picha

huduma ya kwanza kwa mtu aliyeingiwa na uchafu sikioni

Post hii inahusu huduma ya kwanza kwa mtu aliyeingiwa na uchafu au kitu chochote sikioni. Sikio ni mojawapo ya milango ya fahamu ambapo hutumika kusikia, Kuna wakati vitu uingia ndani yake na kuleta madhara

Dalili za mtu aliyeingiza kitu chochote sikioni inawezekana kuwa maharage, mahindi, wadudu na vitu vingine kama hivyo ambavyo hupendelewa na watoto.

Dalili za mtu aliyeingiza kitu sikioni

1. Maumivu makali

2. Maambukizi kwenye sikio

3. Kuvimba ndani ya sikio

4. Sikio kuwa jekundu

5. Kushindwa kusikia vizuri

6. Kutoka uchafu sikioni 

 

Vifuatavyo ni vitu vinavyoweza kuingia sikioni

1. Maharage

2. Mahindi

3. Wadudu

4. Mchanga

5. Toyi

6. Makaratasi madogo madogo

 

Tufanyeje Ili kuepusha Hali ya kuingia maharage, mahindi na vitu vingine kwenye sikio?

1. Watoto wanapaswa kuwa na mwangalizi wakati wa kucheza

2. Watoto wadichezee vitu kama maharage na mahindi

3. Watoto na watu wazima wawe na tahadhari hasa sehemu zile zenye wadudu kama vile nyuki na wadudu wengine wanaoweza kuingia masikio.

 

Huduma ya kwanza

1. Usitumie vitu kama msumari, ama kijitu kuchokoa sikio ili kutoa kitu kilichoingia, kufanya hivi kunaweza kuingiza zaidi hicho kitu

2. Kama kitu kinaonekana kitoe kwa upole kwa kukishika, kama kwa kutumia vipanio maalumu vidogovidogo kama tweezers

3. inamisha sikio kwa hali ambayo tundu iliyoingiwa na kitu itaelekea chini

4. kama aliyeingia ni mdudu tumia mafuta yaliyo na uvuguvugu, yaingize sikioni kisha inamisha kichwa kama ulivyofanya hapo juu. Usitumie njia hii kwa kitua ambacho kio mdudu.

5. tumia maji, ingiza sikioni ili hicho kitu kitoke pamoja na maji. Unaweza kutumia bomba la sindano kufanya hivi.

6. mpeleke mmgonjwa kituo cha afya kama kitu kitashindikana kutoka.

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views 4762

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 ai web app     πŸ‘‰2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     πŸ‘‰3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     πŸ‘‰4 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰5 Dua za Mitume na Manabii     πŸ‘‰6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYENG’ATWA NA NYOKA

Nyoka wapo katka makundi makuu mawili, kuna wenye sumu na wasio na sumu.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu kizunguzungu

Posti hii inahusu zaidi tatizo la kizungu Zungu ni tatizo ambalo utokea kwa watu mbalimbali na kwa sababu tofauti tofauti na pengine mtu akipata kizungu sehemu mbaya anaweza kusababisha majeraha au pengine kupata ulemavu

Soma Zaidi...
Huduma ya Kwanza kwa mwenye kizunguzungu

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu mwenye kizunguzungu

Soma Zaidi...
Dalili za upungufu wa vitamini C mwilini

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za upungufu wa vitamini C mwilini

Soma Zaidi...
Huduma kwa mtoto mdogo anayeumwa

Mtoto mdogo ni mtoto chini ya miaka mitano, yaan kuanzia pale anapozaliwa mpaka anapafikisha miaka mitano

Soma Zaidi...
Imani potofu kuhusu kifua kikuu

Posti hii inahusu zaidi imani potofu waliyonayo Watu kuhusu ugonjwa wa kifua kikuu, hizi ni imani ambazo uwepo kwenye jamii na pengine uweza kuaminika lakini si za ukweli.

Soma Zaidi...