picha

huduma ya kwanza kwa mtu aliyeingiwa na uchafu sikioni

Post hii inahusu huduma ya kwanza kwa mtu aliyeingiwa na uchafu au kitu chochote sikioni. Sikio ni mojawapo ya milango ya fahamu ambapo hutumika kusikia, Kuna wakati vitu uingia ndani yake na kuleta madhara

Dalili za mtu aliyeingiza kitu chochote sikioni inawezekana kuwa maharage, mahindi, wadudu na vitu vingine kama hivyo ambavyo hupendelewa na watoto.

Dalili za mtu aliyeingiza kitu sikioni

1. Maumivu makali

2. Maambukizi kwenye sikio

3. Kuvimba ndani ya sikio

4. Sikio kuwa jekundu

5. Kushindwa kusikia vizuri

6. Kutoka uchafu sikioni 

 

Vifuatavyo ni vitu vinavyoweza kuingia sikioni

1. Maharage

2. Mahindi

3. Wadudu

4. Mchanga

5. Toyi

6. Makaratasi madogo madogo

 

Tufanyeje Ili kuepusha Hali ya kuingia maharage, mahindi na vitu vingine kwenye sikio?

1. Watoto wanapaswa kuwa na mwangalizi wakati wa kucheza

2. Watoto wadichezee vitu kama maharage na mahindi

3. Watoto na watu wazima wawe na tahadhari hasa sehemu zile zenye wadudu kama vile nyuki na wadudu wengine wanaoweza kuingia masikio.

 

Huduma ya kwanza

1. Usitumie vitu kama msumari, ama kijitu kuchokoa sikio ili kutoa kitu kilichoingia, kufanya hivi kunaweza kuingiza zaidi hicho kitu

2. Kama kitu kinaonekana kitoe kwa upole kwa kukishika, kama kwa kutumia vipanio maalumu vidogovidogo kama tweezers

3. inamisha sikio kwa hali ambayo tundu iliyoingiwa na kitu itaelekea chini

4. kama aliyeingia ni mdudu tumia mafuta yaliyo na uvuguvugu, yaingize sikioni kisha inamisha kichwa kama ulivyofanya hapo juu. Usitumie njia hii kwa kitua ambacho kio mdudu.

5. tumia maji, ingiza sikioni ili hicho kitu kitoke pamoja na maji. Unaweza kutumia bomba la sindano kufanya hivi.

6. mpeleke mmgonjwa kituo cha afya kama kitu kitashindikana kutoka.

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views 4432

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 Dua za Mitume na Manabii     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 ai web app    

Post zinazofanana:

Namna ya kumsafisha mgonjwa kinywa

Posti hii inahusu namna ya kumsafisha mgonjwa kinywa,ni njia unazopaswa kufuata wakati unamsafisha mgonjwa kinywa hasa wale walio mahututi.

Soma Zaidi...
Mambo yanayoathiri Uponyaji was jeraha.

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Mambo yanayoweza kuadhiri Uponyaji wa jeraha.jeraha huleta maumivu makali sana, vilevile Uvimbe, kutoa usaha. Pia jeraha hutofautiana katika kupona kwa mtu mzima na Mtoto.

Soma Zaidi...
Upungufu wa damu mwilini

Post inaenda kuzungumzia kuhusiana na upungufu wa damu mwilini ambapo tutaona SABABU na dalili zake lakin upungufu wa damu mwilini hujulikana Kama ANEMIA.

Soma Zaidi...
HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYEPATA JOTO LA JUU ZAIDI (HEAT STROKE)

Hii ni hali inayotokea ambapo wili unakuwa na joto la juu sana tofauti na kawaida.

Soma Zaidi...
Namna ya kumlisha Mgonjwa ambaye hawezi kujilisha mwenyewe ni

Posti hii inahusu njia za kumlisha Mgonjwa ambaye hawezi kujilisha wenyewe, hali hii uwa inawapata wagonjwa wale ambao hawawezi kujilisha wenyewe tunaweza kuwalisha kwa njia zifuatazo.

Soma Zaidi...
Ijue rangi ya mkojo isiyo ya kawaida

Post hii inahusu zaidi rangi isiyo ya kawaida kwenye mkojo, kawaida mkojo huwa na rangi ya kahawia Ila ukiona rangi zifuatazo Kuna shida kwenye mkojo.

Soma Zaidi...