image

Faida za kula Faida za kula Boga

Makala hii inakwenda kukueleza faida za kula maboga, na mbegu zake kwa afya yako

Faida za kula Faida za kula Boga

19. Boga (pumpkin)
Boga ni katika vyakula vya asili walivyotumia mababu zetu toka enzi za zamani sana. Boga ni katika chakula chenye vitamin A. pia boga husaidia katika kushusha presha kwani mna kwenye mbegu za maboga aina ya mafuta pytoestrogens ambayo ndio hupunguza shinikizo la damu (hypertension).

Maboga husaidia katika ku[ata usingizi mnono kwani mna kwenye mbegu za maboga typtophan aina ya amino asid ambayo husaidia katika kurelax. Pia mna beta-carotene na aina zingine za antioxidant ambazo husaidia katika kuzuia kupata cancer.

Maboga ni muhimu katika kuboresha na kuimarisha afya ya nguvu za kiume. Pia chakula hiki ni muhimu kwa afya ya moyo. Kwani kutokana na kambakamba zilizomo kwenye maboga mlaji anakuwa na nafasi ndogo sana ya kuweza kupata mabonjwa ya moyo (coronary heart diseases).

Chakula cha maboga pia husaidia katika kuzuia na mlaji kupata ugonjwa wa kisukari. Pia huimarisha vyema afya ya mwenye kisukari. Chakula hiki husaidia katika ufyonzwaji wa glucose kwenda kwenye tishu za mwili. Pia husaidia katika kubalans kiwango cha sukari ndani ya mwili.

Maboga husaidia katika kuboresha na kuimarisha mfumo wa kinga mwilini (immune system). kwani vitamin C pamoja na beta-carotene husaidia mara dufu katika kuimarisha mfumo wa kinga ili kuweza kupambana na maradhi mbalimbali mwilini. Isitoshe beta-carotene kuweza kubadilishwa kuwa vitamin A, na hali hii huweza kusaidia katika kuzalishwa kwa seli hai nyeupe mwilini ambazo ndio hupambana na maradhi na vijidudu vishambulizi kama bakteria, fangas na virusi.


                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 495


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Faida za kiafya za kula nyama
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula nyama Soma Zaidi...

Faida za kula Nazi
Nazi ni katika matunda bora sana kiafya, Soma faida zake kwa afya yako Soma Zaidi...

Faida za kula nazi
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula nazi Soma Zaidi...

Faida za kula tikiti
Somo hili linalenga kukujuza juu ya umuhimu wa tikiti kwenye afya ya mwili Soma Zaidi...

Faida za tangawizi
Somo Hili linakwenda kukuletea faida za tangawizi Soma Zaidi...

Faida za kiafya za kula mihogo
Some Hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula mihogo Soma Zaidi...

Faida za kula parachichi
Somo hili litakwenda kukueleza na kukuelimisha kuhusu umuhimu wa kula parachichi kiafya Soma Zaidi...

Athari za kula vitamin C kupitiliza
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu athari za kula vitamini C kupitiliza Soma Zaidi...

Faida za kiafya za kula maharagwe, njegere, kund na mbaazi
Soma Zaidi...

Faida za kula ukwaju
Uchachu wa ukwaju, ndio ubora wake, kuna virutubisho vingi kwa kula ukwaju, soma makala hii Soma Zaidi...

Je ulaji wa boga unafaa kwa mgonjwa wa kisukari?
Je ulaji wa boga unafaa kwa mgonjwa wa kisukari? Soma Zaidi...

Faida za kafya za kula asali
Post hii itakwenda kukufundisha faida za kiafya za kula asali Soma Zaidi...