DUA 51 - 60

DUA 51 - 60

51.

DUA 51 - 60


51.34.Dua ya kupanda mnyama/chombo cha usafiri “Bismillah wal-hamdulillahi, sub-haanalladhiy sakhkharalanaa haadhaa wamaa kunnaalahu muq-riniyna wainna ilaa rabbinaa la mun-qalibuuna.“Kwa jina la Allah na sifa zote ni za Allah. Utukufu ni wa yule aliyetutiishia kipando hiki, tusingeweza kukitumia kwa uwezo wetu wenyewe, na kwa Mola wetu ndio marejeo.

52.Dua ya Safari “Allahu akbaru, Allah akbaru, Allahu akbaru, sub-haana lladhiy sakh-kharalanaa hadhaa wamakunnaa lahu muqriniyna, wainnaailaa rabbinna lamunqalibuuna. Allahumma innaa nas-aluka fiy safarinaa hadhal-birri wa-ttaqwa, waminal-a'mali maatar-dhwaa, Allahumma hawwin a'laynaa safaranaa hadha wat-wi a'nnaa budahu, Allahuumma antasw-swaahibu fiy ssafari, wal-khaliyfatu fiyl-ahli. “Allah ni mkubwa, Allah ni mkubwa, Allah ni mkubwa, ametakasika ambaye ametudhalilishia sisi hiki (chombo au mnyama), na hatukuwa sisi kwako ni wenye uwezo, na sisi kwa Mola wetu tutarejeshwa. Ee Allah, hakika sisi tunakuomba katika safari yetu hii wema na ucha Mungu, na katika matendo unayoridhia, Ee, Allah ifanye nyepesi safari yetu hii na ufupishe umbali wake. Ee Allah, wewe ndie mwenzangu katika safari na mchungaji wa familia yangu.

53.Dua ya kupokea habari ya kufurahisha “Al-hamdulillahilladhiy bina-a'matihi tatimmu sw-swaalihaatu." “Shukurani zote anastahiki Allah ambaye kwa neema yake hizi nzuri imekamilika."

54.Dua ya kupokea habari za kuhuzunisha “Al-hamdulillahi a'laa kulli haali" “Shukurani zote anastahiki Allah kwa hali zote."

55.Dua ya kuingia sokoni “Laa illaaha illa llaahu wah-dahu laashariikalahu, lahul-mulku walahul-hamdu, yuh-yi' wayumiitu wahuwa hayyun laa yamuutu wahuwa a'laa kullishay-in qadiiru." “Hakuna Mola ila Allah aliye mpweke, hana mshirika, ni wake ufalme,na ni zake sifa njema, anahuisha na anafisha, naye ni hai asiyekufa, kheri iko mikononi mwake, na yeye juu ya kila kitu ni muweza."

56.Ubora wa kusalimiana Mtume (s.a.w) amesema “Hamtoingia peponi mpaka muamini na hamtaweza kuamini mpaka mpendane. Je, nikufahamisheni jambo ambalo mkilifanya mtapendana? Jambo hili ni kutoleana salaamu." (Muslim) Ukamilifu wa salaamu ya Kiislamu ni “Assalaamu a'laykumu Warahmatullahi wabarakaatuhu." “Amani ya Allah, Rehema zake na Baraka zake ziwe juu yenu." Anayesalimiwa analazimika kujibu kwa kusema: “Waa'laykumu ssalaamu warahmatullahi wabarakaatuhu." “Nanyi pia amani ya Allah, Rehema zake na Baraka zake ziwe juu yenu."

57.Ubora wa kumkumbuka na Kumtukuza Allah wakati wa mapumziko A'bdullaah Ibn Qays (r.a) ameeleza kuwa Mtume (s.a.w) alimuuliza: "Ee 'Abdullah Ibn Qays, ni kufahamishe hazina miongoni mwa hazina za Peponi? Kisha Mtume (s.a.w) akamwambia sema: “Laa haula walaaquwwata illaabillahi." "Hapana uwezo wala nguvu ila kutoka kwa Allah." (Bukhari na Muslimu)

58.Mtume (s.a.w) amesema, maneno anayopenda Allah kuliko yote ni manne “Sub-hanallahi, Wal-hamdulillahi, Walaa ilaaha illallaahu, Wallaahu Akbaru." “Utukufu ni wa Allah, shukurani zote anastahiki Allah, Hapana Mola ila yeye, Allah ni Mkubwa." (Muslimu)

59.Abu Hurayrah (r.a) ameeleza kuwa: Mtume (s.a.w) amesema, "Kuna maneno mawili (2) ambayo ni mepesi katika ulimi na mazito katika mizani na anayopenda Allah, nayo ni: “Sub-haanallahi wabihamdihi, wasubuhaana llaahila'dhiim." “Utukufu ni wa Allah na shukrani zote anastahiki yeye. Utukufu ni wa Allah aliye mkuu." (Bukhari na Muslimu)

60.Jabir Ibn Abdullah (r.a) amesimulia kuwa Mtume (s.a.w) amesema: Hakika dua kubwa ni kusema: “Al-hamdulillaahi" “Shukurani zote anastahiki Allah." Na hakika namna bora ya kumkumbuka Allah (dhikri) ni kusema: “Laailahailla llaaha." “Hapana Mola ila Allah." (Ahmad)


                   



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 160


Download our Apps
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Wajbu wa wazazi kwa watoto wao
Wajibu wa Wazazi kwa Watoto Wazazi wanawajibu kwa watoto wao. Soma Zaidi...

MAANA YA HADITHI SUNNAH
Maana ya SunnahKilugha: Neno sunnah katika lugha ya Kiarabu lina maana ya mwenendo au mila. Soma Zaidi...

Al-Arbauwn An-Nawawiyyah hadithi ya 2: Ujio wa Jibril kwa Mtume (s.a.w)
Hii ni hadithi ya pili katika kitabu cha Arbain Nawawiy Soma Zaidi...

MAANA YA HADITHI SUNNAH
Maana ya SunnahKilugha: Neno sunnah katika lugha ya Kiarabu lina maana ya mwenendo au mila. Soma Zaidi...

Hadithi Ya 31: Upe Ulimwengu Kisogo Allaah Atakupenda
Soma Zaidi...

JINSI YA KUOMBA DUA ILI IKUBALIWE NA ALLAH
Kukubaliwa kwa dua kunategemea mahusiano yako na Allah. hata hivyo kuna baadhi ya mabo ukiyafanya dua yako inaweza kukubaliwa kwa haraka zaidi. Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi ya kuomba dua ikubaliwe. Soma Zaidi...

DUA YA 1 - 10
1. Soma Zaidi...

KATU USITAMANI MAUTI (KIFO) YAANI KUFA, HATA UKIWA NA MARADHI AMA UKIWA MCHAMUNGU UKIWA NI MUOVU MTENDA MADHAMBI MAKUBWA NA MADOGO
Soma Zaidi...

DUA 11 - 20
11. Soma Zaidi...

DUA ZA SWALA
DUA ZA SWALA 1. Soma Zaidi...

Hali ambazo akiwa nazo mwenye kuomba dua dua yake hujibiwa
Post hii inakwenda kukifundisha nibhali zipi ukiwa nazo, basi dua yako kuhubaliwa kwa urahisi. Soma Zaidi...

Jinsi ya kutoa salamu katika uislamu
MAkala hii itakwenda kukufundisha jinsi ya kutoa salamu kwenye uislamu Soma Zaidi...