Post hii inahusu huduma ya kwanza kwa mtu aliyeingiwa na uchafu au kitu chochote sikioni. Sikio ni mojawapo ya milango ya fahamu ambapo hutumika kusikia, Kuna wakati vitu uingia ndani yake na kuleta madhara
Dalili za mtu aliyeingiza kitu chochote sikioni inawezekana kuwa maharage, mahindi, wadudu na vitu vingine kama hivyo ambavyo hupendelewa na watoto.
Dalili za mtu aliyeingiza kitu sikioni
1. Maumivu makali
2. Maambukizi kwenye sikio
3. Kuvimba ndani ya sikio
4. Sikio kuwa jekundu
5. Kushindwa kusikia vizuri
6. Kutoka uchafu sikioni
Vifuatavyo ni vitu vinavyoweza kuingia sikioni
1. Maharage
2. Mahindi
3. Wadudu
4. Mchanga
5. Toyi
6. Makaratasi madogo madogo
Tufanyeje Ili kuepusha Hali ya kuingia maharage, mahindi na vitu vingine kwenye sikio?
1. Watoto wanapaswa kuwa na mwangalizi wakati wa kucheza
2. Watoto wadichezee vitu kama maharage na mahindi
3. Watoto na watu wazima wawe na tahadhari hasa sehemu zile zenye wadudu kama vile nyuki na wadudu wengine wanaoweza kuingia masikio.
Huduma ya kwanza
1. Usitumie vitu kama msumari, ama kijitu kuchokoa sikio ili kutoa kitu kilichoingia, kufanya hivi kunaweza kuingiza zaidi hicho kitu
2. Kama kitu kinaonekana kitoe kwa upole kwa kukishika, kama kwa kutumia vipanio maalumu vidogovidogo kama tweezers
3. inamisha sikio kwa hali ambayo tundu iliyoingiwa na kitu itaelekea chini
4. kama aliyeingia ni mdudu tumia mafuta yaliyo na uvuguvugu, yaingize sikioni kisha inamisha kichwa kama ulivyofanya hapo juu. Usitumie njia hii kwa kitua ambacho kio mdudu.
5. tumia maji, ingiza sikioni ili hicho kitu kitoke pamoja na maji. Unaweza kutumia bomba la sindano kufanya hivi.
6. mpeleke mmgonjwa kituo cha afya kama kitu kitashindikana kutoka.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya upungufu wa vitamin
Soma Zaidi...Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu utaratibu wa lishe kwa watoto
Soma Zaidi...Jiamini A ni katika vitamini inayojulikana sana kuboresha na kuimarisha afya vya macho na uoni. Tafiti zinaonyesha kuwa kuna kundi kubwa la watoto wanaopata tayizobla kutokuona kutokana na ukosefu wa vitamini A vya kutosha.
Soma Zaidi...Posti hii inaelezea kuhusiana na mbinu za kutoa huduma ya kwanza kqa mgonjwa aliyeingiliwa na kitu au uchafu kwenye sikio.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kujikinga na kisukari
Soma Zaidi...Posti inahusu huduma ya kwanza kwa mwenye jeraha linalotoa damu.huduma ya kwanza Ni kumsaidia mtu alie pata jeraha au ajali kabla hajamwona dactari au kufika hospitalinia.
Soma Zaidi...maumivu ya kichwa ni moja ya dalili za kiafya ambazo huashiria hali isiyo ya kawaida. hata hivyo maumivu ya kichwa yanaweza kutokea hata kama sio mgonjwa. Hapa nitakuletea sababu zinazopelekea kuumwa na kichwa mara kwa mara.Maumivu
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi faida za kusafisha vidonda, ni faida ambazo Mgonjwa mwenye vidonge uzipata kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu utaratibu wa lishe kwa wajawazito na wanaonyonyesha
Soma Zaidi...