DUA 51 - 60

DUA 51 - 60

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

51.

DUA 51 - 60


51.34.Dua ya kupanda mnyama/chombo cha usafiri “Bismillah wal-hamdulillahi, sub-haanalladhiy sakhkharalanaa haadhaa wamaa kunnaalahu muq-riniyna wainna ilaa rabbinaa la mun-qalibuuna.“Kwa jina la Allah na sifa zote ni za Allah. Utukufu ni wa yule aliyetutiishia kipando hiki, tusingeweza kukitumia kwa uwezo wetu wenyewe, na kwa Mola wetu ndio marejeo.

52.Dua ya Safari “Allahu akbaru, Allah akbaru, Allahu akbaru, sub-haana lladhiy sakh-kharalanaa hadhaa wamakunnaa lahu muqriniyna, wainnaailaa rabbinna lamunqalibuuna. Allahumma innaa nas-aluka fiy safarinaa hadhal-birri wa-ttaqwa, waminal-a'mali maatar-dhwaa, Allahumma hawwin a'laynaa safaranaa hadha wat-wi a'nnaa budahu, Allahuumma antasw-swaahibu fiy ssafari, wal-khaliyfatu fiyl-ahli. “Allah ni mkubwa, Allah ni mkubwa, Allah ni mkubwa, ametakasika ambaye ametudhalilishia sisi hiki (chombo au mnyama), na hatukuwa sisi kwako ni wenye uwezo, na sisi kwa Mola wetu tutarejeshwa. Ee Allah, hakika sisi tunakuomba katika safari yetu hii wema na ucha Mungu, na katika matendo unayoridhia, Ee, Allah ifanye nyepesi safari yetu hii na ufupishe umbali wake. Ee Allah, wewe ndie mwenzangu katika safari na mchungaji wa familia yangu.

53.Dua ya kupokea habari ya kufurahisha “Al-hamdulillahilladhiy bina-a'matihi tatimmu sw-swaalihaatu." “Shukurani zote anastahiki Allah ambaye kwa neema yake hizi nzuri imekamilika."

54.Dua ya kupokea habari za kuhuzunisha “Al-hamdulillahi a'laa kulli haali" “Shukurani zote anastahiki Allah kwa hali zote."

55.Dua ya kuingia sokoni “Laa illaaha illa llaahu wah-dahu laashariikalahu, lahul-mulku walahul-hamdu, yuh-yi' wayumiitu wahuwa hayyun laa yamuutu wahuwa a'laa kullishay-in qadiiru." “Hakuna Mola ila Allah aliye mpweke, hana mshirika, ni wake ufalme,na ni zake sifa njema, anahuisha na anafisha, naye ni hai asiyekufa, kheri iko mikononi mwake, na yeye juu ya kila kitu ni muweza."

56.Ubora wa kusalimiana Mtume (s.a.w) amesema “Hamtoingia peponi mpaka muamini na hamtaweza kuamini mpaka mpendane. Je, nikufahamisheni jambo ambalo mkilifanya mtapendana? Jambo hili ni kutoleana salaamu." (Muslim) Ukamilifu wa salaamu ya Kiislamu ni “Assalaamu a'laykumu Warahmatullahi wabarakaatuhu." “Amani ya Allah, Rehema zake na Baraka zake ziwe juu yenu." Anayesalimiwa analazimika kujibu kwa kusema: “Waa'laykumu ssalaamu warahmatullahi wabarakaatuhu." “Nanyi pia amani ya Allah, Rehema zake na Baraka zake ziwe juu yenu."

57.Ubora wa kumkumbuka na Kumtukuza Allah wakati wa mapumziko A'bdullaah Ibn Qays (r.a) ameeleza kuwa Mtume (s.a.w) alimuuliza: "Ee 'Abdullah Ibn Qays, ni kufahamishe hazina miongoni mwa hazina za Peponi? Kisha Mtume (s.a.w) akamwambia sema: “Laa haula walaaquwwata illaabillahi." "Hapana uwezo wala nguvu ila kutoka kwa Allah." (Bukhari na Muslimu)

58.Mtume (s.a.w) amesema, maneno anayopenda Allah kuliko yote ni manne “Sub-hanallahi, Wal-hamdulillahi, Walaa ilaaha illallaahu, Wallaahu Akbaru." “Utukufu ni wa Allah, shukurani zote anastahiki Allah, Hapana Mola ila yeye, Allah ni Mkubwa." (Muslimu)

59.Abu Hurayrah (r.a) ameeleza kuwa: Mtume (s.a.w) amesema, "Kuna maneno mawili (2) ambayo ni mepesi katika ulimi na mazito katika mizani na anayopenda Allah, nayo ni: “Sub-haanallahi wabihamdihi, wasubuhaana llaahila'dhiim." “Utukufu ni wa Allah na shukrani zote anastahiki yeye. Utukufu ni wa Allah aliye mkuu." (Bukhari na Muslimu)

60.Jabir Ibn Abdullah (r.a) amesimulia kuwa Mtume (s.a.w) amesema: Hakika dua kubwa ni kusema: “Al-hamdulillaahi" “Shukurani zote anastahiki Allah." Na hakika namna bora ya kumkumbuka Allah (dhikri) ni kusema: “Laailahailla llaaha." “Hapana Mola ila Allah." (Ahmad)


                   

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sunnah Main: Dini File: Download PDF Views 613

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

BAADHI YA DUA ZA KILA SIKU
BAADHI YA DUA ZA KILA SIKU

BAADHI YA DUA ZA KILA SIKU.

Soma Zaidi...
Maswali juu ya Sunnah na hadithi
Maswali juu ya Sunnah na hadithi

Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
MAANA NA FADHILA ZA KUOMBA DUA
MAANA NA FADHILA ZA KUOMBA DUA

DUA Kwa ufupi dua ni kumuomba Allah akuondoshee lililobaya, ama linalo kuudhi ama akupe jambo fulani.

Soma Zaidi...
kuwa mwenye hikma au hekima na faida zake
kuwa mwenye hikma au hekima na faida zake

Elimu, pamoja na ubora wake, hainufaishi bila ya kutumiwa kwa hekima.

Soma Zaidi...
Adabu ya kukaa na kula katika nyumba za watu
Adabu ya kukaa na kula katika nyumba za watu

"Si vibaya kwa kipofu, wala si vibaya kwa kiguru, wala si vibaya kwa mgonjwa, wala kwenu, kama mkila katika nyumba zenu, au nyumba za baba zenu, au nyumba za mama zenu, au nyumba za ndugu zenu, au nyumba za dada zenu, au nyumba za ami zenu, au nyumba za s

Soma Zaidi...
Dua za wakati wa shida na taabu
Dua za wakati wa shida na taabu

Hizi ni Dua ambazo unatakiwa uziombe wakati wa shida na taabu

Soma Zaidi...
MASHARTI YA KUKUBALIWA KWA DUA
MASHARTI YA KUKUBALIWA KWA DUA

MASHART YA KUKUBALIWA KWA DUA.

Soma Zaidi...
dua ya kuomba jambo ufanikiwe
dua ya kuomba jambo ufanikiwe

hii ni damna ya kuomba dua ukubaliwe, dua ya kuomba jambo ufanikiwe

Soma Zaidi...