Maana ya Mirathi na kurithi katika uislamu
Maana ya MirathiMirathi katika Uislamu ni kanuni na taratibu alizoziweka Allah (Sw) katika kuwagawawia na kuwarithisha familia na jamaa, mali aliyoiacha marehemu.
Maana ya Mirathi
Mirathi katika Uislamu ni kanuni na taratibu alizoziweka Allah (Sw) katika kuwagawawia na kuwarithisha familia na jamaa, mali aliyoiacha marehemu. Qur'an inabainisha kuwa, mtu anapofariki dunia, mali yote aliyochuma hurithiwa na Allah (Sw), kisha Yeye huigawa na kuwarithisha watu wanaostahiki, katika uwiano wa haki na uadilifu.ombeni msaada kwa Mwenyezi Mungu na subirini. Ardhi ni ya Mwenyezi Mungu, anamrithisha amtakaye katika waja wake; na mwisho (mwema) ni kwa wamchao. (7:128)
na urithi wa mbingu na ardhi ni wa Mwenyezi Mungu (5 7:10) Ukweli huu unajitokeza pia katika dua ya nabii Zakaria alipomuamba Allah (Sw) amjaalie mtoto. Nabii Zakaria alimwomba Mola wake akasema: Mola wangu! Usiniache peke yangu na Wewe ndiwe mbora wa wanaorithi (21:89)
Mwanamke ana haki ya kurithi
Katika kugawanya na kuirithisha mali kwa wahusika, Allah (Sw) hakumnyima mwanamke haki ya kurithi akiwa mtoto, mke au mama. Wote wanawake na wanaume wanamafungu maalumu Ia kurithi katika mali aliyoiacha marehemu.
"Wanaume wana sehemu katika mali wanayoyachuma wazazi na jamaa walio karibu. Na wanawake (pia) wanayo sehemu katika yale waliyoyaacha wazazi na jamaa walio karibu. Yakiwa kidogo au mengi. (Hizi) ni sehemu zilizofaradhishwa (na Allah (s.w))" (4:7)
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 Dua za Mitume na Manabii 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Jinsi ya kuswali swala ya kuoatwa kwa juwa ama swala ya kuoatwa kwa mwezi.
Post hii itakufundisha kuhusu swala ya kupatwa yaani kupatwa kwa juwa na kupatwa kwa mwezi swalat kusuf na swalat khusuf
Soma Zaidi...Kumswalia maiti, masharti ya swala ya maiti
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Mda wa mwisho wa kula daku mwezi wa ramadhani
Post hii fupi itakwenda kukujulisha utaratibu wa kula daku.
Soma Zaidi...Ni nini maana ya uchumi katika uislamu
Katikabuislamu dhana ya uchumi imetofautiana na dhana ya kidunia hivi leo ambapo kamari na riba ni moja ya vitu muhimu katika uchumi.
Soma Zaidi...Je kama maiti imekatika baadhi ya viungo je viungo vyake tunafata utaratibu gani katika kumuosha na kumkafini?
Assalamu Alaykum Warahmatu-llah Wabarakaatuh Naomba kuuliza: Je kama maiti imekatika baadhi ya viungo je viungo vyake tunafata utaratibu gani katika kumuosha na kumkafini?
Soma Zaidi...