huduma ya kwanza kwa mtu aliyeingiwa na uchafu sikioni

Post hii inahusu huduma ya kwanza kwa mtu aliyeingiwa na uchafu au kitu chochote sikioni. Sikio ni mojawapo ya milango ya fahamu ambapo hutumika kusikia, Kuna wakati vitu uingia ndani yake na kuleta madhara

Dalili za mtu aliyeingiza kitu chochote sikioni inawezekana kuwa maharage, mahindi, wadudu na vitu vingine kama hivyo ambavyo hupendelewa na watoto.

Dalili za mtu aliyeingiza kitu sikioni

1. Maumivu makali

2. Maambukizi kwenye sikio

3. Kuvimba ndani ya sikio

4. Sikio kuwa jekundu

5. Kushindwa kusikia vizuri

6. Kutoka uchafu sikioni 

 

Vifuatavyo ni vitu vinavyoweza kuingia sikioni

1. Maharage

2. Mahindi

3. Wadudu

4. Mchanga

5. Toyi

6. Makaratasi madogo madogo

 

Tufanyeje Ili kuepusha Hali ya kuingia maharage, mahindi na vitu vingine kwenye sikio?

1. Watoto wanapaswa kuwa na mwangalizi wakati wa kucheza

2. Watoto wadichezee vitu kama maharage na mahindi

3. Watoto na watu wazima wawe na tahadhari hasa sehemu zile zenye wadudu kama vile nyuki na wadudu wengine wanaoweza kuingia masikio.

 

Huduma ya kwanza

1. Usitumie vitu kama msumari, ama kijitu kuchokoa sikio ili kutoa kitu kilichoingia, kufanya hivi kunaweza kuingiza zaidi hicho kitu

2. Kama kitu kinaonekana kitoe kwa upole kwa kukishika, kama kwa kutumia vipanio maalumu vidogovidogo kama tweezers

3. inamisha sikio kwa hali ambayo tundu iliyoingiwa na kitu itaelekea chini

4. kama aliyeingia ni mdudu tumia mafuta yaliyo na uvuguvugu, yaingize sikioni kisha inamisha kichwa kama ulivyofanya hapo juu. Usitumie njia hii kwa kitua ambacho kio mdudu.

5. tumia maji, ingiza sikioni ili hicho kitu kitoke pamoja na maji. Unaweza kutumia bomba la sindano kufanya hivi.

6. mpeleke mmgonjwa kituo cha afya kama kitu kitashindikana kutoka.

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Huduma Main: Afya File: Download PDF Views 3818

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Dua za Mitume na Manabii    👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 web hosting    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Huduma kwa wenye ugonjwa wa herpes simplex au vipele kwenye midomo na sehemu za siri

Post hii inahusu zaidi tiba na huduma kwa wenye ugonjwa wa herpes simplex au vipele kwenye midomo na sehemu za siri.

Soma Zaidi...
HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYEPATA JOTO LA JUU ZAIDI (HEAT STROKE)

Hii ni hali inayotokea ambapo wili unakuwa na joto la juu sana tofauti na kawaida.

Soma Zaidi...
Namna ya kutoa huduma ya kwanza

Huduma ya kwanza ni huduma anayopewa mgonjwa au mtu yeyote aliyepata ajali kabla ya kumpeleka hospitalini

Soma Zaidi...
Jinsi ya kutoa huduma ya kwanza kulingana na tatizo

Posti hii inahusu sana mambo ya huduma ya kwanza ambayo huduma ya kwanza inapatikana au inatolewa na mtu yeyote katika jamii .

Soma Zaidi...
Aliyepaliwa na maji huduma ya kwanza itakuwaje

Vipi utamsaidia mti ambaye amepaliwa na maji? Post hii itakwenda kukifundisha jambo hili.

Soma Zaidi...
Faida za tumbo katika mwili wa binadamu

Posti hii inahusu zaidi faida za tumbo,tumbo ni sehemu ya mwili ambayo ushughilika na kutunza chakula,

Soma Zaidi...
Huduma ya kwanz akwa aliyeumwa na nyoka

Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kumsaidia aliyeumwa na nyoka

Soma Zaidi...
Kazi za mifupa mwilinj

Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa mifupa mwilini, mifupa ni mojawapo ya tushy zilizounganika na ufanya kazi kubwa kwenye mwili.

Soma Zaidi...
Namna ya kusaidia vijana wakati wa kubarehe

Post hii inahusu zaidi namna ya kuwasaidia vijana wakati wa kubarehe, ni njia za kuhakikisha kuwa vijana wanakuwa na mwelekeo ,

Soma Zaidi...