Vituo vya kunuia hijjah au umrah
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
- Vituo vya Kunuia Hijja au Umrah.
- Miiqaat, ni vituo vya kunuia Hijjah na Umrah.
- Vituo vitano alivyoviweka Mtume (s.a.w) ni;
- Zul-Hulaifa (Bir-‘Ali).
- Ni cha watu watokao Madinah, kiko kilometa 450 kutoka Makkah.
- Juhfah (Rabigh).
- Ni cha watu watokao Misri na Syria, kiko kilometa 187 kaskazini-magharibi ya Makkah.
- Qurnul-Manaazil (Sail).
- Ni kituo cha watu watokao Najd, kiko kilometa 94 mashariki ya Makkah.
- Makkah.
- Ni kituo cha wakazi wa Makkah na wale wanao nuia Hija mwezi 8, Dhul-Hijah.
- Yalamlam.
- Ni kituo cha watu watokao Yemen, Afrika Mashaiki na Afrika Kusini, kiko kilometa 54 kusini-magharibi ya Makkah.
- Dhaaru-Iraq.
- Ni kituo cha watu kutoka Iraq, Iran, n.k., alichokiweka Khalifah Umar Ibn Khatwaab (r.a) wakati wa ukhalifah wake.
- Kiko kilometa 94 kaskazini –mashariki ya Makkah.
- Jiddah.
- Ni kituo cha wasafiri wa ndege, kiko kilometa 72 kusini ya Makkah.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 web hosting 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 ai web app 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Mda wa mwisho wa kula daku mwezi wa ramadhani
Post hii fupi itakwenda kukujulisha utaratibu wa kula daku.
Soma Zaidi...