Post hii inahusu zaidi dawa ya ALU ila kwa jina jingine huitwa dawa ya mseto,ni aina ya dawa inayotumika kutibu ugonjwa wa malaria ya kawaida.
1. Dawa hii ya ALU ni dawa ambayo utumika kutibu malaria ya kawaida, dawa hii ni muunganiko wa dawa mbili ambazo kwa kirefu zinaitwa Artemether lumefantrine, Artemether usimama kama A, na lumefantrine usimama kama LU kwa hiyo kwa ujumla utengeneza jina la ALU ambapo Artemether ina miligramu ishirini na lumefantrine ina miligramu mia ishirini kwa ujumla dawa hii huwa na jumla ya milligrams mia arobaini.
2. Kama tulivyotangulia kusema kwamba dawa hii utumika kutibu malaria ya kawaida, tunasema utibu malaria ya kawaida kwa sababu ya dalili zake kuwa za kawaida, dalili za malaria ya kawaida ni kama ifuatavyo maumivu kwenye jointi, maumivu ya kichwa, mwili kukosa nguvu, kichefuchefu na kutapika, maumivu ya tumbo la kawaida, kuhisi baridi au kwa watu wengine kutetemeka , dalili hizi hazimfanyi mtu kushindwa kutembea na kufika hospitali na akipata vipimo na kukutwa na malaria ya kawaida anapatiwa vidonge vya ALU au mseto na anapona kabisa na kurudia hali yake ya kawaida.
3. Matumizi ya dawa hii utegemeza umri wa mtu na kilo za mtu, watu wenye kilo kuanzia tano mpaka kumi na tano utumia kidonge kimoja, kidonge cha kwanza ukitumia siku ya kwanza , kidogo cha pili baada ya masaa manane na vidonge vifuatavyo utumika asubuhi na jioni kwa kawaida dozi hiyo utumia siku tatu kama mtu anatumia vidonge kwa mda na kwa wakati.
4. Watu wenye kilo kuanzia kumi na tano mpaka ishirini na tano utumia vidonge viwili, yaani siku ya kuanza anameza vidonda viwili, baada ya masaa nane anameza vidonge vingine viwili na siku zifuatazo anameza vidonge viwili asubuhi na jioni mpaka siku tatu zinaisha. Yaani asubuhi viwili na jioni viwili.
5. Watu kuanzia kilo ishirini na tano mpaka thelathini na tano kwa kawaida umeza vidonge vitatu, yaani siku ya kwanza anameza vidonge vitatu, baada ya masaa manane vidonge vitatu, na anaanza kumeza asubuhi na jioni yaani asubuhi vidonge vitatu na jioni vidonge vitatu mpaka dozi inaisha.
6. Watu wenye kilo kuanzia thelathini na tano na kuendelea kwa kawaida umeza vidonge vinne, yaani siku ya kuanza kutumia dawa anameza vidonge vinne na baada ya masaa manane anameza vidonge vingine vinne na akimaliza hapo anameza vidonge asubuhi na jioni yaani asubuhi vinne na jioni vinne mpaka dozi inaisha , kwa kawa wakati wa kutumia dawa hizi ni vizuri kutumia maji mengi ya kunywa pamoja na kula kushiba kwa sababu kama mtu hajashiba dawa hizi hazifanyi kazi vizuri na uweza kumsumbua mtumiaji kwa hiyo ni vizuri kula na kushiba wakati wa kutumia dawa hizi.
7. Pia dawa hizi uweza juwa na maudhi madogo madogo kama vile kizunguzungu, kutapika, kuishiwa nguvu na pia kupenda kulala mda mwingi, hasa hasa maudhi haya uwapata watu wale ambao hawako na kushiba kabla ya kutumia dawa ni vizuri kabisa kula na kushiba ndipo utumia dawa, pia wakati wa kutumia dawa hizi ni vizuri na ni lazima kutumia dawa za kupunguza maumivu hasa hasa panadol na dawa nyingine ambazo ufanya kazi kama paracetamol.
8. Dawa hizi ya ALU haipaswi kutumiwa na akina mama wenye mimba na pia wale wenye mzio au aleji na dawa hizi , na pia ikiwa mtu anatumia dawa hizi na akatapika baada ya nusu saa kutumia anapaswa kurudia tena kwa sababu dawa haijafanya kazi.
9. Katika matumizi ya dawa hii ni vizuri kabisa kufuata taratibu za wataalamu wa afya ili kupata maelekezo sio kutumia kiholela kwa sababu unaweza kupata matatizo kutokana na matumizi yasiyo sahihi ya dawa hizi ya ALU.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Somo hili linakwenda kukuletea dawa ya kuzuia kuathirika kwa watu walio hatarini kupata VVU
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya carvedilo katika matibabu ya magonjwa, ni mojawapo ya dawa kwenye kundi la beta blockers na pia uhusika katika matibabu ya magonjwa ya moyo kama nyingine.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dawa ya amoxline .jinsi inavyofanya kazi mwilini.pamoja na matumizi yake.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa za cyclophosphamide na mustargen katika kupambana na ugonjwa wa Kansa.
Soma Zaidi...Ampicillin ni antibiotic yenye msingi wa penicillin ambayo inafanya kazi kupambana na maambukizi ya ndani ya bakteria. Ampicillin hufanya kazi ya kuharibu kuta za kinga ambazo bakteria huunda ndani ya mwili wako na kuzuia bakteria wapya kutokeza. Ampici
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya mucolytic katika kutibu kikohozi kwa watu wazima na watoto.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya cephalosporin katika kupambana na bakteria, ni mojawapo ya kundi kati ya makundi ya kupambana na bakteria ambalo ufanya Kazi kama penicillin.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya griseofulvin ni dawa inayotumika kutibu fangasi za kwenye ngozi ambazo usababisha mabaka mabaka kwenye ngozi.
Soma Zaidi...kama unasumbuliwa na fangasi uumeni, nitakujuza dawa yake, sababu za fangasi uumeni, matibabu yake na njia za kuwaepuka
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa zinazofanya kazi ya kupunguza maumivu kwa kawaida dawa hizi ufanya kazi kwa kupitia kwenye mfumo wa fahamu.
Soma Zaidi...