Njia za kupunguza ugonjwa wa zinaa
Posti hii inahusu zaidi njia ambazo zinaweza kutumika Ili kuweza kupunguza kuwepo kwa magonjwa ya zinaa
Njia za kupunguza ugonjwa wa zinaa.
1. Kwanza kabisa tunapaswa kufahamu kuwa ugonjwa wa zinaa uleta matatizo mengi kwenye jamii kwa hiyo tunapaswa kutumia njia mbalimbali Ili kuweza kupunguza ugonjwa huu, kwa hiyo zifuatazo ni mbinu za kupunguza ugonjwa wa zinaa.
2 . kutumia kinga wakati wa kujamiiana na kuwa na mpenzi mmoja.
Kwa kutumia kinga kwa mtu ambaye haumfahamu kama ana maambukizi ni jambo zuri na la busara kwa sababu katika kufanya hivyo maambukizi hayawezi kuwepo, pia kuwa na desturi ya kuwa na mpenzi mmoja na kupima mara kwa mara Ili kuangalia kama Kuna maambukizi yoyote walau kila mwezi kama inawezekana.na pia ikitokea kuna maambukizi ni vizuri kupima nyote na kuhaidi kuwa waaminifu katika mahusiano.
3. Kuachana na Mila na desturi zinazochangia
kuwepo na kuenea kwa magonjwa ya zinaa.
Jamii inapaswa kuachana kabisa na Mila na desturi za zamani ambazo usababisha kuenea kwa magonjwa ya zinaa, kwa mfano kukeketa wasichana kwa kutumia wembe mmoja na pia kitendo cha kurithisha wanawake au wanaume ikitokea mmoja amefariki, kwa hiyo hali hii inapaswa kukoma kabisa na jamii za hivi zipatiwe elimu Ili kuweza kuokoa maisha ya watu na kupunguza madhara yatokanayo na magonjwa haya kama vile ugumba na vifo vya watoto wachanga wanaozaliwa na kaswende.
4. Kutoa elimu kwa wakimbizi na vijana walio kwenye umri wa kubarehe.
Kwa kawaida katika makazi ya wakimbizi Kuna hattari kubwa ya kuwepo kwa magonjwa ya zinaa kwa sababu ya kuwepo kwa watu mbalimbali na waliokusanyika kwa pamoja kwa hiyo wanapaswa kupewa elimu kuhusu madhara ya magonjwa ya zinaa na njia za kuepuka Nazo ambazo ni kuwa na mpenzi mmoja pamoja na kutumia kondom.
5. Vile vina na vijana wanapaswa kuwa na mipaka na kuepukana na matendo ya zinaa katika umri mdogo kwa hiyo wanapaswa kusubiri au hali ikiwa vibaya watumie kinga Ili kuepuka na kuwepo kwa magonjwa ya zinaa.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 Kitau cha Fiqh 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉5 web hosting 👉6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
Je vvu inaweza sababisha mate kujaa mdomoni
Je kujaa kwa mate mdomoni ni dalili ya kuwa na VVU, na je ni zipi dalili za Virusi Vya Ukimwi (VVU) mdomoni?
Soma Zaidi...Maumivu ya kichwa cha mara kwa mara (Migraine): Dalili na tiba.
Migraine si maumivu ya kawaida ya kichwa; ni hali ya mfumo wa neva inayoweza kuathiri vibaya maisha ya kila siku ya mtu. Inajidhihirisha kwa maumivu makali ya upande mmoja wa kichwa, yanayoambatana na kichefuchefu, kutapika, na unyeti mkubwa kwa mwanga na sauti. Makala haya yanafafanua kwa kina kile kinachotokea wakati wa shambulio la migraine, jinsi ya kutofautisha na maumivu mengine ya kichwa, na mikakati ya kitaalamu ya kudhibiti na kutibu hali hii.
Soma Zaidi...Athari za kutotibu fangasi
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu athari za kutokutibu fangasi
Soma Zaidi...Matumizi ya dawa za kulevya na athari zake kwenye ubongo.
Dawa za kulevya hazibadili tu tabia ya mtu, bali zinasababisha mabadiliko ya kudumu kwenye muundo na utendaji kazi wa ubongo. Makala haya yanachambua jinsi dawa hizi zinavyoiba mfumo wa furaha wa ubongo (reward system), na jinsi matumizi yake yanavyoweza kusababisha madhara ya kiakili na kimwili ambayo ni vigumu kuyatengua.
Soma Zaidi...Namna Maambukizi kwenye milija na ovari yanavyotokea
Post hii inahusu zaidi namna Maambukizi kwenye milija na ovari ambayo yanatokea,Mara nyingi usababisha na bakteria wanaoweza kuingia kupitia sehemu mbalimbali.
Soma Zaidi...