HTML - somo la 1: Maana ya HTML na kazi zake
Somo hili linakufundisha maana ya HTML, kwa nini inatumika, na jinsi ya kuandaa simu au kompyuta yako kwa ajili ya kuanza kutengeneza tovuti. Pia tutatengeneza ukurasa wetu wa kwanza wa HTML hatua kwa hatua.
Utangulizi
HTML ni lugha ya msingi inayotumika kutengenezea kurasa za tovuti na blogu. Bila HTML hakuna website inayoonekana duniani. Unaweza kutengeneza tovuti kwa kutumia HTML pekee, kisha ukaboresha baadaye kwa kutumia CSS na JavaScript.
Katika somo hili, tunaanza kwa kukuweka tayari ili uweze kuandika code zako bila shida—iwe unatumia simu au kompyuta.
Sasa tuingie kwenye somo letu…
1. HTML ni nini?
HTML ni ufupisho wa:
-
Hypertext
-
Markup
-
Language
Ni lugha ya kimataifa inayotumiwa kutengeneza kurasa za tovuti (website pages). HTML haihitaji umiliki wa vifaa ghali; unaweza kuanza hata kwa kutumia simu yako ya mkononi.
Ikiwa una ndoto za kuanzisha blog, tovuti ya biashara au portfolio, basi uko mahali sahihi. Mafunzo haya yatakufundisha kuanzia hatua ya mwanzo kabisa hadi kutengeneza tovuti inayoweza kwenda live.
2. Vigezo vya kuanza kujifunza
Ili uweze kufanikiwa kwenye kozi hii, unahitaji:
-
Simu ya smartphone au kompyuta
-
Uwezo wa kusoma na kuandika
-
Utayari wa kujifunza
-
Umakini na ujanja
-
Kufanya mazoezi kila baada ya somo
Kozi ya msingi (Basics) itachukua wiki moja, kisha tutaendelea na hatua ya pili.
3. Namna ya kuandaa kifaa chako (Simu)
Kwa watumiaji wa simu, utatumia app inayoitwa Acode (badala ya TrebEdit kwa sababu Acode ni nyepesi na ya kisasa).
Hatua za kuandaa Acode
-
Pakua app ya Acode kwenye Play Store:
https://play.google.com/store/apps/details?id=com.foxdebug.acodefree -
Fungua Acode
-
Bofya icon ya “folder” kisha tengeneza folder jipya
-
Lipe jina mfano: html-project
-
Ndani ya hilo folder, tengeneza folder lingine liitwe images
-
Rudi kwenye folder la html-project
-
Bonyeza alama ya “+” kutengeneza faili jipya
-
Lipe jina: index.html
-
Lifungue faili hilo
-
Andika au kopia code zifuatazo:
<!DOCTYPE html>
<...help_outlineZoezi la Maswali
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 ai web app 👉6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Jinsi ya Kutatua Tatizo la Mtandao wa Simu
Posti hii inatoa mwongozo rahisi na wa hatua kwa hatua kuhusu jinsi ya kurekebisha matatizo ya mtandao kwenye simu yako ya mkononi. Umejifunza njia za haraka kama kuwasha ‘Upepo’ (Flight Mode), kuwasha upya simu, na kuangalia kadi ya SIM ili kurudisha mawasiliano haraka bila kuhitaji fundi.
Soma Zaidi...Jinsi ya Kuzima Matangazo Yanayojitokeza Kwenye Simu
Je, umechoka kuona matangazo yanayojitokeza ghafla (pop-ups) na kukuvuruga unapotumia simu yako ya mkononi? Makala hii inakupa mwongozo rahisi sana, wa hatua kwa hatua, kuhusu jinsi ya kuzima matangazo hayo yote yanayokera kwenye simu za Android na iPhone. Mwongozo huu umeandikwa kwa lugha rahisi sana ya Kiswahili ili kila mtu, hata wale ambao hawana kabisa elimu ya shule au ujuzi mkubwa wa mambo ya teknolojia, aweze kuelewa vizuri na kusafisha simu yake leo bila msaada wa fundi. Ukisoma somo hili, utajifunza mbinu za kufunga matangazo kwenye Google Chrome, kupitia mipangilio ya ndani ya simu (Settings), na jinsi ya kung'oa programu zote za siri zinazoleta usumbufu huu.
Soma Zaidi...Jinsi ya Kutatua Tatizo la SMS Kutotumwa
Kushindwa kutuma ujumbe wa kawaida wa maandishi (SMS) ni tatizo linalowakera watu wengi kila siku. Makala hii inakueleza kwa lugha rahisi kabisa sababu zinazosababisha ujumbe wako usiende na inakupa hatua 8 rahisi za kurekebisha tatizo hili mwenyewe. Utafiti unaonyesha kuwa asilimia kubwa ya matatizo haya yanatokana na mambo madogo kama kukosa salio, mtandao dhaifu, au namba za vituo vya ujumbe (SMSC) kukosewa kwenye simu yako. Kusoma mwongozo huu kutakusaidia kuokoa muda na pesa bila kulazimika kwenda kwa fundi.
Soma Zaidi...HTML - somo la 10: Maana ya HTML attribute na jinsi zinavyofanya kazi
Katika somo hili utakwenda kijifunza kuhusu HTML attributes na jinsi ambavyo zinafanya kazi
Soma Zaidi...Faida za Screen Protector
Screen Protector ni kifaa chembamba kinachowekwa juu ya skrini ya simu ili kuilinda dhidi ya mikwaruzo, mipasuko na uharibifu mwingine unaoweza kutokea wakati wa matumizi ya kila siku. Watu wengi hununua simu za gharama kubwa lakini husahau kulinda sehemu muhimu zaidi ya simu hiyo, ambayo ni skrini. Makala hii inaelezea kwa kina faida za Screen Protector, aina zake, jinsi ya kuchagua inayofaa, na sababu zinazofanya iwe uwekezaji muhimu kwa kila mwenye simu.
Soma Zaidi...Jinsi ya Kufanya Backup ya Simu
Simu ya mkononi imekuwa sehemu muhimu sana ya maisha yetu ya kila siku. Tunatumia simu kuhifadhi namba za watu tunaowajua, picha za familia, video muhimu, ujumbe, nyaraka, programu na taarifa nyingine nyingi. Lakini tatizo linaweza kutokea wakati wowote. Simu inaweza kupotea, kuharibika, kuibiwa au kufutika taarifa zake kwa bahati mbaya. Hapo ndipo umuhimu wa kufanya backup ya simu unapokuwa mkubwa. Backup ya simu ni njia ya kutengeneza nakala ya taarifa zako muhimu na kuzihifadhi sehemu salama ili uweze kuzirudisha pale unapohitaji. Kwa kufanya backup mara kwa mara, unapunguza hatari ya kupoteza vitu muhimu vilivyokuwa kwenye simu yako. Katika makala hii tutajifunza maana ya backup ya simu, umuhimu wake, njia mbalimbali za kufanya backup kwenye simu za Android na iPhone, vitu vinavyoweza kuhifadhiwa, makosa ya kuepuka na hatua rahisi ambazo kila mtu anaweza kufuata hata kama hana ujuzi mkubwa wa teknolojia.
Soma Zaidi...