Bawasili usababishwa na nini?
Posti hii inahusu zaidi visababishi vya ugonjwa wa Bawasili,kuna watu wengi wanapenda kujua kabisa chanzo cha kuwepo kwa ugonjwa wa Bawasili kwenye jamii na kuna maswali mengi yanayoulizwa kuhusu visababishi vya Bawasili.
Visababishi vya ugonjwa wa Bawasili.
1. Kufunga choo au kukosa choo kwa mda mrefu.
Hii ni sababu ya kwanza kabisa kwa sababu kuna watu ambao hawapati choo au wanabana choo kwa mda mrefu na usababisha kuwepo kwa Bawasili.
2. Wakati wa ujauzito.
Wakati wa ujauzito kuna uwezekano wa kupata ugonjwa wa Bawasili kwa sababu ya kuwepo kwa mgandamizo wa mtoto kupelekea kwenye na sehemu ya haja kubwa , na pia wakati wa kujifungua mtoto anakandamiza sana sehemu ya haja kubwa.
3. Kufanya mapenzi kinyume cha maumbile.
Kuna kipindi watu wanapenda kufanya mapenzi kwenye sehemu ya haja kubwa hali ambayo upelekea kuwepo kwa Bawasili.
4. Uzee.
Pia nao wana uwezekano wa kupata tatizo hili la Bawasili kwa sababu mtu akiweka na kinga za mwili zinashuka hali ambayo Usababisha kupata ugonjwa huu.
5. Pia kuna sababu za kurithi.
Kwa kawaida kuna familia ambayo upata ugonjwa huu mara kwa mara kutoka kwa babu , baba na majukumu kwa hiyo kuna uwezekano wa kupata kama ugonjwa umo kwenye familia.
6. Kuharisha sana na kwa mda mrefu.
Kuna watu ambao wanapatwa na tatizo la kuharisha sana na kwa mda mrefu nao wana uwezekano wa kupata ugonjwa huu wa Bawasili.
7. Matumizi ya vyoo vya kukalia.
Kuna uwezekano mkubwa wa kupata ugonjwa huu kwa sababu ya matumizi ya vyoo vya kukalia kwa mda mrefu ingawa sio wote wanaotumia vyoo hivi kupata Bawasili.
8. Kunyanyua vitu vizito.
Kuna wakati mwingine watu wenye tabia ya kunyanyua vitu vizito wamo hatarini kupata ugonjwa huu wa Bawasili.
9. Kuwepo kwa mfadhaiko au stress.
Kwa kuwepo kwa mfadhaiko wa mara kwa mara usababisha magonjwa mbalimbali ikiwemo na Bawasili.
10. Kuwepo kwa uzito mkubwa na unene wa kupitiliza, kwa kawaida watu wanene na wenye uzito uliopitiliza usababisha kuwepo kwa magonjwa mbalimbali na wako hatarini kupata Bawasili.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 web hosting 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Usafi wa ukeni: Njia sahihi za kuepuka fangasi.
Fangasi wa ukeni (Vaginal Candidiasis) ni tatizo linalotokana na ukuaji wa kupita kiasi wa vimelea aina ya Candida. Ingawa uke una uwezo wa kujisafisha wenyewe kwa kutumia bakteria rafiki (Lactobacilli), mabadiliko ya mazingira ya uke yanaweza kuvuruga uwiano huo na kusababisha maambukizi. Makala hii inatoa mwongozo wa kitaalamu kuhusu namna bora ya kutunza usafi wa uke ili kuzuia fangasi na kudumisha afya ya uzazi.
Soma Zaidi...Vyakula Muhimu kwa Mama Mjamzito
Ujauzito ni kipindi cha kipekee kinachohitaji uangalizi maalum wa lishe. Makala hii inaangazia vyakula muhimu ambavyo kila mama mjamzito anapaswa kuzingatia ili kuhakikisha afya yake na ukuaji bora wa mtoto aliyepo tumboni.
Soma Zaidi...Dalili za moyo kutanuka
Posti hii inahusu zaidi dalili mbalimbali ambazo zinaweza kujitokeza na kuonyesha kwamba moyo umetanuka.
Soma Zaidi...Visababishi vya maambukizi kwenye milija na ovari
Posti hii inahusu zaidi visababishi vya maambukizi kwenye milija na, ni mambo yanayosababisha maambukizi kwenye milija na ovari.
Soma Zaidi...Dalili za malaria
Malaria ni ugonjwa unaosababishwa na mdudu kwa kitaalamu anaitwa Anopheles.na anasambazwa na mbu jike pale anapotafuta chakula hasa wakati akiwa na mimba. Mbu hawa hupenda kuishi kwenye mnyasi, madibwi haswa kwenye maji yaliyo simama.
Soma Zaidi...Bipolar disorders
Bipolar disorder ni hali ya afya ya akili inayohusisha mabadiliko makubwa katika hisia, nishati, na shughuli za kila siku za mtu. Dalili za bipolar disorder zinaweza kuwa kwenye kipindi cha mania na kipindi cha unyogovu, zifuatazo ni dalili za ugonjwa wa bipolar.
Soma Zaidi...