picha

Njia za kupunguza ugonjwa wa zinaa

Posti hii inahusu zaidi njia ambazo zinaweza kutumika Ili kuweza kupunguza kuwepo kwa magonjwa ya zinaa

Njia za kupunguza ugonjwa wa zinaa.

1. Kwanza kabisa tunapaswa kufahamu kuwa ugonjwa wa zinaa uleta matatizo mengi kwenye jamii kwa hiyo tunapaswa kutumia njia mbalimbali Ili kuweza kupunguza ugonjwa huu, kwa hiyo zifuatazo ni mbinu za kupunguza ugonjwa wa zinaa.

 

2 . kutumia kinga wakati wa kujamiiana na kuwa na mpenzi mmoja.

Kwa kutumia kinga kwa mtu ambaye haumfahamu kama ana maambukizi ni jambo zuri na la busara kwa sababu katika kufanya hivyo maambukizi hayawezi kuwepo, pia kuwa na desturi ya kuwa na mpenzi mmoja na kupima mara kwa mara Ili kuangalia kama Kuna maambukizi yoyote walau kila mwezi kama inawezekana.na pia ikitokea kuna maambukizi ni vizuri kupima nyote na kuhaidi kuwa waaminifu katika mahusiano.

 

3. Kuachana na Mila na desturi zinazochangia

 kuwepo na kuenea kwa magonjwa ya zinaa.

Jamii inapaswa kuachana kabisa na Mila na desturi za zamani ambazo usababisha kuenea kwa magonjwa ya zinaa, kwa mfano kukeketa wasichana kwa kutumia wembe mmoja na pia kitendo cha kurithisha wanawake au wanaume ikitokea mmoja amefariki, kwa hiyo hali hii inapaswa kukoma kabisa na jamii za hivi zipatiwe elimu Ili kuweza kuokoa maisha ya watu na kupunguza madhara yatokanayo na magonjwa haya kama vile ugumba na vifo vya watoto wachanga wanaozaliwa na kaswende.

 

4. Kutoa elimu kwa wakimbizi na vijana walio kwenye umri wa kubarehe.

Kwa kawaida katika makazi ya wakimbizi Kuna hattari kubwa ya kuwepo kwa magonjwa ya zinaa kwa sababu ya kuwepo kwa watu mbalimbali na waliokusanyika kwa pamoja kwa hiyo wanapaswa kupewa elimu kuhusu madhara ya magonjwa ya zinaa na njia za kuepuka Nazo ambazo ni kuwa na mpenzi mmoja pamoja na kutumia kondom.

 

5. Vile vina na vijana wanapaswa kuwa na mipaka na kuepukana na matendo ya zinaa katika umri mdogo kwa hiyo wanapaswa kusubiri au hali ikiwa vibaya watumie kinga Ili kuepuka na kuwepo kwa magonjwa ya zinaa.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2345

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii     👉2 Bongolite - Game zone - Play free game     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉5 kitabu cha Simulizi     👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zinazofanana:

Fahamu Ugonjwa wa upungufu wa Adrenali.

Posti hii inaelezea kuhusiana na Ugonjwa wa upungufu wa Adrenali ni ugonjwa ambao hutokea wakati mwili wako hutoa kiasi cha kutosha cha homoni fulani zinazozalishwa na tezi zako za adrenali. ugonjwa huu hutokea katika makundi yote ya umri na huathiri

Soma Zaidi...
Je fangasi ikikaa kwa muda mrefu bila kutibiwa ina madhara gani?

Je umeshawaho kujiuliza maswali mengi kihusu fangasi?. Huyu hapa ni mmoja katika waulizaji waliopata kuuliza rundo la maswali haya. Soma post hii kuona nini ameuliza

Soma Zaidi...
Dalili za macho kuwa makavu

posti hii inaelezea kuhusiana na dalilili na Mambo ya hatari ya Macho makavu  hutokea wakati machozi yako hayawezi kutoa unyevu wa kutosha kwa macho yako. Machozi yanaweza kuwa duni kwa sababu nyingi. Kwa mfano, Macho makavu  yanaweza ku

Soma Zaidi...
Dalili za miguu kufa ganzi

Posti hii inahusu zaidi dalili mbalimbali ambazo Uweza kujitokeza na kuona kwamba ni Dalili za miguu kufa ganzi, pengine utokea kwa watu wote na pengine huwa ni kwa ghafla

Soma Zaidi...
Namna madonda koo yanavyotokea

Posti hii inahusu namna madonda koo yanavyotokea, ni jinsi na namna Magonjwa haya au Maambukizi yanavyotokea na kuweza kusababisha madhara kwa watu.

Soma Zaidi...
KAMA UNASUMBULIWA NA FANGASI

Post hii fupi inakwenda kukujuza juu ya tatizo la fangasi na nini ufanye.

Soma Zaidi...