Dalili za mimba katika mwezi wa kwanza

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za mimba katika mwezi was kwanza

DALILI ZA MIMBA KATIKA MWEZI WA KWANZA (Ndani ya siku 30)Dalili hizi huweza kuonekana kwa urahisi kuliko hizo ambazo zimetajwa hapo juu. Ijapokuwa dalili hizi zinatokea ndani ya mwezi mmoja lakini zinaweza pia kutokea nje ya mwezi mmoja, yaani mpaka miezi mitatu. Sasa hebu tuzione dlili hizo:-

 

1.Kukosa hedthi.Kama ujauzioto ulishika mwanamke hataweza kupata siku zake. Hii ni dalili ambayowanawake wengi wamekuwa wakiamini kama ndio dalili pekee. Yes hii ni katika dalili kubwa ambazo wanawake wengi wameitaja kuwa ndio dalili yao ya kwanza. Unajuwa ni kwa nini? Ni kwa sababu ndio ya pekee wanayoweza kuigundua. Ukweli ni kuwa kukosa hedhi pekee sio dalili ya ujauzito, hedhi inaweza kukosekana kwa sababu kadhaa kama zifuatazo:-

 

A.Mabadiliko ya homoniB.UjauzitoC.MaradhiD.PIDE.VyakulaF.Stress na misongo ya mawazoG.Matumizi ya madawaH.Mabadiliko ya hali ya hewa.

 

Nini mwanamke afanye baada ya kukosa hedhi?.Yes hili ni swali zuri sana. Mwanamke aliyekosa hedhi kwanza aanze kufikiria kama alishiriki tendo la ndoa katika siku hatari ama laa. Kisha aangalie uwepo wa dalili nyingine kama nitakavyozitaja hapo chini. Kama hana dalili yeyote basui aangalie kama anapata maumivu sehemu yeyote, ama uwepo wa maradhi. Kama vyote hana ni vyema apime ujauzito. Kipimo cha mkojo kinaweza kuchelewa kutoa majibu, hivyo kama atapima wiki ya kwanz na asione kitu basi ni vyema akarudia tena wiki inayofata. Maelezo zaidi juu ya kutumia kipimo nitayataja hapo chini.

 

2.Maumivu ya matiti na chuchu, kujaa kwa matiti na mabadiliko ya rangi za chuchu.Dalili hii huwapata wanawake wengi, hata hivyo wapo ambao hawaipati kabisa. Hebu tuanze kuona kwa ufupi dalili hii. Mabadiliko ya rangi ya chuchu na eneo la kuzunguka chuchu. Hii ipoje ni kuwa mwanamke aliyebeba ujauzoto chuchu zake zinaweza kubadilika na kuweka ukiza na weusi. Inaweza kuwa chuchu pekee na na eneo la chini kuzunguka chuchu.

 

Kwa baadhi ya wanawake wao matiti yanauma na yanakuwa kama yamejawa na kaugumu flani. Wakati mwimgine inaweza kuwa titi moja ama yanaweza kuwa yote ama yakapeana zamu. Ila maumivu haya ni maumivu ambayo yanavumilia si makali kiasi cha kushindwa kufanya shughuli za kawaida. Kwa wanawake wengine maumivu haya hutokea pale anapoyaminya matiti yake.

 

Hata hivyo maumivu ya matiti pekee sio dalili ya moja kwa moja kuthibitisha ujauzito. Maumivu ya matiti yanaweza pia kusababishwa na maumivu ya kifua, shida katika homoni ama maradhi mengine. Hivyo bado itahitajika kupuma kupata uhakika.

 

3.Kukojoa mara kwa mara.Wiki kadhaa zimepita toka kuingia, homoni mbalimbali zimezalishwa ndani ya mwili,kwa ajili ya kuhakikisha usalama wa mama na mtoto. Homoni hizi zinapelekea mabadiliko mbalimbali ndani ya mwili wa mama, hivyo kusababisha mapigo ya moyo kuongezeka, mchujo wa damu kuwa mkubwa na uzalishwaji wa mkojo kuongezeka. Hapa mama mjamzito ataanza kuhisi mabadiliko katika kukojoa kojoa. Dalili hii kwa baadhi yao inachelewa kuonekana hadi miezi ya mbele.

4.Mapigo ya moyo kuongezeka.Hapa mwanamke anaweza kujihisi moyo kwenda mbio. Ukweli nikuwa kuna ongezeko la mapigo ya moyo kwa ajili ya kuhakikisha maendeleo ya mtoto aliyetumboni hayaathiriki. Dalili hii pia inaweza kuchelewa kuonekana ndani ya mwezi wa kwanza. Kwa baadhi ya wanawake watajihisi lamda ana presha lakini ukweli ni kuwa hii sio presa ni ongezeko tu la mapigo ya moyo.

 

5.Maumivu ya tumbo.Dalili hii inaweza kutokea hata katika wiki kadhaa za mwanzo. Ila mara nyingi hutokea ndani ya mwezi wa kwanza na ni endelevu. Yaani dalili hii inaweza kuendeea mpaka mtoto atakapozaliwa. Mwanamke awe makini sana na maumivu haya. Maana yanaweza kusababishwa pia na mambo mengine ikiwemo maradhi. Maumivu haya hayawezi kuwa makali kiasi cja kushindwa kufanya kazi za kawaida. Yanaweza kufanana na ya hedhi ama kuwa na uafadhali kidogo.

 

DALILI NYINGINE ZA UJAUZITO1.Uchovu wa mara kwa mara

2.Maumivu ya tumbo mara kwa mara

3.Kichefuchefu

4.Tumbo kukuwa.

5.Mtotockucheza

6.Kuongezeka kwa uzito

7.Kupata kiungulia mara kwa mara

8.Kukosa choo

9.Maumivu ya mgongo

10.Hasira za mara kwa mara

11.Maumivu maeneo ya nyonga

12.Kuharisha

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 13347

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Dua za Mitume na Manabii    👉3 web hosting    👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Maumivu wakati wa hedhi.

Posti hii inahusu zaidi maumivu wakati wa hedhi, haya ni maumivu ambayo utokea wakati wa hedhi kwa wanawake walio wengi, wengine huwa hawayapati kabisa na wengine hutapata na kwa kiwango kikubwa kutegemea na matatizo mbalimbali kama tutakavyoona.

Soma Zaidi...
Ukweli kuhusu njia za uzazi wa mpango.

Posti hii inahusu zaidi ukweli kuhusu njia za uzazi wa mpango, sio kwa imani potofu ambazo Watu utumia kuelezea uzazi wa mpango.

Soma Zaidi...
Fahamu Ute unaotoka wakati wa ujauzito

Posti hii inahusu zaidi Ute unaotoka wakati wa ujauzito, kwa kawaida wakati wa ujauzito Kuna Ute ambao utoka na ni tofauti na kawaida pale mwanamke akiwa Hana mimba.

Soma Zaidi...
Saratani zinazowasumbua watoto.

Posti hii inahusu zaidi saratani zinazowashambulia watoto. Hizi ni aina mbalimbali za saratani ambazo upenda kuwasumbua watoto ambao ni chini ya umri wa miaka mitano na uleta madhara katika kipindi cha makuzi yao.

Soma Zaidi...
Vyanzo vya mwanamke kushindwa kupata ujauzito

Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya mwanamke kushindwa kupata ujauzito, kwa sababu kuna sababu nyingi ambazo Usababisha mwanamke kushindwa kupata ujauzito kama tutakavyoona hapo mbeleni

Soma Zaidi...
Kutokwa maji yan seminal swhemu za siri kwa mwanamke nidalili ya ugojwa gan?

Kutokwa Majimaji sehemu za siri kwa mwanamke sio jambo la kushangaza na kuhisivunaumwa. Majimajivhaya ndio huboresha afya ya uzazi kwa kusafisha na kulinda via vya uzazi. Lakini majimajivhaya yakiwa mengi, ama yanawasha ama yanaharufu haa ndipo kwenye tat

Soma Zaidi...
TATIZO LA KUVIMBA KWA USO NA MIGUU KWA WAJAWAZITO

KUVIMBA VYA MIGUU KWA WAJAWAZITO Kuvimba kwa miguu ni hali inayowapara wengi katika wajawazito.

Soma Zaidi...
NAMNA YA KUBORESHA MBEGU ZA KIUME, NA VYAKULA VYA KUBORESHA NGUVU ZA KIUME

Njoo ujifunze vyakula vya kuboresha mbegu za kiume na nguvu za kiume.

Soma Zaidi...
Uzazi wa mpango kwa njia ya kumwaga manii nje.

Posti hii inahusu zaidi uzazi wa mpango kwa njia ya kumwaga shahawa nje, hii ni njia mojawapo kati ya njia za uzazi wa mpango ambapo mwanaume humwaga nje mbegu ili asimpatie Mama mimba.

Soma Zaidi...