picha

Fahamu vyakula vya nyuzinyuzi

Posti hii moja kwa moja inaenda kuelezea vyakula vya nyuzinyuzi zinazopatikana kwenye matunda na mboga mboga.

  Je, wafahamu kuwa matunda yanafaida nyingi mwilini? 

Moja kwa moja tuone matunda yanayokuwa na nyuzinyuzi na huwa na Faida gani;

 

1. Parachichi; hili Ni tunda lenye nyuzinyuzi na linasaidia uyeyushaji wa chakula tumboni hasa kwa wale wenye Matatizo ya Vidonda vya tumbo, Na nyuzinyuzi hizo Ni muhimu kukinga kuta za utumbo,. Pia husaidia watu wenye maradhi ya upungufh wa damu, kisukari, Matatizo ya mfumo wa Neva na maradhi mengine mengi watu hawa wanatakiwa kula tunda hili kwa wingi ili kuboresha Kinga ya mwili.

 

2.chungwa: nyuzinyuzi zinazopatikana kwenye chungwa huwa na vitamini C pia husaidia kuponesha Vidonda hivyo tunda hili ukilila kula pamoja na nyuzinyuzi zake tafuna mapaka zile kamba zake kwasababu zinasaidia usagaji wa chakula tumboni ( digestion) japo kuwa watu wengi hunyonya maji yalliyopo kwenye chungwa na kutupa nyuzinyuzi haishauriwi kula hivyo.

 

3.Embe;  tunda hili hiwa na nyuzinyuzi nyingi Sana ambazo huweza Kuzuia Saratani, pia huborasha Uwezo wa kumbukumbu na kufikiria kwa wingi hivyo watu tusipuuzie kula embe.

 

4. Nanasi: Ni tunda ambalo Lina sukari na Ni tamu Sana tunda hili Lina nyuzinyuzi ambazo Zina virutubisho vingi na vingine vinauwezo was kuupa mwili wAko Kinga dhidi ya Magonjwa tunda hili Lina vitamini C na madini ya chuma.

 

5. Ndizk mbivu; nyuzinyuzi za kwenye ndizi mbivu husaidia Sana Katika usagaji wa chakula tumboni,pia tunda hili Lina Uwezo wa kuimarisha nishati ya mwili. Mwili kuwa na nguvu na pia huweza kuongeza uzito. Hivyo hushauriwa kwa wale wenye uzito kupitiliza waepuka kutumia ndizi.

 

6. Papai; Hilo Ni tunda ambalo husaidia vitu vingi mwilini Kama vile kuua minyoo na kuondoa mazalia ya minyoo tumboni, na husaidia kwa wale wenye Vidonda vya tumbo Na kuboresha Kinga ya mwili.

 

Na je wafahamu kuwa mboga mboga Zina Faida nyingi mwilini?

 

Mboga mboga hasa za majani husaidia tumbo kusukuma uchafu wote tumboni hasa kwa wale wanaopenda kula vyakula vilivyokobolewa na vigumu kwani Magonjwa yote yanaanzia tumboni ndipo yanasambaa mwilini;.

 

1. Kabeji; ni mojawapo ha mboga yenye nyuzinyuzi ambayo hutibu Matatizo ya choo kigumu, na husaidia kuponesha haraka Vidonda vya tumbo vile vile husaidia kupunguza uzito uliozidi pamoja na kuondoa sumu mwilini.

 

2.Mchicha Hii pia Ni mboga ya majani ambayo Ina nyuzinyuzi nyingi na zinazosadia kuboresha mwili, Kinga ya mwili pia husaidia kwa wale wasioona endapo watatumia kwa wingi mboga hii.

 

3. Matembele; Ni mboga ambazo hupatikana kwenye majani ya viazi ambayo pia hutoa nyuzinyuzi matembele Yana vitamini A na vitamini C ambazo huimarisha Ngozi na fizi, endapo fizi zako zinatoa Damu Ni vyema kutumia matembele kwa wingi kwani husaidia kuponesha na pia mboga hii huwa na protini pia.

 

4. Spinachi; mboga hii pia Ina nyuzinyuzi ambayo Ina potassium kwa wingi, vitamini C na vitamini E ambazo zinasaidia kuimarisha afya ya Ngozi na pia kuimarisha Ngozi da Damu kuganda pia.

 

 Mwisho; hizi Ni baadhi ya mboga mboga na matunda yenye nyuzinyuzi Ila vyakula hivi Ni muhimu Sana endapo vikizingatiwa.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Vyakula Main: Post File: Download PDF Views 11836

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 Bongolite - Game zone - Play free game     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

Faida za kula tikiti

Somo hili linalenga kukujuza juu ya umuhimu wa tikiti kwenye afya ya mwili

Soma Zaidi...
vyakula vya kuongeza damu, dalili zake na sababu za upungufu wa damu

Zijuwe sababu za upungufu wa damu, dalili za upungufu wa damu na kazi za damu mwilini,n avyakula vya kuongeza damu

Soma Zaidi...
Faida za kula Tango

Matunda ya zamani na ya asili, zijuwe faida za kiafya za tango

Soma Zaidi...
Vyakula kwa wagonjwa wa sukari na utaratibu wao wa lishe

Post hii inakwenda kukufundisha utaratibu wa lishe kwa wagonjwa wenye kisukari pamoja na vyakula salamakwao.

Soma Zaidi...