picha

Ijue dawa ya cephalosporin katika kupambana na bakteria

Post hii inahusu zaidi dawa ya cephalosporin katika kupambana na bakteria, ni mojawapo ya kundi kati ya makundi ya kupambana na bakteria ambalo ufanya Kazi kama penicillin.

Fahamu kuhusu dawa ya cephalosporin .

1. Dawa hii ya cephalosporin katika kupambana na bakteria huwa kwenye magroup muhimu matatu ambayo ni kundi la kwanza Lina dawa ya cephalexin, Kundi la pili Lina dawa ya cefamandole na kundi la tatu Lina dawa ya ceftriaxone na celfdimir, makundi yote matatu ufanya Kazi kwa umoja na kuweza kupambana na bakteria na kutibu magonjwa mbalimbali kama tutakavyoona hapo mbeleni.

 

2. Magonjwa mbalimbali ambayo utibiwa na cephalosporin na makundi yake ni kuzuia maambukizi kwenye ngozi, yaani maambukizi yabayoambatana na viupele pamoja na miwasho, kuzuia maambukizi kwenye mifupa na kwennye joint, kuzuia maambukizi kwenye mfumo wa mkojo na maambukizi ya njia za mkojo kwa kitaamu huiitwa UTI, kuzuia maambukizi kwenye tumbo,pia kuzuia maambukizi kwenye sikio hasa ndani ya sikio.

 

3. Dawa hii inawezekana kupitia sehemu mbalimbali kama vile kwenye mdomo au sindano za matakoni na pajani au kwa wakati mwingine upitia kwenye mishipa ya damu , pia dawa hii ikishaingia kwenye mwili inawezekana kusambaa sehemu mbalimbali kama kwenye kondo la nyuma, kwenye maziwa kwa mama anayenyonyesha,na pia kweye maji maji ambayo yapo kwenye ubongo ambayo Kwa kitaamu huiitwa cerebral Spinal fluids.

 

4.pia dawa hii Kuna watu ambao hawapaswi kutumia na Kuna wale wanaopaswa kuitumia kwa taahadhari, ambao hawapaswi kutumia ni wale wenye alleji na cephalosporin na kwa  na wale wenye aleji Kali na penicillin, na wanaopaswa kuitumia kwa taahadhari ni wenye ugonjwa wa Figo wanapaswa kutumia china ya uangalizi maalumu au pengine wapunguziwe dozi, na wale wenye ugonjwa wa kisukari watumie chini ya uangalizi maalumu na kwa akina Mama wenye mimba na wanaonyonyesha wanapaswa kuitumia kwa taahadhari au kwa uangalizi Fulani.

 

5. Pia dawa hii Ina maudhi madogo madogo kwa watumiaji na maudhi hayo yakizidi ni vizuri kuwaona wataalamu wa afya Ili kubadilishiwaa dawa au kupewa huduma nyingine muhimu na maudhi hayo ni kama vile kizunguzungu na kutapika, maumivu ya tumbo na kichwa, upungufu wa damu kwa watumiaji.

 

6. Pia dawa hii haipaswi kutumiwa kiholela Bali utumika kulingana na wataalamu wa afya kwa sababu unaweza kutumia ukiwa nyumbani na hujui kama haipaswi kutumiwa atimaye unajiletea matatizo ya Bure.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Dawa Main: Post File: Download PDF Views 2513

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 web hosting     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

Dawa za mitishamba za kutibu meno

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za mitishamba za kutibu meno

Soma Zaidi...
Fahamu zaidi kuhusiana na Dawa inayotibu shinikizo la damu. iitwayo LASIX

Lasix (Furosemide) iko katika kundi la dawa zinazoitwa vidonge vya maji (loop diuretics) vidonge vya maji. Lasix hutumiwa kupunguza uvimbe mwilini unaosababishwa na kushindwa kwa moyo, ugonjwa wa ini, au ugonjwa wa figo. Kwa matibabu ya dalili nyingi.La

Soma Zaidi...
Njia zinazotumika Ili kumpatia mgonjwa dawa

Posti hii inahusu zaidi njia kuu nne ambazo utumika kumpatia mgonjwa dawa, Ili kumpatia mgonjwa dawa Kuna njia za kutumia kama ifuayavyo.

Soma Zaidi...
Fahamu dawa za kutuliza magonjwa ya akili inayoitwa Chlorpromazine

Post hii inahusu zaidi dawa zinazosaidis katika kutuliza magonjwa ya akili, dawa hii kwa kitaamu huiitwa chlorpromazine ni dawa ambayo utumiwa na watu wenye tatizo la magonjwa ya akili na kwa kiasi kikubwa huwa sawa.

Soma Zaidi...
Fahamu dawa ya carvedilo katika matibabu ya magonjwa ya moyo

Post hii inahusu zaidi dawa ya carvedilo katika matibabu ya magonjwa, ni mojawapo ya dawa kwenye kundi la beta blockers na pia uhusika katika matibabu ya magonjwa ya moyo kama nyingine.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya streptomycin

Post hii inahusu zaidi dawa ya streptomycin ni dawa mojawapo ya kupambana na bakteria hasa wanaoshambulia mfumo wa hewa.

Soma Zaidi...