picha

Fahamu dawa ya sulfonamide dawa inayopambana na maambukizi ya bakteria mwilini.

Post hii inahusu zaidi dawa ya sulphonamide ni mojawapo ya dawa ambayo usaidia kutibu magonjwa mbalimbali yanayosababishwa na bakteria ni dawa au antibiotics ya mda mrefu na pia matumizi yake sio makubwa sana kwa sababu ya kuwepo kwa antibiotics zenye ngu

Fahamu kuhusu dawa ya sulphonamide katika kupambana na bakteria .

1. Dawa hii kwa kawaida usaidia kupambana na maambukizi ya bakteria kwenye sehemu mbalimbali za mwili kama vile maambukizi kwenye sehemu ya ndani na ya nje ya sikio, matibabu ya nimonia, kuzuia maambukizi kwenye mkojo kwa lugha inayoeleweka ni UTI kutibu maambukizi ya bakteria kwenye mfumo wa upumuaji, maambukizi kwenye mifupa ambayo Kwa kitaamu huiitwa osteomyelitis, matibabu kwenye vidonda vilivyoungua, matibabu ya gonorrhea na pia kwenye tumbo kama Kuna maambukizi ya bakteria.

 

2. Pia dawa hii ufanya Kazi kwa kupitiakwenye mmengenyo wa chakula na pia uingia kwenye mzunguko wa damu na kufanya kazi ya kutibu au kupambana na bakteria,Inapambana na bakteria kwa kuzuia kuzaliana kwa bakteria na wale waliokwishazaliana Wana dumaa na hawaendelea kukua hali inayosababisha matibabu yake kufanikiwa zaidi na pia bakteria hao hawawezi kuzaliana tena na pia dawa hii uingilia kwenye nuklia ya bakteria na kuharibu Kila kitu ndani ya seli ya ya bakteria.

 

3.Dawa hii mara nyingi huwa kwenye mfumo wa vidonge kwa hiyo matumizi yake utegemea wataalamu wa afya , vile vile dawa hii utumiwa na watu mbalimbali ila Kuna watu ambao hawapaswi kuitumia hasa wale wenye aleji na dawa hii pamoja na wale wenye aleji na sulfa na wenyewe hawapaswi kutumia, pia Kuna wale wenye ugonjwa wa maumivu ya kichwa Wanaoaswa kuitumia kwa taahadhari kwa sababu dawa hii Ina maudhi ya kuwepo kwa maumivu ya kichwa kwa watumiaji kwa hiyo wakiendelea kuitumia itawafanya maumivu ya kichwa kuongezeka.

 

4. Vile vile dawa hii Ina maudhi madogo madogo ambayo yanaweza kutokea kwa watumiaji maudhi hayo ni kama kuwashwa kwenye mwili mzima na pengine kutokea kwa vi upele vidogo vidogo ambavyo uendelea kuwasha tu, pamoja na hayo Kuna hali ya kichefuchefu ujitokeza, kutapika na maumivu ya tumbo, pia Kuna upungufu w hamu ya kula uweza kujitokeza,na maumivu ya kichwa ya mara kwa mara mpaka dawa itakapoisha mwilini.

 

5.kutokana na kuwepo kwa maudhi madogo madogo ni kawaida kwa watumiaji wa dawa ila maumivu hayo yakizidi ni vizuri kuwaona wataalamu wa afya Ili kubadilishiwaa dawa au kupewa dawa ya kutuliza hayo matokeo ya dawa, pia kwa wale ambao huwa na ugonjwa wa maumivu ya kichwa ni vizuri kabisa kuwepo kwenye uangalizi wa wataalamu wa afya Ili kuweza kuepuka madhara mengine ambayo yanaweza kujitokeza.

 

6. Pia dawa hii haipaswi kutumika kiholela inapaswa kutumiwa kulingana na wataalamu wa afya kwa sababu mda mwingine dawa hii Ina matokeo mbalimbali ambayo yakitokea kwa mtu akiwa nyumbani matatizo yanaweza kuwa magumu kidogo, kwa hiyo kuwaona wataalamu wa afya ni jambo la muhimu kwq sababu unakuwa na uhakika wa kutosha.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Dawa Main: Post File: Download PDF Views 1301

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 web hosting     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 Bongolite - Game zone - Play free game     👉5 ai web app     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

Fahamu dawa ya kuzuia enzymes zinazotengenezwa na bakteria

Post hii inahusu zaidi dawa ya cloxacillin ambayo Iko kwenye kundi mojawapo la penicillin ambalo uzuia enzymes zinazotengenezwa na bakteria.

Soma Zaidi...
Fahamu matumizi ya Dawa iitwayo paracetamol.

Paracetamol kwa jina kingine hujulikana kama(acetaminophen) ni dawa ya kawaida ya kutuliza maumivu ambayo hutumiwa kupunguza aina mbalimbali za maumivu. Paracetamol ndilo jina linalojulikana zaidi katika kutuliza maumivu ya kawaida. Paracetamol inajulik

Soma Zaidi...
Ifahamu dawa ya furosemide.

Post hii inahusu zaidi dawa ya furosemide ni mojawapo ya dawa ambayo ipo kwenye kundi la diuretics na kwa jina linguine huitwa lasix

Soma Zaidi...
Fahamu dawa za cyclophosphamide na mustargen.

Post hii inahusu zaidi dawa za cyclophosphamide na mustargen katika kupambana na ugonjwa wa Kansa.

Soma Zaidi...
Dapsone na kazi zake

Posti hii inahusu zaidi dawa ya Dapsone na kazi zake, hii ni dawa ambayo utumika katika kutibu ugonjwa wa ukimwi, dawa hii ufanya kazi kwa mchanganyiko wa dawa nyingine kama vile Rifampicin na clofaximine.

Soma Zaidi...
Dawa ya penicillin ambayo uzuia asidi ya bakteria.

Post hii inahusu zaidi dawa ya phenoxy-methyl penicillin ambayo upambana na aina ya bakteria ambao utoa sumu Ili kuzuia dawa isifanye kazi.

Soma Zaidi...