Ijue dawa ya cephalosporin katika kupambana na bakteria

Post hii inahusu zaidi dawa ya cephalosporin katika kupambana na bakteria, ni mojawapo ya kundi kati ya makundi ya kupambana na bakteria ambalo ufanya Kazi kama penicillin.

Fahamu kuhusu dawa ya cephalosporin .

1. Dawa hii ya cephalosporin katika kupambana na bakteria huwa kwenye magroup muhimu matatu ambayo ni kundi la kwanza Lina dawa ya cephalexin, Kundi la pili Lina dawa ya cefamandole na kundi la tatu Lina dawa ya ceftriaxone na celfdimir, makundi yote matatu ufanya Kazi kwa umoja na kuweza kupambana na bakteria na kutibu magonjwa mbalimbali kama tutakavyoona hapo mbeleni.

 

2. Magonjwa mbalimbali ambayo utibiwa na cephalosporin na makundi yake ni kuzuia maambukizi kwenye ngozi, yaani maambukizi yabayoambatana na viupele pamoja na miwasho, kuzuia maambukizi kwenye mifupa na kwennye joint, kuzuia maambukizi kwenye mfumo wa mkojo na maambukizi ya njia za mkojo kwa kitaamu huiitwa UTI, kuzuia maambukizi kwenye tumbo,pia kuzuia maambukizi kwenye sikio hasa ndani ya sikio.

 

3. Dawa hii inawezekana kupitia sehemu mbalimbali kama vile kwenye mdomo au sindano za matakoni na pajani au kwa wakati mwingine upitia kwenye mishipa ya damu , pia dawa hii ikishaingia kwenye mwili inawezekana kusambaa sehemu mbalimbali kama kwenye kondo la nyuma, kwenye maziwa kwa mama anayenyonyesha,na pia kweye maji maji ambayo yapo kwenye ubongo ambayo Kwa kitaamu huiitwa cerebral Spinal fluids.

 

4.pia dawa hii Kuna watu ambao hawapaswi kutumia na Kuna wale wanaopaswa kuitumia kwa taahadhari, ambao hawapaswi kutumia ni wale wenye alleji na cephalosporin na kwa  na wale wenye aleji Kali na penicillin, na wanaopaswa kuitumia kwa taahadhari ni wenye ugonjwa wa Figo wanapaswa kutumia china ya uangalizi maalumu au pengine wapunguziwe dozi, na wale wenye ugonjwa wa kisukari watumie chini ya uangalizi maalumu na kwa akina Mama wenye mimba na wanaonyonyesha wanapaswa kuitumia kwa taahadhari au kwa uangalizi Fulani.

 

5. Pia dawa hii Ina maudhi madogo madogo kwa watumiaji na maudhi hayo yakizidi ni vizuri kuwaona wataalamu wa afya Ili kubadilishiwaa dawa au kupewa huduma nyingine muhimu na maudhi hayo ni kama vile kizunguzungu na kutapika, maumivu ya tumbo na kichwa, upungufu wa damu kwa watumiaji.

 

6. Pia dawa hii haipaswi kutumiwa kiholela Bali utumika kulingana na wataalamu wa afya kwa sababu unaweza kutumia ukiwa nyumbani na hujui kama haipaswi kutumiwa atimaye unajiletea matatizo ya Bure.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Dawa Main: Afya File: Download PDF Views 1956

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Dua za Mitume na Manabii    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 web hosting    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Dawa inaitwa koflame ukitumia inashida kwa mama mjamzito? Maumivu ya mgongo na nyonga zinasumbua

Maumivu ya mgongo hutokea sana kwa wajawazito. Ijapokuwa ni hali ya usumbufu sana ila hakikisha hautumii madawa kiholela kutoka maduka ya dawa ama miti shamba. Kwani ukikisea kidogobinawezabhatarisha afya ya mtoto

Soma Zaidi...
Dawa ya kuzuia kuathirika kwa watu walio hatarini kupata VVU

Somo hili linakwenda kukuletea dawa ya kuzuia kuathirika kwa watu walio hatarini kupata VVU

Soma Zaidi...
Ifahamu dawa ya kutibu kifua kikuu

Post hii inahusu zaidi dawa ya Rifampin kama dawa mojawapo ya kutibu kifua kikuu.

Soma Zaidi...
Dawa za kutibu fangasi kwenye kucha

Makala hiii inakwenda kukueleza dawa za kutibu fangasi kwenye kucha.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya loperamide dawa ya kuzuia kuharusha

Post hii inahusu zaidi dawa ya loperamide ni dawa ambayo inazuia kuharisha ni dawa inayofanya kazi kuanzia kwenye utumbo na pia usaidia kutuliza maumivu ya tumbo

Soma Zaidi...
Fahamu matumizi ya Ampicillin.

Ampicillin ni antibiotic yenye msingi wa penicillin ambayo inafanya kazi kupambana na maambukizi ya ndani ya bakteria. Ampicillin hufanya kazi ya kuharibu kuta za kinga ambazo bakteria huunda ndani ya mwili wako na kuzuia bakteria wapya kutokeza. Ampici

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya mucolytic dawa ya kutibu kikohozi

Post hii inahusu zaidi dawa ya mucolytic katika kutibu kikohozi kwa watu wazima na watoto.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya Nystatin

Post hii inahusu zaidi dawa ya Nystatin ni mojawapo ya dawa ambayo utumika kwenye ngozi.

Soma Zaidi...
Ijue Dawa ya lignocaine

Posti hii inahusu zaidi dawa ya lignocaine kama mojawapo ya Dawa ambayo utumika wakati wa upasuaji.

Soma Zaidi...