Namna ya kuongeza na mjamzito ili kupata taarifa zake na kutoa msaada

Namna ya kuongeza na mjamzito ili kupata taarifa zake na kutoa msaada

Posti hii inahusu zaidi namna ya kuongea na Mama mjamzito ili kuweza kugundua tatizo lake na kutoa msaada pale penye uhitaji.

Download Post hii hapa

Namna ya kuongea na mjamzito.

1.Kwana kabisa hakikisha kama kuna mazingira ambayo yatafamfanya ajisikie vizuri na mazingira yawe na vitu vinavyohitajika na uhakikishe kubwa anaweza kukaa vizuri na kuweza kujisikia huru pale unapoongea naye.

 

2.Muulize kuhusu familia yake na watoto alionao kwa sasa na unapaswa kujua anataka kuwa na watoto wangapi, uliza kama anajua tarehe yake ya kujifungua kama hajui hakikisha anatoka kwako anajua tarehe maalum ya kujifungua.

 

3.Pia muuulize kama as mewahi kutumia uzazi wa mpango, na amepata faida gani au hasara zilizopata kutokana na uzazi wa mpango, kama hana taarifa yoyote kuhusu uzazi wa mpango mafundishe ba uhakikishe anajua jinsi ya kutumia uzazi wa mpango.

 

4.Ongea naye kuhusu dawa anazozitumia kwa sababu kuna wengine wanatumia dawa mbalimbali kama vile za kisukari, presha, degedege,na wengine dawa za kuongeza maisha, ongea naye na umpe ushauri kadri unavyoweza kuhusiana na matumizi ya dawa na matokeo yake.

 

5. Muuulize kuhusu matumizi ya vyakula mbalimbali kwa mfano ni vyakula gani anapendelea na kumshauri kuhusu mlo kamili kwa wajawazito hasa vyakula vya kuongeza damu na madini ya chuma anapaswa kuvitumia kwa wingi na pia anapaswa kuachana na vyakula ambavyo havina faida yoyote mwilini kama vile pemba na utumiaji wa mawe wakati wa ujauzito.

 

6.Pia ongea naye kuhusu matumizi ya vileo kama vile matumizi ya madawa ya kulevya, vileo vikali, uvutaji wa sigara, na vitu kama hivyo ambayo usababisha madhara makubwa kwa mtoto wakati akiwa tumboni, kama kuna matumizi yoyote ya vitu kama hivyo elimu inapaswa kutolewa ili kuzuia matumizi ya vileo 

 

7.Pia tunapaswa kujua kama Mama amepata chanjo zinazohitajika wakati wa ujauzito kama vile chanjo ya pepopunda ambayo umkinga mama na mtoto dhidi ya magonjwa ya kupooza na Magonjwa mbalimbali mbalimbali, kama hajapata hakikisha mama anapata chanjo hiyo 

 

8.Pia ongea na Mama kuhusu Maambukizi ya virusi vya ukimwi na matumizi ya madawa na pia kuhusu Magonjwa ya ngono na matumizi ya dawa, mama kama hana taarifa zozote kuhusu hayo anapaswa kupima na kupewa dawa kama kuna Maambukizi.

 

9.Pia Mama anapaswa kuwa na uhusiano mzuri na watu kwa sababu mimba inaweza kumfanya akabalika katika hali isiyo ya kawaida au pengine anaweza kuwa na hasira na watu basi Mama anapaswa kuambiwa wazi kuwa anapaswa kuwa chukuliwa watu Kawaida na kumhakikishia kuwa akijifungua kila kitu kitakuwa sawa.

 

10.Pia tunapaswa kujua hali ya uchumi wa Mama mjamzito kama anaweza kupata mahitaji ya kila siku ya kawaida na kama akifanikiwa wakati wa kujifungua kama ataweza kupata hela ya kununua mahitaji wakati wa kujifungua, kama hawezi tafuta jinsi ya kumsaidia na kumshauri akate bima ya shilingi elfu thelathini kwa watu sita na itaweza kumsaidia wakati wa kujifungua.

Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 811

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Dalili za hatari kwa mama aliyejifungua.
Dalili za hatari kwa mama aliyejifungua.

Posti hii inaelezea kiufupi kabisa kuhusiana na Dalili za hatari kwa mama aliyejifungua.

Soma Zaidi...
Fahamu ugonjwa wa kifafa cha mimba.
Fahamu ugonjwa wa kifafa cha mimba.

Post hii inahusu zaidi Ugonjwa wa kifafa cha mimba ambapo kwa kitaalamu huitwa eclampsia, utokea pale ambapo Mama anapokuwa na degedege wakati wa mimba na baada ya kujiunga.

Soma Zaidi...
Damu, uteute na maji yanayotoka ukeni kipindi cha ujauzito
Damu, uteute na maji yanayotoka ukeni kipindi cha ujauzito

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu damu, uteute na maji yanayotoka ukeni kipindi cha ujauzito

Soma Zaidi...
Dalili za mimba kuanzia week mbili Hadi mwezi
Dalili za mimba kuanzia week mbili Hadi mwezi

Somo hili linakwenda kukueleza baadhi ya dalili za mimba kuanzia week mbili Hadi mwezi

Soma Zaidi...
Mimi naumwa na tumbo chini ya kitovu upande wa kulia, ninapotok kushiriki tendo la ndoa ndonapata maumivu zaid pia nawashwa sehemu za siri itakuwa shida ni nin?
Mimi naumwa na tumbo chini ya kitovu upande wa kulia, ninapotok kushiriki tendo la ndoa ndonapata maumivu zaid pia nawashwa sehemu za siri itakuwa shida ni nin?

Maumivu ya tumbo baada ya tendo la ndoa yanaweza kuwa ni dalili ya maradhi fulani, ama shida kwenye mfumo w uzazi. PID na UTI hutuhumiwa kuwa ni katika sababu hizo. Ila zipo nyingine nyingi tu. Kama ina hali hii vyema ukafika kituo cha afya

Soma Zaidi...
Sababu za maumivu ya tumbo wakatu wa tendo la ndoa
Sababu za maumivu ya tumbo wakatu wa tendo la ndoa

Jifunze sababu kuu zinazosababisha kuhisi maumivu makali ya tumbo wakati wa kushiriki tendo la ndoa

Soma Zaidi...
Ujue Ute kwenye uke
Ujue Ute kwenye uke

Post hii inahusu zaidi Ute ambao umo kwenye uke, Ute huu utofautiana kulingana na hali ya mama aliyonayo, kama mama ana mimba uke utakuwa tofauti na yule ambaye hana mimba au kama Ute una una magonjwa na hivyo utakuwa tofauti.

Soma Zaidi...
Dalili ambazo mwanamke hapaswi kufumbia macho
Dalili ambazo mwanamke hapaswi kufumbia macho

Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo mwanamke hapaswi kufumbia macho.

Soma Zaidi...
Dalili Za hatari ambayo zinaweza kusababisha ugumba
Dalili Za hatari ambayo zinaweza kusababisha ugumba

Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo zilijitokeza zinaweza kusababisha ugumba hasa kwa wanawake, kwa hiyo ni vizuri kabisa kuwa makini kwa Dalili hizi hasa kwa wadada, kama kuna uwezekano wa matibabu tibu mapema ili kuepuka tatizo la kuwa mgumba.

Soma Zaidi...