Menu



huduma ya kwanza kwa mtu aliyeingiwa na uchafu sikioni

Post hii inahusu huduma ya kwanza kwa mtu aliyeingiwa na uchafu au kitu chochote sikioni. Sikio ni mojawapo ya milango ya fahamu ambapo hutumika kusikia, Kuna wakati vitu uingia ndani yake na kuleta madhara

Dalili za mtu aliyeingiza kitu chochote sikioni inawezekana kuwa maharage, mahindi, wadudu na vitu vingine kama hivyo ambavyo hupendelewa na watoto.

Dalili za mtu aliyeingiza kitu sikioni

1. Maumivu makali

2. Maambukizi kwenye sikio

3. Kuvimba ndani ya sikio

4. Sikio kuwa jekundu

5. Kushindwa kusikia vizuri

6. Kutoka uchafu sikioni 

 

Vifuatavyo ni vitu vinavyoweza kuingia sikioni

1. Maharage

2. Mahindi

3. Wadudu

4. Mchanga

5. Toyi

6. Makaratasi madogo madogo

 

Tufanyeje Ili kuepusha Hali ya kuingia maharage, mahindi na vitu vingine kwenye sikio?

1. Watoto wanapaswa kuwa na mwangalizi wakati wa kucheza

2. Watoto wadichezee vitu kama maharage na mahindi

3. Watoto na watu wazima wawe na tahadhari hasa sehemu zile zenye wadudu kama vile nyuki na wadudu wengine wanaoweza kuingia masikio.

 

Huduma ya kwanza

1. Usitumie vitu kama msumari, ama kijitu kuchokoa sikio ili kutoa kitu kilichoingia, kufanya hivi kunaweza kuingiza zaidi hicho kitu

2. Kama kitu kinaonekana kitoe kwa upole kwa kukishika, kama kwa kutumia vipanio maalumu vidogovidogo kama tweezers

3. inamisha sikio kwa hali ambayo tundu iliyoingiwa na kitu itaelekea chini

4. kama aliyeingia ni mdudu tumia mafuta yaliyo na uvuguvugu, yaingize sikioni kisha inamisha kichwa kama ulivyofanya hapo juu. Usitumie njia hii kwa kitua ambacho kio mdudu.

5. tumia maji, ingiza sikioni ili hicho kitu kitoke pamoja na maji. Unaweza kutumia bomba la sindano kufanya hivi.

6. mpeleke mmgonjwa kituo cha afya kama kitu kitashindikana kutoka.

 

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea

Ndio     Hapana     Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views 3076

Share On:

Facebook WhatsApp

Post zinazofanana:

Ijue rangi za mkojo na maana zake katika mwili kuhsu afya yako

Posti hii inahusu zaidi rangi za mkojo na maana zake, hizi ni rangi ambazo uweza kutokea kwenye mkojo wa mtu mmoja na mwingine kwa sababu ya kuwepo kwa magonjwa, chakula,na mtindo wa maisha inawezekana unywaji wa maji au kutokunywa maji.

Soma Zaidi...
Mambo yanayosababisha kupona kwa vidonda.

Posti hii inahusu mambo yanayochangia katika kupona kwa kidonda, ni mambo ambayo yapo kwa mgonjwa mwenyewe kama ifuayavyo.

Soma Zaidi...
Utaratibu wa lishe kwa vijana

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu utaratibu wa lishe kwa vijana

Soma Zaidi...
Huduma ya Kwanza kwa mtu aliyeng'atwa na nyoka

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyeng'atwa na nyoka

Soma Zaidi...
Ratiba ya chanjo ya kifua kikuu

Posti hii inahusu zaidi ratiba ya chanjo ya kuzuia kifua kikuu, hiii ni ratiba ambayo chanjo hii utolewa na ushauri mbalimbali utolewa ili kuweza kufanikisha kazi ya chanjo hii

Soma Zaidi...
Namna ya kuzuia ugonjwa wa kipindupindu,

Post hii inahusu zaidi ugonjwa wa kipindupindu ni ugonjwa unaosababishwa na bakteria kwa kitaalamu huitwa vibrio cholera.

Soma Zaidi...
Faida za tumbo katika mwili wa binadamu

Posti hii inahusu zaidi faida za tumbo,tumbo ni sehemu ya mwili ambayo ushughilika na kutunza chakula,

Soma Zaidi...
Vyakula vya fati na mafuta

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za vyakula vya fati na mafuta

Soma Zaidi...
Ratiba ya chanjo ya Pentavalenti

Posti hii inahusu zaidi chanjo ya pentavalent ni aina ya chanjo ambayo inazuia Magonjwa matano ambayo ni kifadulo, pepopunda, homa ya ini na magonjwa yanayohusiana na upumuaji.

Soma Zaidi...
Madhara ya kutumia dawa bila ushauri wa kitaalamu.

Posti hii inahusu zaidi madhara ya kutumia dawa bila kupata ushauri wa kitaalamu, madhara haya uwapata watu wengi kwa sababu hawajui taratibu za matumizi ya dawa.

Soma Zaidi...