Dua za kumuomba Allah wakati wa shida na tabu ama matatizo


image


Post hii inakwenda kukufundisha dua ambazo ni muhimu kuzisoma wakayi wa shida na taabu.



DUA ZA WAKATI WA SHIDA
1.Dua ya wakati wa taabu
“LAA ILAAHA ILLA-LLAHUL-’ADHIMUL-HALIIMU. LAA ILAAHA ILLA LLAHU RABBULS-SAMAAWATI WARABBUL-ARDHI WARABBUL-’ARSHIL-’KARIIM” (Bukhari)

2.Dua pindi uonaposhetani au unapotishwa na shetani
Ikitokea Mtu ameona shetani au ametishwa na shetani anatakiwa kuleta isti’adha na asema “A’UDHU BILLAHI MINKA” mara tatu kisha aseme “AL’ANUKA BILA’ANATIL-LLAHI TAAMMAH” mara tatu. Hakika shetani anakimbia ukisema maneno hayo. Hatika mapokezi ukimuona shetani akikutisha au hakukutisha soma adhana hakika shetani hukimbia adhana. Katika hadithi alopokea muslim mtume (s.a.w) amesema “hakika shetani hukimbia pindi adhana ya swala inaposomwa”

3.pindi muislamu anapokutana na jambo ambalo halitaki.
Pindi Muislamu anapoutana na jambo ambalo halitaki au jambo baya litakalomuhuzunisha anatakiwa aseme: “QADDARALLAHU WAMAA SHAA-A FA’ALA” na katu asiseme lau.… Yaani lau nisingelifanya hivi lisingenikuta au mifano kama haya. Kwani kusema hivi hufungua milango ya shetani (Muslim na Nisai)

4.pindi muislamu anapopatwa na shaka
Itakapotokea Mtu anashaka katika nafsi yake juu ya jambo anatakiwa aseme: “HUWAL-AWALU WAL-AKHIRU WADHAHIRU WAL BAATWINU WAHUWA BIKULLI SHAY-IN ‘ALIIM” (Abu Daud amepokea adithi hii na sanadi yake ni sahihi)

5.anapopata Muislamu msiba
Msiba ni katika mambo yanayohuzunisha moyo. Msiba sio pekeake kifo hata ukipotelewa na kitu pia ni msiba. Hivyo inapotokea hali kama hii ya kuhuzunisha moyo useme:”INNAA LILLAHI WA INNAA ILAYHIR-RAJI’UUN” Allah amesema kuwa “wape habari njema za furaha wenye subira, ambao wanapopata msiba husema ”INNAA LILLAHI WA INNAA ILAYHIR-RAJI’UUN”

6.Dua pindi unapokasirika.
Mtume (s.a.w) amekataza sana kuwa na tabia ya kukasirika na ni katika usia alokuwa akiwaba masahaba zake. Pindi mtu anapokasirika Mtume amesema anatakiwa aseme: “A’UDHU BILLAHI MINASH-SHAITWAANIR-RAJIIM” hadithi hii ni sahihi.(Bukhari na Muslim).

7.Dua unapokutana na adui
Pindi unapokutana na adui wako kama kwenye vita ama sehemu nyingine iwe usiku ama mchana unatakiwa useme: “ALLAAHUMMA MUNZILAL-KITAABI WA MUJRISAHAABI WAHAAZIMAL-AHZAABI IHZIMHUM WANSUUNAA ‘ALAYHIM” hii dua aliiomba mtume alipokutana na Maadui zake kwenye vita vya Ahzab (Bukhari na Muslim)

8.Dua pindi unapohofia kiongozi
Ikitokea mtu anajambo na anataka kukutana na kiongozi, au amewekwa chini ya ulinzi na kiongozi jabari, muovu ama kwa namna ingine na akawa anahofu kukabiliana na kiongozi huyo anatakiwa aseme: “LAA ILAAHA ILLAAHUWAL-HALIIMUL-KARIIM,,SUBHAANALLAHI RABBIA-SAMAAWATIS-SAB-’I WARABBIL-’ARSHIL-’ADHIIMI. LAA ILAAHA ILLAA ANTA, ‘AZZA JAARUKA WAJALLA THANAAUKA” amesimulia hadithi hii Ibn “Umar.


 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    2 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    3 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    4 Madrasa kiganjani offline    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Masharti ya kukubaliwa kwa dua
Post hii itakwenda kukugundisha masharti yanayofungamana na kukubaliwa kwa dua. Soma Zaidi...

image Dua za kuomba wakati unapokuwa na maumivu kwenye mwili
Posti hii inakwenda kukufundisha dua za kuomba wakati wa kuwa na maumivu kwenye mwili wako. Soma Zaidi...

image Adhkari unazoweza kuomba kila siku
Hapa nitakuletea baadhi tu ya adhkari ambazo ni muhimu kwa muislamu Soma Zaidi...

image Halo ambazo akiwa nazo mwenye kuomba dua dua yake hujibiwa
Post hii inakwenda kukifundisha nibhali zipi ukiwa nazo, basi dua yako kuhubaliwa kwa urahisi. Soma Zaidi...

image Dua za kuondoa wasiwasi, woga na kujikinga na uchawi, na mashetani
Post hii itakufundisha dua za kuomba wakati wa woga, wasiwasi na kujikinga na wachawi na mashetani Soma Zaidi...

image Matamshi ambayo ukimwambia Allah kwenye dua yako basi hujibiwa kwa haraka dua hiyo
Post hii inakwenda kukufundisha matamshi ambayo mtu akiyatamka Allah hujibu dua hiyo kwa urahisi. Soma Zaidi...

image Zijuwe nyakati ambazo ukiomba dua hujibiwa kwa urahisi
Post hii inakwenda kukugundisha ni nyakati zipi ambazo Allah hukubali dua kwa urahisi. Soma Zaidi...

image Namna ambazo Allah hujibu dua ya mwenye kuomba.
Post hii inakwenda kukufundisha namna ama staili ambazo Allah hujibu dua za watu. Soma Zaidi...

image JINSI YA KUOMBA DUA ILI IKUBALIWE NA ALLAH
Kukubaliwa kwa dua kunategemea mahusiano yako na Allah. hata hivyo kuna baadhi ya mabo ukiyafanya dua yako inaweza kukubaliwa kwa haraka zaidi. Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi ya kuomba dua ikubaliwe. Soma Zaidi...

image Ijuwe swala ya Mtume na fadhila zake na jinsi ya kumswalia Mtume.
Post hii itakufundisha jinsi ya kumswalia mtume, pamoja na kuzijuwa fadhila unazopata kwa kumswalia Mtume Soma Zaidi...