ADABU ZA KUOMBA DUA

ADABU ZA KUOMBA DUA.

ADABU ZA KUOMBA DUA


ADABU ZA KUOMBA DUA.
1.kuelekea qibla. Amesimulia Abdallah Ibn Zayd ุฑุถู‰ุงู„ู„ู‡ ุนู†ู‡ kuwa โ€œalitoka Mtume ุตู„ู‘ูŠ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆุณู„ู‘ู… kwenda kuomba dua ya mvua akaelekea kiblaโ€. (amepokea Bukhari).

2.Kunyanyua mikono miwili juu. Amesimulia Abuu Musa ุฑุถู‰ุงู„ู„ู‡ ุนู†ู‡ kuwa โ€œaliomba Mtume ุตู„ู‘ูŠ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆุณู„ู‘ู… dua akanyanyua mikono yake mpaka nikaona weupe wa kwapa lakeโ€ (amepokea Bukhari). Na amesimulia Ibn โ€˜Abas kuwa Mtume ุตู„ู‘ูŠ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆุณู„ู‘ู… amesema โ€ "โ€ ุฅูุฐูŽุง ุฏูŽุนูŽูˆู’ุชูŽ ุงู„ู„ู‘ูŽู‡ูŽ ููŽุงุฏู’ุนู ุจูุจูุทููˆู†ู ูƒูŽูู‘ูŽูŠู’ูƒูŽ ูˆูŽู„ุงูŽ ุชูŽุฏู’ุนู ุจูุธูู‡ููˆุฑูู‡ูู…ูŽุง ููŽุฅูุฐูŽุง ููŽุฑูŽุบู’ุชูŽ ููŽุงู…ู’ุณูŽุญู’ ุจูู‡ูู…ูŽุง ูˆูŽุฌู’ู‡ูŽูƒูŽ โ€œmuombeni Allah kwa matumbo ya viganya vyenu, wala msimuombe kwa migongo ya viganja vyenu.โ€ฆโ€. (amepokea Abuu Daud na Bayhaqiy).

3.Kuanza dua kwa kwa kumsifu Allah na kumshukuru (kama kusema alhamdu lillah โ€ฆ.) na kumswalia Mtume ุตู„ู‘ูŠ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆุณู„ู‘ู…. Amesimulia โ€˜Abdullah Ibn Masโ€™ud ุฑุถู‰ุงู„ู„ู‡ ุนู†ู‡ kuwa nilikuwa nikiswali, wakati Mtume yupo na Abuubakar na โ€˜Umar, basi nilipokaa nikaanza kumshukuru Allah na kumsifu na nikamswalia Mtume ุตู„ู‘ูŠ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆุณู„ู‘ู… kisha nikajiombea dua, akasema mtume ุตู„ู‘ูŠ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆุณู„ู‘ู… โ€˜omba utapewa, omba utapewaโ€™โ€. (amepokea tirmidh kwa isnad sahih). Na katika masimulizi ya Fudailah Ibn โ€˜Ubayd ุฑุถู‰ุงู„ู„ู‡ ุนู†ู‡ amesema โ€œhakika amefundisha mtume ุตู„ู‘ูŠ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆุณู„ู‘ู… uma wake jinsi ya kuomba dua akasema โ€˜pindi anapoomba dua mmoja wenu basi aanze na tahmid (kumshukuru Allah) na thanaai (kumsifu Allah) kisha amswalie Mtume ุตู„ู‘ูŠ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆุณู„ู‘ู… kisha aombe chochote anachotakaโ€™โ€ โ€"โ€ ุฅูุฐูŽุง ุตูŽู„ู‘ูŽู‰ ุฃูŽุญูŽุฏููƒูู…ู’ ููŽู„ู’ูŠูŽุจู’ุฏูŽุฃู’ ุจูุชูŽุญู’ู…ููŠุฏู ุงู„ู„ู‘ูŽู‡ู ูˆูŽุงู„ุซู‘ูŽู†ูŽุงุกู ุนูŽู„ูŽูŠู’ู‡ู ุซูู…ู‘ูŽ ู„ููŠูุตูŽู„ู‘ู ุนูŽู„ูŽู‰ ุงู„ู†ู‘ูŽุจููŠู‘ู ุตู„ู‰ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆุณู„ู… ุซูู…ู‘ูŽ ู„ููŠูŽุฏู’ุนู ุจูŽุนู’ุฏู ุจูู…ูŽุง ุดูŽุงุกูŽ โ€"โ€ (amepokea Abuu Daud, tirmidh, Ibn Hiban na baihaqy).

4.Kuanza kuomba dua kwa kujiombea mwenyewe. Kwa anayetaka kumuombea mtu mwingine dua anatakiwa aanze na kujiombea mwenyewe. Amesimulia Ubaiya Ibn Kโ€™ab ุฑุถู‰ุงู„ู„ู‡ ุนู†ู‡ kuwa ุนูŽู†ู’ ุฃูุจูŽู‰ู‘ู ุจู’ู†ู ูƒูŽุนู’ุจูุŒ ุฃูŽู†ู‘ูŽ ุฑูŽุณููˆู„ูŽ ุงู„ู„ู‘ูŽู‡ู ุตู„ู‰ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆุณู„ู… ูƒูŽุงู†ูŽ ุฅูุฐูŽุง ุฐูŽูƒูŽุฑูŽ ุฃูŽุญูŽุฏู‹ุง ููŽุฏูŽุนูŽุง ู„ูŽู‡ู ุจูŽุฏูŽุฃูŽ ุจูู†ูŽูู’ุณูู‡ู โ€œalikuwa mtume ุตู„ู‘ูŠ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆุณู„ู‘ู… anapomkumbuka mtu na akataka kumuombea dua huanza kwa kujiombea mwenyewe kwanza.โ€ (amepokea tirmidh kwa isnad sahih).

5.Kurudia rudia katika kuomba na kusisitiza maombi yako. Ila usiharakishe majibu kutaka kujibiwa haraka hata ukawa unamlaumu Allah. Amesimulia Abdallah ibn Msโ€™ud ุฑุถู‰ุงู„ู„ู‡ ุนู†ู‡ kuwa alikuwa Mtume ุตู„ู‘ูŠ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆุณู„ู‘ู… anapenda kuomba mara tatutatu na (akawa) anaomba istighfar (msamaha) mara tatutatu. (amepokea Abu Daud kwa isnad salih).

6.Kuwa na yaqini juu ya kujibiwa na kujiepusha na yaliyo haramu. Mtu anatakiwa asiwe na shaka juu ya kujibiwa dua yake. Amesimulia Abuu Hurairah ุฑุถู‰ุงู„ู„ู‡ ุนู†ู‡ kuwa Mtume ุตู„ู‘ูŠ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆุณู„ู‘ู… amesema "โ€ ุงุฏู’ุนููˆุง ุงู„ู„ู‘ูŽู‡ูŽ ูˆูŽุฃูŽู†ู’ุชูู…ู’ ู…ููˆู‚ูู†ููˆู†ูŽ ุจูุงู„ุฅูุฌูŽุงุจูŽุฉู ูˆูŽุงุนู’ู„ูŽู…ููˆุง ุฃูŽู†ู‘ูŽ ุงู„ู„ู‘ูŽู‡ูŽ ู„ุงูŽ ูŠูŽุณู’ุชูŽุฌููŠุจู ุฏูุนูŽุงุกู‹ ู…ูู†ู’ ู‚ูŽู„ู’ุจู ุบูŽุงููู„ู ู„ุงูŽู‡ู โ€"โ€ โ€œmuombeni Allah mkiwa na yakini juu ya kujibiwa na jueni kuwa Allah hakubali dua ya mtu ambaye moyo wake umeghafilika naye. (amepokea Tirmidh na Alhaakim).

7.Usiharakishe kujibiwa. Isitokee mtu akawa na haraka ya kutaka maombi yake yajibiwe kama anavyotaka yeye kwa haraka hata akawa analaumu. Amesemulia Abuuhurairah ุฑุถู‰ุงู„ู„ู‡ ุนู†ู‡ kuwa Mtume ุตู„ู‘ูŠ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆุณู„ู‘ู… amesema "โ€ ูŠูุณู’ุชูŽุฌูŽุงุจู ู„ุฃูŽุญูŽุฏููƒูู…ู’ ู…ูŽุง ู„ูŽู…ู’ ูŠูŽุนู’ุฌูŽู„ู’ ูŠูŽู‚ููˆู„ู ุฏูŽุนูŽูˆู’ุชู ููŽู„ูŽู…ู’ ูŠูุณู’ุชูŽุฌูŽุจู’ ู„ููŠ โ€" โ€œatajibiwa (dua yake ) mmoja wenu maadam hajaharakisha (kujibiwa) akawa anasema nimeomba na wala sijajibiwaโ€. (amepokea Bukhari na Muslim). Na katika masimulizi mengine ya Abuuhrairah kuwa mtume amesema โ€œhataacha mja kujibiwa dua yake maadam hajaomba madhamdhi au kukata uduguโ€. (amepokea Muslim na Abuu Daud). Hii ina maana dua itajibiwa tu ila isiwe ya kuomba madhambi au kukata udugu.

8.Kuitikia โ€œaamiinโ€. Mwenye kuomba dua basi aitikie โ€œaamiinโ€ eidha awe mwenyewe pekee au yupo na kundi la watu. Amesimulia Abuuhurairah ุฑุถู‰ุงู„ู„ู‡ ุนู†ู‡ kuwa Mtume ุตู„ู‘ูŠ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆุณู„ู‘ู… โ€œatakapoomba dua mmoja wenu basi na aitikie โ€˜aamiinโ€™ mwenyeweโ€™โ€. (amepokea Ibn โ€˜Adiy).


                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Download App yetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sunnah Main: Dini File: Download PDF Views 1152

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Kitau cha Fiqh    ๐Ÿ‘‰2 Dua za Mitume na Manabii    ๐Ÿ‘‰3 Simulizi za Hadithi Audio    ๐Ÿ‘‰4 Madrasa kiganjani    ๐Ÿ‘‰5 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰6 web hosting   

Post zinazofanana:

Nafasi ya Elimu na wenye elimu katika Uislamu

Nafasi ya elimu na mwenye elimu katika uislamu inaonkana katika maeneo yafuatayo: Kwanza, Elimu ndio takrima ya kwanza aliyokirimiwa mwanaadamu na Mola wake.

Soma Zaidi...
BAADHI YA DUA ZA KILA SIKU

BAADHI YA DUA ZA KILA SIKU.

Soma Zaidi...
NYAKATI AMBAZO DUA HUJIBIWA

NYAKATI AMBAZO DUA HUJUBIWA.

Soma Zaidi...
NAMNA AMBAZO DUA HUJIBIWA

NAMNA AMBAYO ALLAH HUJIBU DUA.

Soma Zaidi...
Haki za Muislamu kwa Muislamu mwenzie

Katika makala hii utakwenda kujifunza kuhusu haki za Muislamu kwa Muislamu mwenzie

Soma Zaidi...
DUA 94 - 114

DUA ZA KUONDOA WASIWASI, SIHIRI NA UCHAWI 94.

Soma Zaidi...
Utofauti wa dua ya kafiri na dua ya muislamu katika kujibiwa

Posti hii inakwenda kukufundisha ni kwa nini dua ya kafiri inawwza kujibiwa wakati ya muumini haijibiwi.

Soma Zaidi...