Dawa ya Isoniazid na kazi zake
Posti hii inahusu zaidi dawa ya lsoniazid nA kazi zake, ni dawa ambayo inasaidia kutibu kifua kikuu kati ya madawa yaliyoteuliwa na kuwa na sifa ya kutibu kifua kikuu.
Dawa ya Isoniazid na kazi zake.
1.Dawa ya Isoniazid ni dawa ambayo utumika katika vipindi vyote vya kutibu kifua kikuu yaanza kwenye kipindi cha kwanza na cha pili kwa hiyo dawa hii usaidia kufubaza bakteria ambao wanasababisha kifua kikuu na bakteria ushindwa kukua, dawa hii tunaweza kuikuta kwenye mfumo wa vidonge kwa mara nyingi na kwenye mfumo wa maji maji kwa watoto na pengine inaweza kutolewa kwa njia ya kulishwa kwenye mishipa ya damu au kwenye nyama.
2.Katika matumizi ya dawa hii tunapaswa kuwa makini hasa kwa akina Mama wanaotumia njia za uzazi wa mpango kwa sababu hii dawa umaliza nguvu kwa baadhi ya njia za uzazi wa mpango kwa hiyo unaweza kukuta Mama anatumia dawa hizi na njia za uzazi wa mpango akapata mimba kwa hiyo kwa watumiaji wa dawa hii ni vizuri wakaonana na wataalamu wa afya ili kuchaguliwa njia sahihi na muhimu ambazo haziingilian na dawa hii.
3 Katika matumizi ya dawa hii ya Isoniazid kuna maudhi madogo madogo ambayo yanaweza kutokea kama vile matatizo kwenye ini kwa sababu dawa hii upitia kwenye ini, kichefuchefu, kutapika na kuharisha kwa hiyo Mgonjwa akiona dalili za namna hizi anapaswa kujua kuwa ni kwa sababu ya dawa na ikiwa Dalili hizi zimezidi anapaswa kwenda hospitalini ili kuweza kupata ushauri zaidi katika matumizi ya dawa hizi.
4.Pia tunaona kuwa dawa hii inafubaza wadudu wanaosababisha ugonjwa wa kifua kikuu na wagonjwa uweza kupona kwa hiyo tunapaswa kuwaleta wagonjwa wetu hospitali ili waweze kupata dawa na kuepukana na hali ya kusambaa kwa ugonjwa huu kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine maana ndio Tabia yake kama haujatibiwa uweza kusambaa kwa hiyo jamii inapaswa kujua madhara ya ugonjwa huu wa kifua kikuu.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Madrasa kiganjani 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 Kitabu cha Afya 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
Fahamu kuhusu dawa ya streptomycin
Post hii inahusu zaidi dawa ya streptomycin ni dawa mojawapo ya kupambana na bakteria hasa wanaoshambulia mfumo wa hewa.
Soma Zaidi...Fahamu dawa ya aminophylline kutibi maambukizi kwenye mfumo wa upumuaji
Post hii inahusu zaidi dawa ya aminophylline katika kutuliza maambukizi kwenye mfumo wa upumuaji.
Soma Zaidi...Ijue Dawa ya lignocaine
Posti hii inahusu zaidi dawa ya lignocaine kama mojawapo ya Dawa ambayo utumika wakati wa upasuaji.
Soma Zaidi...Dawa ya Albendazole katika kutibu Minyoo.
Posti hii inahusu zaidi dawa ya Albendazole katika kutibu Minyoo, ni Aina mojawapo ya dawa ambayo usaidia kutibu Minyoo inayosababishwa na bakteria mbalimbali.
Soma Zaidi...Fahamu dawa ya ibuprofen katika kutuliza maumivu
Post hii inahusu zaidi dawa ibuprofen katika kutuliza maumivu, ni aina mojawapo ya dawa na yenyewe ufanya kazi kama aspirin na paracetamol
Soma Zaidi...