Dhana ya mirathi na kurithi katika zama za ujahiliya

Mirathi katika jamii za kijahiliKatika jamii nyingi za kijahili kama vile jamii ya Waarabu kabla ya Mtume Muhammad (s.

Dhana ya mirathi na kurithi katika zama za ujahiliya

Mirathi katika jamii za kijahili
Katika jamii nyingi za kijahili kama vile jamii ya Waarabu kabla ya Mtume Muhammad (s.a.w), watoto wadogo ambao hawajafikia baleghe, walemavu na wazee ambao hawakuwa na uwezo wa kupigana vita katika kuihami heshima ya familia na kabila kwa ujumla, hawakupata chochote katika mirathi. Aghalabu katika jamii zote za kijahili mwanamke akiwa binti au mke, au mama au katika uhusiano wowote ule kwa marehemu, hakuwa na haki yoyote ile katika urithi.



Badala yake wanawake wenyewe walifanywa mali ya kurithiwa kwa nguvu na ndugu wa marehemu au mtoto mkubwa wa kiume wa marehemu ambaye hakuzaliwa na huyo mama anayerithiwa. Waliwarithi kama wake au vinginevyo waliwaoza kwa wanaume wengine kwa nguvu kinyume cha ridhaa ya wajane hao. Kwa namna hii wanawake walirithiwa kama sehemu ya mali ya marehemu na waliuzwa na kununuliwa kama bidhaa. Uislamu umepiga marufuku tabia hii katika aya ifuautayo:



Enyi mlioamini! Si halali kwenu kurithi wanawake kwa jeuri. Wala msiwazuie (kuolewa na wanaume wengine) iii mpate kuwanyang 'anya baadhi ya vile mliiyowapa(Hapana ruhusa haya) isipokuwa wawe wamefanya uovu ulio wazi nakaeni nao kwawema " (4:19).


Wala msiwaoe wake waliowaoa baba zenu, ispokuwa yale yaliyokwisha pita. Bila shakajambo hili ni uovu na chukizo na ni njia mbaya. (4:22).




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1064

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Tarstibu za kulipa swaumu ya Ramadhani

Hapa utajifunza namna ambayo utatakiwa kulipa funga ya Ramadhani kwa siku ambazo hukufunga

Soma Zaidi...
Zijuwe sunnha 9 za swala

Post hii inakwenda kukufundisha sunnah 9 za swala. Sunnah hizi ni zile ambazo ukiziwacha swala yako haibatiliki.

Soma Zaidi...
Twahara na umuhimu wake katika uislamu

Katika post hii utajifunza maana ya twahara kiligha na kishria. Pia utajifunza umuhimu wake

Soma Zaidi...
Maana ya talaka na kuacha ama kuachwa

Maana ya TalakaTalaka ni utaratibu wa kuvunja mkataba wa ndoa waliofunga mume na mke wakati wa kufunga ndoa mbele ya mashahidi wawili.

Soma Zaidi...
Dhana ya kumiliki raslimali katika uislamu

Ni ipi raslimali ya halali kuimiliki katika uislamu.

Soma Zaidi...