Hukumu ya kufinga kwa kifuata kuandama kwa mwezi

Ni muda gani unatakiwa ufunge ramadhani, je kuandama kwa mwezi kwa kiona ama hata kusiki.

Kuonekana kwa mwezi wa Ramadhani

Swaumu ya Ramadhani inaanza kwa kuona mwezi baada ya siku ya 29 Shaaban au 30 Shaaban kama tunavyofahamshwa katika hadithi zifu atazo:
“Ibn Umar (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: Msifunge mpaka muuone mwezi umeandama na msiache kufunga mpaka muone mwezi (wa Shawwal) umeandama. Kama kuna mawingu (hukuuona) hesabu kamili (siku 30). Katika simulizi nyingine amesema: Mwezi una masiku 29, kwa hiyo usifunge mpaka uone mwezi umeandama kama kuna mawingu subiri na kamilisha idadi ya siku 30.”
(Bukhari na Muslim)

 


Kutokana na Hadithi hii ni wazi kuwa watu hawaruhusiwi kufunga kwa kufuata kalenda. Inabidi juhudi za kuuangalia mwezi ziwepo kwa umma wa Waislamu tangu mwanandamo wa Shaaban.

 


“Abu Hurairah (r.a) ameeleza kuw a Mtume w a Allah ameagiza: Hesabu mwandamo wa Shaaban kwa ajili ya Ramadhani”. (Tirmidh).

 


Kwanini kufuata mwandamo wa mwezi?

 


Tunafunga kwa kuona mwezi kwa sababu ndivyo alivyotuamrisha Mtume wa Allah (s.w) kama tulivyojifunza kutokana na hadithi zilizonukuliwa hapo juu. Kumtii Mtume (s.a.w) ndio Uislamu. Rejea Qur-an katika aya zifuatazo:

 

“Sema: “Mtiini Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Na mkikengeuka (Allah atakuadhibuni) kwani Allah hawapendi makafiri.” (3:32)

 

“… Na anachokuleteeni Mtume, kipokeeni, na anachowakataza
kiacheni…” (59:7).

 

“Anayemtii Mtume, kwa yakini amemtii Mw enyezi Mungu…” (4:80)

 

Pia amri hii ina hekima yake. Mwaka unaohesabiwa kwa mwandamo wa mwezi una siku 354 kwani kwa wastani mwezi mmoja una siku 29?. Mwaka unaohesabiwa kwa kufuata jua, muda ambao dunia huchukua kulizunguka jua una siku 365, saa 5, dakika 48 na nukta 46. Kwa hiyo ukilinganisha mwaka wa hesabu ya mwezi na mwaka wa hesabu ya jua, utaona kuwa mwaka wa mwezi ni mfupi kwa siku10 hivi. Hivyo mwezi wa Ramadhani hurudi nyuma siku kumi katika kila mwaka ukilinganisha na mwaka wa jua. Hivyo basi, mtu yeyote atakayejaaliwa kufunga muda wa miaka 36 hatakuwa na siku au msimu katika mwaka ambao hakuufunga. Yaani atawahi kufunga siku zote za jua, za mvua, za upepo, za shwari, za kusi, za kaskazi na kadhalika. Kama ingelikuwa inafuatwa kalenda ya mwaka wa jua, wengine daima wangalifunga nyakati za joto tu, wengine nyakati za baridi tu, wengine nyakati za njaa tu, wengine nyakati za mavuno na kadhalika ilimuradi pasingalikuwa na mabadiliko.

 

Ni lazima kila mfungaji aone mwezi?

 


Mwezi wa Ramadhani akiona mtu mmoja muadilifu inatosha na wengine waliobaki itawabidi wafunge. Hivi ndivyo alivyoamrisha Mtume (s.a.w) kama tunavyojifunza katika hadithi zifuatazo:

 


“Ibn Abbas (r.a) ameeleza kuwa Mwarabu wa Jangwani alikuja kwa Mtume (s.a.w) akasema: Hakika nimeuona mwezi wa Ramadhani umeandama. Mtume (s.a.w) akamuuliza: Unashuhudia kuw a hapana Mola ila Allah? “Ndio” alijibu. Akamuuliza tena: Unashuhudia kuwa Muhammad ni Mtume w a Allah? Akajibu “Ndio ”. Akasema (Mtume): Ee Bilal! Watangazie w atu kuw a haw ana budi kufunga kesho”. (Abu Daud, Tirm idh, Nisa i, Ibn Majah).

 


“Ibn Omar (r.a) ameeleza: Watu waliuona mwezi. Kisha nikamfahamisha Mtume (s.a.w): Hakika nimeuona. Kwa hiyo alifunga na aliwaamrisha watu wafunge”. (Abu Daud, Darimi).

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1308

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Uislamu unavyokemea tabia ya ombaomba

Uislamu umekataza tabia ya kuombaomba kama ndio njia ya kuendesha maisha. Pia ukaweka suluhisho la kukomesha tabia hiyo

Soma Zaidi...
Jinsi ya kuelekea qibla katika swala.

Je unadhani ni kwa nini waislamu wanaelekea kibla, na jinsi gani utaweza kukipata kibla.

Soma Zaidi...
Kusimamisha Swala na kuamrisha mema

Swala iliyosimamishwa vilivyo ndiyo nyenzo kuu ya kumtakasa Muislamu na kumpa sifa zinazomuwezesha kustahiki kufanya kazi takatifu ya kusimamisha Uislamu katika jamii.

Soma Zaidi...
Swala ya tahiyatul masjidi yaani maamkizi ya msikitini, pamoja na swala za qabliya na baadiya

Post hii inakwenda kukujuza kuhusu swala za qabliya, baadiya na tahiyatul masjid.

Soma Zaidi...
Ufumbuzi wa tatizo la riba.

Uislamu ndio dini pekee ambayo inatoa ufumbuzi juu ya suala la riba.

Soma Zaidi...