Fahamu dawa za kutuliza aleji au mzio
Post hii inahusu zaidi dawa hydrocortisone kwa kutuliza aleji au mzio, kwa kawaida Kuna mda mtu anapotumia dawa Fulani anakuwa na mabadiliko mbalimbali kama vile kifua kubana , viupele na mambo kama hayo.
Fahamu dawa ya kutuliza aleji .
1. Kama tunavyofahamu kila mtu Kuna kitu ambacho huwa anakitumia na hakipatani na mwili wake kwa sababu Kuna wakati mwingine mwili huwa na viupele mtu anaanza kujikuna, au pengine kifua kinaanza kubana na mambo kama hayo kwa hiyo hali hiyo ikibadilika dawa ya hydrocortisone usaidia kuzuia aleji hasa zinazosababisha na dawa.
2. Dawa hiyo ufanya Kazi ya kutuliza aleji kwa kupambana na hali hiyo au kitu hicho na kukizuia kuleta madhara kwenye mwili wa binadamu, kwa wagonjwa wa asthma mara nyingi huwa na aleji ambazo uwasababishia kifua kubana na pengine kupumua vibaya kwa kutumia dawa ya hydrocortisone hali uweza kuwa ya Kawaida .
3. Dawa hizi utolewa kwa kupulizia mgonjwa kwenye mfumo wa hewa na nyingine zinaweza kupitia kwenye mishipa na pia Kuna nyingine ambazo upewa kwa kumeza na pia zote ufanya kazi Ile Ile ya kusaidia mtu mwenye aleji.
4. Dawa hii ya hydrocortisone Ina milligrams tano ambazo utolewa kwa watoto na milligrams kumi kwa watu wazima na pia utolewa kila baada ya masaa sita mpaka dozi inaisha ,pia dozi yenyewe pamoja na kutegemea umri na pia utegemea uzito wa mtu mmoja na mwingine.
5. Pia dawa hii utolewa kwa watu mbalimbali ila Kuna watu ambao Wana aleji na dawa hii hawapaswi kuitumia au kwa wale wenye presha ya kupanda wanapaswa kutumia dawa hii kwa ushauri wa wataalamu wa afya.
6. Vile vile dawa hii Ina maudhi madogo madogo kama vile mapigo ya moyo kwenda mbio na pia wakati mwingine kuishiwa nguvu na maumivu ya kichwa kwa hiyo tunapaswa kuitumia kwa utaratibu wa wataalamu wa afya.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 kitabu cha Simulizi 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Fahamu zaidi kuhusiana na Dawa inayotibu shinikizo la damu. iitwayo LASIX
Lasix (Furosemide) iko katika kundi la dawa zinazoitwa vidonge vya maji (loop diuretics) vidonge vya maji. Lasix hutumiwa kupunguza uvimbe mwilini unaosababishwa na kushindwa kwa moyo, ugonjwa wa ini, au ugonjwa wa figo. Kwa matibabu ya dalili nyingi.La
Soma Zaidi...Neno la awali
Asalaamu alykum warahmatullah wabarakaatuh Sifanjema zinamstahikia Allah Mola wa viumbe, muumba wa mbingu na ardhi na vilivyomo.
Soma Zaidi...Penicillin dawa ya kutibu maambukizi ya bakteria mwilini
Post hii Inahusu zaidi dawa za kutibu maambukizi yoyote Yale yanayosababishwa na bakteria dawa hizi kwa kitaamu huiitwa antibiotics Kuna dawa mbalimbali zinazotibu maambukizi ya bakteria leo tutaanza na dawa ambayo inaitwa penicillin.
Soma Zaidi...Miungurumo haiishi tumboni nikishika upande wa kushoto wa tumbo kuna maumivu kwa mbali je mm nitumie dawa gan kuondoa tatizo hilo
Kukawa na gesi tumboni kunaweza kuwa ni dalili ya shida kwenye afya, hasa katika mfumo wa chakula. Hali itakuwa sio nzuri endapo utakosea hamu ya kula na kuhisivkushiba muda wowote.
Soma Zaidi...Dawa ya fangasi na dalili za fangasi
hapa utajifunza dalili za fangasi, dawa ya fangasi na aina za fangasi, pia nitakujuza njia za kukabiliana na fangasi
Soma Zaidi...Fahamu dawa ya ibuprofen katika kutuliza maumivu
Post hii inahusu zaidi dawa ibuprofen katika kutuliza maumivu, ni aina mojawapo ya dawa na yenyewe ufanya kazi kama aspirin na paracetamol
Soma Zaidi...