Bawasili usababishwa na nini?
Posti hii inahusu zaidi visababishi vya ugonjwa wa Bawasili,kuna watu wengi wanapenda kujua kabisa chanzo cha kuwepo kwa ugonjwa wa Bawasili kwenye jamii na kuna maswali mengi yanayoulizwa kuhusu visababishi vya Bawasili.
Visababishi vya ugonjwa wa Bawasili.
1. Kufunga choo au kukosa choo kwa mda mrefu.
Hii ni sababu ya kwanza kabisa kwa sababu kuna watu ambao hawapati choo au wanabana choo kwa mda mrefu na usababisha kuwepo kwa Bawasili.
2. Wakati wa ujauzito.
Wakati wa ujauzito kuna uwezekano wa kupata ugonjwa wa Bawasili kwa sababu ya kuwepo kwa mgandamizo wa mtoto kupelekea kwenye na sehemu ya haja kubwa , na pia wakati wa kujifungua mtoto anakandamiza sana sehemu ya haja kubwa.
3. Kufanya mapenzi kinyume cha maumbile.
Kuna kipindi watu wanapenda kufanya mapenzi kwenye sehemu ya haja kubwa hali ambayo upelekea kuwepo kwa Bawasili.
4. Uzee.
Pia nao wana uwezekano wa kupata tatizo hili la Bawasili kwa sababu mtu akiweka na kinga za mwili zinashuka hali ambayo Usababisha kupata ugonjwa huu.
5. Pia kuna sababu za kurithi.
Kwa kawaida kuna familia ambayo upata ugonjwa huu mara kwa mara kutoka kwa babu , baba na majukumu kwa hiyo kuna uwezekano wa kupata kama ugonjwa umo kwenye familia.
6. Kuharisha sana na kwa mda mrefu.
Kuna watu ambao wanapatwa na tatizo la kuharisha sana na kwa mda mrefu nao wana uwezekano wa kupata ugonjwa huu wa Bawasili.
7. Matumizi ya vyoo vya kukalia.
Kuna uwezekano mkubwa wa kupata ugonjwa huu kwa sababu ya matumizi ya vyoo vya kukalia kwa mda mrefu ingawa sio wote wanaotumia vyoo hivi kupata Bawasili.
8. Kunyanyua vitu vizito.
Kuna wakati mwingine watu wenye tabia ya kunyanyua vitu vizito wamo hatarini kupata ugonjwa huu wa Bawasili.
9. Kuwepo kwa mfadhaiko au stress.
Kwa kuwepo kwa mfadhaiko wa mara kwa mara usababisha magonjwa mbalimbali ikiwemo na Bawasili.
10. Kuwepo kwa uzito mkubwa na unene wa kupitiliza, kwa kawaida watu wanene na wenye uzito uliopitiliza usababisha kuwepo kwa magonjwa mbalimbali na wako hatarini kupata Bawasili.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Madrasa kiganjani π2 Dua za Mitume na Manabii π3 Bongolite - Game zone - Play free game π4 Simulizi za Hadithi Audio π5 ai web app π6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Dalili na namna ya kujizuia na malaria
Postii hii inshusiana na dalili na ishara za kujikinga au kuzuia malaria kwa Njia mbalimbali.
Soma Zaidi...Maumivu ya mgongo (Sciatica): Dalili na mazoezi ya kupunguza.
Sciatica ni hali ya maumivu yanayotokana na shinikizo au kuwasha kwa neva ya sciatic, ambayo ndiyo neva ndefu na kubwa zaidi mwilini mwako. Makala haya yanatoa mwongozo wa kitaalamu kuhusu jinsi ya kutambua dalili za sciatica, sababu za msingi zinazoleta maumivu haya, na mfululizo wa mazoezi yaliyothibitishwa kitabibu kusaidia kupunguza maumivu na kurejesha utendaji wa mwili.
Soma Zaidi...Kisukari cha Aina ya 2: Dalili 10 za awali unazotakiwa kuzijua.
βKisukari cha Aina ya 2 (Type 2 Diabetes) ni janga la kimataifa la kiafya linalokua kwa kasi, huku watu wengi wakiishi na hali hii bila kujijua. Post hii inachunguza kwa kina dalili 10 za awali, ikitoa mwongozo wa kitaalamu wa jinsi ya kutambua mabadiliko ya mwili, umuhimu wa utambuzi wa mapema, na hatua za kuzuia madhara ya muda mrefu kupitia mabadiliko ya mtindo wa maisha.
Soma Zaidi...Dalili za jeraha la kawaida kwenye ubongo
Posti hii inahusu zaidi dalili la jeraha la kawaida kwenye ubongo, jeraha la kawaida utokea kwa sababu mbalimbali kama vile kupata ajali na kugongwa na kitu chochote kichwani,
Soma Zaidi...Ni zipi dalili za awali za pumu
Kabla ya kubanwa zaidi na pumu, kuna dalili za awali zinzznza kujitokeza, na hapo ndipo utakapoanza kuchukuwa tahadhari. Makala hii itakwenda kukujulisha zaidi kuhusu dalili hizo.
Soma Zaidi...