DUA Kwa ufupi dua ni kumuomba Allah akuondoshee lililobaya, ama linalo kuudhi ama akupe jambo fulani.
DUA
Kwa ufupi dua ni kumuomba Allah akuondoshee lililobaya, ama linalo kuudhi ama akupe jambo fulani. Na dua ni ibada kama ibada nyingine.
Dua ni jambo lenye kupendeza kama walivyosema maulamaa na masalafi wema walotangulia. Umuhimu wa dua na msisitizo wake unapatikana katika quran na sunnah.
Dua zimesisitizwa sana katika quran na sunnah hata mtume akasema ููููุณูุฃููู ุฃูุญูุฏูููู
ู ุฑูุจูููู ุญูุงุฌูุชููู ุญูุชููู ููุณูุฃููููู ุงููู
ูููุญู โna aombe mmoja wenu haya yake (dua) kwa Allah mpaka chumvi.โฆโ. Hivyo si kuomba mambo kakubwa tu na matatizo tulonayo ila mpaka chumvi.
FADHILA ZA DUA
1.Dua ni ibada. Basi utambue ewe ndugu muislamu kuwa dua ni ibada. Imepokewa hadithi kutoka kwa Nuuman Ibn Bashir ุฑุถูุงููู ุนูู kuw Mtume wa Allah ุตููุงููู ุนููู ูุณูู
amesema "โ ุงูุฏููุนูุงุกู ูููู ุงููุนูุจูุงุฏูุฉูโhakika dua ni ibadaโ (imepokewa na Tirmidh na ameisahihisha).
2.Dua ndio jambo tukufu zaidi kwa Allah kama Mtume ุตููุงููู ุนููู ูุณูู
aliposema katika hadithi iliyosimuliwa na Abu Huraurah ุฑุถูุงููู ุนูู kuwa Mtume amesema โhakuna kitu kitukufu mbele ya Allah kuliko duaโ (imapokewa na tirmidh, imam Ahmad na Alhaakim kwa isnad sahihi)
ููููุณู ุดูููุกู ุฃูููุฑูู
ู ุนูููู ุงูููููู ุชูุนูุงููู ู
ููู ุงูุฏููุนูุงุกู โ
3.Allah anamchukia mtu ambaye hamuombi. Abuu Hurairah ุฑุถูุงููู ุนูู amesema kuwa Mtume ุตููุงููู ุนููู ูุณูู
amesema "โ ู
ููู ููู
ู ููุณูุฃููู ุงูููููู ููุบูุถูุจู ุนููููููู โ"
โmtu yeyote ambaye hamuombi Allah, Allah humchukia mtu huyoโ (amepokea hadithi tirmidh)
4.Allah anapenda kuombwa. Katika masimulizi ya Ibn Masโud ุฑุถูุงููู ุนูู Mtume ุตููู ุงููู ุนููู ูุณููู
amesema โmuombeni Allah katika fadhila zake, hakika Mwenyezimungu Mtukufu (ุบุฒู ูุฌูู) anapenda kuombwaโ (amepokea Tirmidh).
5.Dua ni malango wa rehema. Katika masimulizi ya ibn โUmar ุฑุถูุงููู ุนูู kuwa Mtume ุตููู ุงููู ุนููู ูุณููู
amesema "โ ู
ููู ููุชูุญู ูููู ู
ูููููู
ู ุจูุงุจู ุงูุฏููุนูุงุกู ููุชูุญูุชู ูููู ุฃูุจูููุงุจู ุงูุฑููุญูู
ูุฉู ููู
ูุง ุณูุฆููู ุงูููููู ุดูููุฆูุง ููุนูููู ุฃูุญูุจูู ุฅููููููู ู
ููู ุฃููู ููุณูุฃููู ุงููุนูุงููููุฉู โ"โ โmwenye kufunguliwa mlango wa dua, hufunguliwa mlango wa rehema.โฆโ (amepokea Tirmidh).
6.Dua huondosha mabalaa na majanga. Katika masimulizi ya Ibn โUmar, ุฑุถูุงููู ุนูู Mtume ุตููู ุงููู ุนููู ูุณููู
amesema โhakika dua hunufaisha kwa (hukinga) yale yanayoshuka (yanayotokea), na yale ambayo hayajashuaka ( hayajatokea). Basi jilazimisheni na (kuomba) dua enyi waja wa Allah.
Umeionaje Makala hii.. ?
Hii ni historia ya Imamu Bukhary pamoja na kitabu chake cha sahihul Bukhari.
Soma Zaidi...Hapa nitakuletea baadhi tu ya adhkari ambazo ni muhimu kwa muislamu
Soma Zaidi...DUA ZA KUONDOA MAUMIVU MWILINI Katika uislamu Allah amejaalia dawa katika kufuata sunnah.
Soma Zaidi...Kukubaliwa kwa dua kunategemea mahusiano yako na Allah. hata hivyo kuna baadhi ya mabo ukiyafanya dua yako inaweza kukubaliwa kwa haraka zaidi. Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi ya kuomba dua ikubaliwe.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukupa tahadhari juu ya mambo ya halali na mambo ya haramu.
Soma Zaidi...