Vituo vya kunuia hijjah au umrah
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
- Vituo vya Kunuia Hijja au Umrah.
- Miiqaat, ni vituo vya kunuia Hijjah na Umrah.
- Vituo vitano alivyoviweka Mtume (s.a.w) ni;
- Zul-Hulaifa (Bir-‘Ali).
- Ni cha watu watokao Madinah, kiko kilometa 450 kutoka Makkah.
- Juhfah (Rabigh).
- Ni cha watu watokao Misri na Syria, kiko kilometa 187 kaskazini-magharibi ya Makkah.
- Qurnul-Manaazil (Sail).
- Ni kituo cha watu watokao Najd, kiko kilometa 94 mashariki ya Makkah.
- Makkah.
- Ni kituo cha wakazi wa Makkah na wale wanao nuia Hija mwezi 8, Dhul-Hijah.
- Yalamlam.
- Ni kituo cha watu watokao Yemen, Afrika Mashaiki na Afrika Kusini, kiko kilometa 54 kusini-magharibi ya Makkah.
- Dhaaru-Iraq.
- Ni kituo cha watu kutoka Iraq, Iran, n.k., alichokiweka Khalifah Umar Ibn Khatwaab (r.a) wakati wa ukhalifah wake.
- Kiko kilometa 94 kaskazini –mashariki ya Makkah.
- Jiddah.
- Ni kituo cha wasafiri wa ndege, kiko kilometa 72 kusini ya Makkah.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 ai web app 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
JIFUNZE FIQH
Fahamu darsa mbalimbali za fiqh kama swala, twahara, zaka pamoja na funga. Zijuwe sharti za swala, funga na zaka.
Soma Zaidi...Taratibu za mahari katika uislamu
Hapa utajifunza taratibu za kutaja mahari katika uislamu.
Soma Zaidi...