Wajibu wa Watoto kwa Wazazi
Wajibu wa watoto kwa wazazi wao ni kuwatii katika kiwango cha hali ya juu, kuwaheshimu na kuwahurumia hasa wanapokuwa wazee. Kuwatii wazazi ni kitendo kinachochukua nafasi ya juu sana katika Uislamu. Utii kwa wazazi huchukuwa nafasi baada tu ya Kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Msisitizo wa kuwatii wazazi, kuwaonea huruma na kuwafanyia ihsani uko wazi katika Qur-an:
Na Mola wako amehukumu kuwa msimuabudu yeyote ila Yeye tu. Na (ameagiza) kuwafanyia wema (mkubwa) wazazi. Kama mmoja wao akifikia uzee pamoja nawe, au wote wawili, usiwaambie hata A/i! Wala usiwakemee. Na useme nao kwa msemo wa heshima kabisa. Na uwainamishie bawa ?a unyenyekevu kwa (kuwaonea) huruma na useme: 'Mola wangu! Warehemu (wazee wangu) kama walivyonilea katika utoto ". (17:23-24).
Wazazi, hasa mama, wamestahiki kutiiwa kwa kiwango cha hali ya juu, kuwafanyia ihsani na kuhurumiwa na watoto wao hasa wanapokuwa wazee, iii iwe kama malipo ya kazi ngumu ya kuwalea watoto wao. Mtoto hana malipo ya kumlipa mzazi wake kwa kumzaa na kumlea mpaka kufikia utu uzima wake. Malipo anayotakiwa na Mwenyezi Mungu (s.w)
awalipe wazazi wake kwa taabu zote walizochukua katika kumlea ni kumshukuru Mwenyezi Mungu (s.w) na wazazi wake kwa kumtii Mwenyezi Mungu (s.w) na Mtume na kisha kuwatii wazazi wake, kuwafanyia ihsani na kuwahurumia kama tunavyojifunza katika Qur-an:
Na tumemuusia mwanaadamu (kuwafanyia ihsani) wazazi wake - mama yake amechukua mimba yake kwa udhafujuu ya udhafu na kumnyonyesha katika kipindi cha miaka miwili - (tumemuusia) ya kwamba unishukuru Mimi na wazazi wako, marejeo yenu ni kwangu. (31:14)
Na tumemuusia mwanaadamu afanye wema kwa wazazi wake,.Mama yake amechukua mimba yake kwa taabu. Na ku be ha mimba yake hata kumwachisha ziwa, (uchache wake) ni miezi thelathini (46:15). Pia mtoto mwema, pamoja na kuwatii na kuwahurumia wazazi wake kwa kuwapa kila msaada wanaohitajia, huwaombea dua wakiwa hai au wakiwa wametangulia kufa kwa kusema:
Mola wetu! Unighufirie mimi na wazazi wangu wote wawili na wanaoamini Siku ya Hisabu. (14:41). Utii kwa wazazi unatakiwa uendelezwe hata baada ya kufa kwao kama tunavyojifunza katika hadithi: Abu Usaydi as-Said (r.a) amesimulia: Tulikuwa karibu na Mtume (s.a.w) wakati alpomjia mtu wa ukoo wa Salimah na kumuuliza: Ee Mtume wa mwenyezi Mungu! Kuna utii
mwingine uliobakia kwa wazazi baada ya kutawafu kwao? "Ndio" alUibu Mtume. "Kuwaombea dua, kuwaombea msamaha na maghfira kwa Mwenyezi Mungu (s.w), kutekeleza wasia wao, kuwa na uhusiano mwema na wale mliofahamiana kutokana na wao na kuwaheshimu rafiki zao ". (Abu Daud, Ibn Majah)
Pia katika hadithi iliyosimuliwa na Ibn Umar mtume (s.a.w) amesema:
Utii wa hali ya juu kwa wazazi ni mtu kufanya urafiki na marafiki wa baba yake baada ya kufa kwake. (Muslim).
Hata hivyo, kiwango cha utii na huruma ya mtoto kwa wazazi wawili kinatofautiana. Mama anastahiki kupata nafasi ya kwanza ndio baba afuatie kama tunavyojifunza katika hadithi:
Abu Hurairah amesimulia kuwa mtu mmoja aliuliza: Ee Mtume wa Mwenyezi Mungu! Ni nani hasa anayestahiki upendo wangu wa hali ya juu? 'Mama yako ", alijibu Mtume. Kisha akauliza tena: Nani anayefuatia? "Mama yako ", alijibu Mtume. Akauliza tena: Nani anayefuatia? 'Mama yako ' alj/ibu Mtume. Katika maelezo mengine al/ibu Mtume: Mama yako, kisha mama yako, kisha mama yako, kisha baba yako, kisha jamaa zako wa karibu, (Bukhari na Muslim).
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download
Download NowJe! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu
Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Fiqh
Main: Post
File: Download PDF
Share On
Facebook
or
Whatsapp
Views 1921
Sponsored links
๐1
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
๐2
Kitabu cha Afya
๐3
Kitau cha Fiqh
๐4
kitabu cha Simulizi
๐5
Simulizi za Hadithi Audio
๐6
Madrasa kiganjani
Mwenendo wa mwenye kunuia hijjah na umrah
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
Kumuandaa Maiti kabla ya kufa ama kukata roho
Soma Zaidi...
Maana ya swala
Maana ya Swala Maana ya Swala kilugha(a) Kilugha Katika lugha ya Kiarabu neno ยSwalaatย lina maana ya ยombi au ยdua. Soma Zaidi...
NAMNA ZA ZAKA (AINA NA MGAWANYIKO WA ZAKA) ZAKA IPO MAKUNDI MANGAPI?
Soma Zaidi...
haki na hadhi za mwanamke katika jamii inayoishi kiislamu
Soma Zaidi...
Zijuwe nguzo tano za uislamu na maana zake katika sheria ya uislamu
Hili ni somo letu la kwanza kwenye mtiririko huu wa darsa za fiqh. Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya uislamu na nguzo zake. Soma Zaidi...
Haki, wajibu na majukumu katika familia ya kiislamu na majirani zake
Soma Zaidi...
Yanayofaa kwa maamuma katika kumfata imamu kwenye swala ya jamaa
Soma Zaidi...
Hizi ndio suna za swala kwa swala za faradhi na suna
Soma Zaidi...
Jinsi ya kutoa zakat al fitiri na umuhimu wa zakat al fitri kwa waislamu
Hapa utajifunza kuhusu zakat al fitiri, kiwango chake, watu wanaostahili kupewa na kutoa, pia umuhimu wake katika jamii. Soma Zaidi...