Bawasili usababishwa na nini?


image


Posti hii inahusu zaidi visababishi vya ugonjwa wa Bawasili,kuna watu wengi wanapenda kujua kabisa chanzo cha kuwepo kwa ugonjwa wa Bawasili kwenye jamii na kuna maswali mengi yanayoulizwa kuhusu visababishi vya Bawasili.


Visababishi vya ugonjwa wa Bawasili.

1. Kufunga choo au kukosa choo kwa mda mrefu.

Hii ni sababu ya kwanza kabisa kwa sababu kuna watu ambao hawapati choo au wanabana choo kwa mda mrefu na usababisha kuwepo kwa Bawasili.

 

2. Wakati wa ujauzito.

 Wakati wa ujauzito kuna uwezekano wa kupata ugonjwa wa Bawasili kwa sababu ya kuwepo kwa mgandamizo wa mtoto kupelekea kwenye na sehemu ya haja kubwa , na pia wakati wa kujifungua mtoto anakandamiza sana sehemu ya haja kubwa.

 

3. Kufanya mapenzi kinyume cha maumbile.

Kuna kipindi watu wanapenda kufanya mapenzi kwenye sehemu ya haja kubwa hali ambayo upelekea kuwepo kwa Bawasili.

 

4. Uzee.

Pia nao wana uwezekano wa kupata tatizo hili la Bawasili kwa sababu mtu akiweka na kinga za mwili zinashuka hali ambayo Usababisha kupata ugonjwa huu.

 

5. Pia kuna sababu za kurithi.

Kwa kawaida kuna familia ambayo upata ugonjwa huu mara kwa mara kutoka kwa babu , baba na majukumu kwa hiyo kuna uwezekano wa kupata kama ugonjwa umo kwenye familia.

 

6. Kuharisha sana na kwa mda mrefu.

Kuna watu ambao wanapatwa na tatizo la kuharisha sana na kwa mda mrefu nao wana uwezekano wa kupata ugonjwa huu wa Bawasili.

 

7. Matumizi ya vyoo vya kukalia.

Kuna uwezekano mkubwa wa kupata ugonjwa huu kwa sababu ya matumizi ya vyoo vya kukalia kwa mda mrefu ingawa sio wote wanaotumia vyoo hivi kupata Bawasili.

 

8. Kunyanyua vitu vizito.

Kuna wakati mwingine watu wenye tabia ya kunyanyua vitu vizito wamo hatarini kupata ugonjwa huu wa Bawasili.

 

9. Kuwepo kwa mfadhaiko au stress.

Kwa kuwepo kwa mfadhaiko wa mara kwa mara usababisha magonjwa mbalimbali ikiwemo na Bawasili.

 

10. Kuwepo kwa uzito mkubwa na unene wa kupitiliza, kwa kawaida watu wanene na wenye uzito uliopitiliza usababisha kuwepo kwa magonjwa mbalimbali na wako hatarini kupata Bawasili.

 

 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    2 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    3 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    4 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Hatua za kufuata baada ya kuhisi kuwa umeambukizwa na virusi vya HIV
Posti hii inahusu zaidi hatua za kufuata unapohisi umeambukizwa na virus vya ukimwi. Kwa sababu watu wengi wanakuwa na kiwewe anapohisi ameambukizwa na virus vya ukimwi kwa hiyo wanapaswa kufanya yafuatayo. Soma Zaidi...

image Mbinu za kuzuia na kuepukana na maradhi ya uti wa mgongo
Posti hii inahusu zaidi njia au mbinu mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuepukana na tatizo la ugonjwa wa homa ya uti wa mgongo. Soma Zaidi...

image Madhara ya kichaa cha mbwa
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kama mtu hajatibiwa ugonjwa wa kichaa cha mbwa. Soma Zaidi...

image Matibabu ya vidonda vya tumbo
Makala hii inakwenda kukufundisha kuhusu matibabu ya vidonda vyatumbo. Pia utajifunza kwa nini kunakuwa na vidonda vya tumbo sugu. Soma Zaidi...

image Fangasi mdomoni ni dalili ya minyoo aina gani
Zipo aina nyingi za fantasy ambazo ni rahisi kuathiri binadamu. Wipe ambao haiathiri mdomo, nyayo, shemu za siri na kwenye ngozi. Soma Zaidi...

image Dalili za kuwepo kwa kizungu Zungu
Posti hii inahusu zaidi dalili za kuwepo kwa kizungu Zungu,ni Dalili ambazo Uweza kujionyesha kwa mtu ambaye ameshawahi kupatwa na tatizo la kizungu Zungu au hajawahi kupata dalili zenyewe ni kama ifuatavyo. Soma Zaidi...

image Huduma kwa walio na matatizo ya asili nyingi mwilini
Posti hii inahusu zaidi huduma kwa wale ambao tayari wameshakuwa na tatizo la asidi mwilini, ni njia ambazo unaweza kuzitumia ili kuweza kupunguza tatizo hili au Mgonjwa anapoendelea kupata matibabu. Soma Zaidi...

image Njia za kusambaa kwa ugonjwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine
Posti hii inahusu zaidi jinsi magonjwa yanavyosambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine. Soma Zaidi...

image Matibabu kwa mtu mwenye kiungulia
Posti hii inahusu zaidi matibabu kwa mtu mwenye kiungulia,ni tiba ambayo mtu anapaswa kutumia kama ana tatizo la kiungulia Soma Zaidi...

image Heti kama mtu kafany mapenzi na mtu mwe ukimwi siku hihiyo akenda hospitali kapewa dawa kweli hataweza kuwabukizwa
Swali hili limeulizwa na mdau mmoja. Kuwa endapo mtu atafanya ngono zembe na akapata virusi je ataweza kuambukiza. Soma Zaidi...