ambalo watu wengi hukutana nalo ni kupoteza picha kutokana na simu kuharibika, kuibiwa, kupotea au kufutwa kimakosa. Njia salama ya kulinda picha zako ni kuzihifadhi kwenye Cloud. Katika makala hii utajifunza cloud ni nini, jinsi inavyofanya kazi, faida za kuhifadhi picha kwenye cloud, hatua za kuhifadhi picha zako kwa usalama pamoja na mambo muhimu ya kuzingatia ili kuhakikisha kumbukumbu zako zinabaki salama kwa muda mrefu.
Soma Zaidi...HTML - somo la 14: Hatua za kutengeneza website
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza website hatuwa kwa hatuwa
Soma Zaidi...Jinsi ya Kusakinisha (Install) App kwa Usalama
Siku hizi simu za mkononi zimekuwa sehemu muhimu ya maisha ya kila siku. Tunazitumia kuwasiliana, kufanya biashara, kusoma, kulipa bili, kutazama video, kusikiliza muziki na hata kuhifadhi taarifa muhimu. Ili simu iweze kufanya kazi hizi, tunahitaji kusakinisha (install) programu mbalimbali zinazojulikana kama app. Lakini si kila app ni salama. Baadhi ya app zinaweza kuiba taarifa zako binafsi, kuharibu simu, kuonyesha matangazo mengi yasiyofaa au hata kusababisha akaunti zako kuporwa. Ndiyo maana ni muhimu kujifunza jinsi ya kusakinisha app kwa usalama. Katika makala hii utajifunza hatua zote muhimu za kusakinisha app kwa usalama, namna ya kutambua app halisi, mambo ya kuzingatia kabla na baada ya kusakinisha app, pamoja na makosa ambayo watu wengi hufanya bila kujua.
Soma Zaidi...Jinsi ya Kutatua Tatizo la SMS Kutotumwa
Kushindwa kutuma ujumbe wa kawaida wa maandishi (SMS) ni tatizo linalowakera watu wengi kila siku. Makala hii inakueleza kwa lugha rahisi kabisa sababu zinazosababisha ujumbe wako usiende na inakupa hatua 8 rahisi za kurekebisha tatizo hili mwenyewe. Utafiti unaonyesha kuwa asilimia kubwa ya matatizo haya yanatokana na mambo madogo kama kukosa salio, mtandao dhaifu, au namba za vituo vya ujumbe (SMSC) kukosewa kwenye simu yako. Kusoma mwongozo huu kutakusaidia kuokoa muda na pesa bila kulazimika kwenda kwa fundi.
Soma Zaidi...Jinsi ya Kutafuta Simu Iliyopotea
Kupoteza simu ni jambo linaloweza kumpata mtu yeyote wakati wowote. Simu ya kisasa si kifaa cha kupigia simu tu, bali pia huhifadhi picha, namba za watu unaowasiliana nao, ujumbe, taarifa za benki, akaunti za mitandao ya kijamii na taarifa nyingine muhimu. Ndiyo maana kupoteza simu kunaweza kusababisha usumbufu mkubwa na hata hatari ya taarifa binafsi kuibiwa. Habari njema ni kwamba kuna njia mbalimbali zinazoweza kukusaidia kuitafuta simu iliyopotea. Unaweza kutumia huduma zilizopo ndani ya simu kama vile programu za kuitafuta simu, kutumia namba ya simu, kuwasiliana na kampuni ya mtandao, au kutumia taarifa za mwisho zilipoonekana. Makala hii inaeleza hatua kwa hatua jinsi ya kutafuta simu iliyopotea kwa njia rahisi ambayo kila mtu anaweza kuelewa.
Soma Zaidi...