Uislamu unakataza mtu kulaani hovyo

20.

Uislamu unakataza mtu kulaani hovyo

20. Kuepukana na Kulaani Ovyo



Kulaani ovyo kumekatazwa katika Uislamu. Mtu anapolaani wengine anakuwa amejisahau kuwa naye ni mkosaji. Mtume (s.a.w) ametukataza kulaani ovyo katika Hadithi zifuatazo:



Ibn ‘Umar (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: “Si sawa kwa Muumini kuwa mkubwa wa kulaani”. Na katika upokezi mwingine, Mtume amesema, “Si stahiki ya Muumini kuwa mkubwa wa kulaani”. (Tirm idh).



Abu Dard (r.a) amesimulia kuwa amemsikia Mtume wa Allah akisema: “Watu wenye mazoea ya kulaani hawatakuwa mashahidi wala wenye kushufaia katika siku ya Kiyama ”. (Muslim).



Ibn Abbas (ra) ameeleza kuwa upepo ulipeperusha nguo ya mtu. Kwa hiyo aliulaani (upepo). Mtume wa Allah (saw) alisema ; “Usiulaani kwa sababu umeamrishwa ufanye hivyo na kwa sababu laana inakurudia mwenye kulaani kitu kisichostahiki kulaaniwa (kisicho na hatia). (Tirmidh na Abu-Daud).



Muislamu anatakiwa ajiepushe na tabia ya kulaani na badala yake awe mwingi wa kuwasamehe wenye kumkosea na kuwatakia msamaha kwa Allah (s.w) ili naye asamehewe dhambi zake.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 856

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Jinsi ya kuswali kuswali swala ya maiti

Post hii itakufundisha kuhusu swala ya maiti, nguzo za swala ya maiti, sharti za swwla ya maiti na jinsi ya kuiswali.

Soma Zaidi...
Maana ya hadathi na aina zake

Post hii inakwenda kukugundisha maana ya hadathi pamoja na kutaja aina za hadathi

Soma Zaidi...
Watu hawa huruhusiwi kuwaoa katika uislamu

Hapa utajifunza watu ambao ni halali kuwaoa na wale ambao ni haramu kuwaoa.

Soma Zaidi...
Ni zipi najisi katika uislamu

Post hii inakwenda kukupa orodha ya vitu vilivyo najisi.

Soma Zaidi...
Maneno mazuri mbele ya mwenyezi Mungu

kuna adhkari nyingi sana ambazo Mtume wa Allah ametutaka tuwe tunadumu nazo. lajkini kuna adhkari ambayo imekusanya maneno matukufu na yanayopendwa sana na Allah.

Soma Zaidi...