Posti hii inahusu zaidi namna ya kuongea na Mama mjamzito ili kuweza kugundua tatizo lake na kutoa msaada pale penye uhitaji.
Namna ya kuongea na mjamzito.
1.Kwana kabisa hakikisha kama kuna mazingira ambayo yatafamfanya ajisikie vizuri na mazingira yawe na vitu vinavyohitajika na uhakikishe kubwa anaweza kukaa vizuri na kuweza kujisikia huru pale unapoongea naye.
2.Muulize kuhusu familia yake na watoto alionao kwa sasa na unapaswa kujua anataka kuwa na watoto wangapi, uliza kama anajua tarehe yake ya kujifungua kama hajui hakikisha anatoka kwako anajua tarehe maalum ya kujifungua.
3.Pia muuulize kama as mewahi kutumia uzazi wa mpango, na amepata faida gani au hasara zilizopata kutokana na uzazi wa mpango, kama hana taarifa yoyote kuhusu uzazi wa mpango mafundishe ba uhakikishe anajua jinsi ya kutumia uzazi wa mpango.
4.Ongea naye kuhusu dawa anazozitumia kwa sababu kuna wengine wanatumia dawa mbalimbali kama vile za kisukari, presha, degedege,na wengine dawa za kuongeza maisha, ongea naye na umpe ushauri kadri unavyoweza kuhusiana na matumizi ya dawa na matokeo yake.
5. Muuulize kuhusu matumizi ya vyakula mbalimbali kwa mfano ni vyakula gani anapendelea na kumshauri kuhusu mlo kamili kwa wajawazito hasa vyakula vya kuongeza damu na madini ya chuma anapaswa kuvitumia kwa wingi na pia anapaswa kuachana na vyakula ambavyo havina faida yoyote mwilini kama vile pemba na utumiaji wa mawe wakati wa ujauzito.
6.Pia ongea naye kuhusu matumizi ya vileo kama vile matumizi ya madawa ya kulevya, vileo vikali, uvutaji wa sigara, na vitu kama hivyo ambayo usababisha madhara makubwa kwa mtoto wakati akiwa tumboni, kama kuna matumizi yoyote ya vitu kama hivyo elimu inapaswa kutolewa ili kuzuia matumizi ya vileo
7.Pia tunapaswa kujua kama Mama amepata chanjo zinazohitajika wakati wa ujauzito kama vile chanjo ya pepopunda ambayo umkinga mama na mtoto dhidi ya magonjwa ya kupooza na Magonjwa mbalimbali mbalimbali, kama hajapata hakikisha mama anapata chanjo hiyo
8.Pia ongea na Mama kuhusu Maambukizi ya virusi vya ukimwi na matumizi ya madawa na pia kuhusu Magonjwa ya ngono na matumizi ya dawa, mama kama hana taarifa zozote kuhusu hayo anapaswa kupima na kupewa dawa kama kuna Maambukizi.
9.Pia Mama anapaswa kuwa na uhusiano mzuri na watu kwa sababu mimba inaweza kumfanya akabalika katika hali isiyo ya kawaida au pengine anaweza kuwa na hasira na watu basi Mama anapaswa kuambiwa wazi kuwa anapaswa kuwa chukuliwa watu Kawaida na kumhakikishia kuwa akijifungua kila kitu kitakuwa sawa.
10.Pia tunapaswa kujua hali ya uchumi wa Mama mjamzito kama anaweza kupata mahitaji ya kila siku ya kawaida na kama akifanikiwa wakati wa kujifungua kama ataweza kupata hela ya kununua mahitaji wakati wa kujifungua, kama hawezi tafuta jinsi ya kumsaidia na kumshauri akate bima ya shilingi elfu thelathini kwa watu sita na itaweza kumsaidia wakati wa kujifungua.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inahusu zaidi saratani zinazowashambulia watoto. Hizi ni aina mbalimbali za saratani ambazo upenda kuwasumbua watoto ambao ni chini ya umri wa miaka mitano na uleta madhara katika kipindi cha makuzi yao.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza baadhi ya dalili za mimba kuanzia week mbili Hadi mwezi
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukuletea njia za kutatua tatizo la nguvu za kiume
Soma Zaidi...Makala hii inakwenda kukueleza kuhusu siku za kupata mimba na dalili za siku hizo.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi imani potofu kwa mwanamke mwenye mimba, ni Imani ambazo zimekuwepo kwenye jamii kuhusu wanawake wenye mimba.
Soma Zaidi...Hizi ni siku za hatari kupata ujauzito.Siku hizi ndio siku za kupata mimba kwa urahisi
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi watoto mapacha wanaofanana,ni watoto wanaozaliwa wakiwa wanaofanana kwa sura na hata group la damu huwa ni Moja.
Soma Zaidi...Posti hii zaidi kazi ya Dawa ya metronidazole katika kutibu Minyoo, ni aina ya Dawa ambayo imetumiwa na watu wengi wakaweza kupona na kuepukana na minyoo. Zifuatazo ni baadhi ya kazi za metronidazole.
Soma Zaidi...Unaweza kupitiliza siku zako za hedhi kwa sababu nyingi. Post hii itakueleza ni kwa nini umechelewa kupata siku zako.
Soma Zaidi...Post hii itakwenda kukuletea orodha ya vyakla vinavyoaminika kuongeza nguvu za kiume.
Soma Zaidi...