Eda ya kufiwa na hukumu zake

Eda ya kufiwa na hukumu zake

Eda ya Kufiwa


Eda ni kipindi cha kungojelea mwanamke baada ya kupewa talaka au baada ya kufiwa na mumewe. Katika kipindi cha eda ni haramu mwanamke kuolewa na mume mwingine. Ambapo tumejifunza kuwa eda ya kuachwa inaisha baada ya twahara tatu au miezi mitatu (kwa wale wasiopata hedhi) au baada ya kujifungua (kwa mke aliyeachwa), eda ya kuachwa inachukua miezi minne na siku kumi au siku mia moja thelathini (130).


Hukumu ya Eda ya kufiwa inabainishwa katika Qur-an:

Na wale wanaofishwa (wanaokufa) miongoni mwenu na kuacha wake; hawa (wake) wangoje (wasiolewe) miezi mine na siku kumi. Na wanapofikia muda wao (wa kumaliza eda yao hiyo), basi si dhambi juu yenu kwa yale wanayoyafanyia nafsi zao (hao wanawake) kwa yanayowafiki (kufuata) Sharia. Na Mwenyezi Mungu anazo habari za yote mnayoyatenda. Wala Si dhambi kwenu katika kupeleka habari ya posa kwa ishara tu (Si kwa maneno) kuwaoa wake (walio edani), wala (hapana dhambi pia) katika kutia katika nyoyo zenu azma (za kuwaoa) Mwenyezi Mungu anajua kwamba nyinyi mtawakumbuka.

Lakini msifunge nao ahadi kwa Sifl (ya kuwaoa maadam eda haijesha) isipokuwa mseme maneno yaliyo mazuri. Wala msiazimie kufunga ndoa mpaka muda uliyoandikwa (katika eda) ufike mwisho wake. Na jueni ya kwamba Mwenyezi Mungu anayajua yaliyomo katika nafsi zenu, basi mwogopeni. Na jueni kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, (na) Mpole sana. (2:234-235)


Kutokana na aya hizi tunajifunza kuwa kizuka (mwanamke aliyefiwa na mumewe) anapokuwa katika eda harusiwi kuolewa wala hata kuposwa wala hata kudhihirishiwa nia ya kuolewa baada ya eda. Bali ni ruhusa kuweka azma moyoni na kuongea naye kwa wema bila kuidhihirisha azma hiyo.



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2383

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Dua za Mitume na Manabii    👉3 web hosting    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Ni nini maana ya swala

Post hii inakwenda kukugundisha kuhusu maana halisi ya ibada ya swala.

Soma Zaidi...
Twahara na umuhimu wake katika uislamu

Katika post hii utajifunza maana ya twahara kiligha na kishria. Pia utajifunza umuhimu wake

Soma Zaidi...
Kwanini funga imefaradhishwa mwezi wa ramadhani

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mambo yanayopunguza malipo ya funga au swaumu

Mambo haya yanaweza kuharibu funga ya mtu ama kupunguza malipo ya funga.

Soma Zaidi...
Mwenendo wa mwenye kunuia hijjah na umrah

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Yaliyo haramu kwa mtu asiyekuwa na udhu

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu mambo ambauo ni haramu kwa mtu asiye na udhu.

Soma Zaidi...
Swala ya witiri na faida zake, na jinsi ya kuiswali

Hapa utajifunza jinsi ya kuswali swala ya witiri na faida zake kwa mwenye kuiswali.

Soma Zaidi...
Funga ya ramadhan na nyinginezo

Nguzo za uislamu (EDK form 2; dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mtazamo wa uislamu juu ya ndoa ya mke zaidi ya mmoja

Je jamii inachukuliaje swala la kuoa mke zaidi ya mmoja.

Soma Zaidi...
Jinsi Uislamu Ulivyokomesha Biashara ya Utumwa wakati na baada ya Mtume Muhammad (s.a.w)

- Uislamu ulieneza nadharia kuwa wanaadamu wote ni sawa na wote ni watumwa mbele ya Mwenyezi Mungu (s.

Soma Zaidi...