picha

Bawasili usababishwa na nini?

Posti hii inahusu zaidi visababishi vya ugonjwa wa Bawasili,kuna watu wengi wanapenda kujua kabisa chanzo cha kuwepo kwa ugonjwa wa Bawasili kwenye jamii na kuna maswali mengi yanayoulizwa kuhusu visababishi vya Bawasili.

Visababishi vya ugonjwa wa Bawasili.

1. Kufunga choo au kukosa choo kwa mda mrefu.

Hii ni sababu ya kwanza kabisa kwa sababu kuna watu ambao hawapati choo au wanabana choo kwa mda mrefu na usababisha kuwepo kwa Bawasili.

 

2. Wakati wa ujauzito.

 Wakati wa ujauzito kuna uwezekano wa kupata ugonjwa wa Bawasili kwa sababu ya kuwepo kwa mgandamizo wa mtoto kupelekea kwenye na sehemu ya haja kubwa , na pia wakati wa kujifungua mtoto anakandamiza sana sehemu ya haja kubwa.

 

3. Kufanya mapenzi kinyume cha maumbile.

Kuna kipindi watu wanapenda kufanya mapenzi kwenye sehemu ya haja kubwa hali ambayo upelekea kuwepo kwa Bawasili.

 

4. Uzee.

Pia nao wana uwezekano wa kupata tatizo hili la Bawasili kwa sababu mtu akiweka na kinga za mwili zinashuka hali ambayo Usababisha kupata ugonjwa huu.

 

5. Pia kuna sababu za kurithi.

Kwa kawaida kuna familia ambayo upata ugonjwa huu mara kwa mara kutoka kwa babu , baba na majukumu kwa hiyo kuna uwezekano wa kupata kama ugonjwa umo kwenye familia.

 

6. Kuharisha sana na kwa mda mrefu.

Kuna watu ambao wanapatwa na tatizo la kuharisha sana na kwa mda mrefu nao wana uwezekano wa kupata ugonjwa huu wa Bawasili.

 

7. Matumizi ya vyoo vya kukalia.

Kuna uwezekano mkubwa wa kupata ugonjwa huu kwa sababu ya matumizi ya vyoo vya kukalia kwa mda mrefu ingawa sio wote wanaotumia vyoo hivi kupata Bawasili.

 

8. Kunyanyua vitu vizito.

Kuna wakati mwingine watu wenye tabia ya kunyanyua vitu vizito wamo hatarini kupata ugonjwa huu wa Bawasili.

 

9. Kuwepo kwa mfadhaiko au stress.

Kwa kuwepo kwa mfadhaiko wa mara kwa mara usababisha magonjwa mbalimbali ikiwemo na Bawasili.

 

10. Kuwepo kwa uzito mkubwa na unene wa kupitiliza, kwa kawaida watu wanene na wenye uzito uliopitiliza usababisha kuwepo kwa magonjwa mbalimbali na wako hatarini kupata Bawasili.

 

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2692

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉2 Bongolite - Game zone - Play free game     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 Dua za Mitume na Manabii     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Sababu za Kichefuchefu Katika Mimba

​Kichefuchefu na kutapika ni hali ya kawaida inayowapata wanawake wengi wajawazito, maarufu kama "asubuhi yenye kichefuchefu" (morning sickness). Posti hii inaelezea kwa nini hali hii hutokea, mambo yanayoichochea, na jinsi unavyoweza kuikabili ili kupata unafuu.

Soma Zaidi...
Tabia za kujikosoa kupita kiasi na jinsi ya kujenga upendo

​Katika ulimwengu wa kisasa, shinikizo la kuwa "mkamilifu" mara nyingi husababisha watu wengi kuangukia katika mtego wa kujikosoa kupita kiasi. Makala haya yanachunguza asili ya sauti hii ya ndani (inner critic), madhara yake katika afya ya akili, na kutoa mwongozo wa hatua kwa hatua wa jinsi ya kugeuza mtazamo huo kuwa upendo na huruma kwa nafsi yako (self-compassion).

Soma Zaidi...
Je mtu akapima ukimwi na kile kipimo kidogo .je kina usahihi au la ..na pia kama inaonyesha mistari miwili.

Hivi umeshawahi kuwazakuwa jekipimo cha HIV ni sahihi kwa kiasi gani. Unadhani huwa kinakoseaga kutoa majibu?

Soma Zaidi...
Ukweli Kuhusu Punyeto kwa Wanaume

​Punyeto ni suala linalozungumziwa sana katika jamii, na mara nyingi limegubikwa na dhana potofu. Makala haya yanalenga kuweka sawa ukweli wa kisayansi kuhusu mazoea haya, athari zake zinazowezekana, na wakati ambapo inakuwa ni tatizo linalohitaji uangalizi.

Soma Zaidi...
Namna ya kutoa huduma kwa mgonjwa wa Dengue.

Posti hii inahusu zaidi huduma anayopaswa kupata mgonjwa wa ndengue, kwa sababu tunafahamu wazi Ugonjwa huu hauna dawa ila kuna huduma muhimu ambayo anaweza kupata na akaendelea vizuri.

Soma Zaidi...
Unene kupita kiasi wakati wa ujauzito: Athari zake.

Uzito wa mwili wakati wa ujauzito una nafasi muhimu sana katika afya ya mama na mtoto. Ingawa ni kawaida kupata uzito wakati wa kulea mimba, unene uliopitiliza (Obesity) kabla au wakati wa ujauzito huleta changamoto za kiafya zinazoweza kuwa hatari. Makala hii inaangazia athari za unene uliokithiri na jinsi unavyoweza kuathiri mchakato wa ujauzito na uzazi kwa ujumla.

Soma Zaidi...