51.
51.34.Dua ya kupanda mnyama/chombo cha usafiri “Bismillah wal-hamdulillahi, sub-haanalladhiy sakhkharalanaa haadhaa wamaa kunnaalahu muq-riniyna wainna ilaa rabbinaa la mun-qalibuuna.“Kwa jina la Allah na sifa zote ni za Allah. Utukufu ni wa yule aliyetutiishia kipando hiki, tusingeweza kukitumia kwa uwezo wetu wenyewe, na kwa Mola wetu ndio marejeo.
52.Dua ya Safari “Allahu akbaru, Allah akbaru, Allahu akbaru, sub-haana lladhiy sakh-kharalanaa hadhaa wamakunnaa lahu muqriniyna, wainnaailaa rabbinna lamunqalibuuna. Allahumma innaa nas-aluka fiy safarinaa hadhal-birri wa-ttaqwa, waminal-a'mali maatar-dhwaa, Allahumma hawwin a'laynaa safaranaa hadha wat-wi a'nnaa budahu, Allahuumma antasw-swaahibu fiy ssafari, wal-khaliyfatu fiyl-ahli. “Allah ni mkubwa, Allah ni mkubwa, Allah ni mkubwa, ametakasika ambaye ametudhalilishia sisi hiki (chombo au mnyama), na hatukuwa sisi kwako ni wenye uwezo, na sisi kwa Mola wetu tutarejeshwa. Ee Allah, hakika sisi tunakuomba katika safari yetu hii wema na ucha Mungu, na katika matendo unayoridhia, Ee, Allah ifanye nyepesi safari yetu hii na ufupishe umbali wake. Ee Allah, wewe ndie mwenzangu katika safari na mchungaji wa familia yangu.
53.Dua ya kupokea habari ya kufurahisha “Al-hamdulillahilladhiy bina-a'matihi tatimmu sw-swaalihaatu." “Shukurani zote anastahiki Allah ambaye kwa neema yake hizi nzuri imekamilika."
54.Dua ya kupokea habari za kuhuzunisha “Al-hamdulillahi a'laa kulli haali" “Shukurani zote anastahiki Allah kwa hali zote."
55.Dua ya kuingia sokoni “Laa illaaha illa llaahu wah-dahu laashariikalahu, lahul-mulku walahul-hamdu, yuh-yi' wayumiitu wahuwa hayyun laa yamuutu wahuwa a'laa kullishay-in qadiiru." “Hakuna Mola ila Allah aliye mpweke, hana mshirika, ni wake ufalme,na ni zake sifa njema, anahuisha na anafisha, naye ni hai asiyekufa, kheri iko mikononi mwake, na yeye juu ya kila kitu ni muweza."
56.Ubora wa kusalimiana Mtume (s.a.w) amesema “Hamtoingia peponi mpaka muamini na hamtaweza kuamini mpaka mpendane. Je, nikufahamisheni jambo ambalo mkilifanya mtapendana? Jambo hili ni kutoleana salaamu." (Muslim) Ukamilifu wa salaamu ya Kiislamu ni “Assalaamu a'laykumu Warahmatullahi wabarakaatuhu." “Amani ya Allah, Rehema zake na Baraka zake ziwe juu yenu." Anayesalimiwa analazimika kujibu kwa kusema: “Waa'laykumu ssalaamu warahmatullahi wabarakaatuhu." “Nanyi pia amani ya Allah, Rehema zake na Baraka zake ziwe juu yenu."
57.Ubora wa kumkumbuka na Kumtukuza Allah wakati wa mapumziko A'bdullaah Ibn Qays (r.a) ameeleza kuwa Mtume (s.a.w) alimuuliza: "Ee 'Abdullah Ibn Qays, ni kufahamishe hazina miongoni mwa hazina za Peponi? Kisha Mtume (s.a.w) akamwambia sema: “Laa haula walaaquwwata illaabillahi." "Hapana uwezo wala nguvu ila kutoka kwa Allah." (Bukhari na Muslimu)
58.Mtume (s.a.w) amesema, maneno anayopenda Allah kuliko yote ni manne “Sub-hanallahi, Wal-hamdulillahi, Walaa ilaaha illallaahu, Wallaahu Akbaru." “Utukufu ni wa Allah, shukurani zote anastahiki Allah, Hapana Mola ila yeye, Allah ni Mkubwa." (Muslimu)
59.Abu Hurayrah (r.a) ameeleza kuwa: Mtume (s.a.w) amesema, "Kuna maneno mawili (2) ambayo ni mepesi katika ulimi na mazito katika mizani na anayopenda Allah, nayo ni: “Sub-haanallahi wabihamdihi, wasubuhaana llaahila'dhiim." “Utukufu ni wa Allah na shukrani zote anastahiki yeye. Utukufu ni wa Allah aliye mkuu." (Bukhari na Muslimu)
60.Jabir Ibn Abdullah (r.a) amesimulia kuwa Mtume (s.a.w) amesema: Hakika dua kubwa ni kusema: “Al-hamdulillaahi" “Shukurani zote anastahiki Allah." Na hakika namna bora ya kumkumbuka Allah (dhikri) ni kusema: “Laailahailla llaaha." “Hapana Mola ila Allah." (Ahmad)
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Post hii itakwenda kukufundisha sura katika Quran ambazo ni kinga dhidi ya Wachawi, uchawi na Masheitwani.
Soma Zaidi...عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: "كُنْت خَلْفَ رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم يَوْمًا، فَقَالَ: ي...
Soma Zaidi...