Fahamu Ute unaotoka wakati wa ujauzito
Posti hii inahusu zaidi Ute unaotoka wakati wa ujauzito, kwa kawaida wakati wa ujauzito Kuna Ute ambao utoka na ni tofauti na kawaida pale mwanamke akiwa Hana mimba.
Fahamu Ute unaotoka wakati wa ujauzito.
1. Kwanza wakati wa ujauzito Kuna Ute ambao utoka na huwa ni mweupe kwa aina yake na ikitokea Ute huo ukawa na rangi tofauti na nyeupe kunakuwepo na maambukizi.
2. Ute huo uongezeka kwa sababu ya kuongezeka kwa homoni aina ya estrogen kwa sababu ya kufanya kazi mbalimbali kwenye mwili wa Mama wakati wa ujauzito kwa hiyo na Ute wakati wa ujauzito uongezeka zaidi.
3. Kwa upande wa akina Mama kama Kuna Ute wowote unaotoka wanapaswa kuwa makini Ili kuangalia ni Ute wa aje kwa sababu kama ni wa njano panakuwepo na maambukizi na hivyo ni vizuri kabisa kugundua na kuweza kupata matibabu.
4. Kwa sababu mabadiliko ya Ute usababishwa na hali yoyote iliyopo kwenye via vya uzazi kwa sababu kwenye via vya uzazi kama Kuna magonjwa kama vile kaswende na kisonono usababisha na rangi ya Ute kubadilika kwa hiyo kama Kuna aina yoyote ya mabadiliko ni vizuri kutafuta matibabu mapema na iwezekanavyo kwa sababu mtoto akipata maambukizi akiwa tumboni anaweza kupata shida ikiwepo kupoteza maisha.
5. Kwa upande wa akina Mama wajawazito hasa wanaochelewa kuanza clinic wanapaswa kuanza mara Moja Ili kuweza kupata vipimo mbalimbali kama vile vipimo vya magonjwa ya zinaa ikiwemo kaswende na Ukimwi, kwa kufanya hivyo hata kama mama hawezi kuangalia Ute wake hata kama una maambukizi anaweza kujua kama Kuna maambukizi kutokana na vipimo.
6. Kwa hiyo wajawazito wakiona Ute unaongezeka
Wakati wa ujauzito wasishangae wajue kuwa ni kawaida kwa sababu ya kuwepo kwa mabadiliko ya homoni na hasa hasa Ute uongezeka wakati wa kukaribia kujifungua, kwa hiyo wasishangae ni kawaida tu na pakiwepo wasiwasi wowote ni vizuri kuwaona wataalamu wa afya Ili kuweza kupata matibabu zaidi.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Madrasa kiganjani 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 ai web app 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 web hosting 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Mm tumbo linaniuma mara kwa mara na linakua kama linages alaf kichwa kinauma mara kwa mara na nakosa choo wakati mwingine na kiuno kinauma je?inawezakua n ujauzito? Maana nilshirki tendo la ndoa siku ya tano baada ya kutoka hedhi
Dalili za mwanzo za ujauzito zinaweza kuwa ni changamoto kwamwanamke hasa ikiwa ndio mimba yake ya kwanza. Maumivu ya tumbo, kujaa kwa tumbo gesi, kukosa choo ama hamu ya kula na kadhalika huweza pia kuambatana na ujauzito.
Soma Zaidi...Kondo la nyuma kuwa mbele ya mlango wa kizazi
Posti hii inahusu zaidi sababu za kondo la nyuma kuwa mbele ya mlango wa kizazi, kwa kawaida kondo la nyuma huwa nyuma ya mlango wa kizazi ila Kuna wakati kondo la nyuma ujishikisha mbele ya mlango wa kizazi.
Soma Zaidi...Huduma kwa mama mwenye kifafa cha mimba.
Posti hii inahusu zaidi huduma ambazo wajawazito wanaweza kuzipata wakiwa na Dalli au tayari wana kifafa cha mimba.
Soma Zaidi...Niharisha siku ya pili baada ya tendo. Jana hadi leo sijapata choo inawezakua nimeshika ujauzito?
Hivi unadhani kuharisha ni katika dalili za mimba, vipi kuhusu kutopata choo pia inaweza kuwa ni ujauzito?
Soma Zaidi...Hatua kwa hatua: Jinsi ya kulea ujauzito katika miezi tisa.
Safari ya ujauzito ni ya kusisimua, yenye mabadiliko mengi ya kimwili na kihisia. Kulea ujauzito kwa usahihi ni uwekezaji wa afya ya mtoto na mama. Mwongozo huu unatoa hatua kwa hatua jinsi ya kulea ujauzito katika kila trimester ili kuhakikisha mtoto anakuwa salama na mama anabaki na afya njema.
Soma Zaidi...