HTML - somo la 1: Maana ya HTML na kazi zake

Katika somo hili utajifunza maana ya HTML na jinsi inavyofanya kazi

HTML ni ufupisho wa maneno yanayosomeka kama:-

Hypertext

Markup

Language

 

Ni lugha ya komputa inayotumika katika kutengenezea kurasa za tovuti (website) ama blog.Inaungana na lugha nyingine katika kuboresha kurrasa za tovuti ama blog na kuzifanya ziweze kufanya kazi iliyokusudiwa vyema. Unaweza kutumia HTML tu ukatengeneza website yako bila ya lugha nyingine. Hata hivyo muonekano wake hautakuwa vyema sana kama hutatumia nyinggine.

 

Je na wewe una ndoto za kuwa na blog ama website uliyoitengeneza wewe mwenyewe. Mafunzo haya ni kwa ajili yako. Katika mafunzo haya utajifunza namna ya kutengeneza website yako kupitia kiganja chako yaani simu yako ya mkononi. Kama utakuwa na kompyuta hatutakuacha pia.

 

Somo hili la kwanza utajifunza namna ya kuandaa simu yako kwa ajili ya kutengeneza website, ama kwa ajili ya kutumia HTML. Kama tutaenda vyema na mafunzo haya hadi mwisho nakuhakikishia kama Mwenyezi Mungu akitujaalia nguvu, uwezo na uhai, utaweza kutengeneza website yako na kuiweka live.

 

Muda wa masomo haya kwa hatuwa za Awali (Basics) itakuwa na wiki moja. Kisha baada ya hapo hatuwa ya pili ya mafunzo itaendelea. Tafadhali kuwa tayari kujifunza, kuwa muulizaji na mchangiaji:

 

VIGEZO VYA KUJIFUNZA:

  1. Kuwa na simu ya smartphone
  2. Uwe unajuwa kusoma na kuandika
  3. Kuwa tayari kujifunza
  4. Kuwa mjanja
  5. Uwe mwenye kufanyi akazi (fanya mazoezi)

 

NAMNA YA KUANDAA KIFAA CHAKO

KWA WANAOTUMIA SIMU:

  1. Download App inayoitwa TrebEdit. Tumia link hii https://play.google.com/store/apps/details?id=com.teejay.trebedit
  2. Funguwa App yako kisha bofya  Menu
  3. Bofya palipoandikwa Workplace 
  4. Bofya kitufe chenye alama ya kujumlisha chini
  5. Kisha bofya palipandikwa New Project
  6. Andika jina la Project (mimi natumia HTML) kisha bofya save.
  7. Ingia kwenye project uliotengeneza kwa kubofya jina lake, ukurasa mpya utafunguka
  8. Bofya tena kitufe cha alama ya kujumlisha
  9. Bofya palipoandikwa new folder (hapa tunatengeneza folda la kuweka picha tutakazokuja kuzitumia kwenye tovutu tutakayotengeneza)
  10. Andika jina la folda tumia image kisha bofya save.
  11. Baada ya hapo rudi nyuma hatuwa moja kwenye project yako.
  12. Bofya tena jina la project yako
  13. Bofya kitufe cha alama ya kujumlisha
  14. Bofya palipandika New file (hapa ndipo tutakapoanzia kuweka code za kutengeneza tovuti yetu)
  15. Utatkiwa kuandika jina la file hapo andika index.html (hili ndio faili letu la kwanza la tovuti yetu.
  16. <">...

    Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

    Zoezi la Maswali

    help_outlineZoezi la Maswali

    info Jaza maswali yote au baadhi kisha bofya kitufe cha kutuma majibu hapo chini.
    1 HTML ni kifupisho cha maneno __________
    2 HTML hasa inatumika katika kutengenezea ______
    3 Kurasa za wavuti tunaweza kuziona kwenye ____

    Endelea


    Umeionaje Makala hii.. ?

    Nzuri            Mbaya            Save
    Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: HTML Main: ICT File: Download PDF Views 1323

    Share On:

    Facebook WhatsApp
    Sponsored links
    👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

    Post zinazofanana:

    HTML - somo la 15: Jinsi ya kutengeneza website kwa kutumia HTML

    Katika somo hili tutakwenda kutengeneza website yetu kutoka mwanzo hadi mwisho

    Soma Zaidi...
    HTML-somo la 5: Jinsi ya kupangilia munekano wa maudhui kwenye website

    Katika somo hili utajifunza Kuweka picha Kuweka rangi Kuweka linki Kupangilia position na alignment ya maandishi Kuongeza ukubwa wa herufi Kukoment

    Soma Zaidi...
    HTML - somo la 3: Tags za HTML zinazotumiwa katika uandishi

    Katika somo hili nitakuletea orodhabya tag 25 za html ambazo hugumiwa katikabuandishi.

    Soma Zaidi...
    HTML - somo la 7: Vitu vya kuzingatia unapoandika HTML

    Katika somo hili utajifunza sehemu muhimu katika faili la HTML kama vile tag, attribute na element

    Soma Zaidi...
    HTML - somo la 10: Maana ya HTML attribute na jinsi zinavyofanya kazi

    Katika somo hili utakwenda kijifunza kuhusu HTML attributes na jinsi ambavyo zinafanya kazi

    Soma Zaidi...
    HTML - somo la 16: Jinsi ya ku host website bure

    Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ku host website yako bila malipo

    Soma Zaidi...
    HTML- somo la 2: Kazi za HTML, code na tag kwenye website.

    Katika somo somo hili utajifunza maana ya code, tag na mpangilio wa faili la HTML

    Soma Zaidi...
    HTML - somo la 8: Mgawanyiko wa Tag za HTML na kazi zake

    Katika somo hili tunakwenda kugawanya tag za HTML, pia nitakwenda kukuletea tag 70 za HTML

    Soma Zaidi...
    HATML - somo la 4: Jinsi ya kutumia tag za html

    Katka somo hi utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia tag za html ili kupangilia muonekano wa maudhui

    Soma Zaidi...