haki na wajibu kwa wakubwa

haki na wajibu kwa wakubwa

Wajibu wa Wakubwa kwa wadogo na wa Wadogo kwa Wakubwa



Katika utamaduni wa Kiislamu wakubwa kwa umri au kwa Maarifa au kwa mamlaka ya (uongozi), wanawajibika kuwahurumia, kuwapenda, kuwaongoza, kuwaelekeza, kuwashauri na kuwaasa wadogo zao kiumri au kimaarifa au mamlaka. Wakubwa wanawajibika kuwamrisha wadogo zao kufanya mema na wanawajibika kukataza maovu wenyewe wakiwa ni viigizo nyema. Kwa kutumia uzoefu wao wanawajibika kuwaelekeza na kuwaongoza katika njia iliyonyooka, wale walio chini yao kiumri na kimamlaka.
Kwa upande mwingine, wadogo kiumri au kimamlaka wanawajibika kuwatii na kuwaheshimu wale walio juu yao kama tunavyoamrishwa:


"Enyi mlioamini! Mtiini Mwenyezi Mungu na mtiini Mtume na wenye mamlaka juu yenu, walio miongoni mwenu.Na kama mkikhitilafiana juu ya jambo lolote basi lirudisheni kwa Mwenyezi Mungu na Mtume, ikiwa mnamwamini Mwenyezi na siku ya Mwisho. Hiyo ndiyo kheri nayo ma matokeo bora kabisa." (4:59).
Kutokana na aya hii tunawajibika kuwatii wakubwa zetu na wale wenye mamlaka juu yetu, baada ya kumtii Allah (s.w) na Mtume (s.a.w).


Lakini hatuwajibiki kuwatii wakubwa zetu na wenye mamlaka juu yetu kinyume na kumtii Allah (s.w) na Mtume (s.a.w).. Wale wenye mamlaka juu yetu wakituamrisha kumuasi Allah (s.w) na Mtume wake (s.a.w), tuwakatalie kwa heshima huku tukiwarejesha kwa mafundisho ya Qur-an na sunnah kuwa: "Hapana utii kwa kiumbe katika kumuasi Muumba."



Msisitizo wa kuwatii na kuwaheshimu wakubwa zetu kiumri na kimamlaka pia tunaupata katika Hadith zifuatazo:
Ibn Abbas (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: "Si katika sisi (si muumini) yule asiyewahurumia wadogo zetu na kuwaheshimu wakubwa zetu wala haamrishi mema na kukataza mabaya ". (Tirmidh)



Anas (r.a) anaeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: "Kama kijana atamuheshimu mtu mzima kutokana na umri wake, naye Allah atajaalia mtu atakayemheshimu katika uzee wake." (Tirmidh)



Pamoja na msisitizo wa kuwaheshimu wakubwa zetu, hatunabudi kuzingatia mipaka ya Uislamu katika kufanya hivyo. Wakati mwingine kuwaheshimu na kuwatii wakubwa kupita kiasi, hutupelekea kwenye shirk. Kwa kuchelea hili, Mtume (s.a.w) aliwakataza Waislamu kumsifu kupita kiasi kama wakristo walivyofanya kwa mwana wa Maryamu (Issa (a.s) na kumfanya mwana wa Mungu. Hivyo Mtume (s.a.w) ametuelekeza tumsifu kwa kumwita "Mja na Mtume wa Allah".



Pia kwa kuchelea shirk, Mtume (s.a.w) aliwakataza Waislamu wasimsimamie wakati akiingia kwenye mkutano au akipita njiani kama tunavyojifunza katika Hadith zifuatazo:
Anas (r.a) ameeleza: "Hapana mtu tuliyempenda kuliko Mtume wa Allah.Hatukuwa tunamsimamia kwa sababu alikuwa hapendi kusimamiwa." (Tirmidh)
Muawiyah (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: "Yeyote yule anayependa watu wamuheshimu kwa kumsimamia, atarajie kuwa mkazi wa motoni." (Tirmidh, Abu Daud)



Tunajifunza kutokana na Hadithi hizi kuwa "heshima" isipelekee kuwafanya wengine kuwa wanyonge na dhalili na wengine kuwa watukufu na bora. Tunapo heshimu au kuheshimiwa, hatunabudi kuiweka mbele yetu aya ifuatayo:


Enyi watu! Kwa hakika tumekuumbeni (nyote) kwa (yule) mwanamume (mmoja; Adamu) na (yule yule) mwanamke (mmoja; Hawa). Na tumekufanyeni matafa na makabila (mbali mbali) ili mjuane (tu basi siyo mkejeliane).Hakika ahishimiwaye sana miongoni mwenu mbele ya Mwenyezi Mungu ni yule amchaye Mungu zaidi katika nyinyi. Kwa yakini Mwenyezi Mungu ni Mjuzi, Mwenye habari (za mambo yote). (49:13)




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1465

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 web hosting    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Jinsi ya kutoa zakat al fitiri na umuhimu wa zakat al fitri kwa waislamu

Hapa utajifunza kuhusu zakat al fitiri, kiwango chake, watu wanaostahili kupewa na kutoa, pia umuhimu wake katika jamii.

Soma Zaidi...
Swala ya Istikhara na jinsi ya kuiswali

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu swala ya Istikhara

Soma Zaidi...
Ni upibutaratibu wa kuingia eda na kutoka eda

Katika uislamu hakuna sheria ya mwanamke kuingizwa eda na kutolewa eda kama ilivyozoeleka. Endelea na post hii ujifunze zaidi

Soma Zaidi...
Faida na umuhimu wa ndoa katika jamii

Hapa utajifunza faida za ndoa katika Jamii na kwa wanadamu kiafya, kiroho, kiuchumi

Soma Zaidi...
Njia haramu za uchumi.

Njia hizi ni haramu katika kukuza uchumi wako.

Soma Zaidi...
Nini maana ya kusimamisha swala

Post hii inakwenda kukufundisha maana ya kusimamisha swala kama inavyotumika kisheria.

Soma Zaidi...
Wanaostahiki kupewa zakat

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...