61.
61.Mtume (s.a.w) amesema, amali njema ya kudumu ni kusema: “Sub-haanallahi, wal-hamdulillaahi, walaailaha illallaahu walaahu akbaru walaahawla walaaquwwata illaabillaahi." Utukufu ni wa Allah na shukurani zote anastahiki Allah, na Hapana Mola ila Allah na Allah ni mkubwa. Hapana uwezo wala nguvu ila kutoka kwa Allah."
62.Dhikri ya kuleta wakati wa kulala Alikuwa Mtume (s.a.w) akienda kulala usiku, akiweka pamoja viganja vyake kisha akivipulizia na akivisomea suratul-Ikhlas, suratul Falaq na Suratun-Naas, kisha akipangusa kwa hivyo viganja vyake kiasi anachoweza katika mwili wake, akianza kichwani, usoni na mbele (akifanya hivyo mara tatu.) (Bukhari na Muslimu)
63.Mtume (s.a.w) amesema: "Ukienda kulala soma Ayatulkursiyyu kwani Allah ataendelea kukuhifadhi, wala hakukaribii shetani mpaka asubuhi." (Al-Bukhari)
64.Mwenyezi Mungu, hakuna Mola ila yeye, ndiye mwenye uhai wa milele, msimamia kila jambo. Kusinzia hakumshiki wala kulala. Ni vyake (peke yake vyote) vilivyomo mbinguni na vilivyomo ardhini. Na nani huyo awezaye kuombea mbele yake bila ya idhini yake? Anayajua yaliyo mbele yao (viumbe) na (yaliyo) nyuma yao; wala (hao viumbe) hawalijui lolote katika ilimu yake ila kwa alipendalo. Enzi yake imeenea mbinguni na ardhini, wala kuvilinda hivyo hakumshindi; Na yeye (pekee) ndiye aliye juu na ndiye aliye mkuu." (2:255)
65.Alikuwa Mtume (s.a.w) akitaka kulala, anaweka mkono wake wa kulia chini ya shavu lake, kisha anasema: "Allahumma qiniy a'dhaabaka yaumatab-a'thu i'baadaka." "Ee! Allah nikinge mimi kwa adhabu yako siku utakapowafufua waja wako."
66.Pia Mtume (s.a.w) wakati wa kulala alikuwa akisema: “Allahumma Bismika amuutu wa-ahyaa. “Kwa jina lako, Ee Allah ninakufa na nina kuwa hai." uzi na ndiye Mwenye hikima (2:32)
Dua ya kufungulia swala (Duau al-iftitah)
67.Kusoma dua ya kufungulia swala ni sunnah. Katika Hadithi ya Bukhari na Muslim iliyosimuliwa na Abu Hurairah (r.a), baada ya kuhirimia swala Mtume (s.a.w) alikuwa akileta dua ifuatayo:
68.“wajahtu wajhi lilladhi fatwaras-samaawat wal-ardha hanifam-muslima wamaa kaana minal-mushrikina. Inna swalatiy wanusukii, wamah-haya, wamaamatiy, lillahi rabil-alamiina laa sharikalahu wabidhalika umirtu wa-ana minal-mushrikiina.”
Tafsiri:
“Nimeuelekeza uso wangu kwa yule aliyeziumba mbingu na ardhi. Nimeacha dini za upotovu. Mimi si miongoni mwa washirikina. Hakika swala yangu (na ibada zangu zote) na uzima wangu na kufa kwangu (yote) ni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, bwana (Rabbi) wa walimwengu wote. Hana mshirika wake. Na haya ndio niliyoamrishwa na mimi ni wa kwanza walio jisalimisha kikamilifu kwa Mwenyezi Mungu. (6:79, 162-163)
Kusoma al-hamdu (surat al-fatiha)
69.Baada ya kusoma dua ya kufungulia swala mtu atasoma alhamdu. Na kusoma al-hamdu ni nguzo ya swala.Tunasoma suratul-Fatiha kama ifuatavyo:-
70.Bismillahir Rahmaanir Rahiim (1) Alhamdu liLLahi rabbil-’Aalamiin (2). Rrahmaanir Rahiim (3) Maaliki yaumiddiin (4) Iyyaakana‘abudu waiyyaaka nasta‘iin (5) Ih dinasw-swiraatwal mustaqiim (6) Swiraatwa lladhiina an ‘amta ‘alaihim; ghairil maghdhuubi ‘alaihim wala dhw-dhwaaliin (7)
Tafsri:
71.(1) Kwa jina la Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema na mwenye kurehemu: (2) Shukrani zote anastahiki Mwenyezi Mungu, Mola wa Walimwengu wote: (3) Mwingi wa Rehema mwenye kurehemu (4) Mwenye kumiliki siku ya malipo: (5) Wewe tu ndiye tunayekuabudu, na wewe tu ndiye tunaye kuomba msaada: (6) Tuongoze njia iliyonyooka: (7) Njia ya wale uliowaneemesha; siyo (ya wale ) waliokasirikiwa, wala ya wale waliopotea.
Kurukuu.
72.Katika rukuu ni sunnah kusoma dua hii Katika rukuu ni sunnah kumsabihi Allah (s.w) kwa kusema kimya kimya mara tatu au zaidi
73.“Subhana Rabbiyal’Adhiim”
Tafsiri:
74.“Utukufu ni wako Ee Bwana (Mlezi) wangu Uliye mkuu”
Kuitidali (kusimama wima kutoka kwenye rukuu)
75.wakati wa kunyanyuka maneno haya:“sami’a llahu liman hamidahu” Mwenyezi Mungu anamsikia kila mwenye kumhimidi. Na baada ya kusimama sawa ni sunnah kusema “rabbanaa walakal-hamdu”ewe mola wetu sifa zote za ukamilifu ni zako. Pia ni sunnah kusema maneno haya
76.“rabbanaa walakal-hamdu mil-as-samaawati wamil-al-ardhi wamil-amashi-ita minshai-in ba’adah”
Tafsiri:
77.Ewe Mola wetu sifa zote za ukamilifu ni za kwako, kutoka mbinguni, kutoka ardhini na katika vitu vyote vilivyo baina yao (mbingu na ardhi) na kutoka katika vinginevyo unavyo viridhia
Kusujudi
78.utasema kwenye sijda:-
79.“subhaana rabbiyal-a’alaa” Tafsiri:
80.utukufu ni wa kwako Mola uliye tukuka. (mara tatu au zaidi)
Kukaa kati ya sijida mbili.
Katika kikao hiki utasema:-
81.“rabbigh-firliy warhamnii wa’afinii warzuqniy”
Tafsiri:
Ewe Mola wangu nisamehe, na unirehemu, na unipe afya na uniruzuku
Tahiyyatu (maamkizi)
Haya ni maneno yanayosemwa katika kikao cha tahiyatu. Maneno haya ni:-
82.“Attahiyyaatu lillaah, wasw-swalawaatu, watwa-yyibaatu, assalaamu ‘alaika ayyuhannabiyyu, warahmatullaahi wabarakaatuhu, assalaamu ‘alay-naa wa-’alaa ‘ibaadillaahi swswaalihiina. Ash-hadu an-llaailaaha illallaahu wa-ash-hadu anna Muhammadan ‘abduhuu warasuuluhu”.
Tafsiri:
83.“Maamkizi yote ni ya Allah, na swala zote na yote mazuri, Amani iwe juu yako, ewe Mtume na Rehma na Baraka za Allah. Na amani iwe juu yetu na juu ya waja wema wa Allah. Ninashuhudia kuwa hapana Mola ila Allah. Na ninashuhudia kuwa Muhammad ni Mja na, ni Mtume wake”. (Muslim).
Kumswalia Mtume (s.a.w) kwenye tahiyyatu ya mwisho. Zipo aina nyingi za kumswalia Mtume (s.a.w). Hapa utasema maneno yafuatayo:-
84.“Allahumma swalli ‘alaa muhammad wa’alaa aliy Muhammad kamaa swallaita ‘alaa ibraahima wa’alaa ali ibraahim innaka hamiidum-majid. Wabaaik ‘alaa muhammad wa’alaa ali muhammad kamaa barakta ‘alaa ibraahima wa’alaa ali ibraahima innaka hamiidum-majid”
Tafsiri:
Ewe Mola mrehemu Muhammad na wafuasi wake kama ulivyomrehemu Ibrahim na wafuasi wake hakika wewe ni mtukufu na msifiwa wa haki. Ewe Mola mbariki Muhammad na wafuasi wake kama ulivyombariki Ibraahim na wafuasi wake hakika wewe ni wewe ni mtukufu na msifiwa wa haki.
Je! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sunnah Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 532
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi
👉2 Kitau cha Fiqh
👉3 Kitabu cha Afya
👉4 Simulizi za Hadithi Audio
👉5 Madrasa kiganjani
👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Maana ya dua na fadhila zake
Dua ni moja ya Ibada ambazo tunatakiwa kuziganya kila siku. Kuna fadhila nyingi sana za kuomba dua. Post hiibitakwenda kukujuza fadhila za kuomba dua. Soma Zaidi...
Utofauti wa dua ya kafiri na dua ya muislamu katika kujibiwa
Posti hii inakwenda kukufundisha ni kwa nini dua ya kafiri inawwza kujibiwa wakati ya muumini haijibiwi. Soma Zaidi...
AMRI YA KUMFUATA MTUME (s.a.w9)
Amri ya Kumfuata Mtume (s. Soma Zaidi...
ADHKAR NA DUA
ADHKARI MBALIMBALI NA DUA Hapa tutajifunza dua mbalimbali ambazo ni adhkari. Soma Zaidi...
SWALA YA MTUME (s.a.w)
SWALA YA MTUME Kumswalia Mtume (s. Soma Zaidi...
Dua za kuomba wakati unapokuwa na maumivu kwenye mwili
Posti hii inakwenda kukufundisha dua za kuomba wakati wa kuwa na maumivu kwenye mwili wako. Soma Zaidi...
kuwa na kauli njema, na faida zake katika jamii
11. Soma Zaidi...
Hadithi Ya 26: Kila Kiungo Cha Mtu Lazima Kitolewe Sadaka
Soma Zaidi...
Vyanzo vitano vya elimu zote duniani: Chanzo cha Elimu ni Allah (s.w)
Kama tunavyojifunza katika surat ‘Alaq (96:4-5), chanzo cha elimu au mkufunzi wa binadamu ni Allah (s. Soma Zaidi...
Nafasi ya Sunnah (suna) katika Uislamu.
Hapa utajifunza nafasi ya kufuata suna katika Uislamu Soma Zaidi...