Dua za kuomba wakati unapokuwa na hasira ama ukiwa umekasirika


image


Post hii itakueleza ni dua gani unatakiwa uzisome wakati unapokiwa na hasira ama pale unapokasirika.



DUA ZA WAKATI UNAPOKUWA NA HASIRA.
Hashira ni katika matendo ambayo shetani anayapenda sana yatokee kwa mwadadamu. Kwa sababu ya hasira maovu mengine huenda yakatokea kama matusi, kupigana, vifo na mengineyo mengi. Uislamu kama dini iliyokamilika imetowa muongozo mzima juu ya namna ya kukabiliana na hali ya hasira pindi inapotokea. Katika makala hii tunakwenda kuona njia za kukabiliana na hali ya hasira pindi inapotokea.

Njia za kuzuia Hasira
1.Kumlani shetani kwa kusema ‘’a’udhubillahi minashaytwanir- rajiim”: Katika hadithi iliyosimuliwa na Sulayman Ibn Sard amesema: “nilikuwa nimekaa na Mtume (s.a.w), na kulikuwa na watu wawili wanagombana. Mmoja uso umekuwa mwekundu kwa hasira na mishipa ya shingo imemsimama. Mtume (s.a.s) akasema, ‘ninayajuwa maneno ambayo kama atayasema, hasira zote alizo nazo zitaondoka. Kama atasema “a’udhubillahi minash-shaytwaanir- rajiim” hasira zake zote zitaondoka. (amepokea BUkhari)

2.kubakia kimya
Kubakia kimya wakati wa kuwa na hasira ni jambo la busara, kwani ukiendelea kubakia kimya ndio hasira zitatulia. Amesema Mtume (s.a.s) “kama mmoja wenu atapatwa na hasira na abakie kimya (Amepokea Ahmad).

3.Kutokutembea:
Hasira zikitokea kama umesimama usiendelee kwenda au kusimama kwanza kaa chini. Amesema Mtume (s.a.s) “kama mmoja wenu amepatwa na hasira na akiwa amesimama basi na akae chini, hasira zake zitaondoka, na kama hazitaondoka basi na alale” (Amepokea Ahmad).

Kwa ufupi zipo njia nyingi ila hizi tatu ndio nitaishia kwenye makala hii. Tufahamu kuwa kumlani shetani ni njia ya kumkimbiza kwani yeye ndie anayesababisha hasira. Ni vyema ukachukuwa Udhu unapokuwa na hasira na kumlani shetani kwa wingi. Kubakia kimya wakati wa hasira, kukaa kama umesiamama ama kulala ni katika njia za kuondoa hasira

 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    2 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    3 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    4 Madrasa kiganjani offline    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Dua za kuomba wakati unapokuwa na maumivu kwenye mwili
Posti hii inakwenda kukufundisha dua za kuomba wakati wa kuwa na maumivu kwenye mwili wako. Soma Zaidi...

image Halo ambazo akiwa nazo mwenye kuomba dua dua yake hujibiwa
Post hii inakwenda kukifundisha nibhali zipi ukiwa nazo, basi dua yako kuhubaliwa kwa urahisi. Soma Zaidi...

image Utofauti wa dua ya kafiri na dua ya muislamu katika kujibiwa
Posti hii inakwenda kukufundisha ni kwa nini dua ya kafiri inawwza kujibiwa wakati ya muumini haijibiwi. Soma Zaidi...

image Dua 10 ambazo ni muhimu kuziomba kwa kila siku.
Posti hii inakwenda kukupa orodha ya dua 10 ambazo unaweza kuziomba kila siku. Soma Zaidi...

image Dua za kumuomba Allah wakati wa shida na tabu ama matatizo
Post hii inakwenda kukufundisha dua ambazo ni muhimu kuzisoma wakayi wa shida na taabu. Soma Zaidi...

image Adabu za kuomba dua kuifanya dua yako ikubaliwe kwa haraka
Post hii inakwenda kukugundisha adabu zinazotakikana kwa mwenye kuomba dua. Soma Zaidi...

image JINSI YA KUOMBA DUA ILI IKUBALIWE NA ALLAH
Kukubaliwa kwa dua kunategemea mahusiano yako na Allah. hata hivyo kuna baadhi ya mabo ukiyafanya dua yako inaweza kukubaliwa kwa haraka zaidi. Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi ya kuomba dua ikubaliwe. Soma Zaidi...

image Adhkari unazoweza kuomba kila siku
Hapa nitakuletea baadhi tu ya adhkari ambazo ni muhimu kwa muislamu Soma Zaidi...

image Masharti ya kukubaliwa kwa dua
Post hii itakwenda kukugundisha masharti yanayofungamana na kukubaliwa kwa dua. Soma Zaidi...

image Namna ambazo Allah hujibu dua ya mwenye kuomba.
Post hii inakwenda kukufundisha namna ama staili ambazo Allah hujibu dua za watu. Soma Zaidi...