MAANA YA ZAKA NA SADAKA KULUNGA NA KISHERIA PAMOJA NA TOFAUTI ZAO.
MAANA YA ZAKA NA SADAKA KULUNGA NA KISHERIA PAMOJA NA TOFAUTI ZAO.
Maana ya Zakat
        Kilugha: Katika lugha ya Kiarabu neno “zakat” lina maana ya utakaso (Purification). Neno “Zakat” limetumika katika Qur’an kwa maana hii katika aya zifuatazo:
        “Bila shaka amefuzu aliyeitakasa (nafsi yake)” (91 :9).
        “Hakika ameshafuzu aliyejitakasa (na mabaya)” (8 7:14). 
Kisheria: Katika sheria ya Kiislamu “Zakat” ni sehemu ya mali ya tajiri (2.5% au 1/40) anayoitoa kwa kutekeleza amri ya Allah (s.w) na kuwapa wanaostahiki, baada ya kupindukia mwaka au baada ya mavuno iwapo mali hiyo imefikia Nisaab. Nisaab ni kima cha chini cha mali ambacho mtu akiwa nacho au zaidi yake analazimika kutoa Zakat.
        Maana ya Sadaqa
        Kilugha: Katika lugha ya Kiarabu neno “Sadaqa” linatokana na “Sidiq” lenye maana ya ukweli.
        Kisheria: Katika sheria ya Kiislamu Sadaqat ni mali au huduma iinayotolewa au kupewa mtu yoyote anayehitajia kwa ihsani tu bila ya kutarajia malipo yoyote kutoka kwake. Maana ya “Sadaqat” inabainishwa vizuri katika Hadithi zifuatazo:
        1.Jabir na Hudhaifa (r.a) wameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: Kila kitendo kizuri ni Sadaqat”. (Bukhari na Muslim).
        2.Abu Hurairah (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: Katika kila kiungo cha mtu kuna Sadaqat. Kuna Sadaqat katika kila mtu. Kufanya uadilifu kati ya watu wawili ni sadaqat; kumsaidia mtu kupanda mnyama wake anayesafiri naye au kumsaidia mtu kutwika mzigo wake ni sadaqat; neno zuri ni sadaqat na kila hatua mtu anayotembea kwenda kwenye swala ni sadaqat na kuondoa kitu kibaya njiani ni sadaqat”. (Bukhari na Muslim).
TOFAUTI YA ZAKA NA SADAKA
1. Zaka ni nguzo ya Uislamu na ni lazima, lakini dadaka si lazima
2. Zaka hutolewa kwa kiwango maalumu, lakini sadaka haina kiwango maalumu
3. Zaka hutolewa mali, lakini sadaka sio lazima iwe mali
4. Zaka hutolewa ndani ya muda maalumu, lakini sadaka haina muda maalumu
5. Zaka inatolewa kwa watu maalumu, lakini sadaka haijaelezewa watu maalumu wa kuwapatia.
Umeionaje Makala hii.. ?
Taratibu za Kutaliki KiislamuKama palivyo na taratibu za kuoa Kiislamu ndivyo hivyo pia ilivyo katika kuvunja ndoa.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukupa sifa za imamu wa msikitini anayepasa kuswalisha swala ya jamii.
Soma Zaidi...Hapa utajifunza taratibu za kutaja mahari katika uislamu.
Soma Zaidi...