huduma ya kwanza kwa mtu aliyeingiwa na uchafu sikioni
Post hii inahusu huduma ya kwanza kwa mtu aliyeingiwa na uchafu au kitu chochote sikioni. Sikio ni mojawapo ya milango ya fahamu ambapo hutumika kusikia, Kuna wakati vitu uingia ndani yake na kuleta madhara
Dalili za mtu aliyeingiza kitu chochote sikioni inawezekana kuwa maharage, mahindi, wadudu na vitu vingine kama hivyo ambavyo hupendelewa na watoto.
Dalili za mtu aliyeingiza kitu sikioni
1. Maumivu makali
2. Maambukizi kwenye sikio
3. Kuvimba ndani ya sikio
4. Sikio kuwa jekundu
5. Kushindwa kusikia vizuri
6. Kutoka uchafu sikioni
Vifuatavyo ni vitu vinavyoweza kuingia sikioni
1. Maharage
2. Mahindi
3. Wadudu
4. Mchanga
5. Toyi
6. Makaratasi madogo madogo
Tufanyeje Ili kuepusha Hali ya kuingia maharage, mahindi na vitu vingine kwenye sikio?
1. Watoto wanapaswa kuwa na mwangalizi wakati wa kucheza
2. Watoto wadichezee vitu kama maharage na mahindi
3. Watoto na watu wazima wawe na tahadhari hasa sehemu zile zenye wadudu kama vile nyuki na wadudu wengine wanaoweza kuingia masikio.
Huduma ya kwanza
1. Usitumie vitu kama msumari, ama kijitu kuchokoa sikio ili kutoa kitu kilichoingia, kufanya hivi kunaweza kuingiza zaidi hicho kitu
2. Kama kitu kinaonekana kitoe kwa upole kwa kukishika, kama kwa kutumia vipanio maalumu vidogovidogo kama tweezers
3. inamisha sikio kwa hali ambayo tundu iliyoingiwa na kitu itaelekea chini
4. kama aliyeingia ni mdudu tumia mafuta yaliyo na uvuguvugu, yaingize sikioni kisha inamisha kichwa kama ulivyofanya hapo juu. Usitumie njia hii kwa kitua ambacho kio mdudu.
5. tumia maji, ingiza sikioni ili hicho kitu kitoke pamoja na maji. Unaweza kutumia bomba la sindano kufanya hivi.
6. mpeleke mmgonjwa kituo cha afya kama kitu kitashindikana kutoka.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
Namna ya kumsaidia mgonjwa aliye na Maambukizi kwenye milija na ovari
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuwasaidia wagonjwa waliopata maambukizi kwenye milija na ovari, ni wagonjwa waliopata maambukizi kwenye milija na ovari.
Soma Zaidi...Vifaa vya kutumia wakati wa kusafisha vidonda.
Posti hii inahusu zaidi vifaa vya kutumia wakati wa kusafisha vidonda, ni vifaa muhimu ambavyo mara nyingi kutwa hospitalini.
Soma Zaidi...Huduma ya kwanza kwa mwenye uchafu kwenye sikio.
Posti hii inaelezea kuhusiana na mbinu za kutoa huduma ya kwanza kqa mgonjwa aliyeingiliwa na kitu au uchafu kwenye sikio.
Soma Zaidi...Madhara ya kuchelewa kutibu tatizo la kiafya
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea endapo tatizo halijatibiwa.
Soma Zaidi...Fahamu kuhusu vitamini K na kazi zake mwilini
vitamini k ni moja katika vitamini vinavyoitajika sana mwilini. Je unazijuwa athari za upungufu wa vitamini k mwilini?
Soma Zaidi...Upungufu wa damu wa madini (anemia ya upungufu wa madini)
upungufu wa damu wa madini ya chuma ni aina ya kawaida ya upungufu wa damu hali ambayo damu haina chembe nyekundu za damu zenye afya. Seli nyekundu za damu hubeba oksijeni kwa tishu za mwili. Bila chuma cha kutosha, mwili wako hauwezi kutoa dutu ya k
Soma Zaidi...