Menu



Mtoto wa tajiri na mtoto wa maskini ( sehemu ya nne)

Post hii inahusu zaidi watoto Hawa wawili wakiwa kwenye kituo cha mapumziko ambapo mtoto wa tajiri anabugia soda aliyopewa na yule mwalimu pia tumbo linaanza tena na anaanza kuendesha

Mtoto wa tajiri na mtoto wa maskini .

1. Basi baada ya wale watoto wawili kukutana na mwalimu wa Ile shule, Hawa watoto hawakujua kwamba ni mwalimu Bali ni msamaria mwema tu, basi watoto Hawa walinunuliwa soda , mtoto wa maskini kwa sababu alikuwa na kiasi na wazazi wake walimwambia kwamba asitumie vitu vya kula njiani  kwa mara nyingi alitunza Ile soda ila mtoto wa tajiri kwa sababu ya kula kula kila mara alibugia Ile soda na kwa sababu tumbo lilikuwa halijakaa vizuri alianza kuendesha tena.

 

2. Basi yule mtoto badala ya kukimbilia chooni alijichafua kwenye nguo zake na akasubilia kusafishwa kama kawaida yake , Bali yule mwalimu alimwambia mwanangu hauko nyumbani na pia wazazi wako hawapo hapa jikaze ujisafishe kwa sababu yule mtoto wa maskini aliona jinsi wale makonda walivyomsafisha na yeye akachukua maji akammwagia maji na mwalimu akamwambia ajisafishe na yeye akajisafisha na kwa sababu ilikuwa usiku kidogo baridi lilikuwa ni kama lote  mwalimu akamwonea huruma akaamua kumuomba number ya wazazi wake na kuwapigia.

 

3. Basi baada ya kusikia sauti ya wazazi wake alilia kwa sauti kubwa na kuanza kusema kwa nini mmenitesa kwa nini hamkunifundisha maisha na mbona watoto wenzangu hawana shida hapa mimi mtaniua kama maisha ni hivi hamjanitendea haki mwenzangu aliambiwa kila kitu hata hajaaibika hata kidogo na wazazi wakalaumiana wao kwa wao, basi mtoto akasema sitapanda tena gari la jumla nataka gari la binafsi , kwa sababu baba Ela zilikuwepo aliongea na yule mwalimu Ili wakodi gari la binafsi na yule mtoto wa maskini pamoja na yule mwalimu walikodiwa gari na wakasafiri mpaka shuleni, yule mtoto wa tajiri alifurahi sana na yule mtoto wa maskini alikuwa akishangaa kila kitu.

 

4. Basi baada ya kufika pale shuleni mwalimu akajitambulisha wazi kwamba yeye ni mkuu wa shule pale yule mtoto wa tajiri aliumia sana kwa sababu alikuwa hataki kuhaibika na akikumbuka alichokifanya shuleni, kwa hiyo wanafunzi wakapelekwa bwenini, wakaweka vitu vyao mwalimu alishangaa kuona mtoto wa maskini akiwa na ki mzima kidogo na mtoto wa tajiri ana kila kitu na begi kubwa na ka thamani kubwa kwa hito mwalimu akaona tofauti kati ya wake watoto kati ya vitu walivyonavyo na kati ya tabia zao. 

 

5. Basi wakapelekwa mezani kupata chakula wakakuta ni ugali wa Dona maharage na pia maji ya kunywa , yule mtoto wa maskini akamshukuru Mungu kwa kuona chakula cha aina Ile na mtoto wa tajiri aliangua kilio kuona chakula kile kwa sababu alikuwa hajawahi kuona na watu wote wakaamka na wafanyakazi wakashangaa yule mtoto.

Itaendelea

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea

Ndio     Hapana     Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Jamvini Main: Post File: Download PDF Views 1487

Share On:

Facebook WhatsApp

Post zinazofanana:

WAKATI WA KUFUMBUKA SEHEMU YA 1

Post hii inahusu zaidi hadithi mpya na nzuri inayoitwa wakati wa Kufumbuka, ni hadithi inayohusu maisha ya kawaida ambapo watu ushindwa kudhamini watu wa karibu nao na kuona watu wa mbali ndio wenye maana ila shida zikifika ndipo wanaona umuhimu wao.

Soma Zaidi...
Hadithi za alif lela u lela

Haya ni masimulizi ya Hadithi za alif lela u lela

Soma Zaidi...
Mwendelezo wa hadithi ya mahusiano ya vijana wawili

Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya mahusiano ya vijana wawili baada ya kuhamia shule mpya.

Soma Zaidi...
USALITI (sehemu ya tatu)

Post hii ni mwendelzo wa hadithi ya ukweli ambayo imetokea siku sio nyingi jinsi Moses alipoacha kumwoa Rhoda naye akachanganyikiwa takribani miaka kama mitano hivi.

Soma Zaidi...
Mafundisho kutokana na hadithi ya Binti mfalme

Posti hii inahusu zaidi mafundisho ambayo tunayapata kutoka kwa binti mfalme, tunapotoa hadithi sio kusoma na kufurahia tu ila kuna mafundisho muhimu katika maisha yetu.

Soma Zaidi...
Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili

Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili, hapa tunaona Jackie anajibu barua ya Julius kwa kusema yafuatayo.

Soma Zaidi...
Usichofahamu kuhusu mazoezi

Posti hii inahusu zaidi mambo muhimu ambayo hufahamu kuhusu mazoezi,ni mambo ambayo utokea au no matokeo mazuri kwa watu wanaofanya sana mazoezi.

Soma Zaidi...
Hadithi katika kijiji cha burugo

 Posti hii inahusu zaidi jinsi ya watu walivyoishi katika kijiji cha burugo .tunajuwa hadithi ni sehemu mojawapo ya kubirudisha na kujifunza kitu flani kutoka kwenye jamii .

Soma Zaidi...
Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili

Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili, kuhusu hadithi hii ni pale Jackie anaandikiwa barua na Julius ili apotezwe akili na wavulana wengine kwa sababu Jackie aliwapita darasani.

Soma Zaidi...
Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili

Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili,ambapo Mama yake na Jackie pamoja na jack wakiwa hospital na jack anaendelea kumwita Julius kila mara.

Soma Zaidi...