image

Fahamu kuhusu dawa ya ALU au kwa lugha nyingine ni dawa ya mseto

Post hii inahusu zaidi dawa ya ALU ila kwa jina jingine huitwa dawa ya mseto,ni aina ya dawa inayotumika kutibu ugonjwa wa malaria ya kawaida.

Fahamu kuhusu dawa ya mseto au ALU.

1. Dawa hii ya ALU ni dawa ambayo utumika kutibu malaria ya kawaida, dawa hii ni muunganiko wa dawa mbili ambazo kwa kirefu zinaitwa Artemether lumefantrine, Artemether usimama kama A, na lumefantrine usimama kama LU kwa hiyo kwa ujumla utengeneza jina la ALU ambapo Artemether ina miligramu ishirini na lumefantrine ina miligramu mia ishirini kwa ujumla dawa hii huwa na jumla ya milligrams mia arobaini.

 

2. Kama tulivyotangulia kusema kwamba dawa hii utumika kutibu malaria ya kawaida, tunasema utibu malaria ya kawaida kwa sababu ya dalili zake kuwa za kawaida, dalili za malaria ya kawaida ni kama ifuatavyo maumivu kwenye jointi, maumivu ya kichwa, mwili kukosa nguvu, kichefuchefu na kutapika, maumivu ya tumbo la kawaida, kuhisi baridi au kwa watu wengine kutetemeka , dalili hizi hazimfanyi mtu kushindwa kutembea na kufika hospitali na akipata vipimo na kukutwa na malaria ya kawaida anapatiwa vidonge vya ALU au mseto na anapona kabisa na kurudia hali yake ya kawaida.

 

3. Matumizi ya dawa hii utegemeza umri wa mtu na kilo za mtu, watu wenye kilo kuanzia tano mpaka kumi na tano utumia kidonge kimoja, kidonge cha kwanza ukitumia siku ya kwanza , kidogo cha pili baada ya masaa manane na vidonge vifuatavyo utumika asubuhi na jioni kwa kawaida dozi hiyo utumia siku tatu kama mtu anatumia vidonge kwa mda na kwa wakati.

 

4. Watu wenye kilo kuanzia kumi na tano mpaka ishirini na tano utumia vidonge viwili, yaani siku ya kuanza anameza vidonda viwili, baada ya masaa nane anameza vidonge vingine viwili na siku zifuatazo anameza vidonge viwili asubuhi na jioni mpaka siku tatu zinaisha. Yaani asubuhi viwili na jioni viwili.

 

5. Watu kuanzia kilo ishirini na tano mpaka thelathini na tano kwa kawaida umeza vidonge vitatu, yaani siku ya kwanza anameza vidonge vitatu, baada ya masaa manane vidonge vitatu, na anaanza kumeza asubuhi na jioni yaani asubuhi vidonge vitatu na jioni vidonge vitatu mpaka dozi inaisha.

 

6. Watu wenye kilo kuanzia thelathini na tano na kuendelea kwa kawaida umeza vidonge vinne, yaani siku ya kuanza kutumia dawa anameza vidonge vinne na baada ya masaa manane anameza vidonge vingine vinne na akimaliza hapo anameza vidonge asubuhi na jioni yaani asubuhi vinne na jioni vinne mpaka dozi inaisha , kwa kawa wakati wa kutumia dawa hizi ni vizuri kutumia maji mengi ya kunywa pamoja na kula kushiba kwa sababu kama mtu hajashiba dawa hizi hazifanyi kazi vizuri na uweza kumsumbua mtumiaji kwa hiyo ni vizuri kula na kushiba wakati wa kutumia dawa hizi.

 

7. Pia dawa hizi uweza juwa na maudhi madogo madogo kama vile kizunguzungu, kutapika, kuishiwa nguvu na pia kupenda kulala mda mwingi, hasa hasa maudhi haya uwapata watu wale ambao hawako na kushiba kabla ya kutumia dawa ni vizuri kabisa kula na kushiba ndipo utumia dawa, pia wakati wa kutumia dawa hizi ni vizuri na ni lazima kutumia dawa za kupunguza maumivu hasa hasa panadol na dawa nyingine ambazo ufanya kazi kama paracetamol.

 

8. Dawa hizi ya ALU haipaswi kutumiwa na akina mama wenye mimba na pia wale wenye mzio au aleji na dawa hizi , na pia ikiwa mtu anatumia dawa hizi na akatapika baada ya nusu saa kutumia anapaswa kurudia tena kwa sababu dawa haijafanya kazi.

 

9. Katika matumizi ya dawa hii ni vizuri kabisa kufuata taratibu za wataalamu wa afya ili kupata maelekezo sio kutumia kiholela kwa sababu unaweza kupata matatizo kutokana na matumizi yasiyo sahihi ya dawa hizi ya ALU.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 3475


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Fahamu zaidi kuhusiana na Dawa inayotibu shinikizo la damu. iitwayo LASIX
Lasix (Furosemide) iko katika kundi la dawa zinazoitwa vidonge vya maji (loop diuretics) vidonge vya maji. Lasix hutumiwa kupunguza uvimbe mwilini unaosababishwa na kushindwa kwa moyo, ugonjwa wa ini, au ugonjwa wa figo. Kwa matibabu ya dalili nyingi.La Soma Zaidi...

Fahamu dawa ya aminophylline kutibi maambukizi kwenye mfumo wa upumuaji
Post hii inahusu zaidi dawa ya aminophylline katika kutuliza maambukizi kwenye mfumo wa upumuaji. Soma Zaidi...

Fahamu kazi za homoni katika kupamba na kansa.
Post hii inahusu zaidi homoni mbalimbali ambazo upambana na kansa, hizi homoni zikitumika vizuri matokeo yake huwa na mazuri pia kwa wagonjwa wa kansa. Soma Zaidi...

Fahamu kuhusu dawa ya parental Artusnate dawa ya kutibu malaria sugu
Post hii inahusu zaidi dawa ya Parental Artusnate ni dawa inayotumika kutibu ugonjwa wa malaria sugu kama tutakavyoona hapo baadaye. Soma Zaidi...

Matibabu ya ugonjwa wa uti wa mgongo
Posti hii inahusu zaidi matibabu kwa mgonjwa wa uti wa mgongo, kwa kawaida tunajua kuwa homa hii ya uti wa mgongo usababisha na wadudu mbalimbali kama vile bakteria, virus, fungasi, sumu mbalimbali kama vile madini ya lead na arseni, na vitu kama vile Mag Soma Zaidi...

Ifahamu dawa ya epinephrine kwa kutuliza aleji
Post hii inahusu zaidi dawa ya epinephrine kwa kutuliza aleji ni dawa ambayo imependekezwa kutuliza aleji kama dawa ya hydrocortisone, Prednisone hazipo au zimeshindwa kufanya kazi. Soma Zaidi...

Fahamu matumizi ya Dawa iitwayo Aspirin.
Aspirini Ni dawa ya kutuliza maumivu.Majina yanayoaminika zaidi katika kutuliza maumivu sasa yanapatikana kwa njia mbadala inayookoa gharama kwa kutumia Aspirini. Aspirini inayopendwa na familia kwa miongo kadhaa, mara nyingi hutumiwa kupunguza maumivu y Soma Zaidi...

Ifahamu dawa ya isoniazid katika kupambana na ugonjwa wa TB
Post hii inahusu zaidi dawa ya isoniazid katika mapambano na kifua kikuu, tunafahamu kabisa kwamba kifua kikuu ni hatari katika jamii kwa hiyo dawa ya isoniazid ni mkombozi katika mapambano na kifua kikuu. Soma Zaidi...

Fahamu dawa za kutibu mafua
Post hii inahusu dawa za kutibu mafua ambazo ni cough seppessants na nasal congestion ni dawa ambazo zimependekezwa kwa ajili ya kutibu mafua. Soma Zaidi...

Dawa ya fangasi kwenye mdomo na ulimi
Utajifunza dalili za fangasi mdomoni na ulimini, sababu za fangasi wa mdomoni na ulimini, matibabu yeke na njia za kukabiliana nao Soma Zaidi...

Dawa ya quinenes katika kutibu Malaria
Post hii inahusu zaidi dawa e quinine katika kutibu Malaria ni dawa inayotibu Ugonjwa wa Malaria ikiwa dawa nyingine zimeshindwa kufanya kazi. Soma Zaidi...

Dawa ya fangasi na dalili za fangasi
hapa utajifunza dalili za fangasi, dawa ya fangasi na aina za fangasi, pia nitakujuza njia za kukabiliana na fangasi Soma Zaidi...