Namna ya kuongeza na mjamzito ili kupata taarifa zake na kutoa msaada


image


Posti hii inahusu zaidi namna ya kuongea na Mama mjamzito ili kuweza kugundua tatizo lake na kutoa msaada pale penye uhitaji.


Namna ya kuongea na mjamzito.

1.Kwana kabisa hakikisha kama kuna mazingira ambayo yatafamfanya ajisikie vizuri na mazingira yawe na vitu vinavyohitajika na uhakikishe kubwa anaweza kukaa vizuri na kuweza kujisikia huru pale unapoongea naye.

 

2.Muulize kuhusu familia yake na watoto alionao kwa sasa na unapaswa kujua anataka kuwa na watoto wangapi, uliza kama anajua tarehe yake ya kujifungua kama hajui hakikisha anatoka kwako anajua tarehe maalum ya kujifungua.

 

3.Pia muuulize kama as mewahi kutumia uzazi wa mpango, na amepata faida gani au hasara zilizopata kutokana na uzazi wa mpango, kama hana taarifa yoyote kuhusu uzazi wa mpango mafundishe ba uhakikishe anajua jinsi ya kutumia uzazi wa mpango.

 

4.Ongea naye kuhusu dawa anazozitumia kwa sababu kuna wengine wanatumia dawa mbalimbali kama vile za kisukari, presha, degedege,na wengine dawa za kuongeza maisha, ongea naye na umpe ushauri kadri unavyoweza kuhusiana na matumizi ya dawa na matokeo yake.

 

5. Muuulize kuhusu matumizi ya vyakula mbalimbali kwa mfano ni vyakula gani anapendelea na kumshauri kuhusu mlo kamili kwa wajawazito hasa vyakula vya kuongeza damu na madini ya chuma anapaswa kuvitumia kwa wingi na pia anapaswa kuachana na vyakula ambavyo havina faida yoyote mwilini kama vile pemba na utumiaji wa mawe wakati wa ujauzito.

 

6.Pia ongea naye kuhusu matumizi ya vileo kama vile matumizi ya madawa ya kulevya, vileo vikali, uvutaji wa sigara, na vitu kama hivyo ambayo usababisha madhara makubwa kwa mtoto wakati akiwa tumboni, kama kuna matumizi yoyote ya vitu kama hivyo elimu inapaswa kutolewa ili kuzuia matumizi ya vileo 

 

7.Pia tunapaswa kujua kama Mama amepata chanjo zinazohitajika wakati wa ujauzito kama vile chanjo ya pepopunda ambayo umkinga mama na mtoto dhidi ya magonjwa ya kupooza na Magonjwa mbalimbali mbalimbali, kama hajapata hakikisha mama anapata chanjo hiyo 

 

8.Pia ongea na Mama kuhusu Maambukizi ya virusi vya ukimwi na matumizi ya madawa na pia kuhusu Magonjwa ya ngono na matumizi ya dawa, mama kama hana taarifa zozote kuhusu hayo anapaswa kupima na kupewa dawa kama kuna Maambukizi.

 

9.Pia Mama anapaswa kuwa na uhusiano mzuri na watu kwa sababu mimba inaweza kumfanya akabalika katika hali isiyo ya kawaida au pengine anaweza kuwa na hasira na watu basi Mama anapaswa kuambiwa wazi kuwa anapaswa kuwa chukuliwa watu Kawaida na kumhakikishia kuwa akijifungua kila kitu kitakuwa sawa.

 

10.Pia tunapaswa kujua hali ya uchumi wa Mama mjamzito kama anaweza kupata mahitaji ya kila siku ya kawaida na kama akifanikiwa wakati wa kujifungua kama ataweza kupata hela ya kununua mahitaji wakati wa kujifungua, kama hawezi tafuta jinsi ya kumsaidia na kumshauri akate bima ya shilingi elfu thelathini kwa watu sita na itaweza kumsaidia wakati wa kujifungua.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    2 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    3 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    4 Download App zetu hapa ujifunze zaidi    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Dalili za tezi dume ambayo hazijashuka (cryptorchidism)
Tezi dume ambayo haijashuka si ya kawaida kwa ujumla, lakini ni ya kawaida kwa wavulana waliozaliwa kabla ya wakati.na muda mwingine zikipanda tumboni huwa hazishuki kabisa kwenye korodani. Soma Zaidi...

image Ugonjwa wa kupoteza kumbukumbu.
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa kupoteza kumbukumbu ambao kwa kitaalamu huitwa Dementia ugonjwa huu uwapata wale ambao umri umekwenda lakini kwa wakati mwingine Usababishwa na vitu mbalimbali kama tutakavyoona. Soma Zaidi...

image Umuhimu wa kupiga push up kiafya
Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kupiga push up kiafya, ni mambo au faida zipatikanazo ki afya kwa wapigaji wa push up kama ifuatavyo. Soma Zaidi...

image Vyakula vya kupunguza presha ya kupanda
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu vyakula ambavyo vinaweza kupunguza presha ya kupanda Soma Zaidi...

image Hernia
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu ugonjwa wa hernia Soma Zaidi...

image Mishipa ya machozi kufunga kwa mtoto.
Posti inahusu nzaidi kufunga kwa mishipa ya machozi ya mtoto kwa kawaida mishipa ya mtoto inapaswa kufunguka baada ya mwaka mmoja lakini kwa wengine ubaki imefungwa hata baada ya mwaka mmoja na kusababisha madhara mbalimbali kwa mtoto. Soma Zaidi...

image Jifunze jinsi ya kumsaidia mwenye kifafa
Kifafa hakiambukizi na ugonjwa wa ubongo lakini kifafa pia hakiathiri akili au ubongo Ila kikiwa kifafa Cha kudumu na Cha nguvu ndio huweza kuadhiri. Pia Kuna kifafa Cha mimba na kifafa Cha kawaida.kifafa Cha mimba ndio kinahatari Sana kuliko Cha Kawaida. Soma Zaidi...

image Matibabu ya vidonda sugu
Some Hili linakwenda kukueleza kuhusu matibabu ya vidonda vya tumbo sugu Soma Zaidi...

image Maambukizi kwenye mifupa
Posti hii inahusu zaidi Maambukizi kwenye mifupa ambayo kwa kitaalamu huitwa Osteomyelitis, ugonjwa huu uaribu zaidi kwenye mifupa na sehemu nyingine ambazo zinakaribia kwenye mifupa Soma Zaidi...

image Dalili za ujauzito: Nini kinatokea kwanza
Je, unafahamu dalili za mwanzo za ujauzito? Kutoka kwa kichefuchefu hadi uchovu, ujue nini cha kutarajia. Soma Zaidi...