MAANA YA ZAKA NA SADAKA KULUNGA NA KISHERIA PAMOJA NA TOFAUTI ZAO

MAANA YA ZAKA NA SADAKA KULUNGA NA KISHERIA PAMOJA NA TOFAUTI ZAO.

MAANA YA ZAKA NA SADAKA KULUNGA NA KISHERIA PAMOJA NA TOFAUTI ZAO

MAANA YA ZAKA NA SADAKA KULUNGA NA KISHERIA PAMOJA NA TOFAUTI ZAO.


Maana ya Zakat



Kilugha: Katika lugha ya Kiarabu neno “zakat” lina maana ya utakaso (Purification). Neno “Zakat” limetumika katika Qur’an kwa maana hii katika aya zifuatazo:
“Bila shaka amefuzu aliyeitakasa (nafsi yake)” (91 :9).
“Hakika ameshafuzu aliyejitakasa (na mabaya)” (8 7:14).


Kisheria: Katika sheria ya Kiislamu “Zakat” ni sehemu ya mali ya tajiri (2.5% au 1/40) anayoitoa kwa kutekeleza amri ya Allah (s.w) na kuwapa wanaostahiki, baada ya kupindukia mwaka au baada ya mavuno iwapo mali hiyo imefikia Nisaab. Nisaab ni kima cha chini cha mali ambacho mtu akiwa nacho au zaidi yake analazimika kutoa Zakat.



Maana ya Sadaqa



Kilugha: Katika lugha ya Kiarabu neno “Sadaqa” linatokana na “Sidiq” lenye maana ya ukweli.
Kisheria: Katika sheria ya Kiislamu Sadaqat ni mali au huduma iinayotolewa au kupewa mtu yoyote anayehitajia kwa ihsani tu bila ya kutarajia malipo yoyote kutoka kwake. Maana ya “Sadaqat” inabainishwa vizuri katika Hadithi zifuatazo:



1.Jabir na Hudhaifa (r.a) wameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: Kila kitendo kizuri ni Sadaqat”. (Bukhari na Muslim).



2.Abu Hurairah (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: Katika kila kiungo cha mtu kuna Sadaqat. Kuna Sadaqat katika kila mtu. Kufanya uadilifu kati ya watu wawili ni sadaqat; kumsaidia mtu kupanda mnyama wake anayesafiri naye au kumsaidia mtu kutwika mzigo wake ni sadaqat; neno zuri ni sadaqat na kila hatua mtu anayotembea kwenda kwenye swala ni sadaqat na kuondoa kitu kibaya njiani ni sadaqat”. (Bukhari na Muslim).



TOFAUTI YA ZAKA NA SADAKA


1. Zaka ni nguzo ya Uislamu na ni lazima, lakini dadaka si lazima


2. Zaka hutolewa kwa kiwango maalumu, lakini sadaka haina kiwango maalumu


3. Zaka hutolewa mali, lakini sadaka sio lazima iwe mali


4. Zaka hutolewa ndani ya muda maalumu, lakini sadaka haina muda maalumu


5. Zaka inatolewa kwa watu maalumu, lakini sadaka haijaelezewa watu maalumu wa kuwapatia.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 3812

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Hadathi ya kati na kati

Posti hiibinakwenda kukufundisha kuhusu hadathi ya kati na kati.

Soma Zaidi...
Nguzo za swala ya maiti

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Je ni kwa nini lengo la finga halifikiwi kwa wafungaji

Lengo la funga ni kuwa mchamungu sasa ni kwa nini wafungaji hawalifikii lengo hili na kuwa wachamungu.

Soma Zaidi...
Je ni nani mwenye haki ya kutaliki

Hapabutajifunza endapp mwanamke anahitaji kuachwa ni nini anatakiwa afanye.

Soma Zaidi...
Maana ya Funga ya ramadhani kisheria na Aina za funga

Amesema mtume (s.a.w) kuwa Allah (s.w) amesema: kila amali ya mwanaadamu ni kwa ajili yake isipokuwa funga.

Soma Zaidi...