Tunahitaji kuwa na protini mwilini. Kuna baadhi ya makundi ya watu wanahitaji protini zaidi. Je unawajuwa hao ni kina nana?, na je unauwa kazi za protini mwilini na athari za upungufu wake? endelea na makala hii.
Katika viinilishe muhimu mwili unavyohitaji amabavyo ni fati, protini, vitamini na wanga na mafuta mwili unahitaji protini kwa kiasi kikubwa kila siku. mwili unaweza kuibadili protini kuwa fati lakini si fati kuwa protini. hivyo protini ni kiinilishe muhimu zaidi ndani ya miili yetu. Katika makala hii nimekuandalia mambo muhimu unayopaswa kuyajuwa kuhusu protini na vyakula vya protini, faida zake na hasara zake. Madhara ya kiafya yanayohusiana na protini pamoja na kuyaepuka madhara hayo. Makala hii imeandaliwa wa kufuata nukuu na makala kutoka kwa wataalamu wa Afya na lishe.
YALIYOMO
Katika makala hii tutakwenda kuona
MUKTASARI KUHUSU PROTINI.
Protini ni chembechembe zinazotokea kwa njia ya asili (bila ya kutengenezwa) na zimetokana na asidi za amono (amino acid) zilizounganishwa kwa kutupia bondi za peptide. Neno protini asili yake ni lugha ya Kigiriki ”proteios” likiwa na maana ya kuwa ni kitu kinachopewa nafasi ya kwanza. Yaani protini ni viinilishe “nutrients” ambazo ni muhimu sana mwilini kuliko viinilishe vingine. Neno hili limeanzaka kutumiwa karne ya 19 mwaka 1838 na Mkemia kutoka Swedih Jöns Jacob Berzelius.
Protini huweza kutofautiana namna zilivyo kutoka kiumbe kimoja na chingine, pia protini huweza kutofautiana kutoka kiungo kimoja kwenda kingine. Kwa mfano protini za kwenye macho ni tofauti na zile za kwenye moyo, ini na figo. Kila kiumbe hai kina protini, na pia protini huhusika katika michakato tata kwenye miili ya viumbe hai, kwa mfano protini huhusika katika kutengeneza antibodies ambazo hutengeneza kinga na kupambana na maradhi na wadudu shambulizi kama bakteria na virusi. Protini hutengeneza enxymes ambazo ndizo hutumika katika kumeng’enya chakula. Pia protini hutengeneza homoni (hormones)
Baada ya kukila chakula chenye protini chakula kinaanza kumengenywa kinapofika kwenye tumbo na utumbo, kisha hufyonzwa kwenye utumbo mdogo na kuingia kwenye mirija ya damu. Pindi chembechembe za protini zinapoingia kwenye damu, damu huanza kusafirisha protini kwenda maeneo mbalimbali ya mwili yanayohitajia protini. Huko protini zitaingia kwenye seli za mwili. Ndani ya seli mchakato kwa kuvunjwa vunjwa protini ili kutumiwa zaidi hufanyika. Ndani ya seli mchakato huu jhufanyka kwenye sehemu inayotambulika kitaalamu kama ribosomes
Miili ya wanyama haina uwezo wa kuhifadhi protini kwa matumizi ya baadaye. Hivyo kama mtu atakula protini nyingi, mwili utaibadili protini kuwa fati na baadaye kutumika kutengeneza nishati ndani ya mwili. Na endapo mtu hataweza kupata protini za kutosha mwili utaanda kuangalia maeneo yenye protini ndingi kama misuli, kisha mwili utaanza kuvunja protini iliyomo mule na kuipeleka maeneo mengine na hapa mtua ataanza kukonda na kupoteza nyama na hatimaye kufariki kama hatapata chakula chenye protini.
VYAKULA VYENYE PROTINI
Tunaweza kupata protini kwenye mimea jamii ya mikunde kama kunde na maharagwe. Pia kiasi kikubwa cha protini tunaweza kukipata kwa kula mayai, nyama, samaki, dagaa na maziwa. Pia tunaweza kupata protini kwa kula nafaka kama mchele na nafaka zingine. Ulaji wa mboga za majani unaweza pia kutupatia protini kwa kiasi kidogo. Wadudu kama kukbikukbi, senene na wengineo pia wanaweza kutupatia protini.
Kwa kifupi vyakula vinavyotupatia protini ni pamoja na :-
KAZI ZAPROTINI NA VYAKULA VYA PROTINI MWILINI
Kwa kuwa sasa tunajua vyanzo vya protini sana ni vyemna tukaziona kazi za protini ndani ya miili yetu. Waandishi wengi wamekuwa wakiandika kazi za protini, na kuziorodhesha katika kazinyingi. Lakini katika makala hii itakuletea kazi zilizo kuu za protini.
Kazi za protini mwilini:-
UPUNGUFU WA VYAKULA VYA PROTINI
Kama tulizoona faida za protini ndani ya miili yetu basi pia itambulike kuwa kuna hasara kubwa za kiafya endapo mtu atashindwa kupata protini za kutosheleza ndani ya miili yetu. Hapo chini nitakuorodheshea tu baadhi ya madhara ya kukosa protini ya kutosha:
ULAJI WA PROTINI KUPITILIZA
Kwa upande wa pili ulaji wa protini nje ya kiwango unaweza kuleta athari hasi katika afya ya mlaji. Zifuatazo ni madhara ya kula vyakula vya protini kupitiliza
Je! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu
Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF
Share On
Facebook
or
Whatsapp
Imesomwa mara 1541
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi
👉2 Madrasa kiganjani
👉3 Kitau cha Fiqh
👉4 Kitabu cha Afya
Namna ya kumsaidia mtoto mwenye degedege
Degedege ni ugonjwa unaoshambulia sana watoto chini ya miaka mitano,na uwaletea matatizo mengi pamoja na kuwepo kwa ulemavu na vifo vingi vinavyosababishwa na ugonjwa huu. Soma Zaidi...
Upungufu wa maji
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya upungufu wa maji mwilini Soma Zaidi...
Umuhimu wa asidi iliyokwenye tumbo( kwa kitaalamu huitwa HCL)
Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa asidi iliyo kwenye tumbo kwa kitaalamu huitwa HCL, ni asidi inayofanya kazi nyingi hasa wakati wa kumengenya chakula. Soma Zaidi...
Njia za kujikinga na kisukari
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kujikinga na kisukari Soma Zaidi...
Sababu za kumsafisha mgonjwa kinywa
Posti hii inahusu zaidi sababu za kumsafisha mgonjwa kinywa, Mgonjwa akiwa anaumwa na pia anakula chakula ni lazima asafishwe kinywa Ili kuweza kuepuka madhara mengine yanayoweza kujitokeza kwa sababu ya kuwepo kwa uchafu kinywani. Soma Zaidi...
Kazi za chanjo ya polio
Posti hii inahusu zaidi kazi ya chanjo za polio na kazi zake,hii ni chanjo ambayo unazuia maambukizi ya Virusi vinavyosababisha polio. Soma Zaidi...
Haya hayawezi kuambukiza UKIMWI
Somo hili linakwenda kukuletea mambo ambayo hayawezi kuambukiza UKIMWI Soma Zaidi...
Upungufu wa vyakula na madhara yake
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya upungufu wa vyakula Soma Zaidi...
Ratiba ya chanjo ya Pentavalenti
Posti hii inahusu zaidi chanjo ya pentavalent ni aina ya chanjo ambayo inazuia Magonjwa matano ambayo ni kifadulo, pepopunda, homa ya ini na magonjwa yanayohusiana na upumuaji. Soma Zaidi...
Vifaa vya kutumia wakati wa kusafisha vidonda.
Posti hii inahusu zaidi vifaa vya kutumia wakati wa kusafisha vidonda, ni vifaa muhimu ambavyo mara nyingi kutwa hospitalini. Soma Zaidi...
Imani potofu juu ya chanjo.
Post hii inahusu zaidi Imani potofu juu ya chanjo kwa watoto na akina Mama, ni baadhi ya Imani waliyonayo watu juu ya chanjo. Soma Zaidi...
Malengo ya kutibu ukoma
Posti hii inahusu zaidi malengo ya kutibu ukoma, ni malengo ambayo yamewekwa na wizara ya afya ili kuweza kutokomeza ukoma kwenye jamii Soma Zaidi...