Fahamu Ute unaotoka wakati wa ujauzito
Posti hii inahusu zaidi Ute unaotoka wakati wa ujauzito, kwa kawaida wakati wa ujauzito Kuna Ute ambao utoka na ni tofauti na kawaida pale mwanamke akiwa Hana mimba.
Fahamu Ute unaotoka wakati wa ujauzito.
1. Kwanza wakati wa ujauzito Kuna Ute ambao utoka na huwa ni mweupe kwa aina yake na ikitokea Ute huo ukawa na rangi tofauti na nyeupe kunakuwepo na maambukizi.
2. Ute huo uongezeka kwa sababu ya kuongezeka kwa homoni aina ya estrogen kwa sababu ya kufanya kazi mbalimbali kwenye mwili wa Mama wakati wa ujauzito kwa hiyo na Ute wakati wa ujauzito uongezeka zaidi.
3. Kwa upande wa akina Mama kama Kuna Ute wowote unaotoka wanapaswa kuwa makini Ili kuangalia ni Ute wa aje kwa sababu kama ni wa njano panakuwepo na maambukizi na hivyo ni vizuri kabisa kugundua na kuweza kupata matibabu.
4. Kwa sababu mabadiliko ya Ute usababishwa na hali yoyote iliyopo kwenye via vya uzazi kwa sababu kwenye via vya uzazi kama Kuna magonjwa kama vile kaswende na kisonono usababisha na rangi ya Ute kubadilika kwa hiyo kama Kuna aina yoyote ya mabadiliko ni vizuri kutafuta matibabu mapema na iwezekanavyo kwa sababu mtoto akipata maambukizi akiwa tumboni anaweza kupata shida ikiwepo kupoteza maisha.
5. Kwa upande wa akina Mama wajawazito hasa wanaochelewa kuanza clinic wanapaswa kuanza mara Moja Ili kuweza kupata vipimo mbalimbali kama vile vipimo vya magonjwa ya zinaa ikiwemo kaswende na Ukimwi, kwa kufanya hivyo hata kama mama hawezi kuangalia Ute wake hata kama una maambukizi anaweza kujua kama Kuna maambukizi kutokana na vipimo.
6. Kwa hiyo wajawazito wakiona Ute unaongezeka
Wakati wa ujauzito wasishangae wajue kuwa ni kawaida kwa sababu ya kuwepo kwa mabadiliko ya homoni na hasa hasa Ute uongezeka wakati wa kukaribia kujifungua, kwa hiyo wasishangae ni kawaida tu na pakiwepo wasiwasi wowote ni vizuri kuwaona wataalamu wa afya Ili kuweza kupata matibabu zaidi.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 kitabu cha Simulizi 👉3 Madrasa kiganjani 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
Mimba Changa Hukaa Wiki Ngapi?
Katika lugha ya kawaida, "mimba changa" inarejelea miezi mitatu ya kwanza ya ujauzito, inayojulikana kitaalamu kama trimester ya kwanza. Kipindi hiki ni muhimu sana kwa ukuaji wa viungo vya mtoto na mabadiliko ya mwili wa mama. Makala hii inaelezea muda huu unavyohesabiwa na kile kinachotokea ndani ya kipindi hicho.
Soma Zaidi...Njia za uzazi wa mpango kwa akina Mama kuanzia miezi sita baada ya kujifungua mpaka mwaka mmoja
Posti hii inahusu zaidi njia za uzazi wa mpango kwa mama aliyejifungua kuanzia miezi sita mpaka mwaka mmoja.
Soma Zaidi...Mtoto anaanz kucheza kwa mda gan
Kuna watoto wengine huanza kucheza mapema kuliko watoto wengine. Tunapozungumzia kucheza kwa mtoto aliye tumboni yaani mimba hapa inatubidi tuangalie kwa undani zaidi, je ni muda gani mtoto ataanza kucheza?
Soma Zaidi...Dalili za mama mjamzito akikaribia kujifungua
Post hii inazungumzia mama wajawazito Mara tu mama anapohisi kuwa yeye ni mjamzito anashauriwa kuanza clinic.na clinic hizi zinasaidia kuwapatia wakina mama elimu,namna ya kumkinga Mtoto asipatwe na maradhi Kama UKIMWI. Pia mama anapoanza clinic
Soma Zaidi...Madhara ya vidonge vya P2
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kwa sababu ya kutumia mara kwa mara vidonge vya P2,
Soma Zaidi...Lazima matiti kuuma ka mimba changa?
Kuuma mwa matiti ni moka ya Ichiro kuwa huwenda ni ujauzito. Hii haimaanishi etindio mjamzito, zipo dalili nyingi za ujauzito. Hata hivyo kuona dalili za ujauzito haimaanishi umepata tayari ujauzito. Kwanza fanya vipimondipo Upate uhakika
Soma Zaidi...