HTML - somo la 1: Maana ya HTML na kazi zake
Somo hili linakufundisha maana ya HTML, kwa nini inatumika, na jinsi ya kuandaa simu au kompyuta yako kwa ajili ya kuanza kutengeneza tovuti. Pia tutatengeneza ukurasa wetu wa kwanza wa HTML hatua kwa hatua.
Utangulizi
HTML ni lugha ya msingi inayotumika kutengenezea kurasa za tovuti na blogu. Bila HTML hakuna website inayoonekana duniani. Unaweza kutengeneza tovuti kwa kutumia HTML pekee, kisha ukaboresha baadaye kwa kutumia CSS na JavaScript.
Katika somo hili, tunaanza kwa kukuweka tayari ili uweze kuandika code zako bila shida—iwe unatumia simu au kompyuta.
Sasa tuingie kwenye somo letu…
1. HTML ni nini?
HTML ni ufupisho wa:
-
Hypertext
-
Markup
-
Language
Ni lugha ya kimataifa inayotumiwa kutengeneza kurasa za tovuti (website pages). HTML haihitaji umiliki wa vifaa ghali; unaweza kuanza hata kwa kutumia simu yako ya mkononi.
Ikiwa una ndoto za kuanzisha blog, tovuti ya biashara au portfolio, basi uko mahali sahihi. Mafunzo haya yatakufundisha kuanzia hatua ya mwanzo kabisa hadi kutengeneza tovuti inayoweza kwenda live.
2. Vigezo vya kuanza kujifunza
Ili uweze kufanikiwa kwenye kozi hii, unahitaji:
-
Simu ya smartphone au kompyuta
-
Uwezo wa kusoma na kuandika
-
Utayari wa kujifunza
-
Umakini na ujanja
-
Kufanya mazoezi kila baada ya somo
Kozi ya msingi (Basics) itachukua wiki moja, kisha tutaendelea na hatua ya pili.
3. Namna ya kuandaa kifaa chako (Simu)
Kwa watumiaji wa simu, utatumia app inayoitwa Acode (badala ya TrebEdit kwa sababu Acode ni nyepesi na ya kisasa).
Hatua za kuandaa Acode
-
Pakua app ya Acode kwenye Play Store:
https://play.google.com/store/apps/details?id=com.foxdebug.acodefree -
Fungua Acode
-
Bofya icon ya “folder” kisha tengeneza folder jipya
-
Lipe jina mfano: html-project
-
Ndani ya hilo folder, tengeneza folder lingine liitwe images
-
Rudi kwenye folder la html-project
-
Bonyeza alama ya “+” kutengeneza faili jipya
-
Lipe jina: index.html
-
Lifungue faili hilo
-
Andika au kopia code zifuatazo:
<!DOCTYPE html>
<...help_outlineZoezi la Maswali
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Jinsi ya Kufanya Backup ya Simu
Simu ya mkononi imekuwa sehemu muhimu sana ya maisha yetu ya kila siku. Tunatumia simu kuhifadhi namba za watu tunaowajua, picha za familia, video muhimu, ujumbe, nyaraka, programu na taarifa nyingine nyingi. Lakini tatizo linaweza kutokea wakati wowote. Simu inaweza kupotea, kuharibika, kuibiwa au kufutika taarifa zake kwa bahati mbaya. Hapo ndipo umuhimu wa kufanya backup ya simu unapokuwa mkubwa. Backup ya simu ni njia ya kutengeneza nakala ya taarifa zako muhimu na kuzihifadhi sehemu salama ili uweze kuzirudisha pale unapohitaji. Kwa kufanya backup mara kwa mara, unapunguza hatari ya kupoteza vitu muhimu vilivyokuwa kwenye simu yako. Katika makala hii tutajifunza maana ya backup ya simu, umuhimu wake, njia mbalimbali za kufanya backup kwenye simu za Android na iPhone, vitu vinavyoweza kuhifadhiwa, makosa ya kuepuka na hatua rahisi ambazo kila mtu anaweza kufuata hata kama hana ujuzi mkubwa wa teknolojia.
Soma Zaidi...HTML - somo la 3: Tags za HTML zinazotumiwa katika uandishi
Katika somo hili nitakuletea orodhabya tag 25 za html ambazo hugumiwa katikabuandishi.
Soma Zaidi...Faida za Screen Protector
Screen Protector ni kifaa chembamba kinachowekwa juu ya skrini ya simu ili kuilinda dhidi ya mikwaruzo, mipasuko na uharibifu mwingine unaoweza kutokea wakati wa matumizi ya kila siku. Watu wengi hununua simu za gharama kubwa lakini husahau kulinda sehemu muhimu zaidi ya simu hiyo, ambayo ni skrini. Makala hii inaelezea kwa kina faida za Screen Protector, aina zake, jinsi ya kuchagua inayofaa, na sababu zinazofanya iwe uwekezaji muhimu kwa kila mwenye simu.
Soma Zaidi...Jinsi ya Kurejesha Backup ya Simu
Umewahi kupoteza picha, video, majina ya watu, au mazungumzo muhimu baada ya simu kuharibika, kuibiwa, au kufanya factory reset? Hali hii huwatokea watu wengi, lakini habari njema ni kwamba unaweza kuvirejesha ikiwa uliwahi kutengeneza backup ya simu yako. Katika makala hii utajifunza backup ya simu ni nini, kwa nini ni muhimu, jinsi ya kurejesha backup kwenye simu za Android na iPhone, matatizo yanayoweza kujitokeza wakati wa kurejesha backup, pamoja na njia za kuyatatua. Mwisho wa makala hii utakuwa na uelewa wa kutosha wa jinsi ya kurudisha taarifa zako kwa usalama na kwa urahisi.
Soma Zaidi...Jinsi ya kutengeneza cheti kwa kutumia HTML
Katika post hii utakwenda kujifunz ajinsi ya kutengeneza cheti kwa kutumia html na css.
Soma Zaidi...HTML - somo la 13: Jinsi ya kugawa ukurasa wa HTML
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kugawanya ukurasa wa HTML katika column
Soma Zaidi...