image

Fahamu Ute unaotoka wakati wa ujauzito

Posti hii inahusu zaidi Ute unaotoka wakati wa ujauzito, kwa kawaida wakati wa ujauzito Kuna Ute ambao utoka na ni tofauti na kawaida pale mwanamke akiwa Hana mimba.

Fahamu Ute unaotoka wakati wa ujauzito.

1. Kwanza wakati wa ujauzito Kuna Ute ambao utoka na huwa ni mweupe kwa aina yake na ikitokea Ute huo ukawa na rangi tofauti na nyeupe kunakuwepo na maambukizi.

 

2. Ute huo uongezeka kwa sababu ya kuongezeka kwa homoni aina ya estrogen kwa sababu ya kufanya kazi mbalimbali kwenye mwili wa Mama wakati wa ujauzito kwa hiyo na Ute wakati wa ujauzito uongezeka zaidi.

 

3. Kwa upande wa akina Mama kama Kuna Ute wowote unaotoka wanapaswa kuwa makini Ili kuangalia ni Ute wa aje kwa sababu kama ni wa njano panakuwepo na maambukizi na hivyo ni vizuri kabisa kugundua na kuweza kupata matibabu.

 

4. Kwa sababu mabadiliko ya Ute usababishwa na hali yoyote iliyopo kwenye via vya uzazi kwa sababu kwenye via vya uzazi kama Kuna magonjwa kama vile kaswende na kisonono usababisha na rangi ya Ute kubadilika kwa hiyo kama Kuna aina yoyote ya mabadiliko ni vizuri kutafuta matibabu mapema na iwezekanavyo kwa sababu mtoto akipata maambukizi akiwa tumboni anaweza kupata shida ikiwepo kupoteza maisha.

 

5. Kwa upande wa akina Mama wajawazito hasa wanaochelewa kuanza clinic wanapaswa kuanza mara Moja Ili kuweza kupata vipimo mbalimbali kama vile vipimo vya magonjwa ya zinaa ikiwemo kaswende na Ukimwi, kwa kufanya hivyo hata kama mama hawezi kuangalia Ute wake hata kama una maambukizi anaweza kujua kama Kuna maambukizi kutokana na vipimo.

 

6. Kwa hiyo wajawazito wakiona Ute unaongezeka 

Wakati wa ujauzito wasishangae wajue kuwa ni kawaida kwa sababu ya kuwepo kwa mabadiliko ya homoni na hasa hasa Ute uongezeka wakati wa kukaribia kujifungua, kwa hiyo wasishangae ni kawaida tu na pakiwepo wasiwasi wowote ni vizuri kuwaona wataalamu wa afya Ili kuweza kupata matibabu zaidi.



           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2022/07/06/Wednesday - 04:21:31 pm     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 16841


Download our Apps
πŸ‘‰1 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰2 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰3 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Ni vipi nitagundua kuwa nina ujauzito?
Hali ya ujauzito huanza kutabirika Mara tu ya kujamiana, pia chemikali (hormon) za mwili huanza mchakato wa kuongeza na kupunguza utendaji kazi wa kemikali hizo mfano.follical stimulating hormon (FSH) na lutenazing hormon kuivisha yai tayari kwa kutengen Soma Zaidi...

Dalili za mwanzo za ujauzito katika wiki ya kwanza
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za mwanzo za ujauzito katika wiki ya kwanza Soma Zaidi...

Dalili za mimba kuanzia week mbili Hadi mwezi
Somo hili linakwenda kukueleza baadhi ya dalili za mimba kuanzia week mbili Hadi mwezi Soma Zaidi...

Zijuwe Dalili za minyoo na dalili kuu 9 za minyoo
Utajifunza dalili za minyoo, sababu za minyoo na namna ya kujiepusha na minyoo. Dalili kuu 5 za minyoo mwilini Soma Zaidi...

mimi mara ya mwisho kubleed ilikuwa tareh 3/9 nilisex tarehe 4 je ni kwel nna mimba maana hadi sasa sijableed au ni kawaida tu
Je unaijuwa siku yako hatari ya kupata mimba. Na itakuwaje kama tayari umebeba mimba changa. Nakala hii inakwenda kukushauri machache kuhusu maswali haya. Soma Zaidi...

mim ninaujauzito wa mwezi mmoja lakini naona kama hali fulani ya damu inanitoka sehemu ya Siri inafanana na damu ya wakati wa period
Kutokuwa na damu wakati wa ujauzito ni hali uliyo ya kawida lakini inapaswa kujuwa sifa za damu hiyo nabje unatoka kwa namna gani. Kama unasumbuliwa na tatizo hili makala hii ni kwa ajili yako. Soma Zaidi...

Mimi nilipima na kipimo mwenyewe nkakuta mistari miwili iliokoza lkn nikifanya tendo nakua naumia sana tatizo ni Nini docta
Je anapatwa maumivu 😭 makali wakati wa tendo la ndoa ama ukiwa katika hedhi? Soma makala hii hadi mwisho Soma Zaidi...

Fahamu siku za kubeba mimba na zisizo za kubeba mimba.
Posti hii inahusu zaidi siku za kubeba mimba na zisizo za kubeba mimba , tunapaswa kujua hivi Ili kuweza kupanga uzazi na kuepuka njia ambazo ni hatarishi kwa afya zetu. Soma Zaidi...

Zijue Dalili za hatari kwa Mama mjamzito
Posti hii inahusu zaidi dalili za hatari kwa Mama mjamzito, ni Dalili ambazo ujitokeza kwa Mama mjamzito, hizi Dalili zisipofanyiwa kazi mapema zinaweza kuleta shida kwa Mama kwa hiyo jamii nzima inapaswa kujua Dalili hizi na kuchukua hatua endapo zitajio Soma Zaidi...

Nini husababisha mtoto kukosa maji kabla ya kuzaliwa?
inaweza kutokea kuwa mtoto aliye tumboni akaishiwa maji hata kabla ya kuzaliwa. yes hali hii huweza kuwapata baadhiya watoto. Soma Zaidi...

Fahamu ugonjwa wa kifafa cha mimba.
Post hii inahusu zaidi Ugonjwa wa kifafa cha mimba ambapo kwa kitaalamu huitwa eclampsia, utokea pale ambapo Mama anapokuwa na degedege wakati wa mimba na baada ya kujiunga. Soma Zaidi...

Maambukizi kwenye kitovu cha mtoto.
Posti hii inahusu zaidi Maambukizi kwenye kitovu cha mtoto, ni Maambukizi ambayo yanaweza kutokea kwenye kitovu cha mtoto pale ambapo mtoto amezaliwa inawezekana ni kwa sababu ya hali ya mtoto au huduma kuanzia kwa wakunga na wale wanaotumia mtoto. Soma Zaidi...