picha

Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Bawasili

Posti hii inahusu zaidi juu ya ugonjwa wa Bawasili, ni ugonjwa unaotokea kwenye njia ya haja kubwa hali ambayo upelekea kuwepo kwa uvimbe au nyama ambazo uonekana hadi nje, kwa lugha ya kitaalamu ujulikana kama haemorrhoid au pokea.

Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Bawasili.

1. Pamoja na kuwepo kwa Ugonjwa huu kuna aina mbili za Ugonjwa wa Bawasili kuna Bawasili ya nje ambayo uonekana kwa nje na kuna Bawasili ya ndani ambayo uonekana kwa ndani kwa hiyo tutaziona moja baada ya nyingine.

 

2. Bawasili ya nje. 

Aina hii ya Bawasili utokea katika eneo la mwisho kabisa la mfereji wa haja kubwa  na kuambatana na maumivu makali kwa mgonjwa na pia utokea miwasho wa ngozi katika sehemu hiyo  mara nyingi katika sehemu hiyo mishipa ya damu yaani veini upasuka  na damu kuganda  hivyo kusababisha aina hii ya Bawasili ambapo kwa kitaalamu huitwa thrombosed haemorrhoid.

 

3. Pia aina ya pili ya Bawasili ni Bawasili ya ndani.

Aina hizi ya Bawasili ni tofauti na ya kwanza hii kwa kawaida utokea ndani ya mfereji wa haja kubwa pia nayo uambatana na Maumivu ambayo Usababisha Mgonjwa kuumia sana na pengine miwasho inaweza kutokea kwa nje .

 

4. Baada ya kuona aina kuu mbili za Bawasili yaani Bawasili ya ndani na nje na matokeo yake ni hali ya kuwepo kwa maumivu makali yanayoambatana na miwasho, kwa hiyo ni vizuri kabisa kutafuta matibabu ili kuweza kuondokana na tatizo hili kwa sababu watu walio wengi wanapuuza kuwepo kwa dawa hospitalini wanakimbilia dawa mbadala ambazo kwa wakati mwingine zinaweza kusababisha madhara zaidi kuliko kuponesha .

 

5. Kwa hiyo baada ya kuona aina hizi ni vizuri kuwaona wataalamu wa afya na kuachana na mila potovu kabisa ambazo zinaweza kuleta madhara zaidi, kwa hiyo kwa watumiaji wa dawa mbadala ambazo uaminika na walio wengi ni vizuri kuzitumia ila tahadhari ni lazima na kama hali ikiwa mbaya katika matumizi ya dawa mbadala ni vizuri kabisa kumwona mtaalamu wa afya na kumweleza kila kitu kwa ukweli ili kusaidia katika kudili na tatizo.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2226

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰2 Simulizi za Hadithi Audio     πŸ‘‰3 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰4 Dua za Mitume na Manabii     πŸ‘‰5 ai web app     πŸ‘‰6 Bongolite - Game zone - Play free game    

Post zinazofanana:

Jinsi ya kuishi na mtu mwenye matatizo ya afya ya akili.

​Kuishi na mtu anayekabiliwa na changamoto za afya ya akili ni safari inayohitaji subira, elimu, na mipaka ya kijamii iliyo thabiti. Makala haya yanatoa mwongozo wa kitaalamu kuhusu namna ya kutoa msaada bila kupoteza ustawi wako mwenyewe. Tunachambua mbinu za mawasiliano, umuhimu wa kutoa nafasi, na jinsi ya kuunda mazingira ya kuaminiana, huku tukisisitiza umuhimu wa msaada wa kitaalamu na utunzaji binafsi kwa walezi (caregivers

Soma Zaidi...
Watu walio hatarini kupata fangasi

Somo hili linakwenda kukuletea baadhi ya watu walio hatarini kupata fangasi

Soma Zaidi...
Sababu za kuwa na afya ya akili

Afya ya akili ni hali ya mtu kuwa na akili timamu kiroho,kimwili ,na Kwa mazingira yake yote yaliyomzunguka na anaweza kuamua kitu akiwa katika ukamilifu, zifuatazo ni sababu za kuwa na Afya ya akili.

Soma Zaidi...
Fangasi wanaojulikana kama Blastomyces

Fangasi wanaojulikana kama Blastomyces, hawa ni fangasi wanaosababisha maradhi yajulikanayo kama blastomycosis.

Soma Zaidi...
Dawa za kutuliza vvu zinaongeza damu

Hakuna dawa ya UKIMWI ya kutibu kuondoa virusi mwilini, lakini zipo dawa za kuweza kupunguza makali ya virusi hawa. Hivi unesha jiuliza kuwa je zile dawa zinaongeza damu?

Soma Zaidi...
je kukohoa kunaweza kuwa ni dalili ya minyoo?

Dalili za minyoo zipo nyingi kama kuumwa na tumbo, tumbo kujaa gesi, uchovu, kukosa hamu ya kula, kupata choo chenye uteute na kupunguwa uzito. je kukohoa kunaweza kuwa ni dalili ya minyoo?

Soma Zaidi...