picha

Bawasili usababishwa na nini?

Posti hii inahusu zaidi visababishi vya ugonjwa wa Bawasili,kuna watu wengi wanapenda kujua kabisa chanzo cha kuwepo kwa ugonjwa wa Bawasili kwenye jamii na kuna maswali mengi yanayoulizwa kuhusu visababishi vya Bawasili.

Visababishi vya ugonjwa wa Bawasili.

1. Kufunga choo au kukosa choo kwa mda mrefu.

Hii ni sababu ya kwanza kabisa kwa sababu kuna watu ambao hawapati choo au wanabana choo kwa mda mrefu na usababisha kuwepo kwa Bawasili.

 

2. Wakati wa ujauzito.

 Wakati wa ujauzito kuna uwezekano wa kupata ugonjwa wa Bawasili kwa sababu ya kuwepo kwa mgandamizo wa mtoto kupelekea kwenye na sehemu ya haja kubwa , na pia wakati wa kujifungua mtoto anakandamiza sana sehemu ya haja kubwa.

 

3. Kufanya mapenzi kinyume cha maumbile.

Kuna kipindi watu wanapenda kufanya mapenzi kwenye sehemu ya haja kubwa hali ambayo upelekea kuwepo kwa Bawasili.

 

4. Uzee.

Pia nao wana uwezekano wa kupata tatizo hili la Bawasili kwa sababu mtu akiweka na kinga za mwili zinashuka hali ambayo Usababisha kupata ugonjwa huu.

 

5. Pia kuna sababu za kurithi.

Kwa kawaida kuna familia ambayo upata ugonjwa huu mara kwa mara kutoka kwa babu , baba na majukumu kwa hiyo kuna uwezekano wa kupata kama ugonjwa umo kwenye familia.

 

6. Kuharisha sana na kwa mda mrefu.

Kuna watu ambao wanapatwa na tatizo la kuharisha sana na kwa mda mrefu nao wana uwezekano wa kupata ugonjwa huu wa Bawasili.

 

7. Matumizi ya vyoo vya kukalia.

Kuna uwezekano mkubwa wa kupata ugonjwa huu kwa sababu ya matumizi ya vyoo vya kukalia kwa mda mrefu ingawa sio wote wanaotumia vyoo hivi kupata Bawasili.

 

8. Kunyanyua vitu vizito.

Kuna wakati mwingine watu wenye tabia ya kunyanyua vitu vizito wamo hatarini kupata ugonjwa huu wa Bawasili.

 

9. Kuwepo kwa mfadhaiko au stress.

Kwa kuwepo kwa mfadhaiko wa mara kwa mara usababisha magonjwa mbalimbali ikiwemo na Bawasili.

 

10. Kuwepo kwa uzito mkubwa na unene wa kupitiliza, kwa kawaida watu wanene na wenye uzito uliopitiliza usababisha kuwepo kwa magonjwa mbalimbali na wako hatarini kupata Bawasili.

 

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2632

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Bongolite - Game zone - Play free game     πŸ‘‰2 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     πŸ‘‰4 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰5 ai web app     πŸ‘‰6 web hosting    

Post zinazofanana:

Ishara za Mpenzi Asiye Mwaminifu

​Kuhisi mashaka katika mahusiano ni jambo linaloweza kuleta fadhaa kubwa. Post hii inachunguza ishara mbalimbali za tabia zinazoweza kuashiria kutokuwa mwaminifu, huku ikisisitiza umuhimu wa mawasiliano na ushahidi kabla ya kuhukumu.

Soma Zaidi...
Mlo kwa wagonjwa wa figo wanaochujwa damu

Posti hii inahusu zaidi mlo kwa wagonjwa wa figo wanaochujwa damu, ni wagonjwa ambao figo zao zimeharibika na zimeshindwa kufanya kazi au pengine kuna uchafu mwingi mwilini ambao uchujwa kwa hiyo kuna vyakula muhimu ambavyo wagonjwa wa figo wanapaswa kutu

Soma Zaidi...
Tabia za kujikosoa kupita kiasi na jinsi ya kujenga upendo

​Katika ulimwengu wa kisasa, shinikizo la kuwa "mkamilifu" mara nyingi husababisha watu wengi kuangukia katika mtego wa kujikosoa kupita kiasi. Makala haya yanachunguza asili ya sauti hii ya ndani (inner critic), madhara yake katika afya ya akili, na kutoa mwongozo wa hatua kwa hatua wa jinsi ya kugeuza mtazamo huo kuwa upendo na huruma kwa nafsi yako (self-compassion).

Soma Zaidi...
Sababu za kuumwa na tumbo, chini ya kitomvu ama upande wa kulia

Post hii inakwenda kukutajia baadhi tu ya sababu zinazopelekea kuumwa na tumbo. Hali hizi zinawweza kuwapata watu wa jinsia zote katika umri wowote ule. Ijapokuwa nyingine si kwa wote ni kwa baadhi ya watu. hapa nitakuletea sababu 5 tu.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa vitiligo, chanzo, dalili na matibabu yake

Katika post hii utajifunza kuhusu ugonjwa wa vitiligo, chanzo chake, dalili zake na matibabu yaje

Soma Zaidi...
DALILI ZA SELIMUDU

Posti hii inazungumzia ishara na dalili za SELIMUDU ambao kitaalamu huitwa Sickle cell Anemia.selimudu ni aina ya kurithi ya Anemia — hali ambayo hakuna chembechembe nyekundu za damu zenye afya za kutosha kubeba oksijeni ya kutos

Soma Zaidi...