MASHART YA KUKUBALIWA KWA DUA.
MASHART YA KUKUBALIWA KWA DUA.
1.kuchunga adabu za dua kama zilivyotajwa hapo juu.
2.Kuwa twahara nje na ndani. Yaani kujiepusha na mambo maovu na machafu ya siri na yasiyo ya siri. Amesema Mtume ุตููู ุงููู ุนููู ูุณููู
โhakika Allah ni mzuri na anapenda (vitu) vizuri.โฆโ. (amepekea Bukhari na Muslim)
Hivyo mtu anatakiwa ahakikishe ni mzuri ndani na nje.
3.kujiweka mbali na yaliyo haramu yote, na kujiepusha kula na kunywa bya haramu au kuvaa vilivyo haramu. Amesema Mtume ุตููู ุงููู ุนููู ูุณููู
โukitaka dua maombi yako basi kifanye kizuri chakula chako (kisiwe cha haramu) โ (amepekea Bukhari na Muslim). Na pia katika hadithi ndefu iliyo sahihi katika kuwa mtume anashangaa mtu ambaye chakula chake haramu, kinywaji chake haramu, a mavazi yake haramu. Isitoshe mtu huyu amechafuka na manywele yapo timtim. Vipi atajibiwa dua yake mtu huyu. (amepekea Bukhari na Muslim).
4.Kuzingatia nyakati ambazo dua hujibiwa. Tutaziona hapo mbele.
5.Sifa ya dua yenyewe. Tutaona dua zenye sifa ya kujibiwa.
6.Hali inayozunguruka dua. Tutaona hali ambazo dua hujibiwa.
Umeionaje Makala hii.. ?
Wapo watu kadhaa ambao waliomba dua hazirudi. Hapa nitakueleza wawili ambao ni mzazi na msafiri.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukufundisha namna ama staili ambazo Allah hujibu dua za watu.
Soma Zaidi...Hapa utajifunza nafasi ya kufuata suna katika Uislamu
Soma Zaidi...