Posti hii inakwenda kukufundisha dua za kuomba wakati wa kuwa na maumivu kwenye mwili wako.
DUA ZA KUONDOA MAUMIVU MWILINI
Katika uislamu Allah amejaalia dawa katika kufuata sunnah. Hakuna haja ya kumeza dawa za kupunguza maumivu kwa mwenye kumuamini Allah. Ila watu wasielewe vibaya maneno haya, maaana Mtume (s.a.w) amesisitiza watu wajitibu, ila pia ieleweke Allah amejaalia kuwa qurani ni dawa na ni ponyo kwa maradhi na mabo mengine. Leo hapa nimewaandalia dawa ya kuondowa maumivu katika sunnah nayo ni dua ambayo mtume (s.a.w) alikuwa akiwafundisha masahaba waombe pindi wakiwa na maumivu na maradhi.
1.Mtume (s.a.w) alimwambia swahaba kuwa: “weka mkono wako pale unaposikia maumivu katika mwili wako kisha sema “BISMILLAHI” mara tatu kisha useme mara saba (maneno haya): “A’UDHU BILLAHI WAQUDRATIHI MIN-SHARI MAA AJIDU WA-UHAADHIRU”. Hadithi hii ni sahihi na amepokea Muslim, Abu Daud na Ibn Maajah kutokana na masimulizi ya ‘Uthman Ibn Abil-”As.
2.Mtume (s.a.w) alimwambia Mainuna bint Abi Ubay kuwa :”weka mkono wako wa kulia pale panapokupatia maudhi (maumivu) kisha sema “BISMILLAHI ALLAHUMMA DAAWINI BIDAWAAIKA WASHFINII BISHAAIKA WAGHANII BIFADHLIKA ‘AN-MAN SIWAAKA WAHDHUR ‘ANII ADHAAKA” (Amepokea Tabrany)
3.Mume (s.a.w) alimwambia Asmaa bint AbuBakar kuwa: “weka mkono wako (pende maumivu) na useme mara tatu “BISMILLAHI ALLAHUMMA ADH-HAB ‘ANNI SHARRA MAA AJIDU BIDA’AWATIKA NABIYYIKA TWAYYIBIL-MUBAARAKIL-MAKIIN ‘INDAKA. BISMILLAHI “ (Amepokea ibn “Asakir)
4.amesimulia Ibn ‘Abas (r.a) kuwa : “alikuwa Mtume (s.a.w) akitufundisha dua kwa ajili ya maradhi na maumivu yote tunayoyapata kuwa Mtu aseme: ‘BISMILLAHI, A’UDHUBILLAHIL-’ADHIIM MINSHARRI KULLI ‘ARQIN-NA’AARI, WAMINSHARRI HARRIN-NAHAARI” (Amepokea Ahmad, tirmidh na Alhaakim).
Je! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu
Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF
Share On
Facebook
or
Whatsapp
Imesomwa mara 3431
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya
👉2 Madrasa kiganjani
👉3 Kitau cha Fiqh
👉4 kitabu cha Simulizi
Hadithi Ya 40: Kuwa Duniani Kama Vile Mgeni Au Mpita Njia
Soma Zaidi...
hadithi ya 8
عَنْ ابْنِ عُمَرَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا، أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم قَالَ: "أُمِرْتُ أَنْ أُقَاتِلَ النَّاسَ حَتَّى ?... Soma Zaidi...
Hadithi Ya 23: Tohara Ni Nusu Ya Imaan
Soma Zaidi...
UHAKIKI WA HADITHI
Uhakiki wa Hadith za Mtume (s. Soma Zaidi...
ZIJUWE NAMNA ZA KUZUIA HASIRA, NA MADHARA YA HASIRA
28. Soma Zaidi...
Namna ya kumuosha maiti hatua kwa hatua, nguzo na sunnah za josho la maiti
1. Soma Zaidi...
kuwa na kauli njema, na faida zake katika jamii
11. Soma Zaidi...
Fadhila za udhu yaani faida za udhu
Katika makala hii utajifunza faida za kuwa na udhu Soma Zaidi...
Masomo ya Dua na Faida zake Dua
Soma Dua mbalimbali hapa, Soma Zaidi...
DUA 94 - 114
DUA ZA KUONDOA WASIWASI, SIHIRI NA UCHAWI 94. Soma Zaidi...
DUA ZA KUONDOA WASIWASI
DUA ZA KUONDOA MAUMIVU MWILINI Katika uislamu Allah amejaalia dawa katika kufuata sunnah. Soma Zaidi...
Al-Arba'uwn An-Nawawiyyah hadithi ya 1: Nia
huu ni mwanzo wa kitabu hiki cha Matn arbaina Naway Soma Zaidi...