Post hii inakwenda kukufundisha dua ambazo ni muhimu kuzisoma wakayi wa shida na taabu.
DUA ZA WAKATI WA SHIDA
1.Dua ya wakati wa taabu
“LAA ILAAHA ILLA-LLAHUL-’ADHIMUL-HALIIMU. LAA ILAAHA ILLA LLAHU RABBULS-SAMAAWATI WARABBUL-ARDHI WARABBUL-’ARSHIL-’KARIIM” (Bukhari)
2.Dua pindi uonaposhetani au unapotishwa na shetani
Ikitokea Mtu ameona shetani au ametishwa na shetani anatakiwa kuleta isti’adha na asema “A’UDHU BILLAHI MINKA” mara tatu kisha aseme “AL’ANUKA BILA’ANATIL-LLAHI TAAMMAH” mara tatu. Hakika shetani anakimbia ukisema maneno hayo. Hatika mapokezi ukimuona shetani akikutisha au hakukutisha soma adhana hakika shetani hukimbia adhana. Katika hadithi alopokea muslim mtume (s.a.w) amesema “hakika shetani hukimbia pindi adhana ya swala inaposomwa”
3.pindi muislamu anapokutana na jambo ambalo halitaki.
Pindi Muislamu anapoutana na jambo ambalo halitaki au jambo baya litakalomuhuzunisha anatakiwa aseme: “QADDARALLAHU WAMAA SHAA-A FA’ALA” na katu asiseme lau.… Yaani lau nisingelifanya hivi lisingenikuta au mifano kama haya. Kwani kusema hivi hufungua milango ya shetani (Muslim na Nisai)
4.pindi muislamu anapopatwa na shaka
Itakapotokea Mtu anashaka katika nafsi yake juu ya jambo anatakiwa aseme: “HUWAL-AWALU WAL-AKHIRU WADHAHIRU WAL BAATWINU WAHUWA BIKULLI SHAY-IN ‘ALIIM” (Abu Daud amepokea adithi hii na sanadi yake ni sahihi)
5.anapopata Muislamu msiba
Msiba ni katika mambo yanayohuzunisha moyo. Msiba sio pekeake kifo hata ukipotelewa na kitu pia ni msiba. Hivyo inapotokea hali kama hii ya kuhuzunisha moyo useme:”INNAA LILLAHI WA INNAA ILAYHIR-RAJI’UUN” Allah amesema kuwa “wape habari njema za furaha wenye subira, ambao wanapopata msiba husema ”INNAA LILLAHI WA INNAA ILAYHIR-RAJI’UUN”
6.Dua pindi unapokasirika.
Mtume (s.a.w) amekataza sana kuwa na tabia ya kukasirika na ni katika usia alokuwa akiwaba masahaba zake. Pindi mtu anapokasirika Mtume amesema anatakiwa aseme: “A’UDHU BILLAHI MINASH-SHAITWAANIR-RAJIIM” hadithi hii ni sahihi.(Bukhari na Muslim).
7.Dua unapokutana na adui
Pindi unapokutana na adui wako kama kwenye vita ama sehemu nyingine iwe usiku ama mchana unatakiwa useme: “ALLAAHUMMA MUNZILAL-KITAABI WA MUJRISAHAABI WAHAAZIMAL-AHZAABI IHZIMHUM WANSUUNAA ‘ALAYHIM” hii dua aliiomba mtume alipokutana na Maadui zake kwenye vita vya Ahzab (Bukhari na Muslim)
8.Dua pindi unapohofia kiongozi
Ikitokea mtu anajambo na anataka kukutana na kiongozi, au amewekwa chini ya ulinzi na kiongozi jabari, muovu ama kwa namna ingine na akawa anahofu kukabiliana na kiongozi huyo anatakiwa aseme: “LAA ILAAHA ILLAAHUWAL-HALIIMUL-KARIIM,,SUBHAANALLAHI RABBIA-SAMAAWATIS-SAB-’I WARABBIL-’ARSHIL-’ADHIIMI. LAA ILAAHA ILLAA ANTA, ‘AZZA JAARUKA WAJALLA THANAAUKA” amesimulia hadithi hii Ibn “Umar.
Umeionaje Makala hii.. ?
Post hii itakwenda kukugundisha masharti yanayofungamana na kukubaliwa kwa dua.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukupa tahadhari juu ya mambo ya halali na mambo ya haramu.
Soma Zaidi...MAkala hii itakwenda kukufundisha jinsi ya kutoa salamu kwenye uislamu
Soma Zaidi...Zijuwe nyakati ambazo dua inakubaliwa kwa haraka zaidi. Zijuwe nyakati ambazo ukiomba dua hitakubaliwa.
Soma Zaidi...