DART somola 42: Asynchronous programming
Katika somo hili tutakwenda kujifunza concept nyingine ya asynchronous programming.
Asynchronous programming hii ni njia ya kuandika code ambazo zinaruhusu program kufanya kazi nyingi kwa wakati mmoja. Kama vile kusoma na kuandika taarifa za database kutoka kwenye internet, kusoma faili na kudownload. Hizi ni baadhi ya task ambazo hazihitaji kuw ainterrupted.
Synchronous programming hapa program ita run mstari baada ya mstari mara moja tu. ni kwa sababu hapa inahitaji shughuli zote zikamilike ndipo program ielekee kwenye shughuli inayofuata.
Mfano:
void main() {
print("mwanzo");
print("kati");
print("mwisho");
}
Hapo program itaanza na mstari mw akwanza kisha itaprint unaofuata kisha unaofuata mpaka mwisho. Hii ni tofauti na asynchronous ambapo program itaendelea ku print mstari unaofuata bila ya kupoteza muda mapaka imalize shughuli za mstari uliotangulia.
Hivyo tunasema synchronous programming inahitaji kusubiria lakini asynchronous programming haihitaji kusubiria. Hivyo basi asynchronous programming huboresha program.
Mfano wa asynchronous:
void main() {
print("mwanzo");
Future.delayed(Duration(seconds:3),()=>print('kati'));
print("mwisho");
}
Utaona hapo mstari unaoandika kati umetangulia lakini program imeprint mwisho. Hivyo iliendelea mstari unaofuata bila hata ya kusubiria mstari wa nyuma u print.
Kwa nini tunahitaji asynchronous
- Kwa ajili ya kusoma data kwenye insternet
- Kwa ajili ya kuandika data kwenye database
- Ku run program ambazo zinatumia uda mrefefu
- Kusoma data kwenye faili
- Ku download
- Na mengineyo mengi
Ili uweze kutumia asynchronous unatakiw akutumia class inayoitwa future pamoja na keyword kama async na wait. Tutajifunza zaidi kwenye somo linalofuata.
Baadhi ya misemo muhimu ambayo hutumika:
- Synchronous operation hizi ni zile operation (shuguli za program) ambazo huzuia program kufanya shughuli nyingine kabla ya kukamilisha shughuli za nyuma.
- Synchronous function hizi ni function ambazo hufanya synchronous operation
- Asynchronous operation ni operation ambazo zinaruhusu shuguli nyingine kufanyika kabla ya nyingine
- Asynchronous function ni function zinazofanya kazi kwenye asynchronous operation
Mwisho:
Katika somo linalofuata utakwenda kujifunza kuhusu future class kwenye dart.
Future class
Katika somo hili utakwenda ujifunza kuhusu future class na jinsi ambavyo itakavyotumika kwenye dart.
Katika dart future huwakilisha value (thamani) ama error (tatizo) ambalo bado halijatokea, ila hutarajiwa kutokea wakati ujao.
Kwenye dart future hutengenezwa kwa kutumia future class. Hapa mwenyewe utachaguwa je itakee muda gani hiyo operation. Unaweza...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Simulizi za Hadithi Audio 👉2 web hosting 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
DART somo la 18: Dart method zinazotumika kwenye List data type
Katika somo hili utakwenda kujifunza method yhinginge zinazofanya kazi kwenye list data type kwenye Dart.
Soma Zaidi...DART somo la 20: method zinazotumika kwenye map data type kwenye Dart
Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu method ambazo hutumika kwenye map data type
Soma Zaidi...DART - somo la 1: Kazi za dart programming na historia yake
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu kazi za dart language. Pia nimekuandalia istoria fupi ya lugha ya DART.
Soma Zaidi...DART somo la 32: Inheritance kwenye construct method:
Katika masomo yaliopita tumesha jifunza jinsi inheritance inavyokuwa, ila hatujaona kwa namna gani utaweza ku inherit constructor method. Somo hili litashughulika na swla hilo.
Soma Zaidi...DART somo la 44: Jinsi ya ku install mysql kwenye program ya dart
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuunganisha databse na Dart. Pia utajifunza jinsi ya kuset environment kwenye kompyuta ili kuweza kutumia Dart sdk kwenye CMD.
Soma Zaidi...Dart somo la 26: DART OOP maana ya object, na jinsi ya kuitengeneza kwenye OOP
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza Object pamoja na properties. Haa kwa ufupi tutakwenda kujifunza jinsi ya kutumia class.
Soma Zaidi...