Posti hii inahusu zaidi njia au mbinu ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuepuka kuwepo kwa ugonjwa wa Bawasili kwenye jamii, hizi ni njia za awali za kupambana na kuwepo kwa Ugonjwa wa Bawasili.
1. Njia ya kwanza ni kuhakikisha kuwa ukipata haja kubwa fanya haraka kuitoa na usisubiri mda na pia kama kuna tatizo la choo kuwa ngumu ni vizuri kutafuta matibabu ili kuweza kuepuka madhara ya uwepo wa Bawasili.
2. Kuachana na tabia ya kufanya mapenzi kinyume cha maumbile.
Hii ni tabia ambayo imeingia na inatumiwa na watu wengi sana hasa kwa vijana hali inayopelekea kuwepo kwa ugonjwa wa Bawasili na pia kuwepo kwa Maambukizi mbalimbali kwa sababu ya kulegea kwa mishipa ya haja kubwa hali inayosababisha kuwepo kwa Bawasili.
3. Kutibu magonjwa ya kuharisha endapo yametokea.
Kwa kawaida kuharisha kwa mda mrefu usababisha kuwepo kwa Ugonjwa wa Bawasili kwa kufanya hivyo tutaweza kuepuka kuwepo kwa Ugonjwa huu.
4. Kupunguza matumizi ya vyoo vya kukalia.
Kwa wale wanaotumia sana vyoo vya kukalia wanapaswa kupunguza au kutumia njia nyingine ili kuepuka kuwepo kwa Ugonjwa wa Bawasili.
5. Kupunguza tabia ya kunyanyua vitu vizito.
Kwa wale ambao kazi zao mara nyingi ni kunyanyua vitu vizito wanapaswa kupunguza ili kuepuka matatizo ya gonjwa la Bawasili.
6. Kupunguza uzito na unene wa kupitiliza.
Kwa kawaida watu wanene na wenye uzito wa kupitiliza wako kwenye hatari kubwa ya kupata ugonjwa huu.
7. Kuachana na msongo wa mawazo.
Kuna watu ambao wanaweza kila siku kwa sababu ya kuwepo kwa matatizo kwenye maisha yao kwa hiyo tunapaswa kuwakwaza na kutafuta kitu chochote cha kuwafanya waachane na kukaa kwenye mawazo mda wote.
8. Kutoa elimu kwa watu kuhusu Ugonjwa huu. Maana yake, jinsi unavotokea, madhara yake na njia za kufanya ili kuweza kutokomeza kabisa ugonjwa huu kwenye jamii.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Somo hili linakwenda kukuletea orodha ya makunfi ya watu walio hatarini kupata UTI
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi uchunguzi wa kuharisha damu na Tiba yake, ni Ugonjwa ambao unaowashambulia sana watoto hasa wenye chini ya umri wa miaka mitano, kwa hiyo huoaugonjwa tunaweza kuutambua na kutibu kwa njia zifuatazo.
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia kuhusiana na mifuko midogo midogo, iliyobubujika ambayo inaweza kuunda kwenye utando wa mfumo wako wa usagaji chakula. Wao hupatikana mara nyingi katika sehemu ya chini ya utumbo mkubwa (koloni). Hali hiyo inajulikana kama Divert
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia kuhusiana na maumivu ya shingo na ndani yake kunasababu zinazopelekea shingo kupata maumivu.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi huduma anayopaswa kupata mgonjwa wa ndengue, kwa sababu tunafahamu wazi Ugonjwa huu hauna dawa ila kuna huduma muhimu ambayo anaweza kupata na akaendelea vizuri.
Soma Zaidi...Unyogovu (Depression ) ni mojawapo ya ugonjwa wa akili ambao unahusishwa na hisia za huzuni, kukosa matumaini, na kupoteza furaha au shauku katika shughuli za kila siku. Huu si tu hisia ya huzuni iliyokatisha tamaa, bali ni hali sugu inayoweza kuathiri mabadiliko ya mwili, mawazo, na tabia ya mtu. Unyogovu unaweza kutokea kwa sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na mabadiliko ya kemikali katika ubongo, maumbile, mazingira, na matukio mbali mbali katika maisha ambayo kupelekea mgonjwa kuwa hivyo.
Soma Zaidi...VIPIMO VYA MINYOO Haitoshelezi kuwa na dalili pekee ukathibitisha kuwa una minyoo.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za VVU/ UKIMWI
Soma Zaidi...