Uandishi wa Hadithi wakati wa Matabiina

Uandishi wa Hadithi wakati wa Matabiina

Historia ya uandishi wa hadithibwakati wa Matabiina, yaani wafuasi wa maswahaba

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Wakati wa Wafuasi wa masahaba (Tabi'ina)101-200 A.H
Hiki ni kipindi cha wafuasi wa Masahaba wa Mtume (s.a.w) katika karne ya pili Hijiriyyah 101-200 A.H. Katika kipindi hiki walitokea wanazuoni wengi waliojizatiti katika kazi ya ukusanyaji wa Hadith kutoka katika vituo mbali mbali vya mafunzo (Centres of Learning). 

Wafuatao ni baadhi ya wanazuoni wa Hadith (Muhaddithina) waliojitokeza kutoka miji mbali mbali. Ma'mar bin Rashi wa Baghdadi; Said bin Abi Ubadah na Rabia bin Sabin wa Basra; Ibn Harith wa Baghdad; Abdul Malik bin Juraiji wa Makka; Walid bin Mubarrak wa Khurasan; Abu Bakr Shyaban wa Kufa na Sufyan bin Uyaina wa Madina.

Japo wanazuoni hawa walijitahidi sana katika hii kazi ya ukusanyaji Hadith, kazi zao bado hazikuwa zenye kutosheleza; isitoshe sehemu kubwa ya vitabu vyao ilihusu ripoti ya vituo vyao. Baada ya kazi hizi, kilitokea kitabu cha "al-Muwatta" cha Imam Malik bin Anas aliyeishi Madina kati ya 95 A.H na 179 A.H. Kazi ya Imam Malik ndiyo ya kwanza iliyowekwa katika mpango mzuri na kuwa kitabu cha kutegemewa na Umma. Imam Malik alifutu mas-ala ya Uislamu kwa kutegemea Qur-an na Hadith tu. Alianzisha umoja wa "Ahli Hadith" ambao kazi yake ilikuwa ni kukusanya Hadith na kuzitekeleza katika matendo.

Katika wakati huo huo alitokea Imam Abu Hanifa al-Numan bin Thabit (80-150) aliyefutu mas-ala mbali mbali ya Kiislamu kwa hoja na Qiyasi (deductions) baada ya kuzingatia Qur-an, Hadith na Ijma'i (makubaliano ya wanavyuoni). Hakuandika kitabu chochote cha Hadith lakini alikuwa mwanazuoni mkubwa wa "Qur-an na Hadith na alikuwa Muj-tahid na Mcha-Mungu.

Katika kipindi hiki hiki palitokea Maimamu wengine wawili mashuhuri. Imam Muhammad bin Idris al-Shafii (150-240 A.H.) aliyezaliwa Palestine mji wa Ghazza, na mwingine ni Imam Ahmad bin Hambal (164-241 A.H.) aliyezaliwa Baghdad na kujulikana sana kwa kitabu chake cha Isnad ya Ibn Hambali kilichokuwa na Hadith zaidi ya 30,000 alizokusanya.

 

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sunnah Main: Dini File: Download PDF Views 1015

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

MASHARTI YA KUKUBALIWA KWA DUA
MASHARTI YA KUKUBALIWA KWA DUA

MASHART YA KUKUBALIWA KWA DUA.

Soma Zaidi...
KUKUSANYIKA KATIKA DUA
KUKUSANYIKA KATIKA DUA

KUKUSANYIKA KATIKA DUA.

Soma Zaidi...
KUINGIA KWA WAGENI
KUINGIA KWA WAGENI

Download kitabu Hiki Bofya hapa KUINGIA KWA WAGENI Amina na Sadie walimuonea huruma wakamuomba Zubeid amruhusu abakie.

Soma Zaidi...
Maana ya sunnah (suna) na maana ya hadithi
Maana ya sunnah (suna) na maana ya hadithi

Post hii itakufundisha maana ya neno sunnah katika Uislamu. Pia utajifunza maana ya neno hadithi katika uislamu

Soma Zaidi...
NAMNA AMBAZO DUA HUJIBIWA
NAMNA AMBAZO DUA HUJIBIWA

NAMNA AMBAYO ALLAH HUJIBU DUA.

Soma Zaidi...
NAFASI YA SUNNAH KATIKA UISLAMU
NAFASI YA SUNNAH KATIKA UISLAMU

Nafasi ya Sunnah katika UislamuMtume Muhammad (s.

Soma Zaidi...
NAMNA AMBAZO DUA HUJIBIWA
NAMNA AMBAZO DUA HUJIBIWA

NAMNA AMBAYO ALLAH HUJIBU DUA.

Soma Zaidi...
AINA ZA HADITHI
AINA ZA HADITHI

Aina za HadithKuna aina kuu mbili za Hadith- (a) Hadith Nabawiyyi.

Soma Zaidi...
DUA ZENYE MANENO HAYA HUJIBIWA
DUA ZENYE MANENO HAYA HUJIBIWA

SIFA ZA (MANENO NA MATAMSHI YA) DUA YENYE KUJIBIWA.

Soma Zaidi...