MAANA NA FADHILA ZA KUOMBA DUA

DUA Kwa ufupi dua ni kumuomba Allah akuondoshee lililobaya, ama linalo kuudhi ama akupe jambo fulani.

MAANA NA FADHILA ZA KUOMBA DUA


DUA
Kwa ufupi dua ni kumuomba Allah akuondoshee lililobaya, ama linalo kuudhi ama akupe jambo fulani. Na dua ni ibada kama ibada nyingine.

Dua ni jambo lenye kupendeza kama walivyosema maulamaa na masalafi wema walotangulia. Umuhimu wa dua na msisitizo wake unapatikana katika quran na sunnah.

Dua zimesisitizwa sana katika quran na sunnah hata mtume akasema ู„ููŠูŽุณู’ุฃูŽู„ู’ ุฃูŽุญูŽุฏููƒูู…ู’ ุฑูŽุจู‘ูŽู‡ู ุญูŽุงุฌูŽุชูŽู‡ู ุญูŽุชู‘ูŽู‰ ูŠูŽุณู’ุฃูŽู„ูŽู‡ู ุงู„ู’ู…ูู„ู’ุญูŽ โ€œna aombe mmoja wenu haya yake (dua) kwa Allah mpaka chumvi.โ€ฆโ€. Hivyo si kuomba mambo kakubwa tu na matatizo tulonayo ila mpaka chumvi.

FADHILA ZA DUA
1.Dua ni ibada. Basi utambue ewe ndugu muislamu kuwa dua ni ibada. Imepokewa hadithi kutoka kwa Nuuman Ibn Bashir ุฑุถู‰ุงู„ู„ู‡ ุนู†ู‡ kuw Mtume wa Allah ุตู„ูŠุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆุณู„ู… amesema "โ€ ุงู„ุฏูู‘ุนูŽุงุกู ู‡ููˆูŽ ุงู„ู’ุนูุจูŽุงุฏูŽุฉูโ€œhakika dua ni ibadaโ€ (imepokewa na Tirmidh na ameisahihisha).

2.Dua ndio jambo tukufu zaidi kwa Allah kama Mtume ุตู„ูŠุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆุณู„ู… aliposema katika hadithi iliyosimuliwa na Abu Huraurah ุฑุถู‰ุงู„ู„ู‡ ุนู†ู‡ kuwa Mtume amesema โ€œhakuna kitu kitukufu mbele ya Allah kuliko duaโ€ (imapokewa na tirmidh, imam Ahmad na Alhaakim kwa isnad sahihi) ู„ูŽูŠู’ุณูŽ ุดูŽูŠู’ุกูŒ ุฃูŽูƒู’ุฑูŽู…ูŽ ุนูŽู„ูŽู‰ ุงู„ู„ู‘ูŽู‡ู ุชูŽุนูŽุงู„ูŽู‰ ู…ูู†ูŽ ุงู„ุฏู‘ูุนูŽุงุกู โ€œ

3.Allah anamchukia mtu ambaye hamuombi. Abuu Hurairah ุฑุถู‰ุงู„ู„ู‡ ุนู†ู‡ amesema kuwa Mtume ุตู„ูŠุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆุณู„ู… amesema "โ€ ู…ูŽู†ู’ ู„ูŽู…ู’ ูŠูŽุณู’ุฃูŽู„ู ุงู„ู„ู‘ูŽู‡ูŽ ูŠูŽุบู’ุถูŽุจู’ ุนูŽู„ูŽูŠู’ู‡ู โ€" โ€œmtu yeyote ambaye hamuombi Allah, Allah humchukia mtu huyoโ€ (amepokea hadithi tirmidh)

4.Allah anapenda kuombwa. Katika masimulizi ya Ibn Masโ€™ud ุฑุถู‰ุงู„ู„ู‡ ุนู†ู‡ Mtume ุตู„ู‘ูŠ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆุณู„ู‘ู… amesema โ€œmuombeni Allah katika fadhila zake, hakika Mwenyezimungu Mtukufu (ุบุฒู‘ ูˆุฌู„ู‘) anapenda kuombwaโ€ (amepokea Tirmidh).

5.Dua ni malango wa rehema. Katika masimulizi ya ibn โ€˜Umar ุฑุถู‰ุงู„ู„ู‡ ุนู†ู‡ kuwa Mtume ุตู„ู‘ูŠ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆุณู„ู‘ู… amesema "โ€ ู…ูŽู†ู’ ููุชูุญูŽ ู„ูŽู‡ู ู…ูู†ู’ูƒูู…ู’ ุจูŽุงุจู ุงู„ุฏูู‘ุนูŽุงุกู ููุชูุญูŽุชู’ ู„ูŽู‡ู ุฃูŽุจู’ูˆูŽุงุจู ุงู„ุฑูŽู‘ุญู’ู…ูŽุฉู ูˆูŽู…ูŽุง ุณูุฆูู„ูŽ ุงู„ู„ูŽู‘ู‡ู ุดูŽูŠู’ุฆู‹ุง ูŠูŽุนู’ู†ููŠ ุฃูŽุญูŽุจูŽู‘ ุฅูู„ูŽูŠู’ู‡ู ู…ูู†ู’ ุฃูŽู†ู’ ูŠูุณู’ุฃูŽู„ูŽ ุงู„ู’ุนูŽุงูููŠูŽุฉูŽ โ€"โ€ โ€œmwenye kufunguliwa mlango wa dua, hufunguliwa mlango wa rehema.โ€ฆโ€ (amepokea Tirmidh).

6.Dua huondosha mabalaa na majanga. Katika masimulizi ya Ibn โ€˜Umar, ุฑุถู‰ุงู„ู„ู‡ ุนู†ู‡ Mtume ุตู„ู‘ูŠ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆุณู„ู‘ู… amesema โ€œhakika dua hunufaisha kwa (hukinga) yale yanayoshuka (yanayotokea), na yale ambayo hayajashuaka ( hayajatokea). Basi jilazimisheni na (kuomba) dua enyi waja wa Allah.


                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Download App yetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sunnah Main: Dini File: Download PDF Views 826

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Simulizi za Hadithi Audio    ๐Ÿ‘‰2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    ๐Ÿ‘‰3 Bongolite - Game zone - Play free game    ๐Ÿ‘‰4 Kitabu cha Afya    ๐Ÿ‘‰5 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Historia ya Imamu Bukhary Muandishi wa Hadithi za Mtume s.sa. w

Hii ni historia ya Imamu Bukhary pamoja na kitabu chake cha sahihul Bukhari.

Soma Zaidi...
Adhkari unazoweza kuomba kila siku

Hapa nitakuletea baadhi tu ya adhkari ambazo ni muhimu kwa muislamu

Soma Zaidi...
SWALA YA MTUME (s.a.w)

SWALA YA MTUME Kumswalia Mtume (s.

Soma Zaidi...
DUA ZA KUONDOA WASIWASI

DUA ZA KUONDOA MAUMIVU MWILINI Katika uislamu Allah amejaalia dawa katika kufuata sunnah.

Soma Zaidi...
JINSI YA KUOMBA DUA ILI IKUBALIWE NA ALLAH

Kukubaliwa kwa dua kunategemea mahusiano yako na Allah. hata hivyo kuna baadhi ya mabo ukiyafanya dua yako inaweza kukubaliwa kwa haraka zaidi. Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi ya kuomba dua ikubaliwe.

Soma Zaidi...
Al-Arbauwn An-Nawawiyyah hadithi ya 6: ubainifu wa halali na haramu

Post hii inakwenda kukupa tahadhari juu ya mambo ya halali na mambo ya haramu.

Soma Zaidi...