picha

Fahamu dawa ya sulfonamide dawa inayopambana na maambukizi ya bakteria mwilini.

Post hii inahusu zaidi dawa ya sulphonamide ni mojawapo ya dawa ambayo usaidia kutibu magonjwa mbalimbali yanayosababishwa na bakteria ni dawa au antibiotics ya mda mrefu na pia matumizi yake sio makubwa sana kwa sababu ya kuwepo kwa antibiotics zenye ngu

Fahamu kuhusu dawa ya sulphonamide katika kupambana na bakteria .

1. Dawa hii kwa kawaida usaidia kupambana na maambukizi ya bakteria kwenye sehemu mbalimbali za mwili kama vile maambukizi kwenye sehemu ya ndani na ya nje ya sikio, matibabu ya nimonia, kuzuia maambukizi kwenye mkojo kwa lugha inayoeleweka ni UTI kutibu maambukizi ya bakteria kwenye mfumo wa upumuaji, maambukizi kwenye mifupa ambayo Kwa kitaamu huiitwa osteomyelitis, matibabu kwenye vidonda vilivyoungua, matibabu ya gonorrhea na pia kwenye tumbo kama Kuna maambukizi ya bakteria.

 

2. Pia dawa hii ufanya Kazi kwa kupitiakwenye mmengenyo wa chakula na pia uingia kwenye mzunguko wa damu na kufanya kazi ya kutibu au kupambana na bakteria,Inapambana na bakteria kwa kuzuia kuzaliana kwa bakteria na wale waliokwishazaliana Wana dumaa na hawaendelea kukua hali inayosababisha matibabu yake kufanikiwa zaidi na pia bakteria hao hawawezi kuzaliana tena na pia dawa hii uingilia kwenye nuklia ya bakteria na kuharibu Kila kitu ndani ya seli ya ya bakteria.

 

3.Dawa hii mara nyingi huwa kwenye mfumo wa vidonge kwa hiyo matumizi yake utegemea wataalamu wa afya , vile vile dawa hii utumiwa na watu mbalimbali ila Kuna watu ambao hawapaswi kuitumia hasa wale wenye aleji na dawa hii pamoja na wale wenye aleji na sulfa na wenyewe hawapaswi kutumia, pia Kuna wale wenye ugonjwa wa maumivu ya kichwa Wanaoaswa kuitumia kwa taahadhari kwa sababu dawa hii Ina maudhi ya kuwepo kwa maumivu ya kichwa kwa watumiaji kwa hiyo wakiendelea kuitumia itawafanya maumivu ya kichwa kuongezeka.

 

4. Vile vile dawa hii Ina maudhi madogo madogo ambayo yanaweza kutokea kwa watumiaji maudhi hayo ni kama kuwashwa kwenye mwili mzima na pengine kutokea kwa vi upele vidogo vidogo ambavyo uendelea kuwasha tu, pamoja na hayo Kuna hali ya kichefuchefu ujitokeza, kutapika na maumivu ya tumbo, pia Kuna upungufu w hamu ya kula uweza kujitokeza,na maumivu ya kichwa ya mara kwa mara mpaka dawa itakapoisha mwilini.

 

5.kutokana na kuwepo kwa maudhi madogo madogo ni kawaida kwa watumiaji wa dawa ila maumivu hayo yakizidi ni vizuri kuwaona wataalamu wa afya Ili kubadilishiwaa dawa au kupewa dawa ya kutuliza hayo matokeo ya dawa, pia kwa wale ambao huwa na ugonjwa wa maumivu ya kichwa ni vizuri kabisa kuwepo kwenye uangalizi wa wataalamu wa afya Ili kuweza kuepuka madhara mengine ambayo yanaweza kujitokeza.

 

6. Pia dawa hii haipaswi kutumika kiholela inapaswa kutumiwa kulingana na wataalamu wa afya kwa sababu mda mwingine dawa hii Ina matokeo mbalimbali ambayo yakitokea kwa mtu akiwa nyumbani matatizo yanaweza kuwa magumu kidogo, kwa hiyo kuwaona wataalamu wa afya ni jambo la muhimu kwq sababu unakuwa na uhakika wa kutosha.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/12/22/Thursday - 03:05:03 pm Topic: Dawa Main: Afya File: Download PDF Views 1281

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 web hosting    👉6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

Fahamu dawa ya cardiac glycoside katika matibabu ya magonjwa ya moyo

Post hii inahusu zaidi dawa ya cardiac glycoside katika matibabu ya magonjwa ya moyo,dawa maalum ambayo imo kwenye kundi hili la cardiac glycoside ni digoxin, ni dawa muhimu ambayo utumika kwenye mfumo wa vidonge mara nyingi.

Soma Zaidi...
Miungurumo haiishi tumboni nikishika upande wa kushoto wa tumbo kuna maumivu kwa mbali je mm nitumie dawa gan kuondoa tatizo hilo

Kukawa na gesi tumboni kunaweza kuwa ni dalili ya shida kwenye afya, hasa katika mfumo wa chakula. Hali itakuwa sio nzuri endapo utakosea hamu ya kula na kuhisivkushiba muda wowote.

Soma Zaidi...
Namna ya kutumia tiba ya jino.

Posti hii inahusu zaidi namna au njia ya kufanya Ili kuweza kutumia tiba hii ya jino, kwa sababu ya mchanganyiko ambao umekwisha kuwepo kwa hiyo unachumua mchanganyiko unafanya kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
Penicillin dawa ya kutibu maambukizi ya bakteria mwilini

Post hii Inahusu zaidi dawa za kutibu maambukizi yoyote Yale yanayosababishwa na bakteria dawa hizi kwa kitaamu huiitwa antibiotics Kuna dawa mbalimbali zinazotibu maambukizi ya bakteria leo tutaanza na dawa ambayo inaitwa penicillin.

Soma Zaidi...
Dawa ya Rifampicin na kazi zake

Posti hii inahusu zaidi Dawa ya Rifampicin na kazi zake, hii ni dawa mojawapo inayotibu kifua kikuu kati ya Dawa zilizoteuliwa kutibu ugonjwa wa kifua kikuu.

Soma Zaidi...
Fahamu matumizi ya Dawa iitwayo Aspirin.

Aspirini Ni dawa ya kutuliza maumivu.Majina yanayoaminika zaidi katika kutuliza maumivu sasa yanapatikana kwa njia mbadala inayookoa gharama kwa kutumia Aspirini. Aspirini inayopendwa na familia kwa miongo kadhaa, mara nyingi hutumiwa kupunguza maumivu y

Soma Zaidi...
Mgawanyo wa tiba ya kifua kikuu

Post hii inahusu zaidi mgawanyiko wa tiba ya kifua kikuu, kwa kawaida tiba hii imegawanyika katika sehemu kuu mbili.

Soma Zaidi...
Dawa za fangasi ukeni

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za fangasi ukeni

Soma Zaidi...
Fahamu dawa ya aminophylline kutibi maambukizi kwenye mfumo wa upumuaji

Post hii inahusu zaidi dawa ya aminophylline katika kutuliza maambukizi kwenye mfumo wa upumuaji.

Soma Zaidi...
Dawa za maumivu ya jino

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za maumivu ya jino

Soma Zaidi...