DUA 51 - 60

51.

DUA 51 - 60


51.34.Dua ya kupanda mnyama/chombo cha usafiri โ€œBismillah wal-hamdulillahi, sub-haanalladhiy sakhkharalanaa haadhaa wamaa kunnaalahu muq-riniyna wainna ilaa rabbinaa la mun-qalibuuna.โ€œKwa jina la Allah na sifa zote ni za Allah. Utukufu ni wa yule aliyetutiishia kipando hiki, tusingeweza kukitumia kwa uwezo wetu wenyewe, na kwa Mola wetu ndio marejeo.

52.Dua ya Safari โ€œAllahu akbaru, Allah akbaru, Allahu akbaru, sub-haana lladhiy sakh-kharalanaa hadhaa wamakunnaa lahu muqriniyna, wainnaailaa rabbinna lamunqalibuuna. Allahumma innaa nas-aluka fiy safarinaa hadhal-birri wa-ttaqwa, waminal-a'mali maatar-dhwaa, Allahumma hawwin a'laynaa safaranaa hadha wat-wi a'nnaa budahu, Allahuumma antasw-swaahibu fiy ssafari, wal-khaliyfatu fiyl-ahli. โ€œAllah ni mkubwa, Allah ni mkubwa, Allah ni mkubwa, ametakasika ambaye ametudhalilishia sisi hiki (chombo au mnyama), na hatukuwa sisi kwako ni wenye uwezo, na sisi kwa Mola wetu tutarejeshwa. Ee Allah, hakika sisi tunakuomba katika safari yetu hii wema na ucha Mungu, na katika matendo unayoridhia, Ee, Allah ifanye nyepesi safari yetu hii na ufupishe umbali wake. Ee Allah, wewe ndie mwenzangu katika safari na mchungaji wa familia yangu.

53.Dua ya kupokea habari ya kufurahisha โ€œAl-hamdulillahilladhiy bina-a'matihi tatimmu sw-swaalihaatu." โ€œShukurani zote anastahiki Allah ambaye kwa neema yake hizi nzuri imekamilika."

54.Dua ya kupokea habari za kuhuzunisha โ€œAl-hamdulillahi a'laa kulli haali" โ€œShukurani zote anastahiki Allah kwa hali zote."

55.Dua ya kuingia sokoni โ€œLaa illaaha illa llaahu wah-dahu laashariikalahu, lahul-mulku walahul-hamdu, yuh-yi' wayumiitu wahuwa hayyun laa yamuutu wahuwa a'laa kullishay-in qadiiru." โ€œHakuna Mola ila Allah aliye mpweke, hana mshirika, ni wake ufalme,na ni zake sifa njema, anahuisha na anafisha, naye ni hai asiyekufa, kheri iko mikononi mwake, na yeye juu ya kila kitu ni muweza."

56.Ubora wa kusalimiana Mtume (s.a.w) amesema โ€œHamtoingia peponi mpaka muamini na hamtaweza kuamini mpaka mpendane. Je, nikufahamisheni jambo ambalo mkilifanya mtapendana? Jambo hili ni kutoleana salaamu." (Muslim) Ukamilifu wa salaamu ya Kiislamu ni โ€œAssalaamu a'laykumu Warahmatullahi wabarakaatuhu." โ€œAmani ya Allah, Rehema zake na Baraka zake ziwe juu yenu." Anayesalimiwa analazimika kujibu kwa kusema: โ€œWaa'laykumu ssalaamu warahmatullahi wabarakaatuhu." โ€œNanyi pia amani ya Allah, Rehema zake na Baraka zake ziwe juu yenu."

57.Ubora wa kumkumbuka na Kumtukuza Allah wakati wa mapumziko A'bdullaah Ibn Qays (r.a) ameeleza kuwa Mtume (s.a.w) alimuuliza: "Ee 'Abdullah Ibn Qays, ni kufahamishe hazina miongoni mwa hazina za Peponi? Kisha Mtume (s.a.w) akamwambia sema: โ€œLaa haula walaaquwwata illaabillahi." "Hapana uwezo wala nguvu ila kutoka kwa Allah." (Bukhari na Muslimu)

58.Mtume (s.a.w) amesema, maneno anayopenda Allah kuliko yote ni manne โ€œSub-hanallahi, Wal-hamdulillahi, Walaa ilaaha illallaahu, Wallaahu Akbaru." โ€œUtukufu ni wa Allah, shukurani zote anastahiki Allah, Hapana Mola ila yeye, Allah ni Mkubwa." (Muslimu)

59.Abu Hurayrah (r.a) ameeleza kuwa: Mtume (s.a.w) amesema, "Kuna maneno mawili (2) ambayo ni mepesi katika ulimi na mazito katika mizani na anayopenda Allah, nayo ni: โ€œSub-haanallahi wabihamdihi, wasubuhaana llaahila'dhiim." โ€œUtukufu ni wa Allah na shukrani zote anastahiki yeye. Utukufu ni wa Allah aliye mkuu." (Bukhari na Muslimu)

60.Jabir Ibn Abdullah (r.a) amesimulia kuwa Mtume (s.a.w) amesema: Hakika dua kubwa ni kusema: โ€œAl-hamdulillaahi" โ€œShukurani zote anastahiki Allah." Na hakika namna bora ya kumkumbuka Allah (dhikri) ni kusema: โ€œLaailahailla llaaha." โ€œHapana Mola ila Allah." (Ahmad)


                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Download App yetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sunnah Main: Dini File: Download PDF Views 636

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Madrasa kiganjani    ๐Ÿ‘‰2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    ๐Ÿ‘‰3 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰4 Simulizi za Hadithi Audio    ๐Ÿ‘‰5 Kitabu cha Afya    ๐Ÿ‘‰6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Uandishi wa hadithi wakati wa Matabii tabiina (tabiitabiina)

Hii ni historia ya uandishi wa hadithi wakati wa tabii tabiina. Yaani wafuasi wa wale wafuasi wa Masahaba

Soma Zaidi...
Hadithi inayokataza bidaa (bid's) uzushi katika dini

ุนูŽู†ู’ ุฃูู…ูู‘ ุงู„ู’ู…ูุคู’ู…ูู†ููŠู†ูŽ ุฃูู…ูู‘ ุนูŽุจู’ุฏู ุงู„ู„ูŽู‘ู‡ู ุนูŽุงุฆูุดูŽุฉูŽ ุฑูŽุถููŠูŽ ุงู„ู„ูŽู‘ู‡ู ุนูŽู†ู’ู‡ูŽุงุŒ ู‚ูŽุงู„ูŽุชู’: ู‚ูŽุงู„ูŽ: ุฑูŽุณููˆู„ู ุงู„ู„ูŽู‘ู‡ู ุตู„ู‰ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆ ุณู„ู… "...

Soma Zaidi...
ni nyakati zipi ambazo dua hukubaliwa kwa haraka?

Dua ni moja ya ibada ambazo zinamfanya mja awe karibu na Mweznyezi Mungu. Allah amesisitiza tumuombe dua kwa shida zetu zote, pia akaahidi kuwa atatujibu maombi yetu muda wowote tutakao muomba. Sasa ni zipi nyakati nzuri zaidi kuomb adua?

Soma Zaidi...
AINA ZA HADITHI

Aina za HadithKuna aina kuu mbili za Hadith- (a) Hadith Nabawiyyi.

Soma Zaidi...
UKITAKA KUOMBA BASI MUOMBE ALLAH, UKIMKUMBUKA WAKATI WA RAHA ATAKUKUMBUKA WAKATI WA DHIKI, SHIDA NA TAABU

ุนูŽู†ู’ ุนูŽุจู’ุฏู ุงู„ู„ูŽู‘ู‡ู ุจู’ู†ู ุนูŽุจูŽู‘ุงุณู ุฑูŽุถููŠูŽ ุงู„ู„ูŽู‘ู‡ู ุนูŽู†ู’ู‡ูู…ูŽุง ู‚ูŽุงู„ูŽ: "ูƒูู†ู’ุช ุฎูŽู„ู’ููŽ ุฑูŽุณููˆู„ู ุงู„ู„ูŽู‘ู‡ู ุตู„ู‰ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆ ุณู„ู… ูŠูŽูˆู’ู…ู‹ุงุŒ ููŽู‚ูŽุงู„ูŽ: ูŠ...

Soma Zaidi...
NAFASI YA SUNNAH KATIKA UISLAMU

Nafasi ya Sunnah katika UislamuMtume Muhammad (s.

Soma Zaidi...