Njia za kuzuia uwepo wa ugonjwa wa Bawasili.
Posti hii inahusu zaidi njia au mbinu ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuepuka kuwepo kwa ugonjwa wa Bawasili kwenye jamii, hizi ni njia za awali za kupambana na kuwepo kwa Ugonjwa wa Bawasili.
Njia za kuzuia kuwepo kwa ugonjwa wa Bawasili.
1. Njia ya kwanza ni kuhakikisha kuwa ukipata haja kubwa fanya haraka kuitoa na usisubiri mda na pia kama kuna tatizo la choo kuwa ngumu ni vizuri kutafuta matibabu ili kuweza kuepuka madhara ya uwepo wa Bawasili.
2. Kuachana na tabia ya kufanya mapenzi kinyume cha maumbile.
Hii ni tabia ambayo imeingia na inatumiwa na watu wengi sana hasa kwa vijana hali inayopelekea kuwepo kwa ugonjwa wa Bawasili na pia kuwepo kwa Maambukizi mbalimbali kwa sababu ya kulegea kwa mishipa ya haja kubwa hali inayosababisha kuwepo kwa Bawasili.
3. Kutibu magonjwa ya kuharisha endapo yametokea.
Kwa kawaida kuharisha kwa mda mrefu usababisha kuwepo kwa Ugonjwa wa Bawasili kwa kufanya hivyo tutaweza kuepuka kuwepo kwa Ugonjwa huu.
4. Kupunguza matumizi ya vyoo vya kukalia.
Kwa wale wanaotumia sana vyoo vya kukalia wanapaswa kupunguza au kutumia njia nyingine ili kuepuka kuwepo kwa Ugonjwa wa Bawasili.
5. Kupunguza tabia ya kunyanyua vitu vizito.
Kwa wale ambao kazi zao mara nyingi ni kunyanyua vitu vizito wanapaswa kupunguza ili kuepuka matatizo ya gonjwa la Bawasili.
6. Kupunguza uzito na unene wa kupitiliza.
Kwa kawaida watu wanene na wenye uzito wa kupitiliza wako kwenye hatari kubwa ya kupata ugonjwa huu.
7. Kuachana na msongo wa mawazo.
Kuna watu ambao wanaweza kila siku kwa sababu ya kuwepo kwa matatizo kwenye maisha yao kwa hiyo tunapaswa kuwakwaza na kutafuta kitu chochote cha kuwafanya waachane na kukaa kwenye mawazo mda wote.
8. Kutoa elimu kwa watu kuhusu Ugonjwa huu. Maana yake, jinsi unavotokea, madhara yake na njia za kufanya ili kuweza kutokomeza kabisa ugonjwa huu kwenye jamii.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 web hosting 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 ai web app 👉6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
Ujue Ugonjwa wa homa ya ini yenye sumu.
Homa ya ini yenye sumu ni kuvimba kwa ini lako kutokana na kuathiriwa na vitu fulani ambavyo umeathiriwa navyo. Homa ya ini yenye sumu inaweza kusababishwa na pombe, kemikali, dawa za kulevya au viongeza vya lishe.
Soma Zaidi...Sababu za Kichefuchefu Katika Mimba
Kichefuchefu na kutapika ni hali ya kawaida inayowapata wanawake wengi wajawazito, maarufu kama "asubuhi yenye kichefuchefu" (morning sickness). Posti hii inaelezea kwa nini hali hii hutokea, mambo yanayoichochea, na jinsi unavyoweza kuikabili ili kupata unafuu.
Soma Zaidi...Jinsi ya kutafuta msaada wa kisaikolojia (Therapy).
Uamuzi wa kutafuta msaada wa kisaikolojia ni moja kati ya hatua kubwa na za kijasiri unazoweza kuchukua kwa ajili ya afya yako ya akili. Hata hivyo, wengi wetu tunasita kwa sababu hatujui tunaanzia wapi, tunamtafuta nani, na nini kinatokea chumba cha tiba. Makala haya yanakupa mwongozo wa hatua kwa hatua wa jinsi ya kupata mtaalamu sahihi na kuanza safari yako ya uponyaji wa kiakili.
Soma Zaidi...Dalilili za mimba Kuharibika
Kuharibika kwa mimba ni upotevu wa hiari wa ujauzito kabla ya wiki ya 20. Takriban asilimia 10 hadi 20 ya mimba zinazojulikana huisha kwa kuharibika kwa mimba. Lakini idadi halisi labda ni kubwa zaidi kwa sababu mimba nyingi hutokea mapema sana katika u
Soma Zaidi...Huduma kwa wenye Maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuwasaidia Watu wale ambao wana Maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo.
Soma Zaidi...