Njia za kupunguza ugonjwa wa zinaa

Njia za kupunguza ugonjwa wa zinaa

Posti hii inahusu zaidi njia ambazo zinaweza kutumika Ili kuweza kupunguza kuwepo kwa magonjwa ya zinaa

Njia za kupunguza ugonjwa wa zinaa.

1. Kwanza kabisa tunapaswa kufahamu kuwa ugonjwa wa zinaa uleta matatizo mengi kwenye jamii kwa hiyo tunapaswa kutumia njia mbalimbali Ili kuweza kupunguza ugonjwa huu, kwa hiyo zifuatazo ni mbinu za kupunguza ugonjwa wa zinaa.

 

2 . kutumia kinga wakati wa kujamiiana na kuwa na mpenzi mmoja.

Kwa kutumia kinga kwa mtu ambaye haumfahamu kama ana maambukizi ni jambo zuri na la busara kwa sababu katika kufanya hivyo maambukizi hayawezi kuwepo, pia kuwa na desturi ya kuwa na mpenzi mmoja na kupima mara kwa mara Ili kuangalia kama Kuna maambukizi yoyote walau kila mwezi kama inawezekana.na pia ikitokea kuna maambukizi ni vizuri kupima nyote na kuhaidi kuwa waaminifu katika mahusiano.

 

3. Kuachana na Mila na desturi zinazochangia

 kuwepo na kuenea kwa magonjwa ya zinaa.

Jamii inapaswa kuachana kabisa na Mila na desturi za zamani ambazo usababisha kuenea kwa magonjwa ya zinaa, kwa mfano kukeketa wasichana kwa kutumia wembe mmoja na pia kitendo cha kurithisha wanawake au wanaume ikitokea mmoja amefariki, kwa hiyo hali hii inapaswa kukoma kabisa na jamii za hivi zipatiwe elimu Ili kuweza kuokoa maisha ya watu na kupunguza madhara yatokanayo na magonjwa haya kama vile ugumba na vifo vya watoto wachanga wanaozaliwa na kaswende.

 

4. Kutoa elimu kwa wakimbizi na vijana walio kwenye umri wa kubarehe.

Kwa kawaida katika makazi ya wakimbizi Kuna hattari kubwa ya kuwepo kwa magonjwa ya zinaa kwa sababu ya kuwepo kwa watu mbalimbali na waliokusanyika kwa pamoja kwa hiyo wanapaswa kupewa elimu kuhusu madhara ya magonjwa ya zinaa na njia za kuepuka Nazo ambazo ni kuwa na mpenzi mmoja pamoja na kutumia kondom.

 

5. Vile vina na vijana wanapaswa kuwa na mipaka na kuepukana na matendo ya zinaa katika umri mdogo kwa hiyo wanapaswa kusubiri au hali ikiwa vibaya watumie kinga Ili kuepuka na kuwepo kwa magonjwa ya zinaa.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu Rajabu
Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views: 2395

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii     👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 Bongolite - Game zone - Play free game    

Post zinazofanana:

Kazi ya Ini: Jinsi ya kulilinda dhidi ya sumu.

Ini ni kiungo kikubwa zaidi cha ndani mwilini na kinafanya kazi kama "kiwanda cha kusafisha sumu" cha mwili wako. Kazi yake ni muhimu sana kwa uhai, kuanzia kuchuja damu hadi kuyeyusha chakula. Hata hivyo, kutokana na mtindo wa maisha wa kisasa, ini linaweza kulemewa na sumu, jambo linalopelekea maradhi kama ini la mafuta (fatty liver) au uvimbe wa ini (hepatitis). Makala haya yanachambua kazi kuu za ini na mbinu madhubuti za kulilinda dhidi ya uharibifu.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa Kuvimba ubongo (Encephalitis)

Post hii inaelezea kuhusiana na Ugonjwa wa kuvimba kwa ubongo ambao kitaalamu huitwa Encephalitis, Ni Maambukizi ya virusi ni sababu ya kawaida ya hali hiyo. Ugonjwa wa Kuvimba ubongo unaweza kusababisha dalili zinazofanana na Homa, kama vile Homa au

Soma Zaidi...
Sababu za Kichefuchefu Katika Mimba

​Kichefuchefu na kutapika ni hali ya kawaida inayowapata wanawake wengi wajawazito, maarufu kama "asubuhi yenye kichefuchefu" (morning sickness). Posti hii inaelezea kwa nini hali hii hutokea, mambo yanayoichochea, na jinsi unavyoweza kuikabili ili kupata unafuu.

Soma Zaidi...
Njia za kujilinda na kujikinga na UTI

Somo hili linakwenda kukuletea njia za kujilinda na kujikinga na UTI

Soma Zaidi...
Sababu Zinazoweza Kusababisha Majibu ya Uongo ya HIV

​Kupata matokeo ya "positive" (chanya) katika kipimo cha VVU ni jambo linaloweza kuleta hofu kubwa. Hata hivyo, mara chache sana, vipimo vya VVU vinaweza kutoa majibu yanayoitwa false positive (majibu ya uongo), ambapo mtu hana virusi lakini kipimo kinaonyesha anavyo. Makala hii inaelezea mazingira ambayo yanaweza kusababisha hali hii na nini unapaswa kufanya ikiwa utapata matokeo hayo.

Soma Zaidi...
Vyakula Muhimu kwa Mama Mjamzito

Ujauzito ni kipindi cha kipekee kinachohitaji uangalizi maalum wa lishe. Makala hii inaangazia vyakula muhimu ambavyo kila mama mjamzito anapaswa kuzingatia ili kuhakikisha afya yake na ukuaji bora wa mtoto aliyepo tumboni.

Soma Zaidi...