picha

Maana ya Mirathi na kurithi katika uislamu

Maana ya MirathiMirathi katika Uislamu ni kanuni na taratibu alizoziweka Allah (Sw) katika kuwagawawia na kuwarithisha familia na jamaa, mali aliyoiacha marehemu.

Maana ya Mirathi na kurithi katika uislamu

Maana ya Mirathi
Mirathi katika Uislamu ni kanuni na taratibu alizoziweka Allah (Sw) katika kuwagawawia na kuwarithisha familia na jamaa, mali aliyoiacha marehemu. Qur'an inabainisha kuwa, mtu anapofariki dunia, mali yote aliyochuma hurithiwa na Allah (Sw), kisha Yeye huigawa na kuwarithisha watu wanaostahiki, katika uwiano wa haki na uadilifu.ombeni msaada kwa Mwenyezi Mungu na subirini. Ardhi ni ya Mwenyezi Mungu, anamrithisha amtakaye katika waja wake; na mwisho (mwema) ni kwa wamchao. (7:128)


na urithi wa mbingu na ardhi ni wa Mwenyezi Mungu (5 7:10) Ukweli huu unajitokeza pia katika dua ya nabii Zakaria alipomuamba Allah (Sw) amjaalie mtoto. Nabii Zakaria alimwomba Mola wake akasema: Mola wangu! Usiniache peke yangu na Wewe ndiwe mbora wa wanaorithi (21:89)



Mwanamke ana haki ya kurithi
Katika kugawanya na kuirithisha mali kwa wahusika, Allah (Sw) hakumnyima mwanamke haki ya kurithi akiwa mtoto, mke au mama. Wote wanawake na wanaume wanamafungu maalumu Ia kurithi katika mali aliyoiacha marehemu.


"Wanaume wana sehemu katika mali wanayoyachuma wazazi na jamaa walio karibu. Na wanawake (pia) wanayo sehemu katika yale waliyoyaacha wazazi na jamaa walio karibu. Yakiwa kidogo au mengi. (Hizi) ni sehemu zilizofaradhishwa (na Allah (s.w))" (4:7)




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Fiqh Main: Post File: Download PDF Views 2870

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 web hosting     👉5 kitabu cha Simulizi     👉6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

Nguzo za udhu ni sita

Post hii itakufundisha kuhusu nguzo kuu sita za udhu.

Soma Zaidi...
Mafungu ya mirathi katika uislamu

Mafungu ya urithi yaliyotajwa katika haya sita yafutayo:1.

Soma Zaidi...
Haki za maadui katika vita (mateka wa kivita)

Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mafungu ya urithi katika uislamu

Hspa utajifunza viwango maalumu vya kutithi mirathi ys kiislamu.

Soma Zaidi...