haki na wajibu kwa wakubwa

haki na wajibu kwa wakubwa

Wajibu wa Wakubwa kwa wadogo na wa Wadogo kwa Wakubwa



Katika utamaduni wa Kiislamu wakubwa kwa umri au kwa Maarifa au kwa mamlaka ya (uongozi), wanawajibika kuwahurumia, kuwapenda, kuwaongoza, kuwaelekeza, kuwashauri na kuwaasa wadogo zao kiumri au kimaarifa au mamlaka. Wakubwa wanawajibika kuwamrisha wadogo zao kufanya mema na wanawajibika kukataza maovu wenyewe wakiwa ni viigizo nyema. Kwa kutumia uzoefu wao wanawajibika kuwaelekeza na kuwaongoza katika njia iliyonyooka, wale walio chini yao kiumri na kimamlaka.
Kwa upande mwingine, wadogo kiumri au kimamlaka wanawajibika kuwatii na kuwaheshimu wale walio juu yao kama tunavyoamrishwa:


"Enyi mlioamini! Mtiini Mwenyezi Mungu na mtiini Mtume na wenye mamlaka juu yenu, walio miongoni mwenu.Na kama mkikhitilafiana juu ya jambo lolote basi lirudisheni kwa Mwenyezi Mungu na Mtume, ikiwa mnamwamini Mwenyezi na siku ya Mwisho. Hiyo ndiyo kheri nayo ma matokeo bora kabisa." (4:59).
Kutokana na aya hii tunawajibika kuwatii wakubwa zetu na wale wenye mamlaka juu yetu, baada ya kumtii Allah (s.w) na Mtume (s.a.w).


Lakini hatuwajibiki kuwatii wakubwa zetu na wenye mamlaka juu yetu kinyume na kumtii Allah (s.w) na Mtume (s.a.w).. Wale wenye mamlaka juu yetu wakituamrisha kumuasi Allah (s.w) na Mtume wake (s.a.w), tuwakatalie kwa heshima huku tukiwarejesha kwa mafundisho ya Qur-an na sunnah kuwa: "Hapana utii kwa kiumbe katika kumuasi Muumba."



Msisitizo wa kuwatii na kuwaheshimu wakubwa zetu kiumri na kimamlaka pia tunaupata katika Hadith zifuatazo:
Ibn Abbas (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: "Si katika sisi (si muumini) yule asiyewahurumia wadogo zetu na kuwaheshimu wakubwa zetu wala haamrishi mema na kukataza mabaya ". (Tirmidh)



Anas (r.a) anaeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: "Kama kijana atamuheshimu mtu mzima kutokana na umri wake, naye Allah atajaalia mtu atakayemheshimu katika uzee wake." (Tirmidh)



Pamoja na msisitizo wa kuwaheshimu wakubwa zetu, hatunabudi kuzingatia mipaka ya Uislamu katika kufanya hivyo. Wakati mwingine kuwaheshimu na kuwatii wakubwa kupita kiasi, hutupelekea kwenye shirk. Kwa kuchelea hili, Mtume (s.a.w) aliwakataza Waislamu kumsifu kupita kiasi kama wakristo walivyofanya kwa mwana wa Maryamu (Issa (a.s) na kumfanya mwana wa Mungu. Hivyo Mtume (s.a.w) ametuelekeza tumsifu kwa kumwita "Mja na Mtume wa Allah".



Pia kwa kuchelea shirk, Mtume (s.a.w) aliwakataza Waislamu wasimsimamie wakati akiingia kwenye mkutano au akipita njiani kama tunavyojifunza katika Hadith zifuatazo:
Anas (r.a) ameeleza: "Hapana mtu tuliyempenda kuliko Mtume wa Allah.Hatukuwa tunamsimamia kwa sababu alikuwa hapendi kusimamiwa." (Tirmidh)
Muawiyah (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: "Yeyote yule anayependa watu wamuheshimu kwa kumsimamia, atarajie kuwa mkazi wa motoni." (Tirmidh, Abu Daud)



Tunajifunza kutokana na Hadithi hizi kuwa "heshima" isipelekee kuwafanya wengine kuwa wanyonge na dhalili na wengine kuwa watukufu na bora. Tunapo heshimu au kuheshimiwa, hatunabudi kuiweka mbele yetu aya ifuatayo:


Enyi watu! Kwa hakika tumekuumbeni (nyote) kwa (yule) mwanamume (mmoja; Adamu) na (yule yule) mwanamke (mmoja; Hawa). Na tumekufanyeni matafa na makabila (mbali mbali) ili mjuane (tu basi siyo mkejeliane).Hakika ahishimiwaye sana miongoni mwenu mbele ya Mwenyezi Mungu ni yule amchaye Mungu zaidi katika nyinyi. Kwa yakini Mwenyezi Mungu ni Mjuzi, Mwenye habari (za mambo yote). (49:13)




                   


Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1088

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Nini maana ya twahara katika uislamu

Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya twahara katika uislamu. Pia utakwenda kujifunza hukumu za twahara, aina za twahara na mambo mengineyo

Soma Zaidi...
udhaifu wa hoja za kuunga mkono kuzibiti uzazi na uzazi wa mpango

Udhaifu wa Hoja za Kudhibiti Uzazi:Hoja nyingi zinazotolewa kuunga mkono udhibiti wa uzazi zimejengwa juu ya hali na mazingira ya maisha yaliyoletwa na utamaduni na maendeleo ya nchi za Ulaya na Marekani.

Soma Zaidi...
Maana ya shahada

Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Hijjah

Nguzo za uislamu (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Je ni nani mwenye haki ya kutaliki

Hapabutajifunza endapp mwanamke anahitaji kuachwa ni nini anatakiwa afanye.

Soma Zaidi...
Tofauti kati ya zakat na sadaqat

Nguzo za Imani, tofauti kati ya sadaqat na zakat (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Sifa za kuwa maamuma kwenye swala na namna ya kumfuata imamu

Post hii inakwenda kukuelezea sifa za kuwa maamuma na taratibu za kumfuata imamu.

Soma Zaidi...