Dawa ya Isoniazid na kazi zake
Posti hii inahusu zaidi dawa ya lsoniazid nA kazi zake, ni dawa ambayo inasaidia kutibu kifua kikuu kati ya madawa yaliyoteuliwa na kuwa na sifa ya kutibu kifua kikuu.
Dawa ya Isoniazid na kazi zake.
1.Dawa ya Isoniazid ni dawa ambayo utumika katika vipindi vyote vya kutibu kifua kikuu yaanza kwenye kipindi cha kwanza na cha pili kwa hiyo dawa hii usaidia kufubaza bakteria ambao wanasababisha kifua kikuu na bakteria ushindwa kukua, dawa hii tunaweza kuikuta kwenye mfumo wa vidonge kwa mara nyingi na kwenye mfumo wa maji maji kwa watoto na pengine inaweza kutolewa kwa njia ya kulishwa kwenye mishipa ya damu au kwenye nyama.
2.Katika matumizi ya dawa hii tunapaswa kuwa makini hasa kwa akina Mama wanaotumia njia za uzazi wa mpango kwa sababu hii dawa umaliza nguvu kwa baadhi ya njia za uzazi wa mpango kwa hiyo unaweza kukuta Mama anatumia dawa hizi na njia za uzazi wa mpango akapata mimba kwa hiyo kwa watumiaji wa dawa hii ni vizuri wakaonana na wataalamu wa afya ili kuchaguliwa njia sahihi na muhimu ambazo haziingilian na dawa hii.
3 Katika matumizi ya dawa hii ya Isoniazid kuna maudhi madogo madogo ambayo yanaweza kutokea kama vile matatizo kwenye ini kwa sababu dawa hii upitia kwenye ini, kichefuchefu, kutapika na kuharisha kwa hiyo Mgonjwa akiona dalili za namna hizi anapaswa kujua kuwa ni kwa sababu ya dawa na ikiwa Dalili hizi zimezidi anapaswa kwenda hospitalini ili kuweza kupata ushauri zaidi katika matumizi ya dawa hizi.
4.Pia tunaona kuwa dawa hii inafubaza wadudu wanaosababisha ugonjwa wa kifua kikuu na wagonjwa uweza kupona kwa hiyo tunapaswa kuwaleta wagonjwa wetu hospitali ili waweze kupata dawa na kuepukana na hali ya kusambaa kwa ugonjwa huu kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine maana ndio Tabia yake kama haujatibiwa uweza kusambaa kwa hiyo jamii inapaswa kujua madhara ya ugonjwa huu wa kifua kikuu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 web hosting 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Fahamu tiba ya jino
Post hii inahusu zaidi tiba ya jino,ni tiba ya kawaida kwa watu walio na matatizo ya meno, kwa kawaida tunafahamu kwamba jino huwa halina dawa ila dawa yake huwa ni kungoa lakini Leo nawaletea habari njema kwamba jino sio kungoa tena ila Kuna tiba ambayo
Soma Zaidi...Dawa za kutibu kiungulia
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za kutibu kiungulia
Soma Zaidi...Dawa ya kutibu mapunye
DAWA YA MAPUNYEMatibabu ya mapunye inategemea ni wapi mapunjye yapo.
Soma Zaidi...Mgawanyo wa tiba ya kifua kikuu
Post hii inahusu zaidi mgawanyiko wa tiba ya kifua kikuu, kwa kawaida tiba hii imegawanyika katika sehemu kuu mbili.
Soma Zaidi...Fahamu dawa za kutuliza magonjwa ya akili inayoitwa Chlorpromazine
Post hii inahusu zaidi dawa zinazosaidis katika kutuliza magonjwa ya akili, dawa hii kwa kitaamu huiitwa chlorpromazine ni dawa ambayo utumiwa na watu wenye tatizo la magonjwa ya akili na kwa kiasi kikubwa huwa sawa.
Soma Zaidi...