Njia za uzazi wa mpango kwa wanaonyonyesha.
Posti inahusu zaidi njia maalum za uzazi wa mpango kwa wanaonyonyesha,Ni njia za uzazi ambazo wanaonyesha wanatumia kwa sababu kuna njia nyingine zikitumiwa na wanaonyonyesha zinaweza kuleta matatizo kwa watoto au kusababisha maziwa kutokuwa na vitamini v
Njia za uzazi wa mpango kwa wanaonyonyesha.
1. Kwanza kabisa tunajua kuwa maziwa ya Mama yanapaswa kuwa na virutubisho vyote vinavyohitajika kuna wakati mwingine virutubisho hivyo vinaweza kupunguza kwa sababu mbalimbali kama vile madawa, aina ya vyakula na njia mbalimbali za uzazi wa mpango ili kuepuka tatizo hili wanawake wanaonyonyesha wanapaswa kutumia njia zifuatazo.
2.Matumizi ya kitanzini.
Hii njia utumiwa na wanawake wanaonyonyesha kwa sababu haingiliani na uzalishaji wa maziwa, kitanzi hiki kimetengenezwa na madini ya kopa na uwekwa kwenye mlango wa kizazi na kinaweza kukaa kwa mda wa miaka kumi na miwili, kwa hiyo uzuia mbegu za kiume kutokutana na mbegu za kike kwa hiyo mimba haiwezi kutungwa.
3.Pia wanaonyonyesha wanaweza kutumia njiti kwa sababu haingiliani na uzalishaji wa maziwa, huu njiti uwekwa mwilini juu ya mkono na uweza kuzuia mimba kwa kipindi cha miaka mitano, kwa hiyo kina homoni ambayo uzuia yai kupevuka kwa hiyo njia hizi inaweza kuwa na maudhi madogo madogo kama vile kutapika, kichefuchefu na kizungu Zungu na hivyo uisha kwenye miezi ya mwanzo na maisha uendelee kama kawaida.
4.Njia ya kutumia homoni ya progesterone peke yake iwe ya kuchoma au kutumia vidonge, hii ni njia ambayo uzuia yai lisipevuke na pia haingiliani na uzalishaji wa maziwa kwa hiyo mama anayenyonyesha anapaswa kutumia progesterone homoni peke yake asije akachanganya na oestrogen kwa sababu uingiliana na uzalishaji wa maziwa.
5.Pia Mama anaweza kutumia njia ya kunyonyesha kwa miezi sita ya mwanzoni baada ya hapo anaweza kutumia njia yoyote ya uzazi wa mpango, na pia kama familia haina mpango wa watoto wengine wanaweza kutumia njia ya kudumu ambapo wote wawili wanakata mirija inayosafirisha mbegu na yai kwa kufanya hivyo hawawezi kupata watoto tena, kwa hiyo hizi ndio njia pekee kwa wanaonyesha na pia kondomu inaweza kutumika.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 kitabu cha Simulizi 👉3 Kitabu cha Afya 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Mabadiliko ya via vya uzazi kwa Mama mjamzito.
Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye via vya uzazi kwa wajawazito, tunajua kuwa Mama akibeba mimba tu kuna mabadiliko utokea katika sehemu mbalimbali za mwili.
Soma Zaidi...Fahamu dalili za hatari kwa wajawazito.
Posti hii inahusu zaidi dalili za hatari kwa mama mjamzito, kwa sababu kuna baadhi ya Dalili zikitokea kwa mama mjamzito ni vizuri kabisa kuwahi hospitali mara moja.
Soma Zaidi...Tatizo la kutokwa na utelezi wenye damu baada ya hedhi
Posti hii inahusu zaidi dalili mbalimbali za kutokwa na damu baada ya hedhi hili ni tatizo ambalo uwapata wanawake wengi pamoja na akina Mama kwa sababu ya kutokwa na damu yenye utelezi baada ya hedhi.
Soma Zaidi...Mimi kwenye korodani yai moja limezungukwa na majimaji ,na haya maji yamekuwepo toka utotoni mwangu lakin bado sijayaona matatizo yake , je kitaaramu hii inaweza kua na athari gani? ,Naombeni ushauri
Korodani ni kiungo muhimu kwa mwanaume, katika afya ya uzazi. Unaweza kusema ni kiwanda cha kutengeneza mbegu za kiume. Kiungo hiki ni sawa na ovari kwa mwanamke.
Soma Zaidi...Dalili za ongezeko la homoni ya estrogen
Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo mtu anaweza kupata ikiwa homoni ya estrogen imeongezeka, hizi dalili zikitokea mama anapaswa kuwahi hospital ili kuweza kupata matibabu au ushauri zaidi.
Soma Zaidi...Je siku ya kwanza kabisa ya ovulation mimba inakuwa ni uhakika kupata mimba?
Watu wengi wanadhania kuwa kufanya tendo la ndoa katika siku hatari ni lazima kuwa utapata ujauzito. Hili sio sahihi kabisa. Post hii itakwenda kuangalia jambo hili zaidi.
Soma Zaidi...