Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Bawasili
Posti hii inahusu zaidi juu ya ugonjwa wa Bawasili, ni ugonjwa unaotokea kwenye njia ya haja kubwa hali ambayo upelekea kuwepo kwa uvimbe au nyama ambazo uonekana hadi nje, kwa lugha ya kitaalamu ujulikana kama haemorrhoid au pokea.
Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Bawasili.
1. Pamoja na kuwepo kwa Ugonjwa huu kuna aina mbili za Ugonjwa wa Bawasili kuna Bawasili ya nje ambayo uonekana kwa nje na kuna Bawasili ya ndani ambayo uonekana kwa ndani kwa hiyo tutaziona moja baada ya nyingine.
2. Bawasili ya nje.
Aina hii ya Bawasili utokea katika eneo la mwisho kabisa la mfereji wa haja kubwa na kuambatana na maumivu makali kwa mgonjwa na pia utokea miwasho wa ngozi katika sehemu hiyo mara nyingi katika sehemu hiyo mishipa ya damu yaani veini upasuka na damu kuganda hivyo kusababisha aina hii ya Bawasili ambapo kwa kitaalamu huitwa thrombosed haemorrhoid.
3. Pia aina ya pili ya Bawasili ni Bawasili ya ndani.
Aina hizi ya Bawasili ni tofauti na ya kwanza hii kwa kawaida utokea ndani ya mfereji wa haja kubwa pia nayo uambatana na Maumivu ambayo Usababisha Mgonjwa kuumia sana na pengine miwasho inaweza kutokea kwa nje .
4. Baada ya kuona aina kuu mbili za Bawasili yaani Bawasili ya ndani na nje na matokeo yake ni hali ya kuwepo kwa maumivu makali yanayoambatana na miwasho, kwa hiyo ni vizuri kabisa kutafuta matibabu ili kuweza kuondokana na tatizo hili kwa sababu watu walio wengi wanapuuza kuwepo kwa dawa hospitalini wanakimbilia dawa mbadala ambazo kwa wakati mwingine zinaweza kusababisha madhara zaidi kuliko kuponesha .
5. Kwa hiyo baada ya kuona aina hizi ni vizuri kuwaona wataalamu wa afya na kuachana na mila potovu kabisa ambazo zinaweza kuleta madhara zaidi, kwa hiyo kwa watumiaji wa dawa mbadala ambazo uaminika na walio wengi ni vizuri kuzitumia ila tahadhari ni lazima na kama hali ikiwa mbaya katika matumizi ya dawa mbadala ni vizuri kabisa kumwona mtaalamu wa afya na kumweleza kila kitu kwa ukweli ili kusaidia katika kudili na tatizo.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 web hosting 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 ai web app 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Dalili za kuvunjika kwa nyonga
Kuvunjika kwa nyonga ni jeraha kubwa, na matatizo ambayo yanaweza kuhatarisha maisha. Hatari ya kupasuka kwa nyonga huongezeka na umri.
Soma Zaidi...Maumivu ya mgongo (Sciatica): Dalili na mazoezi ya kupunguza.
Sciatica ni hali ya maumivu yanayotokana na shinikizo au kuwasha kwa neva ya sciatic, ambayo ndiyo neva ndefu na kubwa zaidi mwilini mwako. Makala haya yanatoa mwongozo wa kitaalamu kuhusu jinsi ya kutambua dalili za sciatica, sababu za msingi zinazoleta maumivu haya, na mfululizo wa mazoezi yaliyothibitishwa kitabibu kusaidia kupunguza maumivu na kurejesha utendaji wa mwili.
Soma Zaidi...Dawa za kutuliza maumivu na kazi zake
Post hii inahusu zaidi dawa za kupunguza maumivu na kazi zake, ni dawa ambazo upunguza maumivu kwenye mwili wa binadamu.
Soma Zaidi...Kutokwa na uchafu mweupe ukeni: Ni ugonjwa?
Kutokwa na uchafu ukeni ni jambo la kawaida kwa kila mwanamke aliyefikia umri wa kuvunja ungo. Hata hivyo, wengi hukumbwa na hofu pindi wanapoona mabadiliko katika rangi, harufu, au wingi wa uchafu huo. Makala hii inafafanua tofauti kati ya uchafu wa kawaida (physiological discharge) na ule unaoashiria ugonjwa (pathological discharge), na kutoa mwongozo wa wakati wa kutafuta msaada wa kitaalamu.
Soma Zaidi...Vyanzo vya sumu mwilini.
Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya kuwepo kwa sumu mwilini, kwa sababu kuna wakati mwingine tunapata magonjwa na matatizo mbalimbali ya ki afya tunaangaika huku na huko kumbe sababu kubwa ni kuwepo kwa sumu mwilini na vyanzo vya sumu hiyo ni kama ifuatavy
Soma Zaidi...Samahan naomb kujua staili za tendo la ndoa
Post hii inakwenda kujibu swali la muulizaji. Kuhusu syyle za tendo la ndoa
Soma Zaidi...