Post hii inahusu zaidi dawa ya ALU ila kwa jina jingine huitwa dawa ya mseto,ni aina ya dawa inayotumika kutibu ugonjwa wa malaria ya kawaida.
1. Dawa hii ya ALU ni dawa ambayo utumika kutibu malaria ya kawaida, dawa hii ni muunganiko wa dawa mbili ambazo kwa kirefu zinaitwa Artemether lumefantrine, Artemether usimama kama A, na lumefantrine usimama kama LU kwa hiyo kwa ujumla utengeneza jina la ALU ambapo Artemether ina miligramu ishirini na lumefantrine ina miligramu mia ishirini kwa ujumla dawa hii huwa na jumla ya milligrams mia arobaini.
2. Kama tulivyotangulia kusema kwamba dawa hii utumika kutibu malaria ya kawaida, tunasema utibu malaria ya kawaida kwa sababu ya dalili zake kuwa za kawaida, dalili za malaria ya kawaida ni kama ifuatavyo maumivu kwenye jointi, maumivu ya kichwa, mwili kukosa nguvu, kichefuchefu na kutapika, maumivu ya tumbo la kawaida, kuhisi baridi au kwa watu wengine kutetemeka , dalili hizi hazimfanyi mtu kushindwa kutembea na kufika hospitali na akipata vipimo na kukutwa na malaria ya kawaida anapatiwa vidonge vya ALU au mseto na anapona kabisa na kurudia hali yake ya kawaida.
3. Matumizi ya dawa hii utegemeza umri wa mtu na kilo za mtu, watu wenye kilo kuanzia tano mpaka kumi na tano utumia kidonge kimoja, kidonge cha kwanza ukitumia siku ya kwanza , kidogo cha pili baada ya masaa manane na vidonge vifuatavyo utumika asubuhi na jioni kwa kawaida dozi hiyo utumia siku tatu kama mtu anatumia vidonge kwa mda na kwa wakati.
4. Watu wenye kilo kuanzia kumi na tano mpaka ishirini na tano utumia vidonge viwili, yaani siku ya kuanza anameza vidonda viwili, baada ya masaa nane anameza vidonge vingine viwili na siku zifuatazo anameza vidonge viwili asubuhi na jioni mpaka siku tatu zinaisha. Yaani asubuhi viwili na jioni viwili.
5. Watu kuanzia kilo ishirini na tano mpaka thelathini na tano kwa kawaida umeza vidonge vitatu, yaani siku ya kwanza anameza vidonge vitatu, baada ya masaa manane vidonge vitatu, na anaanza kumeza asubuhi na jioni yaani asubuhi vidonge vitatu na jioni vidonge vitatu mpaka dozi inaisha.
6. Watu wenye kilo kuanzia thelathini na tano na kuendelea kwa kawaida umeza vidonge vinne, yaani siku ya kuanza kutumia dawa anameza vidonge vinne na baada ya masaa manane anameza vidonge vingine vinne na akimaliza hapo anameza vidonge asubuhi na jioni yaani asubuhi vinne na jioni vinne mpaka dozi inaisha , kwa kawa wakati wa kutumia dawa hizi ni vizuri kutumia maji mengi ya kunywa pamoja na kula kushiba kwa sababu kama mtu hajashiba dawa hizi hazifanyi kazi vizuri na uweza kumsumbua mtumiaji kwa hiyo ni vizuri kula na kushiba wakati wa kutumia dawa hizi.
7. Pia dawa hizi uweza juwa na maudhi madogo madogo kama vile kizunguzungu, kutapika, kuishiwa nguvu na pia kupenda kulala mda mwingi, hasa hasa maudhi haya uwapata watu wale ambao hawako na kushiba kabla ya kutumia dawa ni vizuri kabisa kula na kushiba ndipo utumia dawa, pia wakati wa kutumia dawa hizi ni vizuri na ni lazima kutumia dawa za kupunguza maumivu hasa hasa panadol na dawa nyingine ambazo ufanya kazi kama paracetamol.
8. Dawa hizi ya ALU haipaswi kutumiwa na akina mama wenye mimba na pia wale wenye mzio au aleji na dawa hizi , na pia ikiwa mtu anatumia dawa hizi na akatapika baada ya nusu saa kutumia anapaswa kurudia tena kwa sababu dawa haijafanya kazi.
9. Katika matumizi ya dawa hii ni vizuri kabisa kufuata taratibu za wataalamu wa afya ili kupata maelekezo sio kutumia kiholela kwa sababu unaweza kupata matatizo kutokana na matumizi yasiyo sahihi ya dawa hizi ya ALU.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download
Download NowJe! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Dawa Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Views 4356
Sponsored links
👉1
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉2
Kitau cha Fiqh
👉3
kitabu cha Simulizi
👉4
Kitabu cha Afya
👉5
Simulizi za Hadithi Audio
👉6
Madrasa kiganjani
Fahamu antibiotics ya asili.
Post hii inahusu zaidi antibiotics ya asili, ni antibiotics inayotumia vitu vya kila siku na ya kawaida na mtu akaweza kupona kabisa na kufanya kazi kama antibiotics ya vidonge vya kawaida. Soma Zaidi...
Dawa ya Carvedilol na kazi yake.
Posti hii inahusu zaidi dawa ya Carvedilol na kazi yake, ni dawa inayotibu au kuzuia mapigo ya moyo ambayo yako juu na kusababisha kulegeza kwa mishipa ya moyo. Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya ketoconazole.
Post hii inahusu zaidi dawa aina ya ketoconazole ni dawa inayotumika kutibu fangasi za kwenye koo. Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya loperamide dawa ya kuzuia kuharusha
Post hii inahusu zaidi dawa ya loperamide ni dawa ambayo inazuia kuharisha ni dawa inayofanya kazi kuanzia kwenye utumbo na pia usaidia kutuliza maumivu ya tumbo Soma Zaidi...
Dawa ya kutibu maumivu ya jino
Utaijuwa Dawa ya maumivu ya jino, sababu za maumivu ya jino na njia za kujikinga na maumivu ya jino Soma Zaidi...
Ifahamu dawa ya furosemide.
Post hii inahusu zaidi dawa ya furosemide ni mojawapo ya dawa ambayo ipo kwenye kundi la diuretics na kwa jina linguine huitwa lasix Soma Zaidi...
Fahamu Dawa inayotibu minyoo iitwayo albenza (albendazole)
Albenza (albendazole) hutumika kutibu magonjwa ya minyoo ya ndani ikiwa ni pamoja na maambukizi ya minyoo ya tegu. Albenza inafanya kazi kukomesha kuenea kwa maambukizo ya minyoo kwenye chanzo, na kukata chanzo chao cha nishati, na hivyo kuzuia kuenea k Soma Zaidi...
Miungurumo haiishi tumboni nikishika upande wa kushoto wa tumbo kuna maumivu kwa mbali je mm nitumie dawa gan kuondoa tatizo hilo
Kukawa na gesi tumboni kunaweza kuwa ni dalili ya shida kwenye afya, hasa katika mfumo wa chakula. Hali itakuwa sio nzuri endapo utakosea hamu ya kula na kuhisivkushiba muda wowote. Soma Zaidi...
Fahamu kazi ya dawa ya ampicillin inayopambana na maambukizi ya bakteria
Post hii inahusu zaidi dawa ya ampicillin, ni mojawapo ya dawa za kutibu maambukizi ya bakteria kwenye mwili wa binadamu ba pia ni dawa ambayo IPO kwenye kundi la penicillin kundi hili kwa kitaa huitwa broad spectrum penicillin Soma Zaidi...
Dawa ya fangasi ukeni
Usisumbuliwe tene na fangasi ukeni, zijuwe hapa dalili za fangasi ukeni, tiba yake na njia za kukabiliana na fangasi ukeni Soma Zaidi...