Maana ya Mirathi na kurithi katika uislamu
Maana ya MirathiMirathi katika Uislamu ni kanuni na taratibu alizoziweka Allah (Sw) katika kuwagawawia na kuwarithisha familia na jamaa, mali aliyoiacha marehemu.
Maana ya Mirathi
Mirathi katika Uislamu ni kanuni na taratibu alizoziweka Allah (Sw) katika kuwagawawia na kuwarithisha familia na jamaa, mali aliyoiacha marehemu. Qur'an inabainisha kuwa, mtu anapofariki dunia, mali yote aliyochuma hurithiwa na Allah (Sw), kisha Yeye huigawa na kuwarithisha watu wanaostahiki, katika uwiano wa haki na uadilifu.ombeni msaada kwa Mwenyezi Mungu na subirini. Ardhi ni ya Mwenyezi Mungu, anamrithisha amtakaye katika waja wake; na mwisho (mwema) ni kwa wamchao. (7:128)
na urithi wa mbingu na ardhi ni wa Mwenyezi Mungu (5 7:10) Ukweli huu unajitokeza pia katika dua ya nabii Zakaria alipomuamba Allah (Sw) amjaalie mtoto. Nabii Zakaria alimwomba Mola wake akasema: Mola wangu! Usiniache peke yangu na Wewe ndiwe mbora wa wanaorithi (21:89)
Mwanamke ana haki ya kurithi
Katika kugawanya na kuirithisha mali kwa wahusika, Allah (Sw) hakumnyima mwanamke haki ya kurithi akiwa mtoto, mke au mama. Wote wanawake na wanaume wanamafungu maalumu Ia kurithi katika mali aliyoiacha marehemu.
"Wanaume wana sehemu katika mali wanayoyachuma wazazi na jamaa walio karibu. Na wanawake (pia) wanayo sehemu katika yale waliyoyaacha wazazi na jamaa walio karibu. Yakiwa kidogo au mengi. (Hizi) ni sehemu zilizofaradhishwa (na Allah (s.w))" (4:7)
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 kitabu cha Simulizi 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 Dua za Mitume na Manabii 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Hali ya kuzuiliana kurithi katika uislamu
KuzuilianaTumeona kuwa wanaume wenye kurithi ni 15 na wanawake wanaorithi ni 10.
Soma Zaidi...Jinsi ya kuswali kuswali swala ya maiti
Post hii itakufundisha kuhusu swala ya maiti, nguzo za swala ya maiti, sharti za swwla ya maiti na jinsi ya kuiswali.
Soma Zaidi...