picha

Ijue dawa ya cephalosporin katika kupambana na bakteria

Post hii inahusu zaidi dawa ya cephalosporin katika kupambana na bakteria, ni mojawapo ya kundi kati ya makundi ya kupambana na bakteria ambalo ufanya Kazi kama penicillin.

Fahamu kuhusu dawa ya cephalosporin .

1. Dawa hii ya cephalosporin katika kupambana na bakteria huwa kwenye magroup muhimu matatu ambayo ni kundi la kwanza Lina dawa ya cephalexin, Kundi la pili Lina dawa ya cefamandole na kundi la tatu Lina dawa ya ceftriaxone na celfdimir, makundi yote matatu ufanya Kazi kwa umoja na kuweza kupambana na bakteria na kutibu magonjwa mbalimbali kama tutakavyoona hapo mbeleni.

 

2. Magonjwa mbalimbali ambayo utibiwa na cephalosporin na makundi yake ni kuzuia maambukizi kwenye ngozi, yaani maambukizi yabayoambatana na viupele pamoja na miwasho, kuzuia maambukizi kwenye mifupa na kwennye joint, kuzuia maambukizi kwenye mfumo wa mkojo na maambukizi ya njia za mkojo kwa kitaamu huiitwa UTI, kuzuia maambukizi kwenye tumbo,pia kuzuia maambukizi kwenye sikio hasa ndani ya sikio.

 

3. Dawa hii inawezekana kupitia sehemu mbalimbali kama vile kwenye mdomo au sindano za matakoni na pajani au kwa wakati mwingine upitia kwenye mishipa ya damu , pia dawa hii ikishaingia kwenye mwili inawezekana kusambaa sehemu mbalimbali kama kwenye kondo la nyuma, kwenye maziwa kwa mama anayenyonyesha,na pia kweye maji maji ambayo yapo kwenye ubongo ambayo Kwa kitaamu huiitwa cerebral Spinal fluids.

 

4.pia dawa hii Kuna watu ambao hawapaswi kutumia na Kuna wale wanaopaswa kuitumia kwa taahadhari, ambao hawapaswi kutumia ni wale wenye alleji na cephalosporin na kwa  na wale wenye aleji Kali na penicillin, na wanaopaswa kuitumia kwa taahadhari ni wenye ugonjwa wa Figo wanapaswa kutumia china ya uangalizi maalumu au pengine wapunguziwe dozi, na wale wenye ugonjwa wa kisukari watumie chini ya uangalizi maalumu na kwa akina Mama wenye mimba na wanaonyonyesha wanapaswa kuitumia kwa taahadhari au kwa uangalizi Fulani.

 

5. Pia dawa hii Ina maudhi madogo madogo kwa watumiaji na maudhi hayo yakizidi ni vizuri kuwaona wataalamu wa afya Ili kubadilishiwaa dawa au kupewa huduma nyingine muhimu na maudhi hayo ni kama vile kizunguzungu na kutapika, maumivu ya tumbo na kichwa, upungufu wa damu kwa watumiaji.

 

6. Pia dawa hii haipaswi kutumiwa kiholela Bali utumika kulingana na wataalamu wa afya kwa sababu unaweza kutumia ukiwa nyumbani na hujui kama haipaswi kutumiwa atimaye unajiletea matatizo ya Bure.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Dawa Main: Post File: Download PDF Views 2228

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉5 Bongolite - Game zone - Play free game     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Fahamu kuhusu dawa za kutibu minyoo

Post hii inahusu zaidi dawa mbalimbali za kutibu minyoo, tunafahamu kabisa minyoo ni ugonjwa ambao uwapata watu mbalimbali hasa watoto.

Soma Zaidi...
DAWA YA FANGASI

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za fangasi

Soma Zaidi...
Faida za vidonge vya zamiconal

Posti hii inahusu zaidi faida za vidonge vya zamiconal, ni baadhi ya faida ambazo upatikana kutokana na vidonge vya zamiconal,ni vidonge ambavyo utibu au kusaidia kwenye matatizo ya viungo vya uzazi.

Soma Zaidi...
Dawa ya kutibu UTI

Nitakujuza dalili za UTI na dawa za kutibu UTI. Pia tutaona njia za kujikinga na UTI pamoja na dalili za UTI

Soma Zaidi...
Fahamu dawa ya kutibu kikohozi inayoitwa expectorant

Post hii inahusu zaidi dawa aina ya expectorant katika matibabu ya kikohozi,ni dawa ambayo usaidia au uzuia kikohozi kuendelea kutokea.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya griseofulvin

Post hii inahusu zaidi dawa ya griseofulvin ni dawa inayotumika kutibu fangasi za kwenye ngozi ambazo usababisha mabaka mabaka kwenye ngozi.

Soma Zaidi...