picha

Dawa ya Isoniazid na kazi zake

Posti hii inahusu zaidi dawa ya lsoniazid nA kazi zake, ni dawa ambayo inasaidia kutibu kifua kikuu kati ya madawa yaliyoteuliwa na kuwa na sifa ya kutibu kifua kikuu.

Dawa ya Isoniazid na kazi zake.

1.Dawa ya Isoniazid ni dawa ambayo utumika katika vipindi vyote vya kutibu kifua kikuu yaanza kwenye kipindi cha kwanza na cha pili kwa hiyo dawa hii usaidia kufubaza bakteria ambao wanasababisha kifua kikuu na bakteria ushindwa kukua, dawa hii tunaweza kuikuta kwenye mfumo wa vidonge kwa mara nyingi na kwenye mfumo wa maji maji kwa watoto na pengine inaweza kutolewa kwa njia ya kulishwa kwenye mishipa ya damu au kwenye nyama.

 

2.Katika matumizi ya dawa hii tunapaswa kuwa makini hasa kwa akina Mama wanaotumia njia za uzazi wa mpango kwa sababu hii dawa umaliza nguvu kwa baadhi ya njia za uzazi wa mpango kwa hiyo unaweza kukuta Mama anatumia dawa hizi na njia za uzazi wa mpango akapata mimba kwa hiyo kwa watumiaji wa dawa hii ni vizuri wakaonana na wataalamu wa afya ili kuchaguliwa njia sahihi na muhimu ambazo haziingilian na dawa hii.

 

3 Katika matumizi ya dawa hii ya Isoniazid kuna maudhi madogo madogo ambayo yanaweza kutokea kama vile matatizo kwenye ini kwa sababu dawa hii upitia kwenye ini, kichefuchefu, kutapika na kuharisha kwa hiyo Mgonjwa akiona dalili za namna hizi anapaswa kujua kuwa ni kwa sababu ya dawa na ikiwa Dalili hizi zimezidi anapaswa kwenda hospitalini ili kuweza kupata ushauri zaidi katika matumizi ya dawa hizi.

 

4.Pia tunaona kuwa dawa hii inafubaza wadudu wanaosababisha ugonjwa wa kifua kikuu na wagonjwa uweza kupona kwa hiyo tunapaswa kuwaleta wagonjwa wetu hospitali ili waweze kupata dawa na kuepukana na hali ya kusambaa kwa ugonjwa huu kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine maana ndio Tabia yake kama haujatibiwa uweza kusambaa kwa hiyo jamii inapaswa kujua madhara ya ugonjwa huu wa kifua kikuu.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Dawa Main: Post File: Download PDF Views 3330

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

Fahamu dawa ya diazepam katika kutuliza kifafa

Post hii inahusu zaidi dawa ya diazepam katika kutuliza kifafa, ni dawa ambayo matumizi yake yanaweza kuingilia pote kwenye kutuliza kifafa na pia kwa wagonjwa wa akili.

Soma Zaidi...
Dawa ya kutibu fangasi wa kwenye mdomo na kinywa

Zipo dawa nyingi ambazo hufahamika katika kutibu fangasi kwenye mdomo ama kinywa. Miongoni mwa dawa hizo hapa nitakuletea baadhi yao. kama wewe pia unasumbuliwa na fangasi wa mdomo basi post hii itakusaidi sana.

Soma Zaidi...
Dawa za kutibu fangasi kwenye kucha

Makala hiii inakwenda kukueleza dawa za kutibu fangasi kwenye kucha.

Soma Zaidi...
Faida za vidonge vya antroextra

Posti hii inahusu zaidi faida za vidonge vya antroextra, ni vidonge kwa ajili ya mifupa, viungo na gegedu, hivi vidonge vimetumiwa na watu wengi na matokeo yake ni mazuri sana, kwa hiyo zifuatazo ni faida za vidonge hivi.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya pyrantel pamoate

Post hii inahusu zaidi dawa ya pyrantel pamoate ni dawa ambayo usaidia kutibu minyoo ambayo kwa kawaida ukaa kwenye utumbo mdogo.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya potassium sparing

Post hii inahusu zaidi dawa ya potassium sparing katika matibabu ya magonjwa ya moyo.

Soma Zaidi...