Namna za kujilinda na fangasi ukeni
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuepuka fangasi za ukeni, ni njia ambazo usaidia kuepuka madhara ya fangasi za ukeni.
. Njia za kuepuka madhara ya fangasi za ukeni
1.Epuka kusafisha sehemu za Siri kwa kutumia vitu vyenye kemikali kali usababisha kuuua bakteria wazuri ambao hukaa sehemu za Siri na kubakiza bakteria wabaya ambao uleta ma
ambukizi kwenye sehemu za Siri, vitu vyenye kemikali kali ni kama vile sabuni, pafuume na mambo kama hayo ambayo ni hatari kwa sehemu za uke.
2.Epuka kutawadha kutoka nyuma kwenda mbele.
Wakati wa kutawadha epuka Ile hali ya kutawadha kutoka nyuma kuelekea mbele, kwa sababu kwenye kinyesi Kuna bakteria ambao wakiingia kwenye sehemu ya uke wanaosababisha fangusi kwenye sehemu za uke kwa hiyo tuna tunapaswa kujitawadha kutoka mbele kwenda nyuma Ili kuepuka kutoa bakteria kutoka kwenye kinyesi kwenda kwenye sehemu za via vya uzazi.
3.Hakikisha kinga ya mwili Iko juu
Katika maisha ya kila mtu tunapaswa kuhakikisha kinga ya mwili Iko juu kwa kiwango kikubwa kwa kula vyakula mbalimbali ambavyo vinaongeza kinga mwilini na kuhakikisha kula vyakula vyenye mlo kamili na sawia,kama vyakula vya protein, vyakula vya mafuta, vyakula vya mafuta,vitamini, madini, mboga za majani na matunda pia unywaji wa maji kwa wingi vyote hivi vikiwa sawia usaidia kujenga mwili na kuwa na kinga.
5.Mtibu mpenzi wako kama ana ugonjwa wa fangasi. Kama una mpenzi wako na umegungua kuwa ana fangasi hakikisha mmeenda hospitalini na kupima na kutumia dawa za kutibu fangasi, pia hakikisha dawa zinamezwa kwa uangalifu na zinaisha kwa mda wake na dawa zikiisha Rudi hospitalini mkapime vizuri na kuhakikisha kuwa ugonjwa imeisha.
6.Punguza matumizi ya vyakula vyenye sukari kwa wingi na pia epuka kutumia marashi kwenye sehemu za Siri kwa sababu uua bakteria ambao ulinda sehemu za mwili na kusababisha maambukizi ya fangasi kwenye uke, pia vyakula vya sukari vinapaswa kupunguzwa na kutumika kwa kiwango kidogo sana.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 Kitabu cha Afya 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 web hosting 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
Namna ya kutibu ugumba kwa Mwanaume.
Posti hii inahusu zaidi namna ya kutibu tatizo la ugumba kwa Mwanaume, ni njia ambazo utumiwa na wataalam mbalimbali Ili kuweza kutibu tatizo la ugumba kwa wanaume.
Soma Zaidi...dalili za mimba changa na siku ya kupata mimba
Jifunze namna ya kuthibitisha dalili za ujauzito kuwa ni za kweli. Tambuwa namna ya kupima mimba na muda mujarabu wa kupima
Soma Zaidi...Kwa nini hujapata siku zako za hedhi.
Unaweza kupitiliza siku zako za hedhi kwa sababu nyingi. Post hii itakueleza ni kwa nini umechelewa kupata siku zako.
Soma Zaidi...Mambo ambayo mama anapaswa kujua akiwa mjamzito
Posti hii inahusu zaidi mambo anyopaswa kujua akiwa mjamzito. Ni mambo muhimu ya kuzingatia kwa mama akiwa mjamzito.
Soma Zaidi...Njia za kugundua kama mtoto amevunjika baada ya kuzaliwa
Post hii inahusu zaidi njia mbalimbali ambazo mtoa huduma anaweza kuzitumia kuangalia kama mtoto amevunjika baada ya kuzaliwa.
Soma Zaidi...Faida na hasara za Kufunga kizazi kwa Wanaume
Posti hii inazungumzia Faida, hasara, na madhara ya Kufunga kizazi kwa Wanaume.
Soma Zaidi...