picha

Bawasili usababishwa na nini?

Posti hii inahusu zaidi visababishi vya ugonjwa wa Bawasili,kuna watu wengi wanapenda kujua kabisa chanzo cha kuwepo kwa ugonjwa wa Bawasili kwenye jamii na kuna maswali mengi yanayoulizwa kuhusu visababishi vya Bawasili.

Visababishi vya ugonjwa wa Bawasili.

1. Kufunga choo au kukosa choo kwa mda mrefu.

Hii ni sababu ya kwanza kabisa kwa sababu kuna watu ambao hawapati choo au wanabana choo kwa mda mrefu na usababisha kuwepo kwa Bawasili.

 

2. Wakati wa ujauzito.

 Wakati wa ujauzito kuna uwezekano wa kupata ugonjwa wa Bawasili kwa sababu ya kuwepo kwa mgandamizo wa mtoto kupelekea kwenye na sehemu ya haja kubwa , na pia wakati wa kujifungua mtoto anakandamiza sana sehemu ya haja kubwa.

 

3. Kufanya mapenzi kinyume cha maumbile.

Kuna kipindi watu wanapenda kufanya mapenzi kwenye sehemu ya haja kubwa hali ambayo upelekea kuwepo kwa Bawasili.

 

4. Uzee.

Pia nao wana uwezekano wa kupata tatizo hili la Bawasili kwa sababu mtu akiweka na kinga za mwili zinashuka hali ambayo Usababisha kupata ugonjwa huu.

 

5. Pia kuna sababu za kurithi.

Kwa kawaida kuna familia ambayo upata ugonjwa huu mara kwa mara kutoka kwa babu , baba na majukumu kwa hiyo kuna uwezekano wa kupata kama ugonjwa umo kwenye familia.

 

6. Kuharisha sana na kwa mda mrefu.

Kuna watu ambao wanapatwa na tatizo la kuharisha sana na kwa mda mrefu nao wana uwezekano wa kupata ugonjwa huu wa Bawasili.

 

7. Matumizi ya vyoo vya kukalia.

Kuna uwezekano mkubwa wa kupata ugonjwa huu kwa sababu ya matumizi ya vyoo vya kukalia kwa mda mrefu ingawa sio wote wanaotumia vyoo hivi kupata Bawasili.

 

8. Kunyanyua vitu vizito.

Kuna wakati mwingine watu wenye tabia ya kunyanyua vitu vizito wamo hatarini kupata ugonjwa huu wa Bawasili.

 

9. Kuwepo kwa mfadhaiko au stress.

Kwa kuwepo kwa mfadhaiko wa mara kwa mara usababisha magonjwa mbalimbali ikiwemo na Bawasili.

 

10. Kuwepo kwa uzito mkubwa na unene wa kupitiliza, kwa kawaida watu wanene na wenye uzito uliopitiliza usababisha kuwepo kwa magonjwa mbalimbali na wako hatarini kupata Bawasili.

 

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2563

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game     👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉3 web hosting     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 ai web app     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

Fahamu Ugonjwa wa kipindupindu.

Kipindupindu ni ugonjwa wa bakteria ambao kawaida huenezwa kupitia maji machafu. Kipindupindu husababisha Kuhara na Upungufu wa maji mwilini.

Soma Zaidi...
vidonda vya tumbo, dalili zake, chanzo chake na tiba yake

Makala hii itakwenda kukupa elimu juu ya vidonda vya tumbo, nini hasa chanzo chake, vipi vinatokea ni zipi dalili zake, ni zipi njia za kujilinda dhidi ya vidonda vya tumbo. Pia tutaangalia matibabu ya kutibi vidonda vya tumbo.

Soma Zaidi...
Dalili za coma

Coma ni hali ya kupoteza fahamu kwa muda mrefu ambayo inaweza kusababishwa na matatizo mbalimbali Jeraha la kichwa , Kiharusi, Tumor ya ubongo, ulevi wa dawa za kulevya au pombe, au hata ugonjwa wa msingi, kama vile Kisukari au maambukizi.

Soma Zaidi...
Je pumu inaweza kusababishwa na virusi ama bakteria?

Hapa utakwenda kujifunza jinsi ambavyo pumu inaweza kuwa na mahusiano kwa kuwepo kwa aina flani ya bakteria ama virusi.

Soma Zaidi...
Je utambuzi wa maambukizi ya ukimwi hupatikana mda gani pale mtu anapoambukizwa

Kuna ukimwi na HIV na kila kimoja kina dalili zake na muda wa kuonyesha hizo dalili.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kujilinda na maradhi ya ini

Hapa nitakueleza namna ambavyounaweza kupunguza hatari ya kupata maradhi ya ini. Kwa njia hizi unaweza kujikina wewe na wengineo na maradhi haya hatari ya ini.

Soma Zaidi...