picha

Njia za uzazi wa mpango kwa wanaonyonyesha.

Posti inahusu zaidi njia maalum za uzazi wa mpango kwa wanaonyonyesha,Ni njia za uzazi ambazo wanaonyesha wanatumia kwa sababu kuna njia nyingine zikitumiwa na wanaonyonyesha zinaweza kuleta matatizo kwa watoto au kusababisha maziwa kutokuwa na vitamini v

Njia za uzazi wa mpango kwa wanaonyonyesha.

1. Kwanza kabisa tunajua kuwa maziwa ya Mama yanapaswa kuwa na virutubisho vyote vinavyohitajika kuna wakati mwingine virutubisho hivyo vinaweza kupunguza kwa sababu mbalimbali kama vile madawa, aina ya vyakula na njia mbalimbali za uzazi wa mpango ili kuepuka tatizo hili wanawake wanaonyonyesha wanapaswa kutumia njia zifuatazo.

 

2.Matumizi ya kitanzini.

Hii njia utumiwa na wanawake wanaonyonyesha kwa sababu haingiliani na uzalishaji wa maziwa, kitanzi hiki kimetengenezwa na madini ya kopa na uwekwa kwenye mlango wa kizazi na  kinaweza kukaa kwa mda wa miaka kumi na miwili, kwa hiyo uzuia mbegu za kiume kutokutana na mbegu za kike kwa hiyo mimba haiwezi kutungwa.

 

3.Pia wanaonyonyesha wanaweza kutumia njiti kwa sababu haingiliani na uzalishaji wa maziwa, huu njiti uwekwa mwilini juu ya mkono na uweza kuzuia mimba kwa kipindi cha miaka mitano, kwa hiyo kina homoni ambayo uzuia yai kupevuka kwa hiyo njia hizi inaweza kuwa na maudhi madogo madogo kama vile kutapika, kichefuchefu na kizungu Zungu na hivyo uisha kwenye miezi ya mwanzo na maisha uendelee kama kawaida.

 

4.Njia ya kutumia homoni ya progesterone peke yake iwe ya kuchoma au kutumia vidonge, hii ni njia ambayo uzuia yai lisipevuke na pia haingiliani na uzalishaji wa maziwa kwa hiyo mama anayenyonyesha anapaswa kutumia progesterone homoni peke yake asije akachanganya na oestrogen kwa sababu uingiliana na uzalishaji wa maziwa.

 

5.Pia Mama anaweza kutumia njia ya kunyonyesha kwa miezi sita ya mwanzoni baada ya hapo anaweza kutumia njia yoyote ya uzazi wa mpango, na pia kama familia haina mpango wa watoto wengine wanaweza kutumia njia ya kudumu ambapo wote wawili wanakata  mirija inayosafirisha mbegu na yai kwa kufanya hivyo hawawezi kupata watoto tena, kwa hiyo hizi ndio njia pekee kwa wanaonyesha na pia kondomu inaweza kutumika.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 11559

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰2 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     πŸ‘‰4 ai web app     πŸ‘‰5 web hosting     πŸ‘‰6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

Tatizo la kutokwa na majimaji kwenye uume.

Posti hii inahusu zaidi tatizo la kutokwa na majimaji kwenye uume, ni tatizo ambalo uwakumba baadhi ya wanaume kwa sababu mbalimbali na pia Ugonjwa huu unatibika hasa kwa wale wanaowahi kupata matibabu.

Soma Zaidi...
Kujaa gesi tumboni

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za kujaa tmgesi tumbon

Soma Zaidi...
Dalili za kujifungua

Makala hii itakwenda kukufundisha dalili za kujifunguwa, hatuwa za kujifunguwa na kuzalisha, pia utajifunza mabo muhimu kabla na wakatii wa kujifungua.

Soma Zaidi...
Sababu za kutokea kwa saratani ya matiti

Saratani ya matiti ji moja kati ya saratani zinazosumbuwa wqnawake wengi. Katika somo hili utajifunza chanzo cha kutokea saratani ya matiti

Soma Zaidi...
Je ?kipimo kikionyesha misitar miwili mmoja hafifu mwingine umekolea ni mimba au sio

Kipimo chamimba cha mkojo, huonyesha nestory miwili kuwa una mimba, na mmoja kuwa huna mimba. Sasa je ukitokea mmoja umekoleana mwingine hafifu? Endelea na pasti Òœï¸ hadi mwisho

Soma Zaidi...