Posti hii inahusu zaidi visababishi vya ugonjwa wa Bawasili,kuna watu wengi wanapenda kujua kabisa chanzo cha kuwepo kwa ugonjwa wa Bawasili kwenye jamii na kuna maswali mengi yanayoulizwa kuhusu visababishi vya Bawasili.
1. Kufunga choo au kukosa choo kwa mda mrefu.
Hii ni sababu ya kwanza kabisa kwa sababu kuna watu ambao hawapati choo au wanabana choo kwa mda mrefu na usababisha kuwepo kwa Bawasili.
2. Wakati wa ujauzito.
Wakati wa ujauzito kuna uwezekano wa kupata ugonjwa wa Bawasili kwa sababu ya kuwepo kwa mgandamizo wa mtoto kupelekea kwenye na sehemu ya haja kubwa , na pia wakati wa kujifungua mtoto anakandamiza sana sehemu ya haja kubwa.
3. Kufanya mapenzi kinyume cha maumbile.
Kuna kipindi watu wanapenda kufanya mapenzi kwenye sehemu ya haja kubwa hali ambayo upelekea kuwepo kwa Bawasili.
4. Uzee.
Pia nao wana uwezekano wa kupata tatizo hili la Bawasili kwa sababu mtu akiweka na kinga za mwili zinashuka hali ambayo Usababisha kupata ugonjwa huu.
5. Pia kuna sababu za kurithi.
Kwa kawaida kuna familia ambayo upata ugonjwa huu mara kwa mara kutoka kwa babu , baba na majukumu kwa hiyo kuna uwezekano wa kupata kama ugonjwa umo kwenye familia.
6. Kuharisha sana na kwa mda mrefu.
Kuna watu ambao wanapatwa na tatizo la kuharisha sana na kwa mda mrefu nao wana uwezekano wa kupata ugonjwa huu wa Bawasili.
7. Matumizi ya vyoo vya kukalia.
Kuna uwezekano mkubwa wa kupata ugonjwa huu kwa sababu ya matumizi ya vyoo vya kukalia kwa mda mrefu ingawa sio wote wanaotumia vyoo hivi kupata Bawasili.
8. Kunyanyua vitu vizito.
Kuna wakati mwingine watu wenye tabia ya kunyanyua vitu vizito wamo hatarini kupata ugonjwa huu wa Bawasili.
9. Kuwepo kwa mfadhaiko au stress.
Kwa kuwepo kwa mfadhaiko wa mara kwa mara usababisha magonjwa mbalimbali ikiwemo na Bawasili.
10. Kuwepo kwa uzito mkubwa na unene wa kupitiliza, kwa kawaida watu wanene na wenye uzito uliopitiliza usababisha kuwepo kwa magonjwa mbalimbali na wako hatarini kupata Bawasili.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Post hii inahusu Zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea Kwa mgonjwa mweye usaha kwenye mapafu.
Soma Zaidi...Saratani ya Mapafu ni aina ya Kansa inayoanzia kwenye mapafu. Mapafu yako ni viungo viwili vya sponji kwenye kifua chako ambavyo huchukua oksijeni unapovuta na kutoa kaboni dioksidi unapotoa nje.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi tatizo la fizi kuachana, ni tatizo ambalo uwakumba watu wengi kwa wakati mwingine unakuta fizi zimeachana kutoka sehemu moja kwa nyingine kwa hiyo tunaweza kuona sababu kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za vidonda vya tumbo sugu
Soma Zaidi...Je unahitaji kujuwa kama umepata ujauzito baada ya kufanya tendo la ndoa? hakika sio rahisi ila kama utakuwa makini utaweza.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za matibabu ya ugonjwa wa saratani,ni ugonjwa ambao unaweza kupona ikiwa umegundulika mapema katika hatua za mwanzo na kama ugonjwa huu umefikia hatua za mwisho Tiba yake huwa ni kupunguza makali ya ugonjwa.
Soma Zaidi...