picha

AINA ZA HADITHI

Aina za HadithKuna aina kuu mbili za Hadith- (a) Hadith Nabawiyyi.

AINA ZA HADITHI

Aina za Hadith
Kuna aina kuu mbili za Hadith
- (a) Hadith Nabawiyyi. 
(b) Hadith Qudusiyyi.

(a)Hadith an-Nabawiyyi
Ni usemi au habari aliyoitoa Mtume (s.a.w) kwa watu kwa maneno yake. Utazikuta Hadith za aina hii zikianza na: Amesema Mtume (s.a.w) " 
Mfano wa Hadith an-Nabawiyyi:
Aysha (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah (Rehema na amani iwe juu yake) amesema: "Yoyote atakayeingiza jambo jipya katika mambo yetu (dini yetu) lisilokuwa la humu, litakataliwa." (Wamekubaliana Bukhari na Muslim)

(b)Hadith Qudusiyyi:
Ni usemi au habari aliyoitoa Mtume (s.a.w) kama alivyoipokea kutoka kwa Allah (s.w) lakini iliyo nje ya Qur-an. Hadith hizi huanza na: Amesema Mtume (s.a.w) kuwa Allah (s.w) kasema: "……." 
Mfano wa Hadith Qudusiyyi:
Abu Huraira (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah (rehema na amani iwe juu yake) amesema: Allah (s.w) amesema: "Ni mwingi wa kujitosheleza kwa kiasi kwamba sihitaji mshiriki yeyote. Kwa hiyo yeyote yule atakaye fanya amali (atakayefanya jambo) kwa ajili ya mtu mwingine pamoja na Mimi Nitaikataa hiyo amali na kuipeleka kwa yule aliyenishirikisha naye." (Imesimuliwa na Muslim, hali kadhalika Ibn Majah). Hadith Qudusiyyi ni chache sana ukizilinganisha na Hadith Nabawiyyi. Idadi yake ni Hadith mia mbili na kidogo tu. 


                   

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sunnah Main: Post File: Download PDF Views 3399

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉2 web hosting     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 kitabu cha Simulizi     👉6 ai web app    

Post zinazofanana:

Dua sehemu 03

Zijuwe njia ambazo Allah hujibu Dua yako. Tambua kama umejibiwa dua yako au bodo, soma darsa za dua hapa.

Soma Zaidi...
Ni siku zipo huitwa Aiyami tashriq?

Aiyami ni wingi wa neno yaumi kwa maana siku. Kwenye uislamu Kuna masimu matukufu kama vile masimu ya tashriq. Je ni yapi hayo? Endelea na makala hii.

Soma Zaidi...
Hali ambazo akiwa nazo mwenye kuomba dua dua yake hujibiwa

Post hii inakwenda kukifundisha nibhali zipi ukiwa nazo, basi dua yako kuhubaliwa kwa urahisi.

Soma Zaidi...