picha

Dhana ya mirathi na kurithi katika zama za ujahiliya

Mirathi katika jamii za kijahiliKatika jamii nyingi za kijahili kama vile jamii ya Waarabu kabla ya Mtume Muhammad (s.

Dhana ya mirathi na kurithi katika zama za ujahiliya

Mirathi katika jamii za kijahili
Katika jamii nyingi za kijahili kama vile jamii ya Waarabu kabla ya Mtume Muhammad (s.a.w), watoto wadogo ambao hawajafikia baleghe, walemavu na wazee ambao hawakuwa na uwezo wa kupigana vita katika kuihami heshima ya familia na kabila kwa ujumla, hawakupata chochote katika mirathi. Aghalabu katika jamii zote za kijahili mwanamke akiwa binti au mke, au mama au katika uhusiano wowote ule kwa marehemu, hakuwa na haki yoyote ile katika urithi.



Badala yake wanawake wenyewe walifanywa mali ya kurithiwa kwa nguvu na ndugu wa marehemu au mtoto mkubwa wa kiume wa marehemu ambaye hakuzaliwa na huyo mama anayerithiwa. Waliwarithi kama wake au vinginevyo waliwaoza kwa wanaume wengine kwa nguvu kinyume cha ridhaa ya wajane hao. Kwa namna hii wanawake walirithiwa kama sehemu ya mali ya marehemu na waliuzwa na kununuliwa kama bidhaa. Uislamu umepiga marufuku tabia hii katika aya ifuautayo:



Enyi mlioamini! Si halali kwenu kurithi wanawake kwa jeuri. Wala msiwazuie (kuolewa na wanaume wengine) iii mpate kuwanyang 'anya baadhi ya vile mliiyowapa(Hapana ruhusa haya) isipokuwa wawe wamefanya uovu ulio wazi nakaeni nao kwawema " (4:19).


Wala msiwaoe wake waliowaoa baba zenu, ispokuwa yale yaliyokwisha pita. Bila shakajambo hili ni uovu na chukizo na ni njia mbaya. (4:22).




                   


Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Fiqh Main: Post File: Download PDF Views 2002

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 ai web app     👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉5 Simulizi za Hadithi Audio     👉6 Bongolite - Game zone - Play free game    

Post zinazofanana:

HUKUMU YA KUUWA MTU (KUMWAGA DAMU) KWENYE UISLAMU

عَنْ ابْنِ مَسْعُودٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم "لَا يَحِلُّ دَمُ امْرِئٍ مُسْلِمٍ [ يشهد أن ل?...

Soma Zaidi...
Njia za kuzuia na kupunguza zinaa katika jamii

(ii) Hatua za Kuzuia Uzinzi JamiiUislamu pamoja na kutoa mafunzo ya maadii yanayomuwezesha mtu binafsi ajiepushe kwa hiari yake na kitendo kibaya cha zinaa, umechukua hatua mbali mbali ambazo huifanya zinaa isiwe kitendo chepesi katika jamii.

Soma Zaidi...
Maana ya shahada

Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Aina za hijjah

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mambo ambayo hayafunguzi funga

Hii ni orodha ya mambo ambayo hayawezi kuharimu funga yako endapo utayafanya.

Soma Zaidi...