Uislamu unakataza mtu kulaani hovyo

20.

Uislamu unakataza mtu kulaani hovyo

20. Kuepukana na Kulaani Ovyo



Kulaani ovyo kumekatazwa katika Uislamu. Mtu anapolaani wengine anakuwa amejisahau kuwa naye ni mkosaji. Mtume (s.a.w) ametukataza kulaani ovyo katika Hadithi zifuatazo:



Ibn ‘Umar (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: “Si sawa kwa Muumini kuwa mkubwa wa kulaani”. Na katika upokezi mwingine, Mtume amesema, “Si stahiki ya Muumini kuwa mkubwa wa kulaani”. (Tirm idh).



Abu Dard (r.a) amesimulia kuwa amemsikia Mtume wa Allah akisema: “Watu wenye mazoea ya kulaani hawatakuwa mashahidi wala wenye kushufaia katika siku ya Kiyama ”. (Muslim).



Ibn Abbas (ra) ameeleza kuwa upepo ulipeperusha nguo ya mtu. Kwa hiyo aliulaani (upepo). Mtume wa Allah (saw) alisema ; “Usiulaani kwa sababu umeamrishwa ufanye hivyo na kwa sababu laana inakurudia mwenye kulaani kitu kisichostahiki kulaaniwa (kisicho na hatia). (Tirmidh na Abu-Daud).



Muislamu anatakiwa ajiepushe na tabia ya kulaani na badala yake awe mwingi wa kuwasamehe wenye kumkosea na kuwatakia msamaha kwa Allah (s.w) ili naye asamehewe dhambi zake.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 891

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

MTAZAMO NA HUKUMU YA KUPANGA UZAZI WA MPANGO KWENYE UISLAMU

Atika uislamu swala la kupanga uzazi linaruhusiwa endapo kutakuwa na sababu maalumu za kisheria.

Soma Zaidi...
Taratibu za kufanya kazi na kuajiri katika uislamu

Post hii itakufundisha taratibu za kuajiri, kufanya kazi na malipo.

Soma Zaidi...
Sifa za imamu wa swala ya jamaa

Post hii inakwenda kukupa sifa za imamu wa msikitini anayepasa kuswalisha swala ya jamii.

Soma Zaidi...
Sunnah za funga ya ramadhan

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Yaliyo haramu kwa mtu asiyekuwa na udhu

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu mambo ambauo ni haramu kwa mtu asiye na udhu.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kiswali swwla ya dhuha na faida zake

Post hii inakwenda kukufunza kuhusu swala ya dhuha, faida zake wakati wa kuiswali swala ya dhuha na jinsi ya kuiswali.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kutwaharisha aina mbalimbali za najisi

Kila najisi ina namna yake ya kutwaharisha, hata hivyo namna hizo hufanana. Katika post hii utakwenda kujifunza jinsi ya kutwaharisha najisi mbalimbali.

Soma Zaidi...