20.
20. Kuepukana na Kulaani Ovyo
Kulaani ovyo kumekatazwa katika Uislamu. Mtu anapolaani wengine anakuwa amejisahau kuwa naye ni mkosaji. Mtume (s.a.w) ametukataza kulaani ovyo katika Hadithi zifuatazo:
Ibn ‘Umar (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: “Si sawa kwa Muumini kuwa mkubwa wa kulaani”. Na katika upokezi mwingine, Mtume amesema, “Si stahiki ya Muumini kuwa mkubwa wa kulaani”. (Tirm idh).
Abu Dard (r.a) amesimulia kuwa amemsikia Mtume wa Allah akisema: “Watu wenye mazoea ya kulaani hawatakuwa mashahidi wala wenye kushufaia katika siku ya Kiyama ”. (Muslim).
Ibn Abbas (ra) ameeleza kuwa upepo ulipeperusha nguo ya mtu. Kwa hiyo aliulaani (upepo). Mtume wa Allah (saw) alisema ; “Usiulaani kwa sababu umeamrishwa ufanye hivyo na kwa sababu laana inakurudia mwenye kulaani kitu kisichostahiki kulaaniwa (kisicho na hatia). (Tirmidh na Abu-Daud).
Muislamu anatakiwa ajiepushe na tabia ya kulaani na badala yake awe mwingi wa kuwasamehe wenye kumkosea na kuwatakia msamaha kwa Allah (s.w) ili naye asamehewe dhambi zake.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Post hii itakufundisha kuhusu swala ya kupatwa yaani kupatwa kwa juwa na kupatwa kwa mwezi swalat kusuf na swalat khusuf
Soma Zaidi...Talaka Kabla ya Jimai:Mwanamume au mwanamke anaweza kughairi na kuamua kuvunja ndoa mapema kabla ya kufanya tendo Ia ndoa.
Soma Zaidi...Hapa utajifunza njia ambazo nenk ya kiislamu hutumia ili kujiendesha
Soma Zaidi...Fahamu darsa mbalimbali za fiqh kama swala, twahara, zaka pamoja na funga. Zijuwe sharti za swala, funga na zaka.
Soma Zaidi...Ugawaji wa mirathi-Mume ana nusu (1/2) = 1/2 -Mama ana sudusi.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukufunza kuhusu swala ya dhuha, faida zake wakati wa kuiswali swala ya dhuha na jinsi ya kuiswali.
Soma Zaidi...