Mabadiliko ya matiti yanayopaswa kutolewa taarifa mara moja
Posti hii inahusu zaidi mabadiliko ya matiti yanayopaswa kutolewa taarifa mapema, kwa sababu ya kuwepo kwa saratani ya matiti, kuna dalili ambazo zikijitokeza zinapaswa kutolewa taarifa mara moja bila kuchelewa kama ifuatavyo.
Mabadiliko ya matiti yanayopaswa kutolewa taarifa mara moja.
1. Kuwepo kwa uvimbe kwenye matiti, kuwepo kwa fundi gumu kama mbegu ndani ya titi au kwapani, hizi ni Dalili za kuripoti mara moja pindi zinapotokea inawezekana kubwa Dalili ya saratani ya matiti au pengine ni ugonjwa wa kawaida unaohitaji tiba mara moja,
2. Pengine matiti yanaweza kuwa na joto la hali ya juu na Dalili za wekundu zinaweza kujitokeza kama si wekundu inaweza kuwa na rangi nyeusi kwenye matiti na kwa wakati mwingine kuna hali ya kubadilika kwa umbo la titi na kuwa kubwa kuliko kawaida au pengine na maumivu yanaongezeka kadri ya ukubwa wa titi linavyoongezeka.
3. Na dalili nyingine ni ngozi kujikunja au kubwa na vitundu na kuifanya iwe na ganda la chungwa kwa dalili hii hakuna maumivu yoyote yanayoweza kujitokeza bali ukilipapasa titi linakuwa gumu na labda Chuchu ndiyo inakuwa inawasha na kutoa maji na pengine hizo Chuchu na sehemu nyingine za titi kubonyea kwa ndani .
4. Dalili nyingine ni pamoja na Chuchu kwa na maumivu makali na pengine kama kutoa maji maji kama hali haikutibiwa inaweza kuleta matatizo makubwa ambayo kuja kuyatibu ni shida kubwa, kwa hiyo tunapaswa kujua kuwa kama mama ananyonyesha na Dalili hizi zinajitokeza hapaswi kabisa kumnyonyesha mtoto anapaswa kutoa taarifa mara moja na kupata huduma hospitalini.
5. Kwa hiyo tunapaswa kuwa macho na makini kuhusu Dalili hizi hatari kwenye matiti, na tunapaswa kuelimisha jamii kujua wazi kubwa hizi zinaweza kuwa ni Dalili za saratani ya matiti, ila mwenye tatizo la namna hii anapaswa kupima na kujua kubwa ni saratani kweli kwa sababu kuna na magonjwa mengine yenye dalili kama hizi. Kwa hiyo saratani ya matiti ipo na inaweza kutibiwa hasa hasa mgonjwa akiwa mapema hospitalini.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 ai web app π2 Bongolite - Game zone - Play free game π3 Madrasa kiganjani π4 Simulizi za Hadithi Audio π5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) π6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
Yafahamu magonjwa nyemelezi kwa watoto chini ya miaka mitano
Posti hii inahusu zaidi magonjwa nyemelezi kwa watoto wadogo chini ya miaka mitano,. Ni magonjwa yanayowapata watoto wadogo kwa sababu kinga Yao bado ni ndogo.
Soma Zaidi...HOMA YA DENGUE, DALILI ZAKE, TIBA YAKE, CHANGO YAKE NA INA SABABISHWA (AMBUKIZWA) NA MBU GANI
Homa ya dengue hupatikana sana Afrika, Asia na baadhi ya maeneo ya Caribbean.
Soma Zaidi...VYANZO VYA VYAKULA VYA FATI, PROTINO NA WANGA NA FAIDA ZAKE
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote
Soma Zaidi...vyakula vya kuongeza damu, dalili zake na sababu za upungufu wa damu
Zijuwe sababu za upungufu wa damu, dalili za upungufu wa damu na kazi za damu mwilini,n avyakula vya kuongeza damu
Soma Zaidi...Faida za mchaichai/ lemongrass
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za mchaichai
Soma Zaidi...Vyakula bora kwa ajili ya afya ya macho.
βMacho ni moja ya viungo muhimu zaidi vinavyokuunganisha na ulimwengu, lakini mara nyingi tunayasahau hadi pale tunapoanza kupata changamoto za kuona. Kama ilivyo viungo vingine, macho yanahitaji virutubisho maalum ili yasibadilike ubora kadiri umri unavyosonga mbele. Makala haya yanakupa orodha ya vyakula bora unayoweza kuingiza kwenye sahani yako leo ili kuimarisha uwezo wako wa kuona
Soma Zaidi...