picha

huduma ya kwanza kwa mtu aliyeingiwa na uchafu sikioni

Post hii inahusu huduma ya kwanza kwa mtu aliyeingiwa na uchafu au kitu chochote sikioni. Sikio ni mojawapo ya milango ya fahamu ambapo hutumika kusikia, Kuna wakati vitu uingia ndani yake na kuleta madhara

Dalili za mtu aliyeingiza kitu chochote sikioni inawezekana kuwa maharage, mahindi, wadudu na vitu vingine kama hivyo ambavyo hupendelewa na watoto.

Dalili za mtu aliyeingiza kitu sikioni

1. Maumivu makali

2. Maambukizi kwenye sikio

3. Kuvimba ndani ya sikio

4. Sikio kuwa jekundu

5. Kushindwa kusikia vizuri

6. Kutoka uchafu sikioni 

 

Vifuatavyo ni vitu vinavyoweza kuingia sikioni

1. Maharage

2. Mahindi

3. Wadudu

4. Mchanga

5. Toyi

6. Makaratasi madogo madogo

 

Tufanyeje Ili kuepusha Hali ya kuingia maharage, mahindi na vitu vingine kwenye sikio?

1. Watoto wanapaswa kuwa na mwangalizi wakati wa kucheza

2. Watoto wadichezee vitu kama maharage na mahindi

3. Watoto na watu wazima wawe na tahadhari hasa sehemu zile zenye wadudu kama vile nyuki na wadudu wengine wanaoweza kuingia masikio.

 

Huduma ya kwanza

1. Usitumie vitu kama msumari, ama kijitu kuchokoa sikio ili kutoa kitu kilichoingia, kufanya hivi kunaweza kuingiza zaidi hicho kitu

2. Kama kitu kinaonekana kitoe kwa upole kwa kukishika, kama kwa kutumia vipanio maalumu vidogovidogo kama tweezers

3. inamisha sikio kwa hali ambayo tundu iliyoingiwa na kitu itaelekea chini

4. kama aliyeingia ni mdudu tumia mafuta yaliyo na uvuguvugu, yaingize sikioni kisha inamisha kichwa kama ulivyofanya hapo juu. Usitumie njia hii kwa kitua ambacho kio mdudu.

5. tumia maji, ingiza sikioni ili hicho kitu kitoke pamoja na maji. Unaweza kutumia bomba la sindano kufanya hivi.

6. mpeleke mmgonjwa kituo cha afya kama kitu kitashindikana kutoka.

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views 4685

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉4 ai web app     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

Madhara ya ulevi

Poshi hii inahusu madhara ya ulevi.Utegemezi wa pombe kwa kawaida humaanisha kuwa mtu anatumia kiasi kikubwa cha pombe na kuna masuala kuhusu kupoteza udhibiti.

Soma Zaidi...
Imani potofu kuhusu kifua kikuu

Posti hii inahusu zaidi imani potofu waliyonayo Watu kuhusu ugonjwa wa kifua kikuu, hizi ni imani ambazo uwepo kwenye jamii na pengine uweza kuaminika lakini si za ukweli.

Soma Zaidi...
Umuhimu wa kupima virus vya ukimwi kwa wajawazito na wanaonyonyesha

Post hii inahusu umuhimu wa kupima virus vya ukimwi kwa mama wajawazito na wanaonyonyesha. Ni hatua ya kupima Mama akiwa mjamzito na wakati wa kunyonyesha ili kuepuka hatari ya kumwambikiza mtoto

Soma Zaidi...
Namna ya kumlisha Mgonjwa ambaye hawezi kujilisha mwenyewe ni

Posti hii inahusu njia za kumlisha Mgonjwa ambaye hawezi kujilisha wenyewe, hali hii uwa inawapata wagonjwa wale ambao hawawezi kujilisha wenyewe tunaweza kuwalisha kwa njia zifuatazo.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu vitamini C na kazi zake

Makala hii itakujulisha kazi kuu za vitamini C mwilini. Hapa pia utatambuwa ni kwa nini tunahitaji vitamini C na wapi tutavipata

Soma Zaidi...
Upungufu wa maji

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya upungufu wa maji mwilini

Soma Zaidi...