Je inafaha kuingizwa eda na kutolewa?

Kuingizwa au Kutolewa EdaKatika sheria ya Kiislamu hapana suala Ia kuingizwa au kutolewa eda na Sheikh.

Je inafaha kuingizwa eda na kutolewa?

Kuingizwa au Kutolewa Eda
Katika sheria ya Kiislamu hapana suala Ia kuingizwa au kutolewa eda na Sheikh. Kizuka huanza eda baada tu ya kufariki mumewe na eda yake huisha mara tu baada ya muda wa miezi mine na siku kumi kuisha. Wala hapana vazi maalum Ia kukalia eda. Si nguo nyeupe, wala nyeusi, wala kuvaa matambara kama baadhi ya watu wanavyoitakidi. Mwanamke mfiwa atabakia nyumbani kwa mumewe au kwa warithi wa mumewe katika sitara kama kawaida anavyotakiwa awe mwanamke yeyote wa Kiislamu na ataendelea kufanya shughuli zake za nyumbani na nje ya nyumbani zilizo katika mipaka ya sheria ya Kiislamu. Wala hapana sheria yoyote ya kukaa nyumbani kivivu-vivu kama wanavyoitakidi watu wengine.



Hekima kubwa ya kuamrishwa kizuka kukaa eda, pamoja na haja ya kuangaliwa uwezekano wa kuachwa na mimba, kunampa kizuka nafasi ya kutulizana na kuliwazika baada ya kupatwa na msiba mkubwa kiasi hicho. Pamoja na kuwa mwanamke baada ya kipindi cha eda huwa huru kutoka nyumbani kwa mumewe marehemu na kuolewa na mume mwingine, akitaka kubakia katika nyumba ya mumewe pamoja na watoto wake, ana haki kisheria kama tunavyojifunza katika aya ifuatayo:


Na wale waliofishwa miongoni mwenu na wakawacha wake, wawausie (warithi wao) kwa ajili ya wake zao kupata matumizi ya mwaka mmoja bila ya kutolewa (katika nyumba za waume zao). Na kama wanawake wenyewe wakiondoka, basi si kosa juu yenu kwa yale waliyoyafanya kwa nafsi zao



wenyewe yanayofuata sharia. Na Mwenyezi Mungu ni mwenye nguvu, mwenye hi/dma. (2:240).
Katika baadhi ya jamii za kijahili pamekuwa na mtindo wa kuwarithi wanawake waliofiwa na waume zao kama mali inavyorithiwa na jamaa wa marehemu. labia hii ya kumdhalilisha mwanamke na kumnyima uhuru wake wa kuolewa na mwanamume ampendaye imepigwa marufuku katika sheria ya Kiislamu kama tunavyojifunza katika aya ifuatayo:


Enyi mlioamini! Si halali kwenu kurithi wanawake kwa jeuri. Wala msiwazulie (kuolewa na waume wengine) iii mpate kuwanyang 'anya baadhi ya vile mlivyowapa (katika urithi wa waume zao...) (4:19)



Ama mwanamke mjane mwenyewe akiridhika kuolewa na ndugu au jamaa wa marehemu mumewe, ili aweze kubakia pale na watoto wake hapana ubaya ili mradi tu wafunge ndoa kama ilivyo katika sheria.





                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 849

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Jinsi ya kuzika maiti wa kiislamu hatuwa kwa hatuwa

Post hii itakufundisha taratibu za kuzika maiti wa kiislamu hatuwa kwa hatuwa.

Soma Zaidi...
Ufafanuzi kuhudu mgogoro wa mwezi ni muda gani mtu aanze kufunga.

Je inapoonekana sehemu moja tufunge duania nzima ama tufunge kwa kuangalia mwandamo katika maenro tunayoishi.

Soma Zaidi...
Kusimamisha swala.

Kwenye kipengele hiki tutajifunza maana ya swala ni nin?. Na masharti ya swala.

Soma Zaidi...
Umuhimu na msisitizowa zakat na sadaqat katika uislamu

Nguzo za uislamu,umuhimu na msisitizowa zakat na sadaqat katika uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Dhamana ya Kuchunga Ahadi Katika Uislamu

Kuchunga au kutekeleza ahadi ni miongoni mwa vipengele muhimu vya tabia ya muumini wa kweli.

Soma Zaidi...
MTAZAMO NA HUKUMU YA KUPANGA UZAZI WA MPANGO KWENYE UISLAMU

Atika uislamu swala la kupanga uzazi linaruhusiwa endapo kutakuwa na sababu maalumu za kisheria.

Soma Zaidi...
Ni upibutaratibu wa kuingia eda na kutoka eda

Katika uislamu hakuna sheria ya mwanamke kuingizwa eda na kutolewa eda kama ilivyozoeleka. Endelea na post hii ujifunze zaidi

Soma Zaidi...
MAANA YA ZAKA NA SADAKA KULUNGA NA KISHERIA PAMOJA NA TOFAUTI ZAO

MAANA YA ZAKA NA SADAKA KULUNGA NA KISHERIA PAMOJA NA TOFAUTI ZAO.

Soma Zaidi...
NI ZIPI NGUZO NA SHARTI KUU ZA SWALA ILI IKUBALIWE

Sharti za SwalaSharti za Swala Sharti za swala ni yale mambo ya lazima anayotakiwa Muislamu ayachunge na kuyatekeleza kabla hajaanza kuswali.

Soma Zaidi...