picha

AINA ZA HADITHI

Aina za HadithKuna aina kuu mbili za Hadith- (a) Hadith Nabawiyyi.

AINA ZA HADITHI

Aina za Hadith
Kuna aina kuu mbili za Hadith
- (a) Hadith Nabawiyyi. 
(b) Hadith Qudusiyyi.

(a)Hadith an-Nabawiyyi
Ni usemi au habari aliyoitoa Mtume (s.a.w) kwa watu kwa maneno yake. Utazikuta Hadith za aina hii zikianza na: Amesema Mtume (s.a.w) " 
Mfano wa Hadith an-Nabawiyyi:
Aysha (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah (Rehema na amani iwe juu yake) amesema: "Yoyote atakayeingiza jambo jipya katika mambo yetu (dini yetu) lisilokuwa la humu, litakataliwa." (Wamekubaliana Bukhari na Muslim)

(b)Hadith Qudusiyyi:
Ni usemi au habari aliyoitoa Mtume (s.a.w) kama alivyoipokea kutoka kwa Allah (s.w) lakini iliyo nje ya Qur-an. Hadith hizi huanza na: Amesema Mtume (s.a.w) kuwa Allah (s.w) kasema: "……." 
Mfano wa Hadith Qudusiyyi:
Abu Huraira (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah (rehema na amani iwe juu yake) amesema: Allah (s.w) amesema: "Ni mwingi wa kujitosheleza kwa kiasi kwamba sihitaji mshiriki yeyote. Kwa hiyo yeyote yule atakaye fanya amali (atakayefanya jambo) kwa ajili ya mtu mwingine pamoja na Mimi Nitaikataa hiyo amali na kuipeleka kwa yule aliyenishirikisha naye." (Imesimuliwa na Muslim, hali kadhalika Ibn Majah). Hadith Qudusiyyi ni chache sana ukizilinganisha na Hadith Nabawiyyi. Idadi yake ni Hadith mia mbili na kidogo tu. 


                   

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sunnah Main: Post File: Download PDF Views 3301

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game     👉2 ai web app     👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 web hosting     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

Muangalie aliye chini yako na usimuangalie aliye juu

Katika hadithi hii utakwenda kujifunza hekma ya kuangalia watu walio chini yako na sio walio juu yako

Soma Zaidi...
BAADHI YA DUA ZA KILA SIKU

BAADHI YA DUA ZA KILA SIKU.

Soma Zaidi...
Dua za kuomba wakati unapokuwa na hasira ama ukiwa umekasirika

Post hii itakueleza ni dua gani unatakiwa uzisome wakati unapokiwa na hasira ama pale unapokasirika.

Soma Zaidi...