Haki na wajibu kwa mayatima

Haki na wajibu kwa mayatima

Wajibu kwa Mayatima



Yatima ni mtoto aliyefiwa na wazazi wake, hasa baba, kabla ya kufikia baleghe. Uislamu unatuhimiza kuwatendea wema yatima na kuwatunzia urithi wao kwa uadilifu mpaka wafikie baleghe yao na kuwa na akili ya kutunza mali.


"... Na wanakuulizajuu ya mayatima: Sema: Kuwatendea mema ndivyo vizuri. Na kama mkichanganyika nao (ndivyo vyema vile vile) ,kwani ni ndugu zenu..." (2:220)
Tunajifunza kutokana na aya hii kuwa tunatakiwa tuwatendee wema mayatima na tuishi nao katika familia kama tunavyoishi na watoto wetu. Kukaa nao pamoja kwa huruma na mapenzi kutawafariji na kuziba pengo Ia kufiwa na mzazi au wazazi wao. Si katika mwenendo wa Kiislamu kuwatenga mayatima kwenye makazi maalumu. Tuishi nao katika familia zetu na tuwasomeshe katika shule wanazosoma watoto wetu.



Kuwanyanyasa mayatima ni katika madhambi makubwa mbele ya Allah (s.w). Si muumini wa kweli yule anayemnyanyasa yatima kama tunavyojifunza katika Qur-an:


".Je, umemuona yule anayekadhibisha dini (asiyeamini malipo ya akhera)? Huyo ni yule anayemsukuma (anayemnyanyasa) yatima." (107:1-2)



Msisitizo wa kuwatendea wema mayatima pia tunaupata katika hadith zifuatazo:
Abu Hurairah (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: "Kaya (familia) bora kuliko zote ni ile ambamo anatendewa wema yatima; na kaya mbovu kuliko zote ni ile ambamo ananyanyaswa yatima." (Ibn Majah)



Sahl bin Sa 'ad (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: 'Mimi na yule anayemlea yatima (kwa wema), akiwa wa kwake au kwa wengine, tutakuwa naye peponi kama hivi - akionyesha kidole cha mwanzo (cha shahada) na kinachofuatia (cha kati) huku vikiwa vimeshikamana bila ya kuachana mwanya wowote ". (Bukhari)
Kuwatendea wema mayatima ni pamoja na kuwatunzia mali zao za urithi kwa uadilifu kama inavyosisitizwa katika Qur-an:


"Na wapeni mayatima mali zao. Wala msibadilishe kibaya kwa kizuri. Wala msile mali zao pamoja na mali zenu. Hakika (yote) hayo nijukumu kubwa." (4:2)



Na wajaribuni mayatima (wanapokuwa karibu ya kubaleghe kama wataweza kutumia fedha zao vizuri wakati watakapobaleghe. Wajaribuni kidogo kidogo) mpaka wafike wakati wa kuoa (kubaleghe). Kama mkiwaona wana akili njema, wapeni mali zao. Wala msizile kwa fujo na kwa haraka ya kwamba watakua (wazitake; hebu tuzile upesi). Na mwenye kuwa tajiri basi ajiepushe (na kuchukua ujira katika kuwafanyia kazi zao). Na atakayekuwa mhitaji basi ale kwa namna inayokubaliwa na Sharia. Na mtakapowapa mali zao, basi wawekeeni mashahidi (/uu ya kuwa Mwenyezi Mungu anatosha kuwa shahidi. (4:6)


Hakika wale ambao wanakula mali ya mayatima kwa dhuluma, bila shaka wanakula moto matumboni mwao; na wataungua katika huo Moto (wa Jahannam) uwakao. (4:10)
Kutokana na aya hizi tunahimizwa kutunza mali za mayatima mpaka watakapofikia umri stahiki ndio tuwakabidhi. Kama tuna uwezo tusitumie chochote kutokana na mali hiyo katika kuwalea. Kama hatuna uwezo tunaruhusiwa tuitumie katika kuwapa mahitaji ya lazima kama vile Elimu, mavazi, n.k; lakini vile vile kwa tahadhari na ungalifu.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1406

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Dhana ya mirathi na kurithi katika zama za ujahiliya

Mirathi katika jamii za kijahiliKatika jamii nyingi za kijahili kama vile jamii ya Waarabu kabla ya Mtume Muhammad (s.

Soma Zaidi...
Lengo la kusimamisha swala kwa mwanadamu

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu lengo la kusimamisha swala.

Soma Zaidi...
Ni ipi hukumu ya kutoa talaka hali ya kuwa umelazimishwa au ukiwa umerukwa na akili

Endapo mtu atamuacha mke pasi na ridhaa yake yaani amelazimishwa ama amemuwacha wakati amerukwa na akili. Je ni ipo hukumu yake.

Soma Zaidi...
Mambo yaliyo haramu kwa mwenye hedhi na nifasi

Katika post hii utakwenda kujifunza mambo ambayo ni haramu kwa mwanamke aliye na hedhi na nifasi

Soma Zaidi...
MARADHI MENGINE 10 YANAYOTOKANA NA MBU ( matende, ngirimaji, homa ya manjano, n.k

Tofauti na maradhi yaliyotajwa hapo juu pia tafiti za kisayansi zimethibitisha kuwepo kwa maradhi mengine hatari yanayosambazwa na mbu, kama vile ngirimaji pamoja na matende.

Soma Zaidi...
Mambo yanayoweza kutoa udhu wako

Post hii itakufundisha mambo ambayo yanabatilisha udhu.

Soma Zaidi...
Namna ya kutawadha yaani kuchukuwa udhu

Kuchukuwavudhu ni ibada, lakini pia ni matendo ya kuufanya mwilivuwe safi. Katika post nitakwenda kukifundisha namna ya kutia udhu katika uislamu.

Soma Zaidi...