Damu, uteute na maji yanayotoka ukeni kipindi cha ujauzito

Damu, uteute na maji yanayotoka ukeni kipindi cha ujauzito

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu damu, uteute na maji yanayotoka ukeni kipindi cha ujauzito

Download Post hii hapa

DAMU NA UTEUTE NA MAJIMAJI YANAYOTOKA UKENI WAKATI WA UJAUZITO:

Majimaji yanayotoka ukeni wakati wa ujauzito (Damu na uteute)Ni kawaida kwa mjamzito kushuhudia kwenye uke wake kutokwa na kama uteute na huongezeka kila mimba inapoendelea kukomaa. Wakatiflani anaweza kuona nguo zake zina madoa ya damu, ama akashuhudia matone kadhaa ya damu. Wapo pia wanaingia hedhi kwa damu chache. Sasa hebu tuangalie kwa ufupi hali hizi:-

 

1.Baada ya kutoka hedhi uke wa mwanamke unakuwa mkavu bila ya kuwa na utelezi telezi. Hiki ni kipindi ambacho mwanamke hawezi kubeba ujauzito. Katika kipindi hiki hata akitia kidole hakitoki na utelezitelezi. Kipindi hiki kinaweza kuchukuwa takribani siki tano hadi 10 inategemea na mzunguruko wa mwanamke. Huu ni kuda mzuri wa kushiriki tendo kwa wale ambao hawahitaji kulea ujauzito.

 

2.Zitakapoanza kuingia siku hatari mwanamke ataanza kuhisi uwepo wa uteute kwenye uke wake anapotia kidole kwa ndani. Siku hizi pia zinatofautiana kulingana na idadi ya mzunguruko. Ila zinaweza kuazia siku ya 11 hadi 14 inaweza pia kuwa chini ya papo lwa baadhi ya wanawake ama juu ya hapo.

 

3.Siku moja kabla ya kukomaa kwa yai na kuwa tayari kwenye mirija ya falopian tayari kutungisha mimba, uteute huu huongezeka zaidi. Sifa za uteute huu ni kuwa ni wenye kuteleza sana ila sio mzito na wenye kunatanata ama kuvutikana. Kwa wanaotumia njia za uzazi wa mpango hasa zile za homoni uteute wao upo muda wowote kwa hiyo ni ngumu sana kwao kuiona hali hii.

 

4.Siku ya hatario zaidi mwanamke atapata mabadiliko ya hamu ya kutaka kushiriki tendo la ndoa. Yaani hamu itaongezeka zaidi siku hii kuliko siku iliyotangulia. Hapa kwa wale ambao hawataki ujauzito sio siku salama kwao kushiriki tendo landoa.

 

5.Uteute huu katika siku hizi kuandaliwa kwa ajili ya kusaidia mbegu za kiume ziweze kusafiri vyema, kuogelea vyema na kulifikia yai. Pia kuhakikisha kuwa mbegu za kiume haziathiriwi na asidi ya tumboni kwa mama kwa kiasi kikubwa. Hivyo uteute huu katika kipindi hiki ni muhimu sana.

 

6.Kali hii inaweza kudumu kwa masiku kadhaa toka 14 hadi 17 kwa makadirio inaweza kupungua ama kuongezeka kulingana na mzunguruko wa mwanamke. Baada ya hapo kama mwanamke alibeba ujauzito majimaji haya yanaongezeka uzito saa na kuwa yenye kunata na kufanana na utelezi wa yai pindi unapolibanja. Baada ya mimba majimaji haya yataendelea kutoka na kuongezeka na kuwa mazito zaidi hadi atakapojifungua.

 

Katika ujauzito majimaji haya yanakazi ya kulinda njia ya kuingilia kwenye mji wa mimba dhidi ya mashambulizi na aambukizi ya bakteria. Yaani kuhakikisha kuwa hakuba bakteria ama fangasi atakayeweza kuingia na kumzuru mtoto tumboni.

 

7.Kama hakuna ujauzito uliobebwa majimaji yataanza kurudi kutoka hali yake ya kawaida na kuwa safi, yenye harufu kwa mbali ila si harufu ya kukera, pia yanaweza kuwa na rangi ya maziwa hivi.

 

Majimaji haya pia nayaweza kuashiria shida kwenye afya endapo yatakuwa na sifa hizi:-A.Yana rangi ya njao, kijani ama buluuB.Yana harufu kali mbayaC.Yanakusababishia muwasho kwenye uke na mashavu ya ukeD.Yanakusababishia kuvimba kwa uke na mashavu ya uke

 

8.Ama kuhusu kutokwa na damu, ikiwa chache ni kawaida. Ikiwa unaambatana na maumivu makali ya tumbo, ama maumivi makali ya kichwa na homa, basi vyema kumuona daktari kwa ushauri zaidi. Kama nilivtotangulia kusema kuna wanawake wanapata hedhi wakiwa wajawazito. Wenyewe wanaita kupunguzia, kwa ufupi hii si hedhi na pia haiashirii kama kuna tatizo. Ila kama inatoka nyingi na kuambatana na maumivu yasiyo ya kawaida ni vyema kumuona daktari

Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 3216

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Dali za udhaifu wa mbegu za kiume.
Dali za udhaifu wa mbegu za kiume.

Posti hii inahusu zaidi Dalili ambazo zinaweza kujitokeza na zikaonesha kwamba mbegu za kiume ni dhaifu au ni chache.

Soma Zaidi...
Je siku ya kwanza kabisa ya ovulation mimba inakuwa ni uhakika kupata mimba?
Je siku ya kwanza kabisa ya ovulation mimba inakuwa ni uhakika kupata mimba?

Watu wengi wanadhania kuwa kufanya tendo la ndoa katika siku hatari ni lazima kuwa utapata ujauzito. Hili sio sahihi kabisa. Post hii itakwenda kuangalia jambo hili zaidi.

Soma Zaidi...
Maumivu ya tumbo wakati wa tendo la ndoa
Maumivu ya tumbo wakati wa tendo la ndoa

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo wakati wa tendo la ndoa

Soma Zaidi...
Njia za kuzuia Malaria kwa wajawazito
Njia za kuzuia Malaria kwa wajawazito

Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuzuia Malaria kwa wajawazito na watoto wao wakiwa bado tumboni, tunajuwa wazi kuwa wajawazito wakipata Malaria inaweza kupelekea mimba kutoka kwa hiyo ili kuzuia tatizo hili zifuatazo ni njia zilizowekwa ili kuz

Soma Zaidi...
siku za hatari
siku za hatari

Hizi ni siku za hatari kupata ujauzito.Siku hizi ndio siku za kupata mimba kwa urahisi

Soma Zaidi...
 Fahamu Faida za Uzazi wa mpango
Fahamu Faida za Uzazi wa mpango

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Faida za Uzazi wa mpango. Uzazi wa mpango ni huduma ambazo hutoa chaguo kwa familia kuwa na idadi ya watoto wanaotaka katika muda maalum, wanahisi na mbinu iliyoamuliwa.

Soma Zaidi...
Dalili za mwanzo za ujauzito katika wiki ya kwanza
Dalili za mwanzo za ujauzito katika wiki ya kwanza

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za mwanzo za ujauzito katika wiki ya kwanza

Soma Zaidi...
Je ukitokea mchubuko wakati wa ngono unaweza pata ukimwi?
Je ukitokea mchubuko wakati wa ngono unaweza pata ukimwi?

Kupata Ukimwi ama HIV hufungamana na mambo mengi. Si kila anayefanya ngono zembe nabmuathiria naye lazima aathirike. Hiivsibkweli, ila tangu kuwa hali hii ni hatari kwani kupata maambukizi ni rahisi sana.

Soma Zaidi...
Hatari ya kutokwa na damu wakati wa ujauzito
Hatari ya kutokwa na damu wakati wa ujauzito

Posti hii inahusu zaidi hatari za kutokwa na damu wakati wa ujauzito, hali hii utokea wakati wa ujauzito ambapo Kuna baadhi ya wajawazito utokwa na damu jambo ambalo hatupaswi kutarajia kwa sababu tunafahamu kabisa mama akishapata ujauzito na damu zinakom

Soma Zaidi...
Upungufu wa homoni ya cortisol
Upungufu wa homoni ya cortisol

Posti hii inahusu zaidi upungufu wa homoni hii ya cortisol,hii ni homoni ambayo utokana na tezi glang(adrenal gland) kufanya kazi kupitiliza hali ambayo mara nyingi husababishwa na msongo wa mawazo wa mda mrefu, yaani wale watu ambao mda mwingi huwa wenye

Soma Zaidi...