picha

Njia za kupunguza ugonjwa wa zinaa

Posti hii inahusu zaidi njia ambazo zinaweza kutumika Ili kuweza kupunguza kuwepo kwa magonjwa ya zinaa

Njia za kupunguza ugonjwa wa zinaa.

1. Kwanza kabisa tunapaswa kufahamu kuwa ugonjwa wa zinaa uleta matatizo mengi kwenye jamii kwa hiyo tunapaswa kutumia njia mbalimbali Ili kuweza kupunguza ugonjwa huu, kwa hiyo zifuatazo ni mbinu za kupunguza ugonjwa wa zinaa.

 

2 . kutumia kinga wakati wa kujamiiana na kuwa na mpenzi mmoja.

Kwa kutumia kinga kwa mtu ambaye haumfahamu kama ana maambukizi ni jambo zuri na la busara kwa sababu katika kufanya hivyo maambukizi hayawezi kuwepo, pia kuwa na desturi ya kuwa na mpenzi mmoja na kupima mara kwa mara Ili kuangalia kama Kuna maambukizi yoyote walau kila mwezi kama inawezekana.na pia ikitokea kuna maambukizi ni vizuri kupima nyote na kuhaidi kuwa waaminifu katika mahusiano.

 

3. Kuachana na Mila na desturi zinazochangia

 kuwepo na kuenea kwa magonjwa ya zinaa.

Jamii inapaswa kuachana kabisa na Mila na desturi za zamani ambazo usababisha kuenea kwa magonjwa ya zinaa, kwa mfano kukeketa wasichana kwa kutumia wembe mmoja na pia kitendo cha kurithisha wanawake au wanaume ikitokea mmoja amefariki, kwa hiyo hali hii inapaswa kukoma kabisa na jamii za hivi zipatiwe elimu Ili kuweza kuokoa maisha ya watu na kupunguza madhara yatokanayo na magonjwa haya kama vile ugumba na vifo vya watoto wachanga wanaozaliwa na kaswende.

 

4. Kutoa elimu kwa wakimbizi na vijana walio kwenye umri wa kubarehe.

Kwa kawaida katika makazi ya wakimbizi Kuna hattari kubwa ya kuwepo kwa magonjwa ya zinaa kwa sababu ya kuwepo kwa watu mbalimbali na waliokusanyika kwa pamoja kwa hiyo wanapaswa kupewa elimu kuhusu madhara ya magonjwa ya zinaa na njia za kuepuka Nazo ambazo ni kuwa na mpenzi mmoja pamoja na kutumia kondom.

 

5. Vile vina na vijana wanapaswa kuwa na mipaka na kuepukana na matendo ya zinaa katika umri mdogo kwa hiyo wanapaswa kusubiri au hali ikiwa vibaya watumie kinga Ili kuepuka na kuwepo kwa magonjwa ya zinaa.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/05/11/Wednesday - 10:40:05 pm Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 2063

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 ai web app    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Sababu za vidonda sugu vya tumbo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za vidonda vya tumbo sugu

Soma Zaidi...
Matatizo yanayosababisha mshtuko wa moyo.

Mshtuko wa moyo hutokea wakati mtiririko wa damu kwa moyo umezuiwa, mara nyingi kwa mkusanyiko wa mafuta, cholesterol na vitu vingine, ambayo huunda plaque katika mishipa inayolisha moyo (mishipa ya moyo). Mtiririko wa damu ulioingiliwa unaweza kuharibu

Soma Zaidi...
Dalili za UTI upande wa wanawake

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za UTI upande wa wanawake

Soma Zaidi...
Ufahamu ugonjwa wa UTI na dalili zake hasa kwa wajawazito

Wajawazito wanaposumbuliwa na ugonjwa wa UTI, dalili za UTI na namna ya Kujikinga na UTI

Soma Zaidi...
Dalili za UKIMWI

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za UKIMWI

Soma Zaidi...
Dalili za fangasi ukeni

Post hii inakwenda kukujulisha dalili za kuwa huwenda una fangasi sehemu zako za siri.

Soma Zaidi...
Dalili za moyo kushindwa kufanya kazi (heart failure)

post inaonyesha dalili mbalimbali za Kushindwa kwa moyo, wakati mwingine hujulikana kama kutofaulu kwa moyo, hutokea wakati misuli ya moyo wako haisukuma damu kama inavyopaswa. Hali fulani, kama vile ateri nyembamba katika moyo wako (Ugonjwa wa ateri y

Soma Zaidi...
DALILI ZA MIMBA BAADA YA TENDO LA NDOA

Je unahitaji kujuwa kama umepata ujauzito baada ya kufanya tendo la ndoa? hakika sio rahisi ila kama utakuwa makini utaweza.

Soma Zaidi...
Mambo ya kufanya kama una kiungulia

Posti hii inahusu zaidi mambo ambayo unapaswa kufanya kama una tatizo la kiungulia.

Soma Zaidi...
Dalili za tonsillitis (mafindo mafindo)

Tonsillitis kwa kiswahili hujulikana kama mafundomafundo ambayo hutokea pande mbili karibu na Koo na huwa na uvimbe na zikikaa kwa muda bila matibabu hutoa usaha.Dalili na dalili za ugonjwa wa tonsillitis ni pamoja na

Soma Zaidi...