HTML - somo la 1: Maana ya HTML na kazi zake
Somo hili linakufundisha maana ya HTML, kwa nini inatumika, na jinsi ya kuandaa simu au kompyuta yako kwa ajili ya kuanza kutengeneza tovuti. Pia tutatengeneza ukurasa wetu wa kwanza wa HTML hatua kwa hatua.
Utangulizi
HTML ni lugha ya msingi inayotumika kutengenezea kurasa za tovuti na blogu. Bila HTML hakuna website inayoonekana duniani. Unaweza kutengeneza tovuti kwa kutumia HTML pekee, kisha ukaboresha baadaye kwa kutumia CSS na JavaScript.
Katika somo hili, tunaanza kwa kukuweka tayari ili uweze kuandika code zako bila shida—iwe unatumia simu au kompyuta.
Sasa tuingie kwenye somo letu…
1. HTML ni nini?
HTML ni ufupisho wa:
-
Hypertext
-
Markup
-
Language
Ni lugha ya kimataifa inayotumiwa kutengeneza kurasa za tovuti (website pages). HTML haihitaji umiliki wa vifaa ghali; unaweza kuanza hata kwa kutumia simu yako ya mkononi.
Ikiwa una ndoto za kuanzisha blog, tovuti ya biashara au portfolio, basi uko mahali sahihi. Mafunzo haya yatakufundisha kuanzia hatua ya mwanzo kabisa hadi kutengeneza tovuti inayoweza kwenda live.
2. Vigezo vya kuanza kujifunza
Ili uweze kufanikiwa kwenye kozi hii, unahitaji:
-
Simu ya smartphone au kompyuta
-
Uwezo wa kusoma na kuandika
-
Utayari wa kujifunza
-
Umakini na ujanja
-
Kufanya mazoezi kila baada ya somo
Kozi ya msingi (Basics) itachukua wiki moja, kisha tutaendelea na hatua ya pili.
3. Namna ya kuandaa kifaa chako (Simu)
Kwa watumiaji wa simu, utatumia app inayoitwa Acode (badala ya TrebEdit kwa sababu Acode ni nyepesi na ya kisasa).
Hatua za kuandaa Acode
-
Pakua app ya Acode kwenye Play Store:
https://play.google.com/store/apps/details?id=com.foxdebug.acodefree -
Fungua Acode
-
Bofya icon ya “folder” kisha tengeneza folder jipya
-
Lipe jina mfano: html-project
-
Ndani ya hilo folder, tengeneza folder lingine liitwe images
-
Rudi kwenye folder la html-project
-
Bonyeza alama ya “+” kutengeneza faili jipya
-
Lipe jina: index.html
-
Lifungue faili hilo
-
Andika au kopia code zifuatazo:
<!DOCTYPE html>
<...help_outlineZoezi la Maswali
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
Jinsi ya Kuzima Matangazo Yanayojitokeza Kwenye Simu
Je, umechoka kuona matangazo yanayojitokeza ghafla (pop-ups) na kukuvuruga unapotumia simu yako ya mkononi? Makala hii inakupa mwongozo rahisi sana, wa hatua kwa hatua, kuhusu jinsi ya kuzima matangazo hayo yote yanayokera kwenye simu za Android na iPhone. Mwongozo huu umeandikwa kwa lugha rahisi sana ya Kiswahili ili kila mtu, hata wale ambao hawana kabisa elimu ya shule au ujuzi mkubwa wa mambo ya teknolojia, aweze kuelewa vizuri na kusafisha simu yake leo bila msaada wa fundi. Ukisoma somo hili, utajifunza mbinu za kufunga matangazo kwenye Google Chrome, kupitia mipangilio ya ndani ya simu (Settings), na jinsi ya kung'oa programu zote za siri zinazoleta usumbufu huu.
Soma Zaidi...HTML - somo la 3: Tags za HTML zinazotumiwa katika uandishi
Katika somo hili nitakuletea orodhabya tag 25 za html ambazo hugumiwa katikabuandishi.
Soma Zaidi...Sababu Zinazofanya Betri Iishe Haraka
Betri ni sehemu muhimu sana ya simu, kompyuta mpakato, saa janja na vifaa vingine vya kielektroniki. Hata hivyo, watu wengi hukutana na tatizo la betri kuisha haraka bila kujua chanzo chake. Wakati mwingine tatizo halitokani na ubora wa simu au betri, bali hutokana na namna kifaa kinavyotumika kila siku. Katika makala hii utajifunza sababu kuu zinazofanya betri iishe haraka, jinsi ya kutambua tatizo, pamoja na njia rahisi za kuongeza muda wa matumizi ya betri. Maelezo haya yameandikwa kwa lugha rahisi ili kila mtu ayaelewe, hata kama hana ujuzi wa teknolojia.
Soma Zaidi...Jinsi ya Kufuta Data za Simu Ukiwa Mbali
Kupoteza simu au kuibiwa kwa simu ni jambo linaloweza kumpata mtu yeyote. Simu zetu siku hizi hazitumiki tu kupiga simu na kutuma ujumbe, bali pia huhifadhi taarifa nyingi muhimu kama picha, video, namba za simu, akaunti za mitandao ya kijamii, taarifa za benki, barua pepe na nyaraka binafsi. Ikiwa simu itaangukia mikononi mwa mtu asiye mwaminifu, taarifa hizo zinaweza kutumiwa vibaya. Njia moja ya kujilinda ni kujifunza jinsi ya kufuta data za simu ukiwa mbali. Hii ina maana kwamba unaweza kuondoa taarifa zote zilizomo kwenye simu yako hata kama simu hiyo haipo karibu nawe. Njia hii husaidia kulinda faragha yako na kuzuia watu wengine kuona au kutumia taarifa zako binafsi. Katika makala hii tutajifunza maana ya kufuta data za simu ukiwa mbali, sababu za kufanya hivyo, hatua za kufuata, mambo muhimu ya kuzingatia kabla ya kufuta taarifa, pamoja na ukweli muhimu kuhusu usalama wa simu
Soma Zaidi...Jinsi ya Kutatua Tatizo la Mtandao wa Simu
Posti hii inatoa mwongozo rahisi na wa hatua kwa hatua kuhusu jinsi ya kurekebisha matatizo ya mtandao kwenye simu yako ya mkononi. Umejifunza njia za haraka kama kuwasha ‘Upepo’ (Flight Mode), kuwasha upya simu, na kuangalia kadi ya SIM ili kurudisha mawasiliano haraka bila kuhitaji fundi.
Soma Zaidi...Jinsi ya Kuunganisha Simu na Wi-Fi
Wi-Fi ni njia rahisi inayowezesha simu kuunganishwa na intaneti bila kutumia bando la kawaida la simu. Kwa kutumia Wi-Fi, mtu anaweza kutumia intaneti kwa gharama ndogo au wakati mwingine bila gharama yoyote, hasa anapokuwa sehemu yenye mtandao wa Wi-Fi kama nyumbani, kazini, shuleni, hotelini au sehemu nyingine za umma. Kuunganisha simu na Wi-Fi ni jambo rahisi ambalo mtu yeyote anaweza kufanya hata kama hajawahi kutumia teknolojia sana. Unachohitaji ni simu yenye uwezo wa kutumia Wi-Fi, jina la mtandao wa Wi-Fi, na nenosiri kama mtandao huo umefungwa. Makala hii inaelezea hatua kwa hatua jinsi ya kuunganisha simu na Wi-Fi, mambo ya kuzingatia wakati wa kutumia Wi-Fi, sababu zinazoweza kufanya simu ishindwe kuunganishwa, pamoja na faida za kutumia mtandao wa Wi-Fi.
Soma Zaidi...