FAHAMU VYAKULA VYA NYUZINYUZI


image


Posti hii moja kwa moja inaenda kuelezea vyakula vya nyuzinyuzi zinazopatikana kwenye matunda na mboga mboga.


  Je, wafahamu kuwa matunda yanafaida nyingi mwilini? 

Moja kwa moja tuone matunda yanayokuwa na nyuzinyuzi na huwa na Faida gani;

 

1. Parachichi; hili Ni tunda lenye nyuzinyuzi na linasaidia uyeyushaji wa chakula tumboni hasa kwa wale wenye Matatizo ya Vidonda vya tumbo, Na nyuzinyuzi hizo Ni muhimu kukinga kuta za utumbo,. Pia husaidia watu wenye maradhi ya upungufh wa damu, kisukari, Matatizo ya mfumo wa Neva na maradhi mengine mengi watu hawa wanatakiwa kula tunda hili kwa wingi ili kuboresha Kinga ya mwili.

 

2.chungwa: nyuzinyuzi zinazopatikana kwenye chungwa huwa na vitamini C pia husaidia kuponesha Vidonda hivyo tunda hili ukilila kula pamoja na nyuzinyuzi zake tafuna mapaka zile kamba zake kwasababu zinasaidia usagaji wa chakula tumboni ( digestion) japo kuwa watu wengi hunyonya maji yalliyopo kwenye chungwa na kutupa nyuzinyuzi haishauriwi kula hivyo.

 

3.Embe;  tunda hili hiwa na nyuzinyuzi nyingi Sana ambazo huweza Kuzuia Saratani, pia huborasha Uwezo wa kumbukumbu na kufikiria kwa wingi hivyo watu tusipuuzie kula embe.

 

4. Nanasi: Ni tunda ambalo Lina sukari na Ni tamu Sana tunda hili Lina nyuzinyuzi ambazo Zina virutubisho vingi na vingine vinauwezo was kuupa mwili wAko Kinga dhidi ya Magonjwa tunda hili Lina vitamini C na madini ya chuma.

 

5. Ndizk mbivu; nyuzinyuzi za kwenye ndizi mbivu husaidia Sana Katika usagaji wa chakula tumboni,pia tunda hili Lina Uwezo wa kuimarisha nishati ya mwili. Mwili kuwa na nguvu na pia huweza kuongeza uzito. Hivyo hushauriwa kwa wale wenye uzito kupitiliza waepuka kutumia ndizi.

 

6. Papai; Hilo Ni tunda ambalo husaidia vitu vingi mwilini Kama vile kuua minyoo na kuondoa mazalia ya minyoo tumboni, na husaidia kwa wale wenye Vidonda vya tumbo Na kuboresha Kinga ya mwili.

 

Na je wafahamu kuwa mboga mboga Zina Faida nyingi mwilini?

 

Mboga mboga hasa za majani husaidia tumbo kusukuma uchafu wote tumboni hasa kwa wale wanaopenda kula vyakula vilivyokobolewa na vigumu kwani Magonjwa yote yanaanzia tumboni ndipo yanasambaa mwilini;.

 

1. Kabeji; ni mojawapo ha mboga yenye nyuzinyuzi ambayo hutibu Matatizo ya choo kigumu, na husaidia kuponesha haraka Vidonda vya tumbo vile vile husaidia kupunguza uzito uliozidi pamoja na kuondoa sumu mwilini.

 

2.Mchicha Hii pia Ni mboga ya majani ambayo Ina nyuzinyuzi nyingi na zinazosadia kuboresha mwili, Kinga ya mwili pia husaidia kwa wale wasioona endapo watatumia kwa wingi mboga hii.

 

3. Matembele; Ni mboga ambazo hupatikana kwenye majani ya viazi ambayo pia hutoa nyuzinyuzi matembele Yana vitamini A na vitamini C ambazo huimarisha Ngozi na fizi, endapo fizi zako zinatoa Damu Ni vyema kutumia matembele kwa wingi kwani husaidia kuponesha na pia mboga hii huwa na protini pia.

 

4. Spinachi; mboga hii pia Ina nyuzinyuzi ambayo Ina potassium kwa wingi, vitamini C na vitamini E ambazo zinasaidia kuimarisha afya ya Ngozi na pia kuimarisha Ngozi da Damu kuganda pia.

 

 Mwisho; hizi Ni baadhi ya mboga mboga na matunda yenye nyuzinyuzi Ila vyakula hivi Ni muhimu Sana endapo vikizingatiwa.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Madrasa kiganjani       ðŸ‘‰    2 Hadiythi za alif lela u lela       ðŸ‘‰    3 Jifunze fiqh       ðŸ‘‰    4 Magonjwa na afya       ðŸ‘‰    5 Maktaba ya vitabu       ðŸ‘‰    6 Mafunzo ya html kwa kiswahili    





Je una umaswali, maoni ama mapendekezo?
Download App yetu kuwasiliana nasi




Post Nyingine


image ZIJUWE FIGO, KAZI ZA FIGO NA NAMNA YA KULINDA FIGO DHIDI YA MARADHI
Je unatambuwa namna fgo inavyofanya kazi, unazijuwa kazikuu za fogo mwilini, na je unajuwa namna ya kujilinda dhidi ya maradhi ya figo?. Basi makala hii itakujuza kuhusu masomo haya1 Soma Zaidi...

image Dalili za upungufu wa vitamini C mwilini
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za upungufu wa vitamini C mwilini Soma Zaidi...

image Fahamu kuhusu vitamini K na kazi zake mwilini
vitamini k ni moja katika vitamini vinavyoitajika sana mwilini. Je unazijuwa athari za upungufu wa vitamini k mwilini? Soma Zaidi...

image Vyakula salama kwa mwenye kisukari
Somo hili linakwenda kukuletea orodha ya vyakula salama kwa mwenye kisukari Soma Zaidi...

image Faida za kiafya za kula kisamvu
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula kisamvu Soma Zaidi...

image Vyakula vinavyosaidia katika kusafisha ini
Post hii inahusu zaidi baadhi ya vyakula ambavyo vinaweza kutumika ili kuweza kuweka ini kwenye hali yake ya kawaida. Soma Zaidi...

image Dalili za fangasi wa sehemu za Siri kwa wanawake
Somo hili linakwenda kukuletea dalili za fangasi wa sehemu za Siri kwa wanawake Soma Zaidi...

image Vyakula vya vitamin B
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za vyakula vya vitamin B Soma Zaidi...

image Kazi na mdalasini katika kutibu matatizo ya homoni.
Posti hii inahusu zaidi kazi ya mdalasini katika matibabu ya homoni kwa wanawake. Soma Zaidi...

image Vyakula muhimu kwa afya ya uzazi wa mwanaume
Vyakula vya kuongeza Nguvu za kiume Soma Zaidi...