Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Bawasili
Posti hii inahusu zaidi juu ya ugonjwa wa Bawasili, ni ugonjwa unaotokea kwenye njia ya haja kubwa hali ambayo upelekea kuwepo kwa uvimbe au nyama ambazo uonekana hadi nje, kwa lugha ya kitaalamu ujulikana kama haemorrhoid au pokea.
Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Bawasili.
1. Pamoja na kuwepo kwa Ugonjwa huu kuna aina mbili za Ugonjwa wa Bawasili kuna Bawasili ya nje ambayo uonekana kwa nje na kuna Bawasili ya ndani ambayo uonekana kwa ndani kwa hiyo tutaziona moja baada ya nyingine.
2. Bawasili ya nje.
Aina hii ya Bawasili utokea katika eneo la mwisho kabisa la mfereji wa haja kubwa na kuambatana na maumivu makali kwa mgonjwa na pia utokea miwasho wa ngozi katika sehemu hiyo mara nyingi katika sehemu hiyo mishipa ya damu yaani veini upasuka na damu kuganda hivyo kusababisha aina hii ya Bawasili ambapo kwa kitaalamu huitwa thrombosed haemorrhoid.
3. Pia aina ya pili ya Bawasili ni Bawasili ya ndani.
Aina hizi ya Bawasili ni tofauti na ya kwanza hii kwa kawaida utokea ndani ya mfereji wa haja kubwa pia nayo uambatana na Maumivu ambayo Usababisha Mgonjwa kuumia sana na pengine miwasho inaweza kutokea kwa nje .
4. Baada ya kuona aina kuu mbili za Bawasili yaani Bawasili ya ndani na nje na matokeo yake ni hali ya kuwepo kwa maumivu makali yanayoambatana na miwasho, kwa hiyo ni vizuri kabisa kutafuta matibabu ili kuweza kuondokana na tatizo hili kwa sababu watu walio wengi wanapuuza kuwepo kwa dawa hospitalini wanakimbilia dawa mbadala ambazo kwa wakati mwingine zinaweza kusababisha madhara zaidi kuliko kuponesha .
5. Kwa hiyo baada ya kuona aina hizi ni vizuri kuwaona wataalamu wa afya na kuachana na mila potovu kabisa ambazo zinaweza kuleta madhara zaidi, kwa hiyo kwa watumiaji wa dawa mbadala ambazo uaminika na walio wengi ni vizuri kuzitumia ila tahadhari ni lazima na kama hali ikiwa mbaya katika matumizi ya dawa mbadala ni vizuri kabisa kumwona mtaalamu wa afya na kumweleza kila kitu kwa ukweli ili kusaidia katika kudili na tatizo.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 kitabu cha Simulizi π2 Kitau cha Fiqh π3 Kitabu cha Afya π4 Simulizi za Hadithi Audio π5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Kupunguzwa kwa nguvu za kiume: Sababu za kisaikolojia na kimwili.
Kupungua kwa nguvu za kiume, kitaalamu ikijulikana kama erectile dysfunction (ED), ni hali inayoweza kuathiri ustawi wa kihisia na mahusiano ya kijamii ya mwanamume. Ingawa mara nyingi huchukuliwa kama aibu, ni hali ya kawaida ya kiafya inayoweza kutibiwa. Makala haya yanachambua kwa kina sababu mbalimbali za kisaikolojia na kimwili zinazosababisha hali hii, umuhimu wa utambuzi sahihi, na njia za kurejesha afya ya uzazi na nguvu za kiume.
Soma Zaidi...Dalili za maambukizi kwenye figo
Posti hii inazungumzia kuhusiana na Maambukizi kwenye figo (pyelonephritis) ni aina mahususi ya maambukizi ya njia ya mkojo (UTI) ambayo kwa kawaida huanza kwenye urethra au kibofu chako na kusafiri hadi kwenye figo zako.
Soma Zaidi...Ugonjwa wa kupooza (Stroke): Dalili za mwanzo na kinga.
βUgonjwa wa kupooza, unaojulikana kitabibu kama stroke au cerebrovascular accident (CVA), ni dharura kubwa ya kitabibu inayotokea wakati mtiririko wa damu kwenye sehemu ya ubongo unapoingiliwa au kukatika. Kila sekunde ni muhimu katika kuokoa tishu za ubongo na kupunguza ulemavu wa kudumu. Makala haya yanafafanua dalili za mwanzo, sababu za hatari, na mikakati madhubuti ya kuzuia ugonjwa huu kwa maisha yenye afya bora
Soma Zaidi...Kikohozi kikavu: Chanzo chake na dawa za asili za kutibu.
Kikohozi kikavu ni tatizo linaloathiri mfumo wa upumuaji bila kuzalisha makohozi, mara nyingi likisababishwa na mzio (allergies), maambukizi ya virusi, au asidi ya tumbo kupanda kooni (GERD). Makala haya ya kina yanachambua vyanzo vikuu vya kitaalamu vya changamoto hii na kuorodhesha tiba 6 za asili zilizothibitishwa kisayansi kama vile asali, tangawizi, na binzari. Pia, utajifunza ishara hatari zinazohitaji uononaji wa daktari na ukweli wa kimatibabu kuhusu kikohozi kupitia sehemu ya "Je, Wajua?".
Soma Zaidi...Huduma kwa wenye Maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuwasaidia Watu wale ambao wana Maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo.
Soma Zaidi...Sababu za miguu kufa ganzi.
Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali,za miguu kufa ganzi,ni tatizo ambalo uwakumba watu wengi na walio wengi hawafahamu kabisa ni sababu zipi ambazo uleta tatizo hili.
Soma Zaidi...