picha

Mabadiliko ya matiti yanayopaswa kutolewa taarifa mara moja

Posti hii inahusu zaidi mabadiliko ya matiti yanayopaswa kutolewa taarifa mapema, kwa sababu ya kuwepo kwa saratani ya matiti, kuna dalili ambazo zikijitokeza zinapaswa kutolewa taarifa mara moja bila kuchelewa kama ifuatavyo.

Mabadiliko ya matiti yanayopaswa kutolewa taarifa mara moja.

1. Kuwepo kwa uvimbe kwenye matiti, kuwepo kwa fundi gumu kama mbegu ndani ya titi au kwapani, hizi ni Dalili za kuripoti mara moja pindi zinapotokea inawezekana kubwa Dalili ya saratani ya matiti au pengine ni ugonjwa wa kawaida unaohitaji tiba mara moja,

 

2. Pengine matiti yanaweza kuwa na joto la hali ya juu na Dalili za wekundu zinaweza kujitokeza kama si wekundu inaweza kuwa na rangi nyeusi kwenye matiti na kwa wakati mwingine kuna hali ya kubadilika kwa umbo la titi na kuwa kubwa kuliko kawaida au pengine na maumivu yanaongezeka kadri ya ukubwa wa titi linavyoongezeka.

 

3. Na dalili nyingine ni ngozi kujikunja au kubwa na vitundu na kuifanya iwe na ganda la chungwa kwa dalili hii hakuna maumivu yoyote yanayoweza kujitokeza bali ukilipapasa titi linakuwa gumu na labda Chuchu ndiyo inakuwa inawasha na kutoa maji na pengine hizo Chuchu na sehemu nyingine za titi kubonyea kwa ndani .

 

4. Dalili nyingine ni pamoja na Chuchu kwa na maumivu makali na pengine kama kutoa maji maji kama hali haikutibiwa  inaweza kuleta matatizo makubwa ambayo kuja kuyatibu ni shida kubwa, kwa hiyo tunapaswa kujua kuwa kama mama ananyonyesha na Dalili hizi zinajitokeza hapaswi kabisa kumnyonyesha mtoto anapaswa kutoa taarifa mara moja na kupata huduma hospitalini.

 

5. Kwa hiyo tunapaswa kuwa macho na makini kuhusu Dalili hizi hatari kwenye matiti, na tunapaswa kuelimisha jamii kujua wazi kubwa hizi zinaweza kuwa ni Dalili za saratani ya matiti, ila mwenye tatizo la namna hii anapaswa kupima na kujua kubwa ni saratani kweli kwa sababu kuna na magonjwa mengine yenye dalili kama hizi. Kwa hiyo saratani ya matiti ipo na inaweza kutibiwa hasa hasa mgonjwa akiwa mapema hospitalini.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Vyakula Main: Post File: Download PDF Views 1912

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 web hosting     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Faida za kula Papai

Okoa afya yako kwa kula tunda papai, kwa hakika hutajuta, papai lina virutubisho vingi

Soma Zaidi...
VYAKULA VYA FATI, PROTINO NA WANGA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
Umuhimu wa kula matunda na mboga mboga kila siku.

Mara nyingi tunasikia ushauri wa "kula matunda na mboga mboga," lakini je, umewahi kujiuliza kwa nini hii ni kanuni muhimu zaidi ya lishe bora? Vyakula hivi sio tu kwa ajili ya kuongeza ladha kwenye sahani yako; ni hazina ya virutubisho, viondoa sumu, na nguvu za kinga zinazouwezesha mwili wako kufanya kazi kwa ufanisi na kukuepusha na magonjwa sugu. Makala haya yanakupa sababu za msingi kwa nini unapaswa kuweka mboga na matunda kwenye kila mlo wako.

Soma Zaidi...
Vyakula vya protini na kazi zake

Hapa utajifunza kuhusu kazi za protini mwilini na vyakula vipi vina protini kwa wingi

Soma Zaidi...
Vijuwe virutubisho vilivyomo kwenye parachichi.

Posti hii inahusu zaidi virutubisho vilivyomo kwenye parachichi, tunajua sana kuwa parachichi ina virutubisho vingi ambavyo vinaweza kuleta faida nyingi kwenye mwili kama yalivyo matunda na vyakula vingine.

Soma Zaidi...
RANGI ZA MATUNDA

Jifunze sifa na aina za matunda, vijuwe viruturubisho

Soma Zaidi...