image

DUA 41 - 50

41.

DUA 41 - 50


41..Dua ya kusema unapoanza kula Unapoanza kula hunabudi kusema: “Bismillaahi" “Kwa jina la Allah" Na ukisahau kusema hivyo wakati wa kuanza, ukikumbuka wakati unaendelea kula sema: “Bismillahi fiy awwalihi wa-aakhirihi" “Kwa jina la Allah katika mwanzo wake na mwisho wake" 24.Dua ya kushukuru baada ya kula “Al-hamdulillahilladhii atw-a'maniy hadhaa warazaqaniyhi min ghayri hawlin minniy walaa quwwatin" “Shukurani zote anastahiki Allah ambaye amenilisha chakula hiki bila ya uwezo wala nguvu yoyote kutoka kwangu."

42.Dua ya mgeni kumuombea mwenyeji aliye mlisha chakula “Allahumma baarik-lahum fiymaa razaq-tahum, wagh-fir lahum war-hamhum." 483 Ee Allah, wape baraka kwa hicho ulicho wapa,wasamehe na warehemu."

43.Dua ya kuleta baada ya kupiga chafya Unapopiga chafya hunabudi kusema: “Al-hamdulillaahi" “Sifa zote anastahiki Allah." Kisha ndugu zako Waislamu watasema: “Yar-hamuka llahu." “Allah akurehemu." Kisha utajibu kwa kusema: "Yah-diykumullahu wayusw-lihi baalakum." "Allah akuongozeni na kuwasahilishia mambo yenu." Kama anaeambiwa ni mwanamke
“Utasema yar-hamuki llahu”

44.Dua ya kuwaombea maharusi (waliooana) “Baarakallahulaka,wabaaraka a'layka,wajamaa'baynakumaa fiy khayrin" “Allah akubariki wewe na yeye (mkeo/mumeo) na awaunganishe katika kheri."

45.Dua ya kuleta unapoanza kufanya tendo la ndoa “Bi smi l lahi A l lahumma jannib-nashshay - twaana wajannibish-shytwaana maarazaq-tanaa". “Kwa jina la Allah, Ee Allah muweke shetani mbali nasi na muweke shetani mbali na hicho ulichoturuzuku."

46.Dua ya kuleta unapopandwa na hasira “Au'udhubillaahi minash-shaytwaani rrajiimi" “Najikinga kwa Allah na shetani aliyelaaniwa."

47.Dua ya kuleta mwisho wa kikao (mkutano) "Sub-haanaka llahumma wabihamdika, ash-hadu an-laa ilaha illa anta as-taghfiruka wa-atuubu ilayka." "Utukufu ni wako, Ee Allah, nakutukuza. Ninashuhudia kuwa hapana Mola ila wewe. Nakuomba msamaha na ninatubia kwako."

48.Dua unayomuombea yule aliyekufanyia jambo zuri “Jazaka llahu khayran" “Allah akulipe kheri."

49.Dua ya kuomba kuepushwa na shirk “Allahumma inniy au'udhubika an-ush-rika bika waanaaaa'lamu, wa-astagh-firuka limaa laa-aa'lamu." "Ewe Allah, najikinga kwako nisikushirikishe huku nikijua na naomba unisamehe kwa lile (baya) nitakalolifanya bila kujua."

50.33.Dua ya kupokelea sadaqa au zawadi "Baarakallahu fiykum." “Baraka za Allah ziwe juu yenu." Na aliyetoa zawadi/swadaqa na akaombewa hivi atajibu "Wafiyhim baarakallahu." "Pia Allah awabariki."


                   



           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 245


Download our Apps
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Historia ya Imamu Bukhary Muandishi wa Hadithi za Mtume s.sa. w
Hii ni historia ya Imamu Bukhary pamoja na kitabu chake cha sahihul Bukhari. Soma Zaidi...

dua ya kuomba jambo ufanikiwe
hii ni damna ya kuomba dua ukubaliwe, dua ya kuomba jambo ufanikiwe Soma Zaidi...

KAMA HUNA HAYA BASI FAJA UNACHOTAKA
عَنْ أَبِي مَسْعُودٍ عُقْبَةَ بْنِ عَمْرٍو الْأَنْصَارِيِّ الْبَدْرِيِّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عل?... Soma Zaidi...

Hadithi ya tatu:ukarimu na kusaidiana
Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

DUA 85 - 93
SWALA YA MTUME 85. Soma Zaidi...

Hadithi Ya 39: Allaah Amewasamehe Umma Wake Kukosea Na Kusahau Kwa Ajili Yake ( Mtume صلى الله عليه وسلم )
Soma Zaidi...

Jinsi ya kutoa salamu katika uislamu
MAkala hii itakwenda kukufundisha jinsi ya kutoa salamu kwenye uislamu Soma Zaidi...

Dua za kuondoa wasiwasi, woga na kujikinga na uchawi, na mashetani
Post hii itakufundisha dua za kuomba wakati wa woga, wasiwasi na kujikinga na wachawi na mashetani Soma Zaidi...

DUA 11 - 20
11. Soma Zaidi...

MAANA NA FADHILA ZA DUA
DUA Kwa ufupi dua ni kumuomba Allah akuondoshee lililobaya, ama linalo kuudhi ama akupe jambo fulani. Soma Zaidi...

DUA 32 - 40
32. Soma Zaidi...

DUA ZENYE MANENO HAYA HUJIBIWA
SIFA ZA (MANENO NA MATAMSHI YA) DUA YENYE KUJIBIWA. Soma Zaidi...