FAHAMU DAWA YA SULFONAMIDE DAWA INAYOPAMBANA NA MAAMBUKIZI YA BAKTERIA MWILINI.


image


Post hii inahusu zaidi dawa ya sulphonamide ni mojawapo ya dawa ambayo usaidia kutibu magonjwa mbalimbali yanayosababishwa na bakteria ni dawa au antibiotics ya mda mrefu na pia matumizi yake sio makubwa sana kwa sababu ya kuwepo kwa antibiotics zenye nguvu zaidi kuliko yenyewe,lakina dawa nyingine zikishindikana yenyewe bado inatumika na watu wanapona.


Fahamu kuhusu dawa ya sulphonamide katika kupambana na bakteria .

1. Dawa hii kwa kawaida usaidia kupambana na maambukizi ya bakteria kwenye sehemu mbalimbali za mwili kama vile maambukizi kwenye sehemu ya ndani na ya nje ya sikio, matibabu ya nimonia, kuzuia maambukizi kwenye mkojo kwa lugha inayoeleweka ni UTI kutibu maambukizi ya bakteria kwenye mfumo wa upumuaji, maambukizi kwenye mifupa ambayo Kwa kitaamu huiitwa osteomyelitis, matibabu kwenye vidonda vilivyoungua, matibabu ya gonorrhea na pia kwenye tumbo kama Kuna maambukizi ya bakteria.

 

2. Pia dawa hii ufanya Kazi kwa kupitiakwenye mmengenyo wa chakula na pia uingia kwenye mzunguko wa damu na kufanya kazi ya kutibu au kupambana na bakteria,Inapambana na bakteria kwa kuzuia kuzaliana kwa bakteria na wale waliokwishazaliana Wana dumaa na hawaendelea kukua hali inayosababisha matibabu yake kufanikiwa zaidi na pia bakteria hao hawawezi kuzaliana tena na pia dawa hii uingilia kwenye nuklia ya bakteria na kuharibu Kila kitu ndani ya seli ya ya bakteria.

 

3.Dawa hii mara nyingi huwa kwenye mfumo wa vidonge kwa hiyo matumizi yake utegemea wataalamu wa afya , vile vile dawa hii utumiwa na watu mbalimbali ila Kuna watu ambao hawapaswi kuitumia hasa wale wenye aleji na dawa hii pamoja na wale wenye aleji na sulfa na wenyewe hawapaswi kutumia, pia Kuna wale wenye ugonjwa wa maumivu ya kichwa Wanaoaswa kuitumia kwa taahadhari kwa sababu dawa hii Ina maudhi ya kuwepo kwa maumivu ya kichwa kwa watumiaji kwa hiyo wakiendelea kuitumia itawafanya maumivu ya kichwa kuongezeka.

 

4. Vile vile dawa hii Ina maudhi madogo madogo ambayo yanaweza kutokea kwa watumiaji maudhi hayo ni kama kuwashwa kwenye mwili mzima na pengine kutokea kwa vi upele vidogo vidogo ambavyo uendelea kuwasha tu, pamoja na hayo Kuna hali ya kichefuchefu ujitokeza, kutapika na maumivu ya tumbo, pia Kuna upungufu w hamu ya kula uweza kujitokeza,na maumivu ya kichwa ya mara kwa mara mpaka dawa itakapoisha mwilini.

 

5.kutokana na kuwepo kwa maudhi madogo madogo ni kawaida kwa watumiaji wa dawa ila maumivu hayo yakizidi ni vizuri kuwaona wataalamu wa afya Ili kubadilishiwaa dawa au kupewa dawa ya kutuliza hayo matokeo ya dawa, pia kwa wale ambao huwa na ugonjwa wa maumivu ya kichwa ni vizuri kabisa kuwepo kwenye uangalizi wa wataalamu wa afya Ili kuweza kuepuka madhara mengine ambayo yanaweza kujitokeza.

 

6. Pia dawa hii haipaswi kutumika kiholela inapaswa kutumiwa kulingana na wataalamu wa afya kwa sababu mda mwingine dawa hii Ina matokeo mbalimbali ambayo yakitokea kwa mtu akiwa nyumbani matatizo yanaweza kuwa magumu kidogo, kwa hiyo kuwaona wataalamu wa afya ni jambo la muhimu kwq sababu unakuwa na uhakika wa kutosha.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Magonjwa na afya       ðŸ‘‰    2 Hadiythi za alif lela u lela       ðŸ‘‰    3 Mafunzo ya php       ðŸ‘‰    4 Mafunzo ya html kwa kiswahili       ðŸ‘‰    5 Jifunze fiqh       ðŸ‘‰    6 Madrasa kiganjani    


Je! una maswali, mapendekezo ama maoni? tuma ujumbe wa meseji SMS hapo chini ili kuunganishwa na muhusika au bofya hapa

SMS SMS



Post Nyingine


image Fahamu matumizi ya Dawa iitwayo paracetamol.
Paracetamol kwa jina kingine hujulikana kama(acetaminophen) ni dawa ya kawaida ya kutuliza maumivu ambayo hutumiwa kupunguza aina mbalimbali za maumivu. Paracetamol ndilo jina linalojulikana zaidi katika kutuliza maumivu ya kawaida. Paracetamol inajulikana sana kutibu maumivu ya kichwa, lakini pia inaweza kutumika kwa maumivu ya misuli, homa, mgongo, meno na hata maumivu ya mifupa (arthritis). Soma Zaidi...

image Fahamu kuhusu dawa ya griseofulvin
Post hii inahusu zaidi dawa ya griseofulvin ni dawa inayotumika kutibu fangasi za kwenye ngozi ambazo usababisha mabaka mabaka kwenye ngozi. Soma Zaidi...

image Penicillin dawa ya kutibu maambukizi ya bakteria mwilini
Post hii Inahusu zaidi dawa za kutibu maambukizi yoyote Yale yanayosababishwa na bakteria dawa hizi kwa kitaamu huiitwa antibiotics Kuna dawa mbalimbali zinazotibu maambukizi ya bakteria leo tutaanza na dawa ambayo inaitwa penicillin. Soma Zaidi...

image Matumizi ya dawa ya vidonda vya tumbo
Posti hii inahusu zaidi matumizi ya dawa za vidonda vya tumbo, ili kuweza kutumia dawa hizi ni vizuri kabisa kufuata mashariti kama ifuatavyo. Soma Zaidi...

image Fahamu dawa ya carvedilo katika matibabu ya magonjwa ya moyo
Post hii inahusu zaidi dawa ya carvedilo katika matibabu ya magonjwa, ni mojawapo ya dawa kwenye kundi la beta blockers na pia uhusika katika matibabu ya magonjwa ya moyo kama nyingine. Soma Zaidi...

image Ifahamu dawa ya epinephrine kwa kutuliza aleji
Post hii inahusu zaidi dawa ya epinephrine kwa kutuliza aleji ni dawa ambayo imependekezwa kutuliza aleji kama dawa ya hydrocortisone, Prednisone hazipo au zimeshindwa kufanya kazi. Soma Zaidi...

image Fahamu dawa ya Prednisone katika kupambana na aleji
Post hii inahusu zaidi dawa ya Prednisone ambayo usaidia katika kupambana na aleji. Soma Zaidi...

image Fahamu dawa ya diazepam katika kutuliza kifafa
Post hii inahusu zaidi dawa ya diazepam katika kutuliza kifafa, ni dawa ambayo matumizi yake yanaweza kuingilia pote kwenye kutuliza kifafa na pia kwa wagonjwa wa akili. Soma Zaidi...

image Fahamau madhara ya flagyl (Metronidazole)
Flagyl ni nini? Flagyl (metronidazole) ni antibiotic. Inapigana na bakteria katika mwili wako. Flagyl hutumiwa kutibu maambukizo ya bakteria ya uke, tumbo, ngozi, viungo na njia ya upumuaji. Soma Zaidi...

image Fahamu matumizi ya Ampicillin.
Ampicillin ni antibiotic yenye msingi wa penicillin ambayo inafanya kazi kupambana na maambukizi ya ndani ya bakteria. Ampicillin hufanya kazi ya kuharibu kuta za kinga ambazo bakteria huunda ndani ya mwili wako na kuzuia bakteria wapya kutokeza. Ampicillin ni kiuavijasumu chenye ufanisi mkubwa, na ni mojawapo ya dawa zinazopendekezwa na madaktari. Soma Zaidi...