Menu



Dua za kumuomba Allah wakati wa shida na tabu ama matatizo

Post hii inakwenda kukufundisha dua ambazo ni muhimu kuzisoma wakayi wa shida na taabu.


DUA ZA WAKATI WA SHIDA
1.Dua ya wakati wa taabu
“LAA ILAAHA ILLA-LLAHUL-’ADHIMUL-HALIIMU. LAA ILAAHA ILLA LLAHU RABBULS-SAMAAWATI WARABBUL-ARDHI WARABBUL-’ARSHIL-’KARIIM” (Bukhari)

2.Dua pindi uonaposhetani au unapotishwa na shetani
Ikitokea Mtu ameona shetani au ametishwa na shetani anatakiwa kuleta isti’adha na asema “A’UDHU BILLAHI MINKA” mara tatu kisha aseme “AL’ANUKA BILA’ANATIL-LLAHI TAAMMAH” mara tatu. Hakika shetani anakimbia ukisema maneno hayo. Hatika mapokezi ukimuona shetani akikutisha au hakukutisha soma adhana hakika shetani hukimbia adhana. Katika hadithi alopokea muslim mtume (s.a.w) amesema “hakika shetani hukimbia pindi adhana ya swala inaposomwa”

3.pindi muislamu anapokutana na jambo ambalo halitaki.
Pindi Muislamu anapoutana na jambo ambalo halitaki au jambo baya litakalomuhuzunisha anatakiwa aseme: “QADDARALLAHU WAMAA SHAA-A FA’ALA” na katu asiseme lau.… Yaani lau nisingelifanya hivi lisingenikuta au mifano kama haya. Kwani kusema hivi hufungua milango ya shetani (Muslim na Nisai)

4.pindi muislamu anapopatwa na shaka
Itakapotokea Mtu anashaka katika nafsi yake juu ya jambo anatakiwa aseme: “HUWAL-AWALU WAL-AKHIRU WADHAHIRU WAL BAATWINU WAHUWA BIKULLI SHAY-IN ‘ALIIM” (Abu Daud amepokea adithi hii na sanadi yake ni sahihi)

5.anapopata Muislamu msiba
Msiba ni katika mambo yanayohuzunisha moyo. Msiba sio pekeake kifo hata ukipotelewa na kitu pia ni msiba. Hivyo inapotokea hali kama hii ya kuhuzunisha moyo useme:”INNAA LILLAHI WA INNAA ILAYHIR-RAJI’UUN” Allah amesema kuwa “wape habari njema za furaha wenye subira, ambao wanapopata msiba husema ”INNAA LILLAHI WA INNAA ILAYHIR-RAJI’UUN”

6.Dua pindi unapokasirika.
Mtume (s.a.w) amekataza sana kuwa na tabia ya kukasirika na ni katika usia alokuwa akiwaba masahaba zake. Pindi mtu anapokasirika Mtume amesema anatakiwa aseme: “A’UDHU BILLAHI MINASH-SHAITWAANIR-RAJIIM” hadithi hii ni sahihi.(Bukhari na Muslim).

7.Dua unapokutana na adui
Pindi unapokutana na adui wako kama kwenye vita ama sehemu nyingine iwe usiku ama mchana unatakiwa useme: “ALLAAHUMMA MUNZILAL-KITAABI WA MUJRISAHAABI WAHAAZIMAL-AHZAABI IHZIMHUM WANSUUNAA ‘ALAYHIM” hii dua aliiomba mtume alipokutana na Maadui zake kwenye vita vya Ahzab (Bukhari na Muslim)

8.Dua pindi unapohofia kiongozi
Ikitokea mtu anajambo na anataka kukutana na kiongozi, au amewekwa chini ya ulinzi na kiongozi jabari, muovu ama kwa namna ingine na akawa anahofu kukabiliana na kiongozi huyo anatakiwa aseme: “LAA ILAAHA ILLAAHUWAL-HALIIMUL-KARIIM,,SUBHAANALLAHI RABBIA-SAMAAWATIS-SAB-’I WARABBIL-’ARSHIL-’ADHIIMI. LAA ILAAHA ILLAA ANTA, ‘AZZA JAARUKA WAJALLA THANAAUKA” amesimulia hadithi hii Ibn “Umar.


 

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sunnah Main: Dini File: Download PDF Views 5450

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Uandishi wa Hadithi wakati wa Matabiina

Historia ya uandishi wa hadithibwakati wa Matabiina, yaani wafuasi wa maswahaba

Soma Zaidi...
SHUGHULI ZA KILA SIKU

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
DUA ZA WAKATI WA SHIDA

DUA ZA WAKATI WA SHIDA 1.

Soma Zaidi...
DUA na Adhkar kutoka kwenye quran

hii ni orodha ya dua mbalimbali kutoka kwenye quran. Unaweza kuzitumia dua hizi kujipendekeza kwa Allah na kupata msamaha, neema na mengineyo.

Soma Zaidi...
dua ya kuomba jambo ufanikiwe

hii ni damna ya kuomba dua ukubaliwe, dua ya kuomba jambo ufanikiwe

Soma Zaidi...
NAFASI YA SUNNAH KATIKA UISLAMU

Nafasi ya Sunnah katika UislamuMtume Muhammad (s.

Soma Zaidi...