picha

DART somola 42: Asynchronous programming

Katika somo hili tutakwenda kujifunza concept nyingine ya asynchronous programming.

Asynchronous programming hii ni njia ya kuandika code ambazo zinaruhusu program kufanya kazi nyingi kwa wakati mmoja. Kama vile kusoma na kuandika taarifa za database kutoka kwenye internet, kusoma faili na kudownload. Hizi ni baadhi ya task ambazo hazihitaji kuw ainterrupted.

 

Synchronous programming hapa program ita run mstari baada ya mstari mara moja tu. ni kwa sababu hapa inahitaji shughuli zote zikamilike ndipo program ielekee kwenye shughuli inayofuata.

Mfano:

void main() {

 print("mwanzo");

 print("kati");

 print("mwisho");

}

Hapo program itaanza na mstari mw akwanza kisha itaprint unaofuata kisha unaofuata mpaka mwisho. Hii ni tofauti na asynchronous ambapo program itaendelea ku print mstari unaofuata bila ya kupoteza muda mapaka imalize shughuli za mstari uliotangulia.

 

Hivyo tunasema synchronous programming inahitaji kusubiria lakini asynchronous programming  haihitaji kusubiria. Hivyo basi asynchronous programming huboresha program.

Mfano  wa asynchronous:

void main() {

 print("mwanzo");

 Future.delayed(Duration(seconds:3),()=>print('kati'));

 print("mwisho");

}

 

Utaona hapo mstari unaoandika kati umetangulia lakini program imeprint mwisho. Hivyo iliendelea mstari unaofuata bila hata ya kusubiria mstari wa nyuma u print.

Kwa nini tunahitaji asynchronous

  1. Kwa ajili ya kusoma data kwenye insternet
  2. Kwa ajili ya kuandika data kwenye database
  3. Ku run program ambazo zinatumia uda mrefefu
  4. Kusoma data kwenye faili
  5. Ku download
  6. Na mengineyo mengi

 

Ili uweze kutumia asynchronous unatakiw akutumia class inayoitwa future pamoja na keyword kama async na wait. Tutajifunza zaidi kwenye somo linalofuata.

 

Baadhi ya misemo muhimu ambayo hutumika:

  1. Synchronous operation hizi ni zile operation (shuguli za program) ambazo huzuia program kufanya shughuli nyingine kabla ya kukamilisha shughuli za nyuma.
  2. Synchronous function hizi ni function ambazo hufanya synchronous operation
  3. Asynchronous operation ni operation ambazo zinaruhusu shuguli nyingine kufanyika kabla ya nyingine
  4. Asynchronous function ni function zinazofanya kazi kwenye asynchronous operation

 

Mwisho:

Katika somo linalofuata utakwenda kujifunza kuhusu future  class kwenye dart.

 

 Future class

Katika somo hili utakwenda ujifunza kuhusu future class na jinsi ambavyo itakavyotumika kwenye dart.

 

Katika dart future huwakilisha value (thamani) ama error (tatizo) ambalo bado halijatokea, ila hutarajiwa kutokea wakati ujao.

 

Kwenye dart future hutengenezwa kwa kutumia future class. Hapa mwenyewe utachaguwa je itakee muda gani hiyo operation. Unaweza...

Ingia sasa ili uweze kusoma makala hii yote.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: DART Main: Masomo File: Download PDF Views 1347

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 ai web app     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

DART somo la 36: Abstract class kweye Dart

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu abstract class na abstract method kwenye Dart.

Soma Zaidi...
DART somo la 4: Jinsi ya kuandika na kutumia variable kwenye Dart

Katika somo lililopita tumejifunza kuhusu sintaksia za dart. Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza variable kwenye Dart.

Soma Zaidi...
DART somo la 2: syntax za dart

Katika somo hili tutatkwenda kuziona baadhi ya xyntax yaani kanunu za uandishi wa code za dart.

Soma Zaidi...
DART somo la 34: Static variable kwenye Dart

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu static property na jinsi ambavyo inavyotumika.

Soma Zaidi...
DART somo la 6: Dart operator na jinsi zinavyofanya kazi.

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu operator kwenye Dart, kazi zake na jinsi ya kuzitumia.

Soma Zaidi...
DART somo la 45: Jinai ys kutuma mysql database

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia database ya mysql kwenye Dart. hakikisha umeelewa vyema na kutekeleza yalioelekezwa kutoka kwenye somo lililopita.

Soma Zaidi...