Mtoto wa tajiri na mtoto wa maskini ( sehemu ya nne)


image


Post hii inahusu zaidi watoto Hawa wawili wakiwa kwenye kituo cha mapumziko ambapo mtoto wa tajiri anabugia soda aliyopewa na yule mwalimu pia tumbo linaanza tena na anaanza kuendesha


Mtoto wa tajiri na mtoto wa maskini .

1. Basi baada ya wale watoto wawili kukutana na mwalimu wa Ile shule, Hawa watoto hawakujua kwamba ni mwalimu Bali ni msamaria mwema tu, basi watoto Hawa walinunuliwa soda , mtoto wa maskini kwa sababu alikuwa na kiasi na wazazi wake walimwambia kwamba asitumie vitu vya kula njiani  kwa mara nyingi alitunza Ile soda ila mtoto wa tajiri kwa sababu ya kula kula kila mara alibugia Ile soda na kwa sababu tumbo lilikuwa halijakaa vizuri alianza kuendesha tena.

 

2. Basi yule mtoto badala ya kukimbilia chooni alijichafua kwenye nguo zake na akasubilia kusafishwa kama kawaida yake , Bali yule mwalimu alimwambia mwanangu hauko nyumbani na pia wazazi wako hawapo hapa jikaze ujisafishe kwa sababu yule mtoto wa maskini aliona jinsi wale makonda walivyomsafisha na yeye akachukua maji akammwagia maji na mwalimu akamwambia ajisafishe na yeye akajisafisha na kwa sababu ilikuwa usiku kidogo baridi lilikuwa ni kama lote  mwalimu akamwonea huruma akaamua kumuomba number ya wazazi wake na kuwapigia.

 

3. Basi baada ya kusikia sauti ya wazazi wake alilia kwa sauti kubwa na kuanza kusema kwa nini mmenitesa kwa nini hamkunifundisha maisha na mbona watoto wenzangu hawana shida hapa mimi mtaniua kama maisha ni hivi hamjanitendea haki mwenzangu aliambiwa kila kitu hata hajaaibika hata kidogo na wazazi wakalaumiana wao kwa wao, basi mtoto akasema sitapanda tena gari la jumla nataka gari la binafsi , kwa sababu baba Ela zilikuwepo aliongea na yule mwalimu Ili wakodi gari la binafsi na yule mtoto wa maskini pamoja na yule mwalimu walikodiwa gari na wakasafiri mpaka shuleni, yule mtoto wa tajiri alifurahi sana na yule mtoto wa maskini alikuwa akishangaa kila kitu.

 

4. Basi baada ya kufika pale shuleni mwalimu akajitambulisha wazi kwamba yeye ni mkuu wa shule pale yule mtoto wa tajiri aliumia sana kwa sababu alikuwa hataki kuhaibika na akikumbuka alichokifanya shuleni, kwa hiyo wanafunzi wakapelekwa bwenini, wakaweka vitu vyao mwalimu alishangaa kuona mtoto wa maskini akiwa na ki mzima kidogo na mtoto wa tajiri ana kila kitu na begi kubwa na ka thamani kubwa kwa hito mwalimu akaona tofauti kati ya wake watoto kati ya vitu walivyonavyo na kati ya tabia zao. 

 

5. Basi wakapelekwa mezani kupata chakula wakakuta ni ugali wa Dona maharage na pia maji ya kunywa , yule mtoto wa maskini akamshukuru Mungu kwa kuona chakula cha aina Ile na mtoto wa tajiri aliangua kilio kuona chakula kile kwa sababu alikuwa hajawahi kuona na watu wote wakaamka na wafanyakazi wakashangaa yule mtoto.

Itaendelea



Sponsored Posts


  πŸ‘‰    1 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       πŸ‘‰    2 Madrasa kiganjani offline       πŸ‘‰    3 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       πŸ‘‰    4 Jifunze Fiqh    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms βœ‰ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Siri ya kifo yafichuka
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

image Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili
Post hii inahusu zaidi hadithi ya vijana wawili ambapo mitihani inaisha na wanaanza kuhukumiwa mmoja baada ya mwingine. Soma Zaidi...

image Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili
Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili, kuhusu hadithi hii ni pale Jackie anaandikiwa barua na Julius ili apotezwe akili na wavulana wengine kwa sababu Jackie aliwapita darasani. Soma Zaidi...

image Mwendelezo wa hadithi ya Mama mchoyo na mwehu
Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Mama mchoyo na mwehu, kwa sababu mwehu alikuwa mkarimu alichukua ule mkate akawapstia watoto wa yule mama wakiwa wanatoka shule kwa hiyo tutaona kilichotokea kwa wale watoto. Soma Zaidi...

image Malipo ya wema ni wema
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

image Safari ya nne ya Sinbad
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

image Hadithi ya mzee wa tatu na mbwa wake mwekundu
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

image Binti wa ndotoni
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

image Alif lela ulela
Posti hii inakwenda kukusimulia hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

image Hadithi katika kijiji cha burugo
Β Posti hii inahusu zaidi jinsi ya watu walivyoishi katika kijiji cha burugo .tunajuwa hadithi ni sehemu mojawapo ya kubirudisha na kujifunza kitu flani kutoka kwenye jamii . Soma Zaidi...